MO alishatia Bilioni 20 kitambo na bado anaendelea kugharamika kwa mapenzi ya timu, ni wajinga pekee wanahoji nami nawaelimisha kuwatoa ujinga

MO alishatia Bilioni 20 kitambo na bado anaendelea kugharamika kwa mapenzi ya timu, ni wajinga pekee wanahoji nami nawaelimisha kuwatoa ujinga

Kwanza kuithaminisha 49% ya umiliki wa Simba sc na bil. 20 Ni matusi makubwa sana kwa brand kubwa Kama Simba kwa pesa anazovuna mwamedi pale simba

Hizo gharama anazotoa mwamedi Ni kulipia matangazo yake anayofanyia biashara zake kupitia brand ya Simba.

Anaebisha alete risiti ya malipo ya matangazo yake kwny jezi ya Simba.

KIUFUPI MWAMEDI YUKO PALE SIMBA KIBIASHARA, HANA MAPENZ YYT NA TIMU
Alikuwa na timu zikamshinda ngoja awanyooshe Mikia FC.
 
Wewe ndio umemmilikisha hiyo team au??
Ni wanasimba tuiommilikisha kihalali kabisa, si kwa furaha zile alizotupa akiwa anaingiza bilioni 5 kila mwaka 2017/18 hadi 2020/21,,, unakumbuka simba ilivyokuwa moto wa kuotea mbali ?? unadhani ilikuwa miujiza ya zabibu kudondoka chini ya mpera ?

imekuwa kawiada timu kufuzu robo fainali, ni BILIONI 20 zilizosajili wachezaji wa kimataifa, makocha wazuri, bonasi za mechi, ndege kuwa kama daladala, mahoteli ya nyota tano, n.k.
 
Ni wanasimba tuiommilikisha kihalali kabisa, si kwa furaha zile alizotupa hasa mwanzoni

Pesa zake zilileta mafanikio makubwa sana, Si muujiza !!

imekuwa kawiada timu kufuzu robo fainali, ni BILIONI 20 zilizosajili wachezaji wa kimataifa, makocha wazuri, bonasi za mechi, ndege kuwa kama daladala, mahoteli ya nyota tano, n.k.
Pesa ambazo hao hao wanabodi wanadai huwa anazidai?? Huo sio uwekezaji bali ni unyonyaji
 
Pesa ambazo hao hao wanabodi wanadai huwa anazidai?? Huo sio uwekezaji bali ni unyonyaji
Ni tamaa zao tu, MO alishaweka mzigo na ni halali timu kuwa yake, Mo kafanya mambo makubwa sana kwa pesa alizoweka, sikuhizi kufuzu robo fainali ishakuwa kawaida, timu kubwa kama al ahly zinaijua simba si ya kuibeza, n.k.
 
View attachment 3013139

Imekuwa ni dhahiri kwamba wanasimba wengi hawana elimu ya hizi bilioni 20 na hivyo wana kila haki ya kuzihoji zilipo sababu hawana elimu, Mjinga ni mtu anaebisha sababu hajui hivyo inahitaji aelimishwe nami natoa elimu, lakini hata baada ya kuelimika ukishupaza shingo unapandishwa cheo kuitwa mpumbavu.

Simba ya enzi hizo kabla ya Mo ilikuwa imejichokea, Mo akaahidi kununua asilimia 49 ya umiliki wa timu kwa bilioni 20, Kwa mantiki ya kawaida timu inapopata pesa huwa inawekeza kwenye timu ifanya vizuri zaidi, Mo alianza kutia pesa na kweli tulijionea kwa macho yetu mapinduzi makubwa sana hayajawahi kutokea hapa nchini kwenye soka letu, Kwa misimu minne mfululizo alikuwa anatia bilioni 5 na mwaka 2021 rasmi akamaliza deni lake na kupewa umiliki wa timu.

hayakuwa mazingaombwe ni PESA, Ndizo pesa zilizofanya Simba iwe na wachezaji wzuri ngazi za kimataifa, makocha wenye uzoefu kimataifa, bonas kila mechi, safari za ndege nje na ndani ya nchi kama vile ni daladala, n.k. ni PESA, sio mazingaombwe.

