Morogoro ni Mkoa mzuri namba Moja wa kuishi Tanzania

Morogoro ni Mkoa mzuri namba Moja wa kuishi Tanzania

Kwema Wakuu!

Licha ya Tanzania kuwa na mikoa mingi lakini Mkoa wa Morogoro ndio mkoa namba moja kwa uzuri kwa kuishi. Nitaeleza sababu kama ifuatavyo;

1. Tabia ya nchi na Hali ya Hewa
Mkoa wa Morogoro tabia yake ya nchi na hali ya hewa ni nzuri. Hakuna joto sana wala hakuna baridi sana.

Jua lake ni la kawaida ingawaje nyakati za kiangazi huongezeka kuwa kali lakini ni afadhali zaidi kuliko jua la mikoa mingine.

Kuna msimu miwili ya mvua, masika na kiangazi ambapo hutoa fursa kwa kilimo kuvuna mara mbili kwa mwaka.

Tofauti na baadhi ya mikoa ambayo wanavuna mara moja kutokana na Baridi Kali au Ukame (joto kali).

Vumbi lake sio kali ukilinganisha na baadhi ya mikoa mingine kama Dodoma, Singida, Mbeya, Iringa kipindi cha kipupwe hasa maeneo ya Mufindi.

Maeneo yenye baridi ni milimani huko Mgeta Matombo, Kibati kwenye kilele cha Mlima Muscat huko Turiani.

Tabia ya nchi na hali ya hewa inaufanya mkoa huu kuwa moja ya mikoa tegemezi kwa uzalishaji wa chakula hasa maeneo ya Ifakara, Kilosa, Mvomero na Bonde la Mlali.

2. USO wa nchi(landscape) na Ardhi yenye Rutuba.
Morogoro ni moja Kati ya Mkoa wenye uzuri wa tambarare nzuri na safu ya milima Uluguru.

Tambarare yenye udongo mzuri wenye rutuba ambao unasaidia zaidi kwenye kilimo.
Morogoro hakuna tatizo la chakula na ndio Mkoa unaolisha Mikoa inayoizunguka ikiwemo Dodoma, na Dar es Salaam.

3. Connectivity (miundombinu ya barabara)
Morogoro ndio Mkoa pekee ambao magari yote yanayoenda nchi za nje yanapitia hapo, yakitokea Dar kwenda Zambia, Malawi, South Africa, Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na wakati mwingine Kenya.

Ndio mkoa pekee ambao ukitoka Mkoani huwezi kulala njiani, iwe unatoka Bukoba, Musoma, Mtwara, Songea, Rukwa au Kigoma. Ukienda Morogoro lazima ufike siku hiyohiyo.

Hii ni fursa ya kibiashara iwe kwa usafirishaji wa mizigo inayoingia au kutoka.

Morogoro ndio mkoa pekee ambao huwezi kukosa usafiri muda wowote kwenda Dar es Salaam, kwani usiku kuna mabasi yatokayo mikoa ya mbali ambayo hufika usiku wa saa tano mpaka saa saba.

Pia kuna IT na malori.

Reli ya Tazara, reli ya Kati na sasa SGR zote zimepita hapo Morogoro.

Pia Morogoro ndio Mkoa pekee uliokatikati ya majiji mawili makubwa ambayo ni Dar na Dodoma. Hii kwa watu wenye akili za mbele wanaweza jua fursa hasa kwa nyakati zijazo.

Morogoro ni mkoa wa pili baada ya Dar ambao hakuna basi kutoka mkoa wowote lisiloenda Morogoro au kupita huko.

Hii ni tofauti na mikoa mingine mfano, hakuna gari kutoka Mtwara to Mwanza,
Sumbawanga to Mwanza, hii ni tofauti na mikoa mingi.

4. Unafuu wa Maisha.
Morogoro ni moja ya Mkoa wenye unafuu mkubwa wa maisha kutokana na kuwa na chakula cha kutosha, matunda ya Aina yote.
Vyumba na nyumba za kupanga Morogoro ni nafuu na ni nzuri.

Vipo vyumba kuanzia Tsh 25 vyenye umeme na nyumba za laki na hamsini

Usafiri wa kwenda mjini sio shida na nafuu.
Viwanja na ujenzi wa nyumba ni gharama nafuu.

5. Huduma za kijamii.
Mkoa WA Morogoro unajitahidi Kwa Huduma za kijamii Kama Hospitali, shule, Huduma za kibenki, vyuo vikuu, veta na vyuo vya Kati, Makanisa na Misikiti ya kuabudia ipo.

Huduma ya maji ipo ingawaje Maeneo ya Kihonda na Mkundi bado kuna uhaba kutokana na miundombinu ya maji.

Vituo vya Mafuta ya magari,
Viwanda ambavyo Vijana wengi wamepatiwa Ajira.

Vituo vya kisasa vya Ma Mabasi na abiria, Msamvu Bus Terminal ni moja Kati ya vituo vya mabasi vikubwa Kwa hapa Tanzania baada ya kile cha Magufuli Bus Terminal cha Dar.

Viwanja vya mpira, Kama ulikuwa hujui Kwa Tanzania Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kutoa wachezaji wengi WA mpira wenye kipaji na wanaocheza katika timu kubwa hapa nchini.

Masoko ya nguo na vyakula Morogoro sio tatizo.

Vituo vya redio na televisheni sio ajabu ndio Mkoa unaoshika nafasi ya pili baada ya Dar es salaam.

6. Vivutio
Morogoro ni Mkoa namba mbili Kwa vivutio vya mbuga na hifadhi baada ya Mkoa wa Arusha, Mbuga ya Mikumi na Hifadhi kubwa zaidi Duniani ya Selous inapatikana Morogoro.
Hui ni tofauti na mikoa mingi ambayo haikubahatika kuwa hata na mbuga au hifadhi ya wanyama hata moja, achilia mbali kuwa kubwa.

7. Uwepo wa mito Mingi.
Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kuwa na vyanzo vingi vya maji hasa Mito. Hii ni tofauti na mikoa mingi Tanzania.

8. Ukarimu.
Mkoa WA Morogoro unawatu wenye ukarimu na ndio maana unaweza kumiliki Ardhi Kwa kiwango chochote unachotaka tofauti na baadhi ya mikoa mingi hapa nchi.
Sio ajabu Mkoa wa Morogoro ukakutaba na makabila karibu yote, hasa Waha, Wasukuma, Wachaga, Wapare, Wangoni, wamasai, Wahehe wabena na wakinga, Wanyakyusa, Wanyamwezi, Wabaya na makabila mengine mengi.

Mkoa wa Morogoro ndi9 namba mbili kwa kuwa na wageni wengi WA makabila mengine baada ya Mkoa wa Dar.

Hii ni tofauti na mikoa mingi hapa nchini ambayo mchanganyiko na makabila mengine utakuta ni mdogo.

Kwa kijana anayetaka kuanza maisha na hajui ni Mkoa gani akaanzie basi Morogoro ni moja ya mikoa ambayo unaweza ukaiweka kwenye akili yako.

Karibuni MOROGORO.


Asante sana mkuu kwa Tarifa hii.
umetutajia maeneo mawili yenye changamoto ya kaji katika mkoa wa Morogoro ambayo ni kihonda na mkundi .
Swali langu kwa uzoefu wako ni maeneo gani ambapo naweza pata nyumba ya kupanga kwa bei rafiki (bei nzuri) na kuna uhakika wa huduma muhimu haswa maji na shule nzuri (za msingi za serikali) kwaajili ya elimu kwa vijana pia uhakika wa usafiri wa uma kufika katikati ya mji.

Asante.
 
Asante sana mkuu kwa Tarifa hii.
umetutajia maeneo mawili yenye changamoto ya kaji katika mkoa wa Morogoro ambayo ni kihonda na mkundi .
Swali langu kwa uzoefu wako ni maeneo gani ambapo naweza pata nyumba ya kupanga kwa bei rafiki (bei nzuri) na kuna uhakika wa huduma muhimu haswa maji na shule nzuri (za msingi za serikali) kwaajili ya elimu kwa vijana pia uhakika wa usafiri wa uma kufika katikati ya mji.

Asante.
Bigwa Kila kitu safi changamoto usafiri tu na tope wakati wa mvua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikifika miaka 60 mda utaobakia nitaenda kumalizia Morogoro au Bukoba-Kagera.
 
Huu mkoa tumepambana sana
Kweli fursa ziko vijijini huko porini

Ova
 
Kwema Wakuu!

