Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Kuna sehemu kwenye injili, Yesu anamtoa mapepo jamaa flani hivi, kisha Yesu akayaamuru yale mapepo yawaingie nguruwe waliokuwepo around!

Kwa nilivyoelewa, ni kwamba wale nguruwe walikuwa mali ya raia fulani maeneo hayo.

Sasa, swali langu ni hili, Kwamba kumbe nguruwe walikuwa wanafugwa hata kwenye kipindi kile cha Yesu, tena maeneo yale yale?

Je, walikuwa wanafugwa kwa sababu gani, kama si kwa ajili ya kitoweo?
 
2 Wakorintho 3:1
Je! Tunaanza tena kujisifu wenyewe? Au tunahitaji, kama wengine, barua zenye sifa kuja kwenu, au kutoka kwenu?

2 Wakorintho 3:2
Ninyi ndinyi barua yetu, iliyoandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote;

2 Wakorintho 3:3
mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.

2 Wakorintho 3:4
Na tumaini hilo tunalo mbele za Mungu kwa njia ya Kristo.

2 Wakorintho 3:5
Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lo lote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu.

2 Wakorintho 3:6
Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.

Roho haijui nguruwe ni nini, haijui kuzini ni kitu gani. Ndiyo maana roho inatia uzima
Andiko(Torati) huua
ngoja nikukumbushe kitu..wana wa israel walipokuwa safarin kurud nchi ya ahadi walilishwa mana mpya kila siku,,,,ilikuwa inadondoka kutoka mbinguni mikate ile/mana..... ilikuwa huwezi kutunza mana ya jana ule leo... sasa ni hvyo mpaka sasa mungu aliekataza ndie alieruhusu na sababu amekupa sasa nyny mnang'ang'ania mana ya jana na wakati imeshashuka mpya hio haitakusaidia...... hayo ni mafundisho mapya ya shetan kwakuwa mungu hahubiri hvy tn, tembea na wingu lake anapotembea usikae kwenye jua la jana halitakusidia,,, ujiulizi baada ya kristo na injili kuja kwenye mataifa hakuna mkristo alieshika sabato wala ivyo vyakula kwenye biblia?????
 
Hapa ungesema tu NGURUWE aka KITIMOTO, acha kuzunguka sana.

Kwa taarifa yako, tutaendelea kumtafuna mno. Sisi tumeamua kwenda na neno la usikiite najisi kiumbe alichokupa Bwana..

Kitimoto tamu wazee. Tena ukute ile ya Mboga mboga na ndizi. Haki ya Mungu.
Atuachie my wetu.
 
Warumi 14:1-3
[1]Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.

[2]Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.

[3]Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.
 
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Msabato wewe eti fungu la 9!
 
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Mungu amekataza zinaa pia lakini mnaongoza kuzini ninyi

Hapa nimenunua kilo zangu 4 nikitoka kanisani leo natengeneza roast swaaafi na ugali tunakula familia tena ndani ya familia tuna mhudumu wetu muislamu anakipenda kwelikweli KTM
 
Mungu amekataza zinaa pia lakini mnaongoza kuzini ninyi

Hapa nimenunua kilo zangu 4 nikitoka kanisani leo natengeneza roast swaaafi na ugali tunakula familia tena ndani ya familia tuna mhudumu wetu muislamu anakipenda kwelikweli KTM
Kama kuna mtu anazini anatenda dhambi, Je unayaangalia matendo ya watu kama kundi au kama mtu mmoja mmoja?

Mbinguni hatutaingia kwa matendo ya madhehebi yetu au kwa matendo ya dini zetu bali kwa moyo ulio safi wa kila mcha Mungu.
 
Mungu atakuhukumu kwa kutofata amri zake ayo mengine mnajidanganya tu
 
Kuna sehemu kwenye injili, Yesu anamtoa mapepo jamaa flani hivi, kisha Yesu akayaamuru yale mapepo yawaingie nguruwe waliokuwepo around!

Kwa nilivyoelewa, ni kwamba wale nguruwe walikuwa mali ya raia fulani maeneo hayo.

Sasa, swali langu ni hili, Kwamba kumbe nguruwe walikuwa wanafugwa hata kwenye kipindi kile cha Yesu, tena maeneo yale yale?

Je, walikuwa wanafugwa kwa sababu gani, kama si kwa ajili ya kitoweo?
Hata leo hii Mungu ashuke hapa na afanye miujiza yote na watu waamini yeye kweli Ndiye, bado dhambi itaendelea tu, sisi wanadamu ni viumbe vya ajabu.
 
ujiulizi baada ya kristo na injili kuja kwenye mataifa hakuna mkristo alieshika sabato wala ivyo vyakula kwenye biblia?????
Hili una uhakika nalo? Unajua ibada ya jumapili imekuja siku gani?
 
katika amri zote 10 haipo ya kutokula nguruwe.

maana yake nini??
hii haikuwa dhambi ya kumchukiza Mungu,bali dhambi ya kimila ya watu wa israel.

ni kama amri za kanisa la roma za leo.
 
[3]Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.
Hili fungu ukilibeba kichwa kichwa hakuna dhambi utakemea sababu utaonekana unahukumu watu, na kuhukumu si kwa binadamu bali ni kwa Mungu, Tumejua kuwa kuna dhambi kwa sababu kuna sheria.
 
katika amri zote 10 haipo ya kutokula nguruwe.

maana yake nini??
hii haikuwa dhambi ya kumchukiza Mungu,bali dhambi ya kimila ya watu wa israel.

ni kama amri za kanisa la roma za leo.
Petro alimkatalia Mungu mara tatu kwamba hawezi kula Najisi, na huyu alikuwa mfuasi wa Yesu, Je mafundisho hayo aliyatoa wapi? Na kwanini alikataa ikiwa Mungu ameruhusu tule kila kilicho mbele yetu?
 
Back
Top Bottom