Kimsingi wote wanaomsema Mo wanatakiwa waombe msamaha

Usajili wa wachezaji + signing fee (hasa wachezaji ghali wa nje)
Gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji ili kuwapisha wapya
Mishahara wachezaji (hasa wachezaji ghali wa nje)
Makocha ghali wenye uzoefu mkubwa kimataifa
Usafiri (Safari za ndege mikoani na nje ya nchi, gharama za basi, n.k.)
Malazi (Hoteli za kifahari mikoani na nje ya nchi, Hostel, n.k)
Vyakula na vinywaji (wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, n.k.)
Matibabu kwa wachezaji wenye majeraha
Kiwanja cha Bunju
2021 rejea we are 2024 now
 
Kwanza kuithaminisha 49% ya umiliki wa Simba sc na bil. 20 Ni matusi makubwa sana kwa brand kubwa Kama Simba kwa pesa anazovuna mwamedi pale simba

Hizo gharama anazotoa mwamedi Ni kulipia matangazo yake anayofanyia biashara zake kupitia brand ya Simba.

Anaebisha alete risiti ya malipo ya matangazo yake kwny jezi ya Simba.

KIUFUPI MWAMEDI YUKO PALE SIMBA KIBIASHARA, HANA MAPENZ YYT NA TIMU
Unajua kitu ambacho watanzania tuko nacho vizuri ni kuongea na hasa kwemye criticism.

Kuongea ni kitu rahisi sana ambacho kinaweza kufanywa na mtu yeyote ila linapokuja swala la utendaji ni watu wachache sana wenye kuweza.

Kama matangazo yanalipa kiasi cha kuifanya timu iweze kujiendesha bila mwekezaji kwanini hatukuprint jezi zenye nembo ya Simba ili tupate hela ambazo zingeingia direct kwenye Account ya Simba kuliko kumtafuta mwekezaji ambaye anaenda kunufaikia kupitia brand ya timu?

Kama wewe una amini mwekezaji akiweka matangazo kwenye jezi ya timu yako anaenda kunufaika kwanini usitumie hiyo fursa kujiendesha mwenyewe kwa kuweka matangazo ya Club yako ili uwe unanufaika mwenyewe?

Mpaka unamuachia mtu aweke matangazo yake kwenye jezi yako ili wewe uweze kuendesha timu kupitia hela zake maana yake ni kwamba wewe umeshindwa kupata hiyo faida ambayo saizi unaiona.

Sasa kwanini uwe obsessed na mtu anayepata faida kupitia rotaion ya hela zake?

Vipi wanaomiliki 51% ambayo ni kubwa wao wametoa bei gani mpaka sasa?

Au sisi wenye 51% kazi yetu ni kuchambua faida anazopata mwekezaji kupitia ads?

Kabla ya MO Dewj Simba ilikuwa katika hali gani?

Naskia chinichini kuna mwekezaji ambaye anatajwa kuwa yupo tayari kuichukua Simba, na huyo mwekezaji yupo nyuma ya hao wanaopiga kampeni za Mo atoke

Alikuwa wapi kipindi hicho ambacho Simba ilikuwa inataabika?

So ni wazi kuwa ameanza kuiona value ya Simba kutokana na hela za MO.

No offense lakini namuona kama shangingi wa bar anayefuata meza yenye bia nyingi.

Ni kama Zubeda mke wa Profesa Jay aliyemtoa kijijini sitimbi akila magimbi akijipaka mafuta ya kupikia lakini alipomleta mjini na kuanza kumgharamia demu akaamza kushoboka na mataita wa mjini.

Some spazz gotta say "Ooh MO unajua anapata sana faida halafu anasingizia Simba inampa hasara"

Mimi na wewe kama mashabiki hatufaidiki na chochote kwenye Simba zaidi ya furaha (labda kama kuna wenzangu mpo kwenye payyrol) ni Furaha ambayo tunaipata kupitia matokeo mazuri tu ndio malipo yetu.

Kama MO anapata faida ni non of our business just like Man U au Man City ambazo tunazishabikia kwa mapenzi yetu kwa lengo la kupata furaha.
 
View attachment 3013139

Kufuzu robo fainali mashindano ya caf ishakuwa kawaida, timu kubwa kama al ahly zinaiheshimu simba, Simba ni ya 7 Afrika, wachezaji wa simba wanagombaniwa na klabu kubwa kama Al Ahly, n.k. mnadhani hivi vyote vilitokea kimiujiza, LA HASHA, ni pesa nyingi sana zimetumika, hakunaga cha bure !


