Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

hivi huyu ndo aliyeombewa kupewa PHD ktk Uzi Fulani?
 
Kwezisho,
Siku ile niliomba nipate faragha niswali.
Walinipatia Alhamdulilah.

Nililia na Allah katika sijda kuwa aninusuru kama alivyomnusuru
Issa bin Maryam kuuliwa na Wayahudi.

Alhandulilah Allah SW alipokea dua zangu.
Angalia hapo chini nini kilitokea:

Sasa hapo ikawa nimelipata jingine. Kumbe wauza unga hawakamatwi hadi amri itoke juu. Sasa kama amri haikutoka ndiyo muuza unga atapita aingize sumu zake mitaani? Hili likazidi kunidhihirishia kuwa kukamatwa kwangu hakukuwa na uhusiano wowote na vita dhidi ya mihadarati bali ni vita vile vile vikongwe dhidi ya Uislam.

Nikawa pale usiku kucha. Sasa wakati niko pale wakidhani nimelala. Wakawa wenyewe kwa wenyewe wanazungumza kuhusu hii ‘operation’ neno walilotumia ni kuwa 'leo tume-dial wrong number.' Wakawa wanasema, “Huyu bwana mbona hakuelekea kama muuza unga tena huyu mtu bwana kasoma kweli kweli” Wanadhani mie nimelala kumbe ni macho nawasikiliza. (Vipi utalala katikati ya michongoma?). We umeona jinsi alivyokuwa akijibu na kuchambua mambo.” Hilo ndilo likawa gumzo lao wakinisifia kwa ufasaha na mantiki lakini wakizungumza kwa sauti ya chini kabisa. Hapa ikanidhuhirikia kuwa hawa vijana walikuwa wanatimiza wajibu wao wa kazi tu lakini kiini khasa cha kukamatwa kwangu hawakuwa wanakifahamu.

Walionikamata walikuwa vijana kama wanne na wote walijitambulisha kwa majina ya Kiislam. Nilijua ni waongo kwa kuwa Muislam anonekana katika uso na katika matumizi ya lugha. Ila kitu kimoja lazima nikiri. Wale vijana walikaa na mimi kwa wema na hawakunibughudhi hata kidogo. Hata nilipokuwa nakwenda msalani kijana alienisindikiza alinitaka radhi akasema, ”Nakusindikiza kwa sababu ni sheria lakini sisi tunakustahi kwa hiyo utuwie radhi kwa kukufuta hadi msalani.”

Asubuhi wakubwa wakaja kazini lakini hakuna alienikabili. Walikuwa wakinichungulia kutoka mlangoni kama simba ndani ya kizimba kwenye zoo, nami nikawa najifanya siwaoni. Ndipo akaja mkubwa mmoja tena akaniita kwa jina langu na kwa heshima na bashasha sana, "Bwana Mohamed tuwie radhi sana pamekuwa na makosa kidogo tuwie radhi sasa hivi tutakuruhusu uende nyumbani. ” Akatoka nje akawa akipiga simu. Kisha akarudi ndani akaamrisha nibebewe mizigo yangu na gari la polisi linirudishe nyumbani. Kistaarabu kabisa nikakataa gari ile huku nikifanya maskhara kuwa naogopa gari ya polisi asijepiga simu akasema mrudisheni huyo mtuhumiwa. Ofisi nzima ikacheka. Hapo ndipo wale wakamataji wangu wa usiku wakabeba mizigo yangu nami nafuata nyuma tunatoka nje ya uwanja.
Naam hapo ndipo pembe za mnafiki zilizogundishwa kwa gundi zinapodondoka na kumuacha akiaibika. Ama kweli mnafiki hana aibu. Watu wanapanga njama za kuabisha wenzao kwa dhana za kutunga!!
 
Nafikiri thread yangu ipo wazi tu. Kwa hiyo unataka kunithibitishia wanaowalawiti waislamu huko mahabusu/jela ni wakristo?
Na waziri alisema uchunguzi utafanyika kwa sababu ilikuwa ni tuhuma. Hivyo tuhuma inaweza kuwa kweli au si kweli.
Lakini nisisitize tu kwamba kuhusisha tuhuma za jinai au makosa mengine na UDINI ni kueneza chuki tu.
Achi...
Inatosha mie si mtu wa ubishani.
 
Vita ya majimaji,chini, ya uongozi was kinjekitile ngwale,wale wa piganaji walikuwa wa Islam???,kweli!!!,ushaidi pls
Juan,
Mada hii tumepata kuizungumza kwa kirefu hapa jamvini.
Nakuwekea majibu yangu hapo chini:
Khalidoun,
Haijapata kutokea mnakasha kama ule katika JF.
Hivi ndivyo nilivyofahamishwa na wenyeji walioipokea
barzani.

Wanamajlis,
Naona ukumbi umepoa.

Yuko aliyesema ana maswali kuhusu Nyerere anataka kuniuliza.
Kapotea sijamsikia.

Yuko aliyekuja na mpya kuwa Waislam sio walioanza harakati dhidi
ya ukoloni akataja Maji Maji.

Nikaweka jibu.

Hakuridhika akadai kuwa majibu nimejinukuu mwenyewe kwa hiyo
ni ajua.


451px-Chief_Songea_Mbano.jpg

Chief Songea Mbano

Nikaja na jibu kutola nyaraka za Wajerumani wenyewe waliopigana
na Chief Abdul Rauf bin Songea.

Najua kapata mshtuko kwa kuwa hajapatapo kumsikia Sultan Abdul
Rauf bin Songea
katika Vita Vya Maji Maji ingawa inawezekana kuwa
kasikia Chief Songea Mbano.

Najua ametatazika kama wengi wanavyotatazika hivi sasa wakinisoma.
Hawa ni watu wawili au ni mtu mmoja?

Abdul Rauf bin Songea ndiyo huyu Songea Mbano?
Kuchakachua historia kuna hatari zake na hii ni mojawapo.

Hakuwa anajua kuwa Vita Vya Maji Maji Waislam walisimama dhidi ya
Wajerumani.

Majemadari 60 Waislam walinyongwa na kuzikwa kaburi moja Mahenge,
Songea na kumbukumbu ya iko hapo kwenye kumbukumbu ya Maji Maji
Songea.

Katika kaburi la peke yake amezikwa Sultan Songea Mbano.
Je huyu ndiye yule Abdul Rauf bin Songea?

Kuna mahali Abdul Rauf bin Songea anaitwa kwa jina la ''Chief Songea
Luwafu Mbano.''


Soma hapo chini:
One of these is Chief Songea Luwafu Mbano, from whom the town takes its name. As the most famous of the Ngoni resistance leaders, the Germans honoured ...


CYgjIZKWYAA1G2j.jpg



Hii ''Lwafu,'' ndiyo Rauf?
Huyo hapo juu kwenye picha ndiye Chief Abdul Rauf Songea Mbano

Jemadari Muislam wa Vita Vya Maji Maji.
Angalia hapo chini ghafla majina ya hawa Waislam hayaonekani badala
yake kuna majina mengine lakini ni ya wale wale Waislam walionyongwa:


DSC02264.jpg


Nani huyu anaepotosha haya majina mazuri ya Waislam katika historia
ya Maji Maji?

Sasa soma hapo chini:
Islam has always been the ideology of resistance against colonial rule or any other authority which tried to subjugate Muslims. Consequently, no government in power either indigenous or foreign has ever been kind or supportive to Islam, and likewise Muslims have always been engaged in a continuous struggle to preserve their faith and fight for their rights. Christianity was resisted by Muslims right from the beginning. In any uprising against the colonial government, Muslims took the opportunity to attack missionaries and Christian establishments. Muslim perceived both missionaries and the colonial government as fellow collaborators and therefore enemies to Islam. Islamic radicalism has therefore a long history in the struggle against colonial rule and Christianity. Christianity became a reactionary force siding with the colonial authority. One needs only to read the letter written by the Chief Songea bin Ruuf at the time when he was mobilising his people for war while at the same time trying to cement alliances with other chiefs in Southern Tanganyika and across the River Ruvuma in Mozambique. This letter written to Sheikh and Sultan Mataka bin Hamin Massaninga reads:


''Sultan Songea bin Ruuf writes: To the Shaykh and Sultan Mataka bin Hamis Massaninga. Greetings, etc. I am sending you a letter through Kazembe. We have received an order from God that the Europeans must leave the country. We are in the process of fighting them here. I believe that we have long since been reconciled,[so] send me your children, so that we may make an alliance. I had wanted to send you some cattle as a gift, but am not able to do so, as the war which God desired is continuing. Send me a hundred riflemen, and support me in storming the Boma (Songea).

I am also sending you a flask of the Prophet Muhammad, which contains the means for conquering the Europeans. Have no doubt about it, it possessed great power. And when we have taken the Boma (Songea), we shall go on the stations on the Nyasa together, you and I. Now, let us forget our old quarrels.

This bottle, with a da’wa, has been sent by Chinyalanyala himself, the war leader. He also sends the container (kombe), and sends you many greetings.

If your men will come, then Chinyalanyala himself will come and will give you many of the holy things.

Hassan bin Isma’il greets you.
Many salutations,

Sultan Songea bin Ruuf.” [1]

A point to note here is that this letter, beautiful as it is, it is being doubted by Becker, who maintains that the origins of the letter are dubious.[2] This is the stand which many Christian researchers have taken when faced with the realities of Islam in Tanganyika.


[1] C.H. Becker, ‘Material for the Understanding Islam in German East Africa’, Tanzania Notes and Records, No. 68, February, 1968, p.58.

[2] Ibid.

Angalia jina la Kazembe no. 51 na Hassan bin Ismail no, 53 majina ambayo Chief Abdul
Rauf bin Songea
kayataja katika barua yake.

Angalia neno ''bin'' katika baadhi ya majina kisha jiulize na wapi likawekwa neno ''bin,'' kwa
asiyekuwa Muislam.

DSC02267.jpg


Kaburi la Chief Abdul Rauf Songea Mbano katika Maonyesho ya Taifa ya Maji Maji
Mahenge, Songea ambae kazikwa kwa jina la Songea Mbano.

Kutoka: Mohamed Said, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of The Muslim Struggle Against British Colonialism in Tangnayika, Minerva Press, London 1998."[/TD]

Sultan Songea bin Ruuf huyu hapo juu ndiyo huyu anayoelezwa tena hapa chini kama Chief
Songea Mbano?:


"Anasema hali hiyo ilitokea kwa sababu Chifu Songea Mbano alikuwa ndiyo Jemedari Mkuu wa Jeshi la Wangoni na alikuwa ni hodari sana asiyeogopa lolote kwa hiyo Wajerumani walitaka abakie ili wamtumie kwa malengo yao.

"Yeye Chifu Songea alidai na yeye anyongwe kama walivyonyongwa ndugu zake, basi alinyongwa na Wajerumani ambao waliondoka na kichwa chake wakiwa wamekiweka ndani ya kasha kwenda Ujerumani ambako hakijarudi hadi leo na kiwiliwili chake kuzikwa katika kaburi la peke yake."

(Kutoka:Historia Ya Vita Vya majimaji.)
Wanajamvi,
Naamini mnaiona tofauti iliyopo.

Au hawa ni machifu wawili tofauti?
Nani anahusika na uchakachuaji huu wa majina haya ya Kiislam katika historia ya Vita Vya Maji Maji?
 
Kumbe anayofanya Trump yapo nchi mbalimbali kama za Saudia Saudi Arabia puts 30 Shias on trial for spying for Iran - World - DAWN.COM , Qatar, USA, Bahrain, Tanzania, Germany, Turkey, Australia n.k kuwa ukienda nchi Fulani (Iran, Sudan, Yemen) basi tegemea kupata mahojiano ya ziada na usalama wa taifa/uhamiaji ktk viwanja vyao vya ndege/balozi za nchi nyingi kama nilizozitaja hapo juu kwa uchache.

Hapa Mohamed Said anatufahamisha kuwa alifadhiliwa na Marekani ktk baadhi ya safari zake bila kufahamu kuwa inawezekana pia Marekani inatumia mbinu ya ''kumkumbatia '' mtu ili wamuelewe zaidi (intelligence collection) na hata kutuma taarifa zake kwa nchi ''rafiki''.
 
“Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.
.
Mkuu Maalim jee ya kweli haya?!. Japo Vatican ni nchi na ina ubalozi wake nchini, uliwahi kusikia kuna viza ya kuingia Vatican?!. Immigation wanaangalia mtu umetoka wapi, visa ni ya Italy, na nadhani ndio nchi iliyokuwa ikiongoza kuuza mihadarati ulaya nzima biashara ikimilikiwa na the Mafia na wote ni Wakristu!.

Nimewahi kusafiri kutoka Tanzania na mzungu fulani lakini ni raia wa Tanzania, tukafika Marekani, wote wawili tukaonyesha passport zetu za Tanzania, mwenzagu akaruhusiwa, mimi nikazuiliwa nikachukuliwa picha na alama za vidole ndipo nikaruhusiwa!. Uhalifu ni uhalifu tuu, hauna dini, rangi wala kabila, japo wanaojilipua wengi ni watu wa dini fulani, hatuwatambui kwa dini yao, bali kwa uhalifu wao!, japo magaidi wengi ni watu wa dini fulani lakini hatuwatambui kwa dini yao bali kwa ugaidi wao!.

Ingefanyika sensa ya dini za wahalifu wote walioko magerezani, amini msiamini, watu mngeshangaa humu na kusema mnazingiziwa!. Tembelea hapa
Mapapa 560 wa Madawa ya Kulevya watajwa. Wamo
Kwenye list hii kati ya majina haya 560, majina 120 ni ya asili ya kizungu, majina 320 ya asili ya Kiarabu, majina 119 ni asili ya Kiafrika na jina moja ni la number ya gari.
Jee wajua what does this mean? .
NB. Naombeni sana msichanganye asili ya majina na dini za watu, majina ni majina tuu na dini ni imani, mtu anaweza kuwa na majina ya asili ya Kiarabu na akawa Mwislamu, au Mkristo na mtu mwenye jina la asili ya Kizungu akawa Mwislamu au Mkristo na wenye majina ya asili nao vivyo hivyo.

Mtu ukiisha tanguliza mawazo hasi ya kunyanyaswa kwa sababu ya dini yako, hata pale utakapofanyika ukaguzi wa ziada wa halali kabisa kwa ajili ya kujiridhisha, utaona una nyanyaswa!. Please stopuni hizi negativity, think positive, hata ukiwa treated harshly, lakiwa ukiwa positive kuwa hilo jambo linafanyika in good faith and not an ill motive, utakuwa na amani ndani ya moyo wako.

Mtu yoyote akiwa ni frequent flyer na safarri zenyewe za nchi za mashaka mashaka, kushukiwa ni kawaida!, mimi siamini ulisachiwa kwa ajili ya dini yako..

Hata hivyo pole kwa masahibu yaliyokufika!.

Paskali
 
Paschal,
Naongea kingine na wewe unaongea kingine.

Ugomvi wangu na Wamarekani ulitokana na paper niliyowasilisha
Chuo Kikuu Cha Ibadan.

Ile paper ilibadili hali ya mkutano na kuionyesha US kama nchi
dhalim na katika Tanzania kupitisha Sheria ya Ugaidi, sheria hiyo
imetumika kwa kuwakamata viongozi wa Waislam na kufunga
taasisi zao kwa uonevu.

Wasikilizaji wakaja juu wakasema sheria hiyo haiwezi kupita Nigeria
kwani hiyo itakuwa serikali imetangaza vita na Waislam.

Kutokana na hali hii Wamarekani wakataka kujua mwandishi ni nani
hivyo wakaleta taarifa Dar es Salaam.

Maafisa wa ubalozi wa Tanzania Nigeria walikuwapo pia kwenye mkutano
ule.

Hii ndiyo sababu ya mimi kukamatwa na kuzuliwa kuwa nasambaza u,nga.
Nia ilikuwa kunipa salamu kuwa, ''Big Brother is watching you.''

Kuanzia hapo ikawa kila safari yangu nje ya nchi napata, ''special tratment,''
''passport control,'' na katika, ''security check'' nikichukuliwa kama ''terrorist
sympathiser.''

Pasi yangu iliwekewa alama ya siri.

Ukipenda soma hii paper hapa:
Mohamed Said: ISLAM, TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT
 
Mbona huwa mkiguswa kidogo mnakimbilia kinga ya dini hio ni inferiority complex kwani maovu wameandikiwa watu wa dini Fulani,kama upo sawa acha wafanye kazi yao km hawajakutendea haki zipo mamlaka husika za juu unaweza kwenda kutoa malalamiko yako pia mahakama zipo kukutetea pia. Me MTU akianza kuhususisha dini ktk mambo namuona ana shida kidogo. Wao ufanya kazi Kwa taarifa wape ushiriano na pia ni haki yako kuwa na shahidi kabla ya kupekuliwa.

Airport ipi duniani kupekuliwa mpaka uwe na shahidi?

Hujasafiri nini?

Hiyo ni nyumbani kwako au mitaani.
 
Interface,
Unajua ile paper yangu ilibadili mwelekeo wa ile conference na mimi
nilikuwa kati ya wazungumzaji wa mwisho.

Waamerika ingawa wanajifanya wanajua lakini si kuwa kila kitu kiko
hadhir kwao.

Naamini walishtuka sana nilipowaambia kuwa Waislam wa Tanzania
hawana ugomvi na USA wao wana matatizo yao ya ndani na utawala
ulioko madarakani.

Walishtuka nnilipowaambia kuwa Waislam ndiyo waliopigania uhuru wa
Tanganyika wakianza na kwa kunyanyua silaha dhidi ya Wajerumani.

Walishtuka nilipowaambia kuwa Waislam wa Tanzania wangependa kuwe
na mjadala wa wazi kujadili matatizo haya yote.

Bahati mbaya Sheria ya Ugaidi imesababisha viongozi wao kukamatwa na
taasisi zao kufungwa kwa uonevu tu.

Sasa pale Chuo Kikuu Cha Ibadan kitabu cha Sykes kimekuwa kikisomeshwa
toka 2003.

Wanafunzi na waalimu wakawa wanaijua hali ilivyo Tanzania na hii ndiyo
sababu ya wao kusema Sheria ya Ugaidi haiwezi kupitishwa Nigeria kwani
huko ni kutangaza vita na Waislam.

Waamerika wakawa kwa njia moja nimewavurugia mipango yao.
Yaliyofuatia hapo sasa ni historia.
Sasa kama waislam walipigania vita ya uhuru sisi tuliozaliwa baada ya uhuru yanatuhusu nini? Yanatusaidia nini? Sisi tunajua hii nchi inaitwa Tanzania tutaishi hapa kwa Amani na upendo, Story zenu za mkoloni zimepitwa na wakati, Ongelea mambo ya teknolojia na maendeleo, Dini hizi ni propaganda za waarabu na wazungu, Wao wanakula bata mbaya na wanaenjoy maisha nyie wanawavisha makanzu na mabarakashia na Misalaba
 
Leloo...
Nimesema kuwa nitakuwekeeni kidogo maana ni mkasa mrefu.
Sikutaka kuwachosha wasomaji wangu.

Ila ikiwa unataka kujua nini kiliendelea naweza nikakuwekea
kipande cha mwisho In Sha Allah.
Leta kaka tujue kilichojiri
Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza.

Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo.

Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule afisa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama.

Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri.

Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maofisa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadarati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina.

Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa.

Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imefika siku yangu.

Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kufikiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu.

Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka Tehran mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama.

Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, “Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya.”

Nikawauliza,“Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli?” Wakasema, “Ndiyo maana leo tumekukamata.” Nikawaambia, “Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni “Mzungu wa Unga” kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya.”

Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran?

Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Marekani na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha.

“Mbona hamkunikamata wakati ule?” Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, “Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.

Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu.

Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa.

Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.

Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania?
 
Mkuu Maalim jee ya kweli haya?!. Japo Vatican ni nchi na ina ubalozi wake nchini, uliwahi kusikia kuna viza ya kuingia Vatican?!. Immigation wanaangalia mtu umetoka wapi, visa ni ya Italy, na nadhani ndio nchi iliyokuwa ikiongoza kuuza mihadarati ulaya nzima biashara ikimilikiwa na the Mafia na wote ni Wakristu!.

Nimewahi kusafiri kutoka Tanzania na mzungu fulani lakini ni raia wa Tanzania, tukafika Marekani, wote wawili tukaonyesha passport zetu za Tanzania, mwenzagu akaruhusiwa, mimi nikazuiliwa nikachukuliwa picha na alama za vidole ndipo nikaruhusiwa!. Uhalifu ni uhalifu tuu, hauna dini, rangi wala kabila, japo wanaojilipua wengi ni watu wa dini fulani, hatuwatambui kwa dini yao, bali kwa uhalifu wao!, japo magaidi wengi ni watu wa dini fulani lakini hatuwatambui kwa dini yao bali kwa ugaidi wao!.

Ingefanyika sensa ya dini za wahalifu wote walioko magerezani, amini msiamini, watu mngeshangaa humu na kusema mnazingiziwa!. Tembelea hapa
Mapapa 560 wa Madawa ya Kulevya watajwa. Wamo
Kwenye list hii kati ya majina haya 560, majina 120 ni ya asili ya kizungu, majina 320 ya asili ya Kiarabu, majina 119 ni asili ya Kiafrika na jina moja ni la number ya gari.
Jee wajua what does this mean? .
NB. Naombeni sana msichanganye asili ya majina na dini za watu, majina ni majina tuu na dini ni imani, mtu anaweza kuwa na majina ya asili ya Kiarabu na akawa Mwislamu, au Mkristo na mtu mwenye jina la asili ya Kizungu akawa Mwislamu au Mkristo na wenye majina ya asili nao vivyo hivyo.

Mtu ukiisha tanguliza mawazo hasi ya kunyanyaswa kwa sababu ya dini yako, hata pale utakapofanyika ukaguzi wa ziada wa halali kabisa kwa ajili ya kujiridhisha, utaona una nyanyaswa!. Please stopuni hizi negativity, think positive, hata ukiwa treated harshly, lakiwa ukiwa positive kuwa hilo jambo linafanyika in good faith and not an ill motive, utakuwa na amani ndani ya moyo wako.

Mtu yoyote akiwa ni frequent flyer na safarri zenyewe za nchi za mashaka mashaka, kushukiwa ni kawaida!, mimi siamini ulisachiwa kwa ajili ya dini yako..

Hata hivyo pole kwa masahibu yaliyokufika!.

Paskali
http://www.globalresearch.ca/non-mu...0-of-all-terrorist-attacks-in-america/5333619

Shindana na research na kupayuka.
 
Back
Top Bottom