Movie ya EONII hakuna kitu

Movie ya EONII hakuna kitu

Kwani hao watu wa huko mbele walipofanya makosa hawakukosolewa?
Watengenezaji wa Bongo movie ni nani haswa mpaka kazi zao zisikosolewe?Kukosoa kitu kibovu leo hii imekuwa kosa?
Kwa hiyo unataka tusifie vitu vibovu? Eti kisa wameanza juzijuzi?
Aliyesema nataka walingane na hao waliopo kwenye industry miaka 100 ni nani?Mbona hata wao kazi zao nyingi tu zinakosolewa? Kwa nini za Bongo zisikosolewe?
Au kisa ni muvi ya nyumbani ndio tusiikosoe? Kisa wametumia hela nyingi kuliko Bongo movie nyingine basi ndio tukae kimya hata wakitoa kitu kibovu?
Kitu usipokipenda usiseme? Kukosoa muvi mbovu ndio mnaita roho mbaya? Sasa mtu akiona kitu cha hovyo mnataka akae kimya au? Mnataka asitoe mawazo yake?

Hapa tunaongelea movie, hata haihusiani na uzalendo wala roho mbaya, bali ni maoni ya watu juu ya movie hiyo. Kama wewe ni mpenzi wa movie basi kuna movie mbovu kibao utakuwa umeziona na kwenye thread ya movie kule muvi ikiwa mbovu inapondwa bila kujali ni ya nchi gani. Ila huku kuponda movie mbaya ya Kibongo ndio mnaita roho mbaya na kukosa uzalendo.

Kama mashabiki wa Bongo movie wenyewe wataendelea ku-judge movie kwa kuzingatia hisia kuliko uhalisia basi Bongo movie haitaendelea kamwe. Endeleeni kusifia ushuzi
tabia ya kukatishana tamaa zipo kwenye damu za wabongo
 
JF kuna wajuaji kazi kukosoa tengenezeni yenu tuone mfano
Huhitaji kuwa mpishi kujua chakula hiki kiamu au si kitamu, huhitaji kuwa mwanamziki kujua huu muziki ni mzuri.
Mwisho wa siku masuala ya tupende vya kwetu huwa hayafanyi kazi watu wanapenda vitu vizuri. Ukitaka kujua watu ukitengeneza kitunkizuri cha ndani watanunua tu, ona watu wanavyopenda suti zinazotengenezwa local.
Sijaiona ila sikutegemea iwe woow, la msingi ni mwanzo baada ya hapo wataboresha zaidi na zaidi wakijifunza. Shida inakuwa zaidi kwenye story na script. Inawezekana ingekuwa simple sci-fiction story yenye script nzuri ingependeza zaidi
 
Huhitaji kuwa mpishi kujua chakula hiki kiamu au si kitamu, huhitaji kuwa mwanamziki kujua huu muziki ni mzuri.
Mwisho wa siku masuala ya tupende vya kwetu huwa hayafanyi kazi watu wanapenda vitu vizuri. Ukitaka kujua watu ukitengeneza kitunkizuri cha ndani watanunua tu, ona watu wanavyopenda suti zinazotengenezwa local.
Sijaiona ila sikutegemea iwe woow, la msingi ni mwanzo baada ya hapo wataboresha zaidi na zaidi wakijifunza. Shida inakuwa zaidi kwenye story na script. Inawezekana ingekuwa simple sci-fiction story yenye script nzuri ingependeza zaidi
We director Adam Juma. Serious? Huyuhuyu tunayemjua wa video za miaka ya 2000s. Wangemhusisha Seko Shamte au kutafuta co-directors kutoka nchi jirani hususani bondeni.
Tatizo sisi hatujawahi kuwa serious. Unapoamua kufanya kitu fanya kweli usijaribu.
 
Hivi wewe muvi unaangalia kweli [emoji848][emoji848]
Mimi sio mtu wa movie lakini kwa akili ya kawaida unategemea uangalie movie ya kibongo huku ukiwa na comparison na movie za Hollywood ? budget, technology, experience, skills and knowledge zina fanana? siwezi kwenda kuangalia mechi ya Yanga na Simba huku kichwani nikiwa na fikira za Real Madrid Vs Barcelona
 
Mimi sio mtu wa movie lakini kwa akili ya kawaida unategemea uangalie movie ya kibongo huku ukiwa na comparison na movie za Hollywood ? budget, technology, experience, skills and knowledge zina fanana? siwezi kwenda kuangalia mechi ya Yanga na Simba huku kichwani nikiwa na fikira za Real Madrid Vs Barcelona
Sasa nani amefanya comparison
Mleta mada anasema hiyo movie ni mbaya. Yani ni mbaya tu in general bila kulinganisha na Hollywood wala nini

Muvi ya EONII kama Eonii ndio inayolalamikiwa hapa, mleta mada kaangalia amesema Ile movie hakuna kitu.

Movie za Kibongo nyingi hata usipozilinganisha na Hollywood, zenyewe kama zenyewe tu hazina mvuto
 
Mimi sio mtu wa movie lakini kwa akili ya kawaida unategemea uangalie movie ya kibongo huku ukiwa na comparison na movie za Hollywood ? budget, technology, experience, skills and knowledge zina fanana? siwezi kwenda kuangalia mechi ya Yanga na Simba huku kichwani nikiwa na fikira za Real Madrid Vs Barcelona
Tatizo la hii movie ipo below standard, ni movie ambayo watoto wakiangalia watafurahi lakini mtu mzima huwezi kuangalia hiyo movie ukafurahia. Imagine hata waingizaji wamemezeshwa maneno na anayeangalia anajua kabisa. Movie inaatakiwa iwe na ladha hii haina ladha mana mboga haina chumvi, mafuta, nyanya, vitunguu. Yani harage limechemshwa halafu tumepewa tule.
 
Mwanzo mzuri....Azam juzi walikua wanauza juice leo wako kwenye film industry kama kina TBC na IPP wangeendeleza hivyi tungekua mbali sio kila siku movie location ni mjini na kijijini tu watu wakipiga story za mapenzi.
 
Una low budget halafu unatengeneza movie ya sci-fi lazima utoe boko

Bongo bado hatuna script-writers wazuri sishangai kuona visa katika hiyo movie havieleweki
Hapa ndio shida ilipo hatuna script writers. Takataka zote wanazoonyesha Dstv Itv nk ni mbovu kwasababu script ni mbaya.

Hata uwe na camera nzuri, set design nzuri nk. kama script ni mbaya na content yako itakuwa mbaya vile vile.

Angalau maigizio ya Itv ya zamani walijitahidi kuwa na script nzuri ila sasa hivi ni sifuri.
 
Back
Top Bottom