Imekuwa ni dhahiri kwamba wanasimba wengi hawana elimu ya hizi bilioni 20 na hivyo wana kila haki ya kuzihoji zilipo sababu hawana elimu, Mjinga ni mtu anaebisha sababu hajui hivyo inahitaji aelimishwe nami natoa elimu, lakini hata baada ya kuelimika ukishupaza shingo unapandishwa cheo kuitwa mpumbavu.

Simba ya enzi hizo kabla ya Mo ilikuwa imejichokea, Mo akaahidi kununua asilimia 49 ya umiliki wa timu kwa bilioni 20, Kwa mantiki ya kawaida timu inapopata pesa huwa inawekeza kwenye timu ifanya vizuri zaidi, Mo alianza kutia pesa na kweli tulijionea kwa macho yetu mapinduzi makubwa sana hayajawahi kutokea hapa nchini kwenye soka letu, Kwa misimu minne mfululizo alikuwa anatia bilioni 5 na mwaka 2021 rasmi akamaliza deni lake na kupewa umiliki wa timu.

hayakuwa mazingaombwe ni PESA, Ndizo pesa zilizofanya Simba iwe na wachezaji wzuri ngazi za kimataifa, makocha wenye uzoefu kimataifa, bonas kila mechi, safari za ndege nje na ndani ya nchi kama vile ni daladala, n.k. ni PESA, sio mazingaombwe.

Kimsingi wote wanaomsema Mo wanatakiwa waombe msamaha

Usajili wa wachezaji + signing fee (hasa wachezaji ghali wa nje)
Gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji ili kuwapisha wapya
Mishahara wachezaji (hasa wachezaji ghali wa nje)
Makocha ghali wenye uzoefu mkubwa kimataifa
Usafiri (Safari za ndege mikoani na nje ya nchi, gharama za basi, n.k.)
Malazi (Hoteli za kifahari mikoani na nje ya nchi, Hostel, n.k)
Vyakula na vinywaji (wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, n.k.)
Matibabu kwa wachezaji wenye majeraha
Kiwanja cha Bunju
Aliweka Benki ipi mkuu??
 
20bn plus za wanachama ziko kwenye account gani . Tuache kupiga kelele za Mo peke yake. Leteni balance ya hela za wanachama period.
 
Aliweka Benki ipi mkuu??
kwani manunuzi yote ni kwa mfumo wa benki ?

Naweza kuja kwako nikakwambia nahitaji uniuzie nusu ya umiliki wa hoteli yako kwa njia ya kuikarabati iwe nzuri zaidi, yaani mafundi, vifaa, finishing, ulinzi, n.k. nagharamia mimi. hata Diamond hakuna pesa aliyoweka pale wasafi yeye kaweka jina lake tu, sembuse mtu kupewa umiliki kwa kugharamia ?

Tatizo naloona ni kwamba watanzania wengi elimu bado ni tatizo kubwa sana
 
Umeongea pumba mzee, pesa za matangazo ya bidhaa hayatoshi kuendesha kwa mwaka mzima, kuna fadha za kusajili wachezaji na mishahara ya wafanyakazi pamoja na wachezaji, usafiri wa ndani na nje ya nchi,malazi pamoja gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji na makocha,, bajeti ya Simba ni kiasi gani?

Mo si mmiliki wa timu yeye ana 49% pekee upande wa wanachama wana 51%, upande wa wanachama wanachangia nini au wanachangia kiasi gani
Pesa za matangazo kwenye jezi zingekuwa zinafaida kuliko pesa anazotoa mwekezaji kwenye gharama za uendeshaji wa timu.

Basi Yanga wasingetembeza bakuli kwasababu walikuwa na option ya kutengeneza products nyingi na kuzitia logo ya Yanga kisha wao wakaendelea kuingiza mpunga.

Lakini kingine ambacho wanasahau ni hiki.

Watu wanasema Mo anapata faida kwenye matangazo as if ni upande tu wa Mo unaofaidika kwenye hilo.

Lakini wao hawafikirii pia kupitia malengo ya MO kutangaza biashara yake pia kumeweza kuifanya hata Simba nayo kutangazwa na kujulikana.

