Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

Hii inaonyesha familia wamelipa ransom!

Moja ya masharti ya ransom ni kutozungumza kuhusu tukio lote!

Kama atazungumza kuhusu yaliyomsibu mpaka akarudi basi hiyo itaonyesha kuwa hakulipa ransom na hakuna makubaliano.

Hoja iliyopo mbele yetu kwa sasa, Je, kama amelipa ransom, nini kwa sasa nafasi ya matajiri nchini kuhusiana na usalama wao kwa sababu kulipa ransom ni kufungua mlango wa biashara ya kidnapping and ransom nchini kwa matajiri.

Kosa la kulipa ransom baada ya kutekwa ambalo nchi za kusini mwa Afrika kama Afrika Kusini na Msumbiji walilianza kwa matajiri ndilo kwa sasa linazidi kuwatafuta kwa kasi zaidi.

Je, kuna uwezekano na Tanzania tukaelekea ambako nchi za kusini mwa Afrika ziliko kwenye biashara ya kidnapping and ransom?

Eti ransom..

Acheni kutufanya mafala.....

Labda uniambie waliochukua ransom ni hao hao govt ila usidanganye eti alikua kidnapped na independent kidnappers!
 
Mo maneno yake ya Kwanza baada ya kuombwa aongee kidogo alisema "namshukuru Mungu kwa kuwa niko salama, pia namshukuru mh rais......."

Anamshukuru mh rais kwa kipi? Nimejiuliza maswali yasiyokuwa na majibu

Hili la kumshukuru Raisi labda ni kiwewe.
lakini pia Januari Makamba ana uhusiano gani wa karibu na Mo mbona inaonekana alikuwa wa kwanza kupigiwa simu na Mo?
 
Hakimu-Msomali
PP-msomali
Advocate-msomali
Mshitakiwa-Msomali
Je unategemea nani hapo ataehukumiwa?[emoji3]
 
Kwahiyo kale kamgomo baridi kakutishia kufunga viwanda vyote tarehe 20 ndio kamefanya kazi?
 
Hivi kuna nchi yenye mabwege kuliko Tanzania? Mtekwaji halalamiki katekwa na serikali bali anaishukuru, nyie mnamlazimisha aseme katekwa na serikali!
Sasa ulitaka alalamike ili wamrudie tena????Usiwe bwege hivyo unafikiri tu ndani ya box!Conspirqcy ziko za aina nyingi,nenda kasome mikasa iliyowahi tokea duniani ili upanue uwezo wako wa kufikiri!
 
Ndugu wanabodi,
Ukiiangalia press ya IGP kisha ukaangalia majigambo ya Mambosasa akinesha gari iliyotajwa na IGP kuwa imepatikana na MO akiwa salama kabisa lazima utagundua kuwa kuna picha imechezwa hapa
Lakini yote kwa yote tumshukuru Mungu MO kapatikana salama
Aksante.
Kinachotuchanganya zaidi ni hao watekaji kutumia gari hiyo hiyo kumrudisha MO hadi Gymkana bila kukamatwa japo ulinzi umeimarishwa kila kona.
Hii haihitaji elimu yoyote ya upelelezi kung'amua kuwa kuna mchezo mchafu nyuma ya pazia.
 
Mambosasa: Taarifa siku ya tukio,waliomteka Mo ni wazungu wawili

IGP: waliomteka Mo walikuwa na gari la nchi jirani ila hakulitaja,ila wataalamu wa kufuatilia lile gari walisema ni la Msumbiji

Mo amepatikana Dar es salaam lakin si Msumbiji, wala Afrika Kusini


Baada ya kupatikana:Mambosasa: waliomteka Mo walikuwa wasouth Afrika ,walikuwa wanaongea kilugha

Unaweza ukajiuliza maswali hapa ,kichwa kikaota upara bila kupenda
Cctv yenye drone automated inayofukuzia Gari, yenye eyefish I aangalia ndani na inauwezo kutoa picha ya Techno!!

Tunaambiwa tuwapongeze kufanikisha kupatokana Mo! Just few steps kutoka ikuru! Eneo linalolindwa 24hrs that is why barabara hiyo saa 12 haoiruhusiwi kupita!Maajabu hayaishi nchi yetu hii!
 
Tulia unaonekana unachemka sana.
Vile Vishindo tu vya Jeshi letu la Polisi, vimewafanya watekaji washindwe cha kufanya zaidi ya kusalenda.
Walikuwa wamezingirwa pande zote na hawana cha kufanya, hata kudai pesa walishindwa. Watadai kwa njia gani ?
Watalipwaje ?
Hawakuwa na namna zaidi ya kumwachia
Wangi mmeuangalia huu utekaji kirahisi sana.
Haikuwa rahisi hivyo.
Husikii aibu?
 
Chadema wamechukizwa mno na kupatikana kwa Mo maana kiki yao imebuna.

Shida na Matatizo yanayoipata Tanzania ndiyo ufahari wa Chadema!
 
Wanajitahidi kuua soo ionekane wabongo hawajahusika waliohusika Ni watu Wa nje Ila kwa wajanja tumeelewa mchezo mmeona mmejichanganya mkamuachia moo

Yaani Ni sawa na kuanzisha ugomvi afu ukimbie.. Pressure ya wachunguzi kutoka nje inayofanywa kimya kimya ndio imewapiga KO
 
Tulia unaonekana unachemka sana.
Vile Vishindo tu vya Jeshi letu la Polisi, vimewafanya watekaji washindwe cha kufanya zaidi ya kusalenda.
Walikuwa wamezingirwa pande zote na hawana cha kufanya, hata kudai pesa walishindwa. Watadai kwa njia gani ?
Watalipwaje ?
Hawakuwa na namna zaidi ya kumwachia
Wangi mmeuangalia huu utekaji kirahisi sana.
Haikuwa rahisi hivyo.
Ndugu, wangejua kuwa wamebanwa hivyo wasingeendesha gari ile ile mpaka viwanja vya gymcana
 
Hivi jamaa hajaongea chochote tangu aongee siku aliyetekwa Mo???
 
Hawezi kuja kwani hata yeye mwenyewe alikuwa ameandaliwa cha kutueleza kabla ya kumuachia MO. Hata yale maelezo ktk simu ya MO sio yeye mwenyewe bali walitwit kwa niaba yake. NI AIBU KWA JESHI LA POLISI NA NI AIBU KWA SERIKALI NA NI AIBU KWA NCHI YETU. Mimi ningemshauri Jiwe aachane kabisa na mtoto pendwa kwani tutakuja kuyashuhudia mengi na makubwa zaidi ya haya.
Unaweza kuniambia sababu ya Mo kutekwa ni nini?
 
Ni imani yangu kuwa mpaka sasa familia imeshapoa na kujua angalau kwa juu juu kilichomsibu mtoto wao. Ikumbukwe kuwa familia iliitisha press conference na kuutaarifu uma kuhusu tukio la kupotea kwa Mo. Pia ilitoa ahadi ya tuzo (baunty) kwa atakayefanikisha kupatikana mtoto wao.

Ni maoni yangu kuwa familia ingeitisha PRESS CONFERENCE kuutaarifu uma kuhusu kupatikana kwa Mo. Pia ijibu angalau maswali machache ili kuondoa kelele zinazoendelea kwenye mitandao ya kijamii. Wana wajibu wa kuwaeleza watanzania ukweli wa haya mambo kwa faida yao na ya jamii kwa ujumla.

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom