Morogoro Kusini, Wilaya masikini kuliko zote Tanzania

Morogoro Kusini, Wilaya masikini kuliko zote Tanzania

Almost miaka 20 wanashindwa kujenga ofisi pale Mtamba japo wasogeze huduma karibu na wananchi?
Nakumbuka tangu miaka ya 90 tulikuwa tunasubiri Lori la Matombo Sec ili tupate lift maana kila mwezi lazima waende mjini kuzifuata ofisi
 
Nilikuwa kibungo kitongoji cha Mwalazi kwenye mgodi wa Wasrilanka asee waluguru wa kule na elimu bado sana. Yani kuanzia wazazi hadi walimu na wanafunzi wao wanaenda mto ruvu kuchimba dhahabu, vinyumba kama mabanda ya bata, wao na pombe.
 
Nilikuwa kibungo kitongoji cha Mwalazi kwenye mgodi wa Wasrilanka asee waluguru wa kule na elimu bado sana. Yani kuanzia wazazi hadi walimu na wanafunzi wao wanaenda mto ruvu kuchimba dhahabu, vinyumba kama mabanda ya bata, wao na pombe.
Ukitaka kujua umasikini upo Tanzania sogelea eneo hilo
 
Mabadiliko yanakuja

Kwa mbunge huyo huyo wa ccm!? Kulikuwa na mbunge mmoja wa ccm alishapita alikuwa anaitwa Hamza Mwenegoha alishawahi kuwa naibu waziri wa ujenzi kwa miaka saba lakini jimbo lake wala wilaya nzima hakuna lami.
Huyu mbunge wa sasa.alikuwa katibu wa rais alifanya nini wakati anaitumikia Ikulu ya Tanzania kabla hajawa mbunge
 
Heko kamanda kwa kuliona hili. Yaani uliyoyaona Morogoro kusini ni afadhali kwa kulinganisha na Bukoba Vijijini. CV ya Morogoro kusini ndo hiyo hiyo kwa Bukoba vijijini jimbo lenye kata 29 na ccm imekuwepo tangu enzi mpaka leo. Hakuna hospitali, shule ndo hivyo tena, barabara kama ulivyosema kwa morogoro. Ofisi zake ziko manispaa ya Bukoba. ila kilichoko huko ni gereza la Rwamulumba na ccm. Adios
 
Cha ajabu wilaya kama hizi huwa ndizo ngome kuu ya CCM.
 
Heko kamanda kwa kuliona hili. Yaani uliyoyaona Morogoro kusini ni afadhali kwa kulinganisha na Bukoba Vijijini. CV ya Morogoro kusini ndo hiyo hiyo kwa Bukoba vijijini jimbo lenye kata 29 na ccm imekuwepo tangu enzi mpaka leo. Hakuna hospitali, shule ndo hivyo tena, barabara kama ulivyosema kwa morogoro. Ofisi zake ziko manispaa ya Bukoba. ila kilichoko huko ni gereza la Rwamulumba na ccm. Adios

Afadhal nyinyi mmewekewa gereza huku hata hilo gereza hakuna mkuu
 
mkuu soma alichoandika mleta mada hapa chini halau angalia nilichojibu then jipime kati yangu na wewe nani BWE'GE.
(UONEVU:
wananchi wanaonewa kwa kulipishwa michango na faini zisizo na tija. Kuna mpango wa kila kata kuchangia shilingi elfu moja kulipia vyanzo vya maji mpango huu unaratibiwa na shirika na CARE INTERNATIONAL. Wakati mito Mungu mwenyewe ndiyo kaiumba na ipo tu siku zote toka utotoni kwa bibi na babu zetu na tulikuwa tunatumia bure.
Mbunge ni wa CCM.)



Shida ya sisi watanzania ni kujifanya kujua kila kitu. Hali iliyopo huku ni kama kila kaya na si kata kulipia shilingi 1000 kwa huduma ya mto au kijito kilichopo kwa kampuni hiyo tajwa hapo wakati utunzaji wenyewe unafanywa na wananchi wenyewe kwa hiyo hilo ni dili la kupiga hela za wanyonge. Usikurupuke kutukana watu pasi kujua mantiki ya jambo ubabe kamletee mkeo na watoto wako hii jf home of great thinkers bwe.ge we.
 
mkuu soma alichoandika mleta mada hapa chini halau angalia nilichojibu then jipime kati yangu na wewe nani BWE'GE.
(UONEVU:
wananchi wanaonewa kwa kulipishwa michango na faini zisizo na tija. Kuna mpango wa kila kata kuchangia shilingi elfu moja kulipia vyanzo vya maji mpango huu unaratibiwa na shirika na CARE INTERNATIONAL. Wakati mito Mungu mwenyewe ndiyo kaiumba na ipo tu siku zote toka utotoni kwa bibi na babu zetu na tulikuwa tunatumia bure.
Mbunge ni wa CCM.)

Siyo kosa lako hata jina lako linakusuta
 
mkuu soma alichoandika mleta mada hapa chini halau angalia nilichojibu then jipime kati yangu na wewe nani BWE'GE.
(UONEVU:
wananchi wanaonewa kwa kulipishwa michango na faini zisizo na tija. Kuna mpango wa kila kata kuchangia shilingi elfu moja kulipia vyanzo vya maji mpango huu unaratibiwa na shirika na CARE INTERNATIONAL. Wakati mito Mungu mwenyewe ndiyo kaiumba na ipo tu siku zote toka utotoni kwa bibi na babu zetu na tulikuwa tunatumia bure.
Mbunge ni wa CCM.)

Na wewe umezidi kukejeli wenzako acha utukanwe maana hakuna namna
 
Takwimu za NEC zinaonesha hilo pia ndio jimbo pekee lililoharibu kura NYINGI kuliko majimbo yote Tanzania.

Kwa kuongezea tu ni kwamba jimbo liliharibu kura chache kushinda yote ni kilindi Tanga.
Na bumbuli kwa makamba mkuu
 
Jamani mwambieni abood awasaidie si ana viji sent yule kidogo
 
Kaka yawezekana ya huko morogoro kusini ni 9 kumi nenda wilaya ya Ileje mkoani mbeya kamanda. Yaani nadhani ni mojawapo ya wilaya fukara kabisa hapa nchini.

Kule huwaambii chochote kuhusu ccm yaani 2010 kulikua na diwani mmoja tu wa CHADEMA kata ya chitete Hali kadhalika hata mwaka huu ni mmoja tu toka kata hiyo hiyo. Kuna vijiji ukitaka kwenda toka mbeya mjini unatumia cku 2 kutokana na miundo mbinu mibovu.

Mfano ni kule ikinga na vijiji kama bwenda. Umeme ndo usiseme kati ya vijiji zaidi ya 80 vyenye umeme si zaidi ya vitano. Vijiji kama Itale, shuba, katengere, bufura, Ilanga nk ccm imeota mizizi lakini umasikini ni wa kutisha. Wilaya nzima sidhani kama Kuna hata mwenye PhD kule. Ccm kutoka madarakani kule ni ndoto za rinacha

Ulichoandika ni ukweli mtupu. In fact nilikuwa sijapata kufika Ileje mjini, nilifika mnamo 2013 Desemba. Ile si wilaya, ila ni kijiji kikubwa. Watasubiri sana ili kupata maendeleo. Kutoka pale Mpemba Mbozi kwenda Ileje wilayani ni njia fupi sana, ila haijawekwa lami, mpaka nilishangaa. Lakini huko ndiko kwenye wanazi wa chama tawala ile mbaya!
 
Nmefanya kazi kituo cha afya mvuha, kisha dutumi. Ingawa kwa sasa nimehama wilaya hii kikazi ingawa bado naishi huku na familia yangu. Huku hali ni mbaya sana janani

Nakubaliana na wewe ndugu, barabara zenu ni mbaya sana. Nimefika Mvuha mara ya kwanza mwaka huu, kwa kweli malalamiko yako ni genuine kabisa. Kesho pia naenda kijiji cha Kongwa, kule karibu na mbuga ya Selous, huko tunapita kwenye miti tu ili kufika kijijini, kwa sababu hakuna barabaya ya gari ya kueleweka ili kufika kijijini Kongwa. Kuna mradi nautekeleza kule, wa kuwapekelea umeme watu wa kijiji cha Kongwa. Ilituwia vigumu sana kupeleka mitambo wakati wa mvua, kwa kuwa njia hazipitiki kirahisi kabisa. Poleni sana
 
Back
Top Bottom