Simba kabla ya Mo ilikuwa haina jina kimataifa lakini kupitia MO imejulikana na kuna percent ya pesa imeweza kufaidika. Lakini hiyo watu hawaisemi wanasema ya Mo tu
 
Mo ni mwizi narudia ni mwizi anayenibishia kesho aende kwenye maduka yake yaliyopo mataa ya mnazi mmoja kuelekea mnara wa saa Kuna kanga za Simba zinauzwa zimezalidhwa na kiwanda chake Cha morogoro bila Simba kuwa na mkataba na hawapati hata senti tano.
Watu wanaomtetea mitandaoni Tena anawalipa kijiwe Chao kipo msikitini karibu na Zahri hotel Kama inaelekea DTB bank nyuma ya ofisi zake.
Mo akiondoka hauzidi nusu saa wawekezaji wengine wanajitokeza.
 
Mo ni mwizi narudia ni mwizi anayenibishia kesho aende kwenye maduka yake yaliyopo mataa ya mnazi mmoja kuelekea mnara wa saa Kuna kanga za Simba zinauzwa zimezalidhwa na kiwanda chake Cha morogoro bila Simba kuwa na mkataba na hawapati hata senti tano.
Watu wanaomtetea mitandaoni Tena anawalipa kijiwe Chao kipo msikitini karibu na Zahri hotel Kama inaelekea DTB bank nyuma ya ofisi zake.
Mo akiondoka hauzidi nusu saa wawekezaji wengine wanajitokeza.
unadhani pesa zinazotumika kuwaleta kina Benchikicha zinadondoka kama mvua ?
 
View attachment 3013139
mnadhani hivi vyote vimetokea kimiujiza ? furaha tulizokuwa tunazopata hasa kimataifa mnadhani ni mpera umetoa zabibu ?
  • Kufuzu robo fainali mashindano ya caf ishakuwa kawaida,
  • timu kubwa kama al ahly zinaiheshimu Simba,
  • Simba ni klabu ya 7 kwenye ranking za Afrika,
  • wachezaji wa simba wana soko kubwa wapo waliosajiliwa Al Ahly, Ufaransa, n.k.
  • Makocha wa klabu kubwa Afrika wanatamani kufanya kazi Simba

Imekuwa ni dhahiri kwamba wanasimba wengi hawana elimu ya hizi bilioni 20 na hivyo wana kila haki ya kuzihoji zilipo sababu hawana elimu, Mjinga ni mtu anaebisha sababu hajui hivyo inahitaji aelimishwe nami natoa elimu, lakini hata baada ya kuelimika ukishupaza shingo unapandishwa cheo kuitwa mpumbavu.

Simba ya enzi hizo kabla ya Mo ilikuwa imejichokea, Mo akaahidi kununua asilimia 49 ya umiliki wa timu kwa bilioni 20, Kwa mantiki ya kawaida timu inapopata pesa huwa inawekeza kwenye timu ifanya vizuri zaidi, Mo alianza kutia pesa na kweli tulijionea kwa macho yetu mapinduzi makubwa sana hayajawahi kutokea hapa nchini kwenye soka letu, Kwa misimu minne mfululizo alikuwa anatia bilioni 5 kwa njia ya kuigharamia timu na mwaka 2021 rasmi akamaliza deni lake na kupewa umiliki wa timu.

Wanoulizia aliingiza benki gani hawa ndio kundi wanalodhani kila kitu kinauzwa kwa pesa taslimu, ningependa kuwaeleimisha si kila kitu huuzwa kwa pesa taslimu, Mfano Diamond Platnumz ni mwanahisa wa wasafi tv na radio kapewa hisa za umiliki wa asilimia kadhaa kwa kuweka jina lake tu ambalo lina thamani kiasi flani, Mtu unaweza kuwa na hoteli yako imechoka ukawa unatafuta mwekezaji umuuzie umiliki nusu kwa milioni 100, lakini pia ni sawa hata yeye mwenyewe akifanya ukarabati unaoweza kuthaminika ni milioni 100, Basi ndicho kilichotokea simba, umiliki wa asilimia 49 enzi hizo ulithaminishwa kuwa bilioni 20, Haikuwa lazima Mo atoe pesa cash Taslimu, kilichotokea ni kwamba aliigharamia timu kwa miaka minne kwa thamani iliyofikia bilioni 20 na timu ilipojiridhisha kweli ni kiasi hicho ikampa umiliki, hizi ndizo gharama alizotumia.

