Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Hapa ungesema tu NGURUWE aka KITIMOTO, acha kuzunguka sana.

Kwa taarifa yako, tutaendelea kumtafuna mno. Sisi tumeamua kwenda na neno la usikiite najisi kiumbe alichokupa Bwana..

Kitimoto tamu wazee. Tena ukute ile ya Mboga mboga na ndizi. Haki ya Mungu.
Soma vizuri hayo yalikuwa ni maono tu na nimeweka na tafsiri yake ambayo ipo katika sura hiyohiyo. Nyie mnasomaje Biblia mbona mambo mengine yapo wazi tu-?
 
Usile nguruwe.(Israeli ya kimwili)
Usile nguruwe (usipokee mafundisho wa wachungaji wasaliti/mbwa mwitu, rejea Mathayo. Hii ni kwa sisi Waisrael kiroho)

NB: tunamuabudu Mungu katika roho na KWELI. Hakuna madhara wala dhambi kumla nguruwe.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
Ni kwanini Petro alimkatalia Mungu mara tatu kuchinja na kula wanyama wale aliokuwa ameletewa? na hakula mpaka chombo kikaondolewa,

Hayo mafundisho yeye aliyapata wapi?
 
Petro alimkatalia Mungu mara tatu kwamba hawezi kula Najisi, na huyu alikuwa mfuasi wa Yesu, Je mafundisho hayo aliyatoa wapi? Na kwanini alikataa ikiwa Mungu ameruhusu tule kila kilicho mbele yetu?
petro ni kutoka katika taifa hilo hilo lililozishika sheria za tolati,enzi na enzi.

hata aliotembea nao Yesu na kulala nao haina maana walimuelewa 100% bado wengi iliwachukua muda,kama mtume paulo.
 
Na hapa je??

Wakolosai 2:16-17
[16]Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

[17]mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.
Naaaaam Naaaaam
 
Na hapa je??


1 Timotheo 4:1-5
[1]Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

[2]kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

[3]wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

[4]Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;

[5]kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
Barikiwaa sanaaa.
 
Lete Andiko linalosema agano la Kale lilifutwa...
Soma waebrani 6,7 na 8. Hayo yote ni kivuli tu kumuelezea kristo. Ndio maana hatuna kuhani mkuu, sadaka za kuteketeza, au hema ambalo ndiko pekee Mungu alipatikana. Cha ajabu reality iliyokuja ndio Yesu ila watu bado mnajifichia kwenye kivuli.
 
Soma waebrani 6,7 na 8. Hayo yote ni kivuli tu kumuelezea kristo. Ndio maana hatuna kuhani mkuu, sadaka za kuteketeza, au hema ambalo ndiko pekee Mungu alipatikana. Cha ajabu reality iliyokuja ndio Yesu ila watu bado mnajifichia kwenye kivuli.
God bless you
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Chakula ni utamaduni,
Yesu alisema ya kuwa "..amri iliyokuu kuliko zote ni upendo..."

"..Mpende jirani yako kama nafsi yako.."

Mambo ya kitimoto yalikuwa katika torati ya Musa, kwa maana watu waliishi katika sheria.

Kwa sasa tunaishi katika Amri za Mungu ( hakuna amri inayoongelea chakula)

Mnajipa mzigo mzito kiimani ilihali hamuwezi kutenda hata yaliyo ya kawaida katika maisha? Chakula huingia kinywani kisha tumboni na huenda chooni.

Imani yako ndiyo msingi wa hukumu.
Mnajihesabia haki kwa kuwa tu hamli kitimoto!?
 
Vyovyote iwavyo hakuna bado duniani ktk kizazi hiki anayeweza kutoka hadharani hata Yesu ashuke leo aruhusu tumdanganye kwa utani kwamba tumezifuata amri zake japo kwa 5%.

Sinywi pombe nazini,sizini naiba,siibi nasengenya,sisengenyi nakula nguruwe (wengine wanasema ni dhambi kula nguruwe) sili Nguruwe wake za watu siwaachi wake za watu siwaachi natamani visivyokuwa vyangu in short taja dhambi unayoijua hakuna asiyeitenda ninyi watu wenye imani kali mnafanya maisha yanakuwa magumu huku ya kwenu hamjayatengeneza.

Ondoeni kwanza udhaifu wenu ambao kimsingi hata ninyi wenyewe hamuwezi kuuondoa sababu bado mna hulka ya ubinadamu kama wale mnaotaka wabadilike walivyo na wanavyotarajia Mungu awaondolee udhaifu huo.
Fine tunatenda dhambi na hata Biblia imeandika tukisema hatuna dhambi tunajidanganya na tunamfanya Yesu Kristo kuwa Muongo kasome Yohana 1:8–10,

Je kutenda kwetu dhambi (maana hata kuwaza ni dhambi) Kutufunge midomo tusiwaseme watu wengine wanaopotoka?
 
