MO alishatia Bilioni 20 kitambo na bado anaendelea kugharamika kwa mapenzi ya timu, ni wajinga pekee wanahoji nami nawaelimisha kuwatoa ujinga

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768

mnadhani hivi vyote vimetokea kimiujiza ? furaha tulizokuwa tunazopata hasa kimataifa mnadhani ni mpera umetoa zabibu ?
  • Kufuzu robo fainali mashindano ya caf ishakuwa kawaida,
  • timu kubwa kama al ahly zinaiheshimu Simba,
  • Simba ni klabu ya 7 kwenye ranking za Afrika,
  • wachezaji wa simba wana soko kubwa wapo waliosajiliwa Al Ahly, Ufaransa, n.k.
  • Makocha wa klabu kubwa Afrika wanatamani kufanya kazi Simba

Imekuwa ni dhahiri kwamba wanasimba wengi hawana elimu ya hizi bilioni 20 na hivyo wana kila haki ya kuzihoji zilipo sababu hawana elimu, Mjinga ni mtu anaebisha sababu hajui hivyo inahitaji aelimishwe nami natoa elimu, lakini hata baada ya kuelimika ukishupaza shingo unapandishwa cheo kuitwa mpumbavu.

Simba ya enzi hizo kabla ya Mo ilikuwa imejichokea, Mo akaahidi kununua asilimia 49 ya umiliki wa timu kwa bilioni 20, Kwa mantiki ya kawaida timu inapopata pesa huwa inawekeza kwenye timu ifanya vizuri zaidi, Mo alianza kutia pesa na kweli tulijionea kwa macho yetu mapinduzi makubwa sana hayajawahi kutokea hapa nchini kwenye soka letu, Kwa misimu minne mfululizo alikuwa anatia bilioni 5 kwa njia ya kuigharamia timu na mwaka 2021 rasmi akamaliza deni lake na kupewa umiliki wa timu.

Wanoulizia aliingiza benki gani hawa ndio kundi wanalodhani kila kitu kinauzwa kwa pesa taslimu, ningependa kuwaeleimisha si kila kitu huuzwa kwa pesa taslimu, Mfano Diamond Platnumz ni mwanahisa wa wasafi tv na radio kapewa hisa za umiliki wa asilimia kadhaa kwa kuweka jina lake tu ambalo lina thamani kiasi flani, Mtu unaweza kuwa na hoteli yako imechoka ukawa unatafuta mwekezaji umuuzie umiliki nusu kwa milioni 100, lakini pia ni sawa hata yeye mwenyewe akifanya ukarabati unaoweza kuthaminika ni milioni 100, Basi ndicho kilichotokea simba, umiliki wa asilimia 49 enzi hizo ulithaminishwa kuwa bilioni 20, Haikuwa lazima Mo atoe pesa cash Taslimu, kilichotokea ni kwamba aliigharamia timu kwa miaka minne kwa thamani iliyofikia bilioni 20 na timu ilipojiridhisha kweli ni kiasi hicho ikampa umiliki, hizi ndizo gharama alizotumia.

  • Usajili wa wachezaji + signing fee (hasa wachezaji ghali wa nje)
  • Gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji ili kuwapisha wapya
  • Mishahara wachezaji (hasa wachezaji ghali wa nje)
  • Makocha ghali wenye uzoefu mkubwa kimataifa
  • Usafiri (Safari za ndege mikoani na nje ya nchi, gharama za basi, n.k.)
  • Malazi (Hoteli za kifahari mikoani na nje ya nchi, Hostel, n.k)
  • Vyakula na vinywaji (wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, n.k.)
  • Matibabu kwa wachezaji wenye majeraha
  • Kiwanja cha Bunju

hayakuwa mazingaombwe ni PESA !!!
 
Kwanza kuithaminisha 49% ya umiliki wa Simba sc na bil. 20 Ni matusi makubwa sana kwa brand kubwa Kama Simba kwa pesa anazovuna mwamedi pale simba

Hizo gharama anazotoa mwamedi Ni kulipia matangazo yake anayofanyia biashara zake kupitia brand ya Simba.

Anaebisha alete risiti ya malipo ya matangazo yake kwny jezi ya Simba.

KIUFUPI MWAMEDI YUKO PALE SIMBA KIBIASHARA, HANA MAPENZ YYT NA TIMU
 
View attachment 3013139

Imekuwa ni dhahiri kwamba wanasimba wengi hawana elimu ya hizi bilioni 20 na hivyo wana kila haki ya kuzihoji zilipo sababu hawana elimu.
Kakutuma mjinga wewe ama? Hivi mnawajua wahindi au mnawaskia. Aondoke bana. Hajaweka hiyo pesa hakuna ushahidi wa kibenki. Mjinga mmoja wewe. Anawahadaa na vihela vya hapa na pale wakati ni timu yenye potential kubwa sana. Hamna akili.
 
Mwamedi mhuni Sana,

Zikiingiaga tu zile pesa za caf ndo utaskia zile kauli zake jinsi gani Simba sc inavomtia hasara

Lengo tu zisihojiwe, kisingizio Ni alitoa pesa za usajili na mishahara ya wachezaji.

Simba ingekua inamtia hasara angeiachia Tu.
 
Swali fikirishi kwanini muonekano wa Hundi ulikuwa wa bilioni 20, kumbe alikuwa analipa kwa dose tuanzie hapo kwanza yanakuja maswali mengine, kwakifupi huyo siyo muwekezaji halisi kwa maana km timu inahitaji bilioni 5 nadhani wanachama wanaweza kuzichanga
 
Huna utofauti na mtu anaeuza ngombe kadhoofu, mgonjwa, n.k. Mwenye pesa akianza kumlisha vizuri, kumtibu, kumuogesha, n.k. unaanza kulalamika pesa uliyopewa haikutosha.
 
Umeongea pumba mzee, pesa za matangazo ya bidhaa hayatoshi kuendesha kwa mwaka mzima, kuna fadha za kusajili wachezaji na mishahara ya wafanyakazi pamoja na wachezaji, usafiri wa ndani na nje ya nchi,malazi pamoja gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji na makocha,, bajeti ya Simba ni kiasi gani?

Mo si mmiliki wa timu yeye ana 49% pekee upande wa wanachama wana 51%, upande wa wanachama wanachangia nini au wanachangia kiasi gani
 
Una vinasaba vya UNYANI.
 
Kakutuma mjinga wewe ama? Hivi mnawajua wahindi au mnawaskia. Aondoke bana. Hajaweka hiyo pesa hakuna ushahidi wa kibenki. Mjinga mmoja wewe. Anawahadaa na vihela vya hapa na pale wakati ni timu yenye potential kubwa sana. Hamna akili.
Team ndo ashapewa na hamna cha kufanya
 
Mwamedi mhuni Sana,

Zikiingiaga tu zile pesa za caf ndo utaskia zile kauli zake jinsi gani Simba sc inavomtia hasara

Lengo tu zisihojiwe, kisingizio Ni alitoa pesa za usajili na mishahara ya wachezaji.

Simba ingekua inamtia hasara angeiachia Tu.
Ni mali yake aliyoivujia jasho kuipata, wacha ale matunda yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…