Morogoro Day Trip: Kwa Wakazi wa Dar & Pwani

Morogoro Day Trip: Kwa Wakazi wa Dar & Pwani

Umenikumbusha mbali. Kwakweli ni ka experience kazuuuri japo nilitaka kufika morning site ila nikakata moto njiani[emoji1787]

Mandhari, hewa saaafi, kaubaridi kwa mbali.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni experience nzuri sana ila usiombe kukata moto, sisi tulipanda milima ya Udzungwa kule Sanje waterfalls kuna top na bottom, unachagua uende wapi

Yani ile tumefika tu top, nilijitupa chali huku nahema juu juu nikasema sirudii tena, Sasa hivi mlima pekee ninaoutamani ni Kilimanjaro tu mingine sitaki kuisikia
 
🤣🤣🤣🤣🤣Vimilima vya Goba tu vinanitoaga jasho vya huko naweza Anza kulia bureee
Basi anza mazoezi kabla ya kupanda milima mikubwa, kama vimiinuko vya Goba, Makabe, Msumi huviwezi basi kauzito kaangaliwe upya🤣
 
Salam wakuu.

Hii special kwa wakazi wa Dar na Pwani.

Najua mnakuaga busy sana, sana na kuna muda mnakosa ata muda wa kupumzisha akili na mwili, sababu ya muda na kipato kwa wengine.

Kuna hii Hiking Day trip ya kwenda Morogoro na kurudi, unaweza have some fun na uka relax sana mwili na akili.

Maandazi.
Kwakua muda mwingi itakua ni kupanda milima, vaa tu nguo utakazo kua comfortable mfano raba, Tshirt, buti. Mfano my outfit ilikua hivi:
View attachment 2820162

ila kama utakua na earpods kama unapenda podcast & music, na mfuko wa rambo kwaajili ya kuweka cm incase mvua ikikuchapa. Vingine labda maji au kopo la maji na hela ya emergency ata buku 5.

Mwanzo.
Unatoka Dar au Pwani na kwenda Moro kwa Bus, na ukifika Moro Msamvu unachukua bajaji hadi town then boda hadi kwa Mkuu wa Mkoa hapo ndio hiking itapoanzia.

Kama utakua na private car, unaweza enda hadi pale kwa mkuu wa mkoa kuna walinzi wanaweza kukuangalizia gari hadi utakaposhuka.

Safari
Utaanza mdogo mdogo kupanda milima ya Uluguru utapishana na vijiji mbalimbali ambapo utaona na kujifunza shughuli mbalimbali wanazofanya sana sana za kilimo.

View attachment 2820174

Vitu utakavyofanya.
1. Kwanza hiking.
View attachment 2820166

2. Pili, Forest walking.
View attachment 2820167

3. Tatu, utaona water falls mbalimbali maarufu zaidi ikiwa Choma waterfalls ila sikwenda kwasababu ya usalama kipindi cha mvua. Hii ni ndogo.
View attachment 2820168

4. Nne, kama utataka camping kuna mahala Wanafanya camping unaweza lala msituni lakini tuassume hii ni day trip kwahiyo hii hatutaidiscuss sana.
View attachment 2820176

5, Tano utakaa mbali na makelele ya mji.
View attachment 2820169

6, Sita, utakutana na wakazi wa uko wengi ni wakulima na wako friendly sana.
View attachment 2820173
Mfano wa mashamba zaidi:
View attachment 2820180
7. Saba, unaweza kuogelea. Maji ya baridi sana.

8. Nane, utajifunza jinsi wanavyo sambaza maji (kama DAWASA) ila kwa gravity. Aisee.

9, Tisa uta enjoy sana kama mtu wa nature.

View attachment 2820170
View attachment 2820181
Gharama.
Safari ya Dar to Moro ni Elfu 10 kwenda na 10 kurudi jumla 20.

Bodaboda na bajaji kutoka Msamvu to Town haizidi elfu 5 jumla.

Kula na snacks itategemea na tumbo lako tuassume elfu 10.

Jumla kuu 35 elfu.

Muda:
Ukifika kwa mkuu wa Mkoa saa 4 Tegemea kuspend kama masaa 6-8 kuanzia kupanda hadi kushuka. Kutegemea speed yako na jinsi utakavopenda kuzunguka.

Vitu vya kunote:
Chukua kopo la maji, yakiisha utayakuta uko juu ya mtoni.
Mkiwa wawili poa zaidi kupeana company ila ata solo unaweza.
Mtandao sio wa kuutegemea sana.
Msimu wa mvua hautabiriki dakika yoyote inamwagika.