Wakolosai 2:16-17
[16]Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
Kuhukumu ni kazi ya Mungu kazi yetu sisi ni kusema ukweli pale tunapoona mtu anapotoka, Ni fungu hilohilo watu huwa wanalitumia kuisema sabato ila wanasahau kwamba watu ambao paulo alikuwa anawambia hapo walikuwa wanaishika sabato pamoja na paulo mwenyewe. Soma matendo ya Mitume 17:2 Inasema "Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake, akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akitumia Maandiko Matakatifu."
 
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Mbinguni hatuingii Kwa kipimo Cha kula chakula, tutaingia Kwa kufanya matendo mema na ROHO nyeupe ambayo sio ya visasi wala husda
 
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Yaani ujumbe tu wa Kumwambia Petrol aongozane na wale wasio wayahudi ilimkazimu kutumia Wanyama?

Maono unayachukulia poa eti ilikuwa maono tu......mbona hakutumia Ng'ombe ambaO hazibishaniwi?
 
Fine tunatenda dhambi na hata Biblia imeandika tukisema hatuna dhambi tunajidanganya na tunamfanya Yesu Kristo kuwa Muongo kasome Yohana 1:8–10,

Je kutenda kwetu dhambi (maana hata kuwaza ni dhambi) Kutufunge midomo tusiwaseme watu wengine wanaopotoka?
Bold kubwa,tusitumie maandiko matakatifu ku-justify udhaifu wetu na mimi nikikwambia kasome Luka 6:41-45 andiko mahsusi kwa wanaojifanya wasafi kiimani unadhani tutafika?

Kila mmoja amepewa utashi wa kung’amua mema na mabaya na kila mtu Mungu anampa muda wa kujirudi usitumie nguvu nyingi kwa ajili ya wengine huku wewe hatma yako huijui.
 
Hili una uhakika nalo? Unajua ibada ya jumapili imekuja siku gani?
Mimi siyo mtaalam sana kwenye mambo ya dini. Naomba msaada ni kitabu gani na aya ipi kwenye Biblia iliyoelekeza kuwa ibada ni lazima ifanyike JUMAMOSI? Msaada please.
 
Usile nguruwe.(Israeli ya kimwili)
Usile nguruwe (usipokee mafundisho wa wachungaji wasaliti/mbwa mwitu, rejea Mathayo. Hii ni kwa sisi Waisrael kiroho)

NB: tunamuabudu Mungu katika roho na KWELI. Hakuna madhara wala dhambi kumla nguruwe.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
Kimwingiacho mtu hakimtii unajisi kwani hicho hutoka na kuingia chooni, bali unajisi ni Yale yatokayo moyoni mwake... Wivu, chuki nk........

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
 
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Wewe kama huli, sisi wenzako tunakula. Wasabato kuna wakati mnatuonea sana wivu sisi wala Kitimoto.

Mbona Wachina wanakula mbwa, nyoka, chatu, paka, vyura, nk. Lakini hamuwasemi? Hii siyo poa kabisa.
 
Vyovyote iwavyo hakuna bado duniani ktk kizazi hiki Mkristo anayeweza kutoka hadharani hata Yesu ashuke leo aruhusu tumdanganye kwa utani kwamba tumezifuata amri zake japo kwa 5%.

Sinywi pombe nazini,sizini naiba,siibi nasengenya,sisengenyi nakula nguruwe (wengine wanasema ni dhambi kula nguruwe) sili Nguruwe wake za watu siwaachi wake za watu siwaachi natamani visivyokuwa vyangu in short taja dhambi unayoijua hakuna asiyeitenda ninyi watu wenye imani kali mnafanya maisha yanakuwa magumu huku ya kwenu hamjayatengeneza.

Ondoeni kwanza udhaifu wenu ambao kimsingi hata ninyi wenyewe hamuwezi kuuondoa sababu bado mna hulka ya ubinadamu kama wale mnaotaka wabadilike walivyo na wanavyotarajia Mungu awaondolee udhaifu huo.
Kinachowaponza watu aina ya mtoa mada ni unafiki. Wao wanafikiri dhambi ni kunywa pombe na kula tu kitimoto. Ila mambo mengine wanaona ni ruksa kufanya! Jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo.
 
Back
Top Bottom