  • Usajili wa wachezaji + signing fee (hasa wachezaji ghali wa nje)
  • Gharama za kuvunja mikataba ya wachezaji ili kuwapisha wapya
  • Mishahara wachezaji (hasa wachezaji ghali wa nje)
  • Makocha ghali wenye uzoefu mkubwa kimataifa
  • Usafiri (Safari za ndege mikoani na nje ya nchi, gharama za basi, n.k.)
  • Malazi (Hoteli za kifahari mikoani na nje ya nchi, Hostel, n.k)
  • Vyakula na vinywaji (wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, n.k.)
  • Matibabu kwa wachezaji wenye majeraha
  • Kiwanja cha Bunju

hayakuwa mazingaombwe ni PESA, Ndizo pesa zilizofanya Simba iwe na wachezaji wzuri ngazi za kimataifa, makocha wenye uzoefu kimataifa, bonas kila mechi, safari za ndege nje na ndani ya nchi kama vile ni daladala, n.k. ni PESA, sio mazingaombwe.

Kimsingi wote wanaomsema Mo wanatakiwa waombe msamaha
Ndiyo kusema wakati hayo yote yanafanyika timu haikuwa na mapato yake nje ya udhamini wa Mwekezaji?
Yaani mapato yaliyotokana na gate collection, fedha za CAF, wadhamini kama Sportpesa, Mbet, Azam Media, nk!!!
 
Swali fikirishi kwanini muonekano wa Hundi ulikuwa wa bilioni 20, kumbe alikuwa analipa kwa dose tuanzie hapo kwanza yanakuja maswali mengine, kwakifupi huyo siyo muwekezaji halisi kwa maana km timu inahitaji bilioni 5 nadhani wanachama wanaweza kuzichanga
wanachama wapi?
 
Ni wanasimba tuiommilikisha kihalali kabisa, si kwa furaha zile alizotupa akiwa anaingiza bilioni 5 kila mwaka 2017/18 hadi 2020/21,,, unakumbuka simba ilivyokuwa moto wa kuotea mbali ?? unadhani ilikuwa miujiza ya zabibu kudondoka chini ya mpera ?

imekuwa kawiada timu kufuzu robo fainali, ni BILIONI 20 zilizosajili wachezaji wa kimataifa, makocha wazuri, bonasi za mechi, ndege kuwa kama daladala, mahoteli ya nyota tano, n.k.
Ni documents gani Simba Sc ilisaini na mwekezaji...

Ya kwamba asilimia 49 ya hisa zake zitalipwa kwa mfumo wa matumizi ya timu?

Kitu usichokijua we mbwiga, kwasasa tunapambana wajumbe wa bodi upande wa wanachama wajiuzulu then turudi kuzaa na mwekezaji.
 
Swali fikirishi kwanini muonekano wa Hundi ulikuwa wa bilioni 20, kumbe alikuwa analipa kwa dose tuanzie hapo kwanza yanakuja maswali mengine, kwakifupi huyo siyo muwekezaji halisi kwa maana km timu inahitaji bilioni 5 nadhani wanachama wanaweza kuzichanga
Hakuna mwekezani anayelipa zote kwa maramoja bali huwa mnakubalina schedules.Kama mnaona za Mohammed haIkuwa za maana mngeziacha hizo fedha na siyo kuItumbua harafu baada ya kufaidi ndo mnadai ushahidi wa pesa.
Ukitaka ushaidi waulize viongozi walikuwa wansema kila kitu Kiko vizuri
 
Ni documents gani Simba Sc ilisaini na mwekezaji...

Ya kwamba asilimia 49 ya hisa zake zitalipwa kwa mfumo wa matumizi ya timu?

Kitu usichokijua we mbwiga, kwasasa tunapambana wajumbe wa bodi upande wa wanachama wajiuzulu then turudi kuzaa na mwekezaji.
Mambo ni kimya kimya hapa bongo, Umewahi kuuona hata mkataba original wa jezi wa Simba na Vunja bei ???
 
Ndiyo kusema wakati hayo yote yanafanyika timu haikuwa na mapato yake nje ya udhamini wa Mwekezaji? Yaani mapato yaliyotokana na gate collection, fedha za CAF, wadhamini kam Sportpesa, Mbet, Azam Media, nk!!!
Kawaulize wazee wa Simba, watu washajenga na kununua magari ya kifahari.
 
Back
Top Bottom