View attachment 2820178
View attachment 2820172
Njia zinateleza sana, kuanguka muda wowote.
View attachment 2820171
View attachment 2820177
Hitimisho.
Hiking na nature sio ya kila mtu ila siku ukitaka kujaribu, jaribu.

Wakazi wa Moro wanaweza ongezea baadhi ya vitu nilivyosahau.

Pamoja.
Hongera sana mkuu. kuna siku nilenda hapo nikiwa na babe wangu. tulitoka mjini moro kwa taxi, ilipoishia tukapanda boda, mpaka kwenye maporomoko fulani hivi
Katika ku enjoy hapo kulikuwa na kundi la watu wamekuja kushangaa sisi. Bwanaeeeh ,dogo mmoja akajirusha kwenye maji, akawa hatokezi juu tena. alipopatikana akawa amekata moto, haonyeshi dalili za kupumua.
Shughuli ilikuwa kumtoa huko mlimani na kumfikisha town ili apate msaada
Baadae nasikia alikata moto. ni pazuri ila kupata msaada ndo changamoto
 
Safi sana chief umenikumbusha mwaka 2014 nilipanda huko na group la majamaa ,mabonge yenye vitambi hayakutoboa tuliyaacha katikati huko juu Kuna campsite Moja wanahuduma poa sana tulinunua mbuzi na kuku wakutosha tukaacha mabonge yasimamie nyama choma na supu tukishuka kileleni tuishi vizuri na gambe kiufupi Mzee wakaz umeelezea vizuri sana uzoefu wako
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni experience nzuri sana ila usiombe kukata moto, sisi tulipanda milima ya Udzungwa kule Sanje waterfalls kuna top na bottom, unachagua uende wapi

Yani ile tumefika tu top, nilijitupa chali huku nahema juu juu nikasema sirudii tena, Sasa hivi mlima pekee ninaoutamani ni Kilimanjaro tu mingine sitaki kuisikia
Aaaah ile siku sitakaa niisahau maana nilikurupuka tu baada ya kupata kampani na by then sikuwa na mazoezi yoyote.
Shughuli kubwa ikawa kushuka sasa, miguu haitaki, nilitamani nikae chini nijiburuze🤣🤣🤣🤣

Kilimanjaro yenyewe nilishindwa🤣
Hebu tuanze kwanza na hii ya Morning site then tujipange kwa kilimanjaro baby.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni experience nzuri sana ila usiombe kukata moto, sisi tulipanda milima ya Udzungwa kule Sanje waterfalls kuna top na bottom, unachagua uende wapi

Yani ile tumefika tu top, nilijitupa chali huku nahema juu juu nikasema sirudii tena, Sasa hivi mlima pekee ninaoutamani ni Kilimanjaro tu mingine sitaki kuisikia
Uduzungwa naionaga imekaa shagalabagala haivutii kupanda eti🙆🙆🙆
 
Morning site kitaambo dah,, wakati tuko primary enz hizo tulitembea sana huko juu,, tulikuwa tunachokoza ile mimbwa ya kizungu alafu tunakimbia 🤣,, unarudi home shat jekundu 😂,,

Mwezi mtukufu tulikuwa tunashinda huko juu,, cheze maji lakini wapi swaum iko palepale 🥺,,

Sijafika pale kwa kilele mnarani,,,

Ila kwingine tayar,,

Safi mtoa mada wapeleke wakajionee
Dah ndio mitaa yenu nini? Kuzuri sana aisee kipindi cha mvua kuna hali ya hewa moja amazing.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni experience nzuri sana ila usiombe kukata moto, sisi tulipanda milima ya Udzungwa kule Sanje waterfalls kuna top na bottom, unachagua uende wapi

Yani ile tumefika tu top, nilijitupa chali huku nahema juu juu nikasema sirudii tena, Sasa hivi mlima pekee ninaoutamani ni Kilimanjaro tu mingine sitaki kuisikia
Hahaa.. Sanje unafikia wapi? Ruaha pale kwenye kiwanda cha Sukari au? Nataka nijaribu siku.
 
Hongera sana mkuu. kuna siku nilenda hapo nikiwa na babe wangu. tulitoka mjini moro kwa taxi, ilipoishia tukapanda boda, mpaka kwenye maporomoko fulani hivi
Katika ku enjoy hapo kulikuwa na kundi la watu wamekuja kushangaa sisi. Bwanaeeeh ,dogo mmoja akajirusha kwenye maji, akawa hatokezi juu tena. alipopatikana akawa amekata moto, haonyeshi dalili za kupumua.
Shughuli ilikuwa kumtoa huko mlimani na kumfikisha town ili apate msaada
Baadae nasikia alikata moto. ni pazuri ila kupata msaada ndo changamoto
Dah pole kwa familia ya dogo ila ndio maisha.
 
Back
Top Bottom