Licha ya Tanzania kuwa na mikoa mingi lakini Mkoa wa Morogoro ndio mkoa namba moja kwa uzuri kwa kuishi. Nitaeleza sababu kama ifuatavyo;

1. Tabia ya nchi na Hali ya Hewa
Mkoa wa Morogoro tabia yake ya nchi na hali ya hewa ni nzuri. Hakuna joto sana wala hakuna baridi sana.

Jua lake ni la kawaida ingawaje nyakati za kiangazi huongezeka kuwa kali lakini ni afadhali zaidi kuliko jua la mikoa mingine.

Kuna msimu miwili ya mvua, masika na kiangazi ambapo hutoa fursa kwa kilimo kuvuna mara mbili kwa mwaka.

Tofauti na baadhi ya mikoa ambayo wanavuna mara moja kutokana na Baridi Kali au Ukame (joto kali).

Vumbi lake sio kali ukilinganisha na baadhi ya mikoa mingine kama Dodoma, Singida, Mbeya, Iringa kipindi cha kipupwe hasa maeneo ya Mufindi.

Maeneo yenye baridi ni milimani huko Mgeta Matombo, Kibati kwenye kilele cha Mlima Muscat huko Turiani.

Tabia ya nchi na hali ya hewa inaufanya mkoa huu kuwa moja ya mikoa tegemezi kwa uzalishaji wa chakula hasa maeneo ya Ifakara, Kilosa, Mvomero na Bonde la Mlali.

2. USO wa nchi(landscape) na Ardhi yenye Rutuba.
Morogoro ni moja Kati ya Mkoa wenye uzuri wa tambarare nzuri na safu ya milima Uluguru.

Tambarare yenye udongo mzuri wenye rutuba ambao unasaidia zaidi kwenye kilimo.
Morogoro hakuna tatizo la chakula na ndio Mkoa unaolisha Mikoa inayoizunguka ikiwemo Dodoma, na Dar es Salaam.

3. Connectivity (miundombinu ya barabara)
Morogoro ndio Mkoa pekee ambao magari yote yanayoenda nchi za nje yanapitia hapo, yakitokea Dar kwenda Zambia, Malawi, South Africa, Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na wakati mwingine Kenya.

Ndio mkoa pekee ambao ukitoka Mkoani huwezi kulala njiani, iwe unatoka Bukoba, Musoma, Mtwara, Songea, Rukwa au Kigoma. Ukienda Morogoro lazima ufike siku hiyohiyo.

Hii ni fursa ya kibiashara iwe kwa usafirishaji wa mizigo inayoingia au kutoka.

Morogoro ndio mkoa pekee ambao huwezi kukosa usafiri muda wowote kwenda Dar es Salaam, kwani usiku kuna mabasi yatokayo mikoa ya mbali ambayo hufika usiku wa saa tano mpaka saa saba.

Pia kuna IT na malori.

Reli ya Tazara, reli ya Kati na sasa SGR zote zimepita hapo Morogoro.

Pia Morogoro ndio Mkoa pekee uliokatikati ya majiji mawili makubwa ambayo ni Dar na Dodoma. Hii kwa watu wenye akili za mbele wanaweza jua fursa hasa kwa nyakati zijazo.

Morogoro ni mkoa wa pili baada ya Dar ambao hakuna basi kutoka mkoa wowote lisiloenda Morogoro au kupita huko.

Hii ni tofauti na mikoa mingine mfano, hakuna gari kutoka Mtwara to Mwanza,
Sumbawanga to Mwanza, hii ni tofauti na mikoa mingi.

4. Unafuu wa Maisha.
Morogoro ni moja ya Mkoa wenye unafuu mkubwa wa maisha kutokana na kuwa na chakula cha kutosha, matunda ya Aina yote.
Vyumba na nyumba za kupanga Morogoro ni nafuu na ni nzuri.

Vipo vyumba kuanzia Tsh 25 vyenye umeme na nyumba za laki na hamsini

Usafiri wa kwenda mjini sio shida na nafuu.
Viwanja na ujenzi wa nyumba ni gharama nafuu.

5. Huduma za kijamii.
Mkoa WA Morogoro unajitahidi Kwa Huduma za kijamii Kama Hospitali, shule, Huduma za kibenki, vyuo vikuu, veta na vyuo vya Kati, Makanisa na Misikiti ya kuabudia ipo.

Huduma ya maji ipo ingawaje Maeneo ya Kihonda na Mkundi bado kuna uhaba kutokana na miundombinu ya maji.

Vituo vya Mafuta ya magari,
Viwanda ambavyo Vijana wengi wamepatiwa Ajira.

Vituo vya kisasa vya Ma Mabasi na abiria, Msamvu Bus Terminal ni moja Kati ya vituo vya mabasi vikubwa Kwa hapa Tanzania baada ya kile cha Magufuli Bus Terminal cha Dar.

Viwanja vya mpira, Kama ulikuwa hujui Kwa Tanzania Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kutoa wachezaji wengi WA mpira wenye kipaji na wanaocheza katika timu kubwa hapa nchini.

Masoko ya nguo na vyakula Morogoro sio tatizo.

Vituo vya redio na televisheni sio ajabu ndio Mkoa unaoshika nafasi ya pili baada ya Dar es salaam.

6. Vivutio
Morogoro ni Mkoa namba mbili Kwa vivutio vya mbuga na hifadhi baada ya Mkoa wa Arusha, Mbuga ya Mikumi na Hifadhi kubwa zaidi Duniani ya Selous inapatikana Morogoro.
Hui ni tofauti na mikoa mingi ambayo haikubahatika kuwa hata na mbuga au hifadhi ya wanyama hata moja, achilia mbali kuwa kubwa.

7. Uwepo wa mito Mingi.
Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kuwa na vyanzo vingi vya maji hasa Mito. Hii ni tofauti na mikoa mingi Tanzania.

8. Ukarimu.
Mkoa WA Morogoro unawatu wenye ukarimu na ndio maana unaweza kumiliki Ardhi Kwa kiwango chochote unachotaka tofauti na baadhi ya mikoa mingi hapa nchi.
Sio ajabu Mkoa wa Morogoro ukakutaba na makabila karibu yote, hasa Waha, Wasukuma, Wachaga, Wapare, Wangoni, wamasai, Wahehe wabena na wakinga, Wanyakyusa, Wanyamwezi, Wabaya na makabila mengine mengi.

Mkoa wa Morogoro ndi9 namba mbili kwa kuwa na wageni wengi WA makabila mengine baada ya Mkoa wa Dar.

Hii ni tofauti na mikoa mingi hapa nchini ambayo mchanganyiko na makabila mengine utakuta ni mdogo.

Kwa kijana anayetaka kuanza maisha na hajui ni Mkoa gani akaanzie basi Morogoro ni moja ya mikoa ambayo unaweza ukaiweka kwenye akili yako.

Karibuni MOROGORO.
Safi sana mkuu nilikuwa nataka kujua bei za vyumba na frem kwa morogoro mjini na kuzunguka mitaa yake
 
Kwema Wakuu!

Licha ya Tanzania kuwa na mikoa mingi lakini Mkoa wa Morogoro ndio mkoa namba moja kwa uzuri kwa kuishi. Nitaeleza sababu kama ifuatavyo;

1. Tabia ya nchi na Hali ya Hewa
Mkoa wa Morogoro tabia yake ya nchi na hali ya hewa ni nzuri. Hakuna joto sana wala hakuna baridi sana.

Jua lake ni la kawaida ingawaje nyakati za kiangazi huongezeka kuwa kali lakini ni afadhali zaidi kuliko jua la mikoa mingine.

Kuna msimu miwili ya mvua, masika na kiangazi ambapo hutoa fursa kwa kilimo kuvuna mara mbili kwa mwaka.

Tofauti na baadhi ya mikoa ambayo wanavuna mara moja kutokana na Baridi Kali au Ukame (joto kali).

Vumbi lake sio kali ukilinganisha na baadhi ya mikoa mingine kama Dodoma, Singida, Mbeya, Iringa kipindi cha kipupwe hasa maeneo ya Mufindi.

Maeneo yenye baridi ni milimani huko Mgeta Matombo, Kibati kwenye kilele cha Mlima Muscat huko Turiani.

Tabia ya nchi na hali ya hewa inaufanya mkoa huu kuwa moja ya mikoa tegemezi kwa uzalishaji wa chakula hasa maeneo ya Ifakara, Kilosa, Mvomero na Bonde la Mlali.

2. USO wa nchi(landscape) na Ardhi yenye Rutuba.
Morogoro ni moja Kati ya Mkoa wenye uzuri wa tambarare nzuri na safu ya milima Uluguru.

Tambarare yenye udongo mzuri wenye rutuba ambao unasaidia zaidi kwenye kilimo.
Morogoro hakuna tatizo la chakula na ndio Mkoa unaolisha Mikoa inayoizunguka ikiwemo Dodoma, na Dar es Salaam.

3. Connectivity (miundombinu ya barabara)
Morogoro ndio Mkoa pekee ambao magari yote yanayoenda nchi za nje yanapitia hapo, yakitokea Dar kwenda Zambia, Malawi, South Africa, Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na wakati mwingine Kenya.

Ndio mkoa pekee ambao ukitoka Mkoani huwezi kulala njiani, iwe unatoka Bukoba, Musoma, Mtwara, Songea, Rukwa au Kigoma. Ukienda Morogoro lazima ufike siku hiyohiyo.

Hii ni fursa ya kibiashara iwe kwa usafirishaji wa mizigo inayoingia au kutoka.

Morogoro ndio mkoa pekee ambao huwezi kukosa usafiri muda wowote kwenda Dar es Salaam, kwani usiku kuna mabasi yatokayo mikoa ya mbali ambayo hufika usiku wa saa tano mpaka saa saba.

Pia kuna IT na malori.

Reli ya Tazara, reli ya Kati na sasa SGR zote zimepita hapo Morogoro.

Pia Morogoro ndio Mkoa pekee uliokatikati ya majiji mawili makubwa ambayo ni Dar na Dodoma. Hii kwa watu wenye akili za mbele wanaweza jua fursa hasa kwa nyakati zijazo.

Morogoro ni mkoa wa pili baada ya Dar ambao hakuna basi kutoka mkoa wowote lisiloenda Morogoro au kupita huko.

Hii ni tofauti na mikoa mingine mfano, hakuna gari kutoka Mtwara to Mwanza,
Sumbawanga to Mwanza, hii ni tofauti na mikoa mingi.

4. Unafuu wa Maisha.
Morogoro ni moja ya Mkoa wenye unafuu mkubwa wa maisha kutokana na kuwa na chakula cha kutosha, matunda ya Aina yote.
Vyumba na nyumba za kupanga Morogoro ni nafuu na ni nzuri.

Vipo vyumba kuanzia Tsh 25 vyenye umeme na nyumba za laki na hamsini

Usafiri wa kwenda mjini sio shida na nafuu.
Viwanja na ujenzi wa nyumba ni gharama nafuu.

5. Huduma za kijamii.
Mkoa WA Morogoro unajitahidi Kwa Huduma za kijamii Kama Hospitali, shule, Huduma za kibenki, vyuo vikuu, veta na vyuo vya Kati, Makanisa na Misikiti ya kuabudia ipo.

Huduma ya maji ipo ingawaje Maeneo ya Kihonda na Mkundi bado kuna uhaba kutokana na miundombinu ya maji.

Vituo vya Mafuta ya magari,
Viwanda ambavyo Vijana wengi wamepatiwa Ajira.

Vituo vya kisasa vya Ma Mabasi na abiria, Msamvu Bus Terminal ni moja Kati ya vituo vya mabasi vikubwa Kwa hapa Tanzania baada ya kile cha Magufuli Bus Terminal cha Dar.

Viwanja vya mpira, Kama ulikuwa hujui Kwa Tanzania Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kutoa wachezaji wengi WA mpira wenye kipaji na wanaocheza katika timu kubwa hapa nchini.

Masoko ya nguo na vyakula Morogoro sio tatizo.

Vituo vya redio na televisheni sio ajabu ndio Mkoa unaoshika nafasi ya pili baada ya Dar es salaam.

6. Vivutio
Morogoro ni Mkoa namba mbili Kwa vivutio vya mbuga na hifadhi baada ya Mkoa wa Arusha, Mbuga ya Mikumi na Hifadhi kubwa zaidi Duniani ya Selous inapatikana Morogoro.
Hui ni tofauti na mikoa mingi ambayo haikubahatika kuwa hata na mbuga au hifadhi ya wanyama hata moja, achilia mbali kuwa kubwa.

7. Uwepo wa mito Mingi.
Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kuwa na vyanzo vingi vya maji hasa Mito. Hii ni tofauti na mikoa mingi Tanzania.

8. Ukarimu.
Mkoa WA Morogoro unawatu wenye ukarimu na ndio maana unaweza kumiliki Ardhi Kwa kiwango chochote unachotaka tofauti na baadhi ya mikoa mingi hapa nchi.
Sio ajabu Mkoa wa Morogoro ukakutaba na makabila karibu yote, hasa Waha, Wasukuma, Wachaga, Wapare, Wangoni, wamasai, Wahehe wabena na wakinga, Wanyakyusa, Wanyamwezi, Wabaya na makabila mengine mengi.

Mkoa wa Morogoro ndi9 namba mbili kwa kuwa na wageni wengi WA makabila mengine baada ya Mkoa wa Dar.

Hii ni tofauti na mikoa mingi hapa nchini ambayo mchanganyiko na makabila mengine utakuta ni mdogo.

Kwa kijana anayetaka kuanza maisha na hajui ni Mkoa gani akaanzie basi Morogoro ni moja ya mikoa ambayo unaweza ukaiweka kwenye akili yako.

Karibuni MOROGORO.
Morogoro ndiyo mkoa pekee ambapo mtu yoyote ambaye hakai Dar akifika atavutiwa kukaa pale.

Morogoro ndiyo mkoa pekee wenye wapiga debe wenye customer care kubwa kuliko ofisi yoyote nchini.

Ukishuka kwenye gari unapokelewa kwa salamu, unabebewa begi, unasindikizwa mpaka lodge na unapelekwa sehemu ya chakula, asubuhi tena anakufuata anakubebea kila kitu tena mpaka kwenye gari anakuonyesha siti kisha anakutakia safari njema. Wanashangaza sana
 
Wilaya gani ya Morogoro unapendekeza kwa mgeni kuanzia maisha kati ya Ifakara,Kilosa,Kilombero na nyinginezo yenye unafuu wa.shida ya maji

Wilaya karibu zote Moro zina fursa tu zakutosha anzia ifakara na kuendelea
 
Wilaya karibu zote Moro zina fursa tu zakutosha anzia ifakara na kuendelea
Nimeona wengi wanasema kuna changamoto ya maji,hivyo najaribu kuangalia yenye unafuu wa upatikanaji maji.....binafsi nilipenda nianze kilosa au ifakara japo sijawahi fika
 
Sijawahi kupenda kuishi miji isiyo kuwa na bahari au ziwa..napenda sana beaches na samaki wale fresh.

Kuhusu moro wanamiwa mitamu sana na milaini huwa nikipita msamvu lazima nichukue yakutosha kula na kupelekea familia.

Uzuri wa moro ni upatikanaji wa chakula kwa wingi.

Makazi huniondoi dsm na kanda ya ziwa especially mwanza na bkb.

#MaendeleoHayanaChama
 
Sijawahi kupenda kuishi miji isiyo kuwa na bahari au ziwa..napenda sana beaches na samaki wale fresh.

Kuhusu moro wanamiwa mitamu sana na milaini huwa nikipita msamvu lazima nichukue yakutosha kula na kupelekea familia.

Uzuri wa moro ni upatikanaji wa chakula kwa wingi.

Makazi huniondoi dsm na kanda ya ziwa especially mwanza na bkb.

#MaendeleoHayanaChama

Karibu Sana MKUU.
Mji kasoro bahari
 
Nikiwa kama Mwana Moro, nasema asante sana kwa mkoa wetu kupata nafasi ya kuzungumziwa JF...

Karibu Moro......... Wenyewe tunakula ugali na nguruka, na kachumbari. Siku imepitaaaaaaaaaaa
 
Nimekaa sana hapo sema moro imebadilika sana watani zangu mnachoma sana moto milimani ndo maana panaharibika ..moro ilikua moro kweli asubuhi ukungu km mko rusia mlima kuja kuuona vizuri ni mchana maana ukungu unaifunika milima harafu ukionekana maji yanatililika milimani dah....one of the best enjoyment hua haitoki kichwani ..kwa swala la misosi hapo hela yako tu utakula kuanzia matunda,samaki sema sio wengi km wanavyooagiza nguruka,nyama mpaka yule haram kwa moro utakimbia mwenyewe .
 
Back
Top Bottom