Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?

Who the he'll are TEC!?? Wewe kweli mkatoliki kobe. Unaifahamu Canon law of infallibility? Kwa ufahamisho tu hizi ni sauti za watanzania milioni 20 wakatoliki. Hili tamko tutalikuta kigangoni jumapili. Ni utii tu.
Teuzi zinawasumbua
 
Hawa watu Huwa wanaleta shida sana pindi Kiongozi akiwa sio wa upande wao.
Unamtazamo duni sana broo

Hawa Tec kila utawala huwa wanatoa waraka kila kunapojitokeza jambo lisilo sawa kwa wananchi

Hauko sawa kwa sabb, Tec ni watu walio na kundi kubwa nyuma yao miongoni mwao akiwapo na Pascal Mayalla,

Huyu huyu amabaye ni Miongoni mwa walionyuma na hao Tec anatokea kuhoji kuhusu waraka wa viongozi wake tena kwa hoja yenye nguvu,

Wewe badala ya kujiongeza kwamba, kinachozungumzwa hapa si cha kidini bali ni la jambo linalogusa jamii ukiachia mbali maoni yao

Sasa nyie, endeleeni kutokuwapinga hao viongozi wenu wakitoa waraka mkihofia kwenda kinyume nao ni kujitenga na dini yenu!

Nasema hivi!

watu wenye fikira pana na walioelimika na mkichwa wako vizuri, Suala la Dini huwa linamuda wake maalumu na sio kila pahala

Achaneni na mitazamo ya kijinga yenye udini,

Tec wapingwe kwa hoja na siyo kuingiza mambo ya dini!
 
Hakuna kingine wanaogopa influence ya mwarabu,wanajua uislam ulifika Tanganyika kupitia mwarabu,bila ujio wa mwarabu pasingekua na uislam,wanajua mwarabu ana pesa,pesa zitaleta miradi Kama shule na hospital ambazo wao wametumia kuvuna waamini
DP WORLD waje wajenge misikiti kila kitongoji na walete maimam 1000000 hakuna shida. Lakini raslimali zetu kwa mikataba ya kimangungu Noooooppo
 
Kama nyie waandishi wa habari mmeshindwa kusimamia taaluma zenu, mmegeuka chawa, mnanunulika kama viazi, unadhani na wao Wana Akili kama zenu?
 
Uwepo wa dini ni kulinda haki na usawa; kabla ya kuwepo kwa dini binadamu wa zamani waliadhibiwa kwa mateso makali na ya kikatili. i.e kuchunwa ngozi huku ukiwa unajiona.
 
Mbona wanasiasa wanaenda sana kuhutubia (sio kusali tu) kwenye makanisa na kwenye misikiti? Au hujawahi kuwaona?

Siasa ni maisha, inamhusu kila mtu.
 
Jamaa nimemshangaa sana
Kuna baadhi ya watu wanasomewa tu maandiko.
Akisoma mwenyewe atagundua kuwa kuna wakati wafalme walizuiwa na manabii kufanya maamuzi fulani ambayo yangeangamiza taifa.

Na waliokaidi yaliwakuta makubwa.
Mfano kuna mmoja aliambiwa na nabii mmoja asiende vitani lakini manabii wengine wakamwambia aende baada ya kuingiwa na pepo la uongo, mfalme akamuona yule mmoja kama adui yake. Kilichomkuta sasa baada ya kwenda...

Kwahivyo, kama wao viongozi wanaapa kwa kutumia vitabu vya dini hawana budi kuwaheshimu viongozi wa dini kuhusiana na mstakabali wa taifa! Taifa ni letu sote
 
Habari jamii forum.

Naomba nieleze au na mm nichangie mada maana naona hizi mada zimekuwa nyingi sana na nyingi zinaelezea kuwa kama watu wanapinga huu mradi wa bandari.

Ilinapokuja swala la taifa mambo yote yanakuwa yanakaa pembeni, udini, siasa na ukabila maana hapa watatu wanatetea mali za Tanzania

Swala lolote linalo gusa mali au ardhi ya Tanzania tunatakiwa kuweka mambo yote pembeni. Wazee na baba zetu walivitunza na kuvieshimu sana iweje sisi leo tuwe wepesi kiasi hicho kukubali kila kitu bila ya kuoji au kukosoa.

Hivi vyote vilikuja kutoka nje,

#Siasa zilikuja
#Dini zilikuja
#Jina lilikuja

ILA TAMADUNI NA TANGANYIKA ZILIKUWEPO KABLA YA VYOTE HIVYO.

Atupaswi kukaa kmya maana machifu na watemi walipigania na wanakemea mambo aya kila siku. Ata walipo lala uko bado wanakemea aya mambo.

#Tusiwafanyie maamuzi vizazi vyetu vya kesho kwa sababu ya matumbo yetu ya leo na familia zetu. Sisi mbna wazee wetu awajatufanyia maamuzi ndomana mpaka leo vitu vipo Ardhi ipo.

#Kukosoa au kushauli si umpangie mtu wa kukosoa atokee wapi au aweje. Mtu yeyote ana haki ya kukosoa pale ambapo anaona akupo sawa. Tanznaia ni ya watanzania wote sio ya watu wachache.

#Wabunge pia tumewachagua sisi. Kwaiyo wakiwa wanafanya mambo kwa maslai yao pia tuna haki ya kukemea na kutoa maoni yetu. Sisi ndo tuwe waweka pale walipo. Awatakiwi kwenda kinyume na sisi mabosi zake ambao ndo tumemuweