Mpaka leo hii sijui kwanini mchezaji wa mpira nchini Tanzania analipwa sh milioni 5 halafu mwalimu wa shule ya Msingi analipwa sh. Laki 3

Bro mchezaji analipwa na serikali? Au huko ulaya mwalimu analipwa kiasi gani na tiger woods mcheza golf ni kiasi gani?
 
Mkuu niamini mimi. Hii michezo mingine ni kama njia ya kuwapumbaza watu ili wasifanye mambo ya msingi ya kimaisha. Nakuhakikishia hiyo michezo isingekuepo hao vijana wangeenda uwanjani kucheza wao na kujifurahisha wala wasingekufa kwa stress. Chunguza kwa makini utakubali..

Mfano jamii zinazoishi maporini huko mbona wanabuni michezo yao na wanaishi kwa furaha
 
You are the true son of your father
 
ili kazi iwe na mshahara hutegemea mambo mengi
1. Unazalisha au huzalishi
Ukiwa mzalishaji automatic malipo huwa makubwa

2. Umeajiriwa na nani?
Mwalimu anaajiriwa na serikali ambayo yenyewe pia ina njaa ila mchezaji anaajiriwa na matajiri


3. Unafanya kazi na nani?
Mwalimu anafanya kazi na wanafunzi ila mchezaji mpira unaangaliwa na watu wengi ikiwemo matajiri , wenye vyeo nk

4. Law of demand and supply
Wachezaji wote wa Tanzania hawazidi idadi ya walimu wa mkoa wa Dar es salaam, hadi inafikia mchezaji anawindwa na timu zaidi ya 5 kwa mara moja.
_ Kama mchezaji anagombaniwa , mwenye kulipa vizuri ndio atampata

5. ( KWA UMUHIMU)
_ Kipaji hulipa hulipa kuliko Elimu

Unaweza ukawa na fundi pikipikki au magari , unakuta kwa siku anakuingizia 100,000+ wakati huo mwalimu hana uwezo wa kuingiza hata 20,000

Hapo fundi bodaboda unaweza kumlipa 30,000 ila mwalimu utamlipa 10 tu
 
Kwa lengo tu la kubishana hebu tujiulize..

Hivi mcheza mpira ana add value gani kwenye maisha yetu ukilinganisha na daktari?

Mfano wacheza mpira wasingekuepo kungekua na athari gani ambayo tungepata kama binadamu?
Nasikia wanarefresh mind zetu eti
 
Kwasababu elimu sio biashara wala entertainment ni kazi ya wito. Wakiweka mshahara mikubwa usije shangaa wanasiasa wanataka kuwa walimu.
 
Kitu ambacho watu wengi hawajui pia, michezo inaisaidia sana serikali! Serikali zinapenda kuona watu wake wakiwa occupied na vitu vya kijinga jinga na ushabiki wa vitu kama michezo nk ili watu hao wawe rahisi ku control na wasikumbuke KUHOJI mambo ya msingi kuhusu maisha yao!
 
Kuna kitabu niliwahi kusoma (SELL LIKE CRAZY)

Kuna sehemu mwandishi amesema , " THERE IS DIFFERENCE BETWEEN BEING BUSY AND BEING PRODUCTIVE"

Walimu na madaktari wapo busy ila sio productive ( pesa)


Mpira ni biashara productive (inazalisha pesa nyingi)


Siku zote boss huwa haoni tabu kutoa pesa ndefu kwa wanaomsaidia kuzalisha (wafanyakazi wake)
 
Vilabu vyote vinasajiliwa kwa mujibu wa sheria za serikali. Bodi ya ligi ipo chini ya serikali,serikali inaweza kuratibu, kuelekeza na kupanga viwango elekezi vya mishahara ya wachezaji
Mpira wa nchi gani unaendeshwa kama hivyo????
 
Mpira hauzalishi kivile kwa maana ya viingilio, ila umeunganishwa na biashara kupitia matangazo ya biashara za wadhamini na runinga.
 
Vilabu vyote vinasajiliwa kwa mujibu wa sheria za serikali. Bodi ya ligi ipo chini ya serikali,serikali inaweza kuratibu, kuelekeza na kupanga viwango elekezi vya mishahara ya wachezaji
Sio kweli, serikali inaweza kupanga kiwango cha chini tu ila haiwezi kulimit


Hospitali binafsi ikiamua kumuajiri mtu ikamlila 50M kwa mwezi , serikali haiwezi kukataa maana haiwahusu

Hivyohivyo kwenye mpira
 
Walimu na madaktari wapo busy ila sio productive ( pesa)
Mkuu unajua bila madaktari hakuna mchezaji yoyote atakaethubutu kuingia uwanjani?

Imagine we ni mchezaji halafu ujue kabisa ukiumia au ukivunjika hakuna mtu wa kukutibu, utacheza? Hiyo productivity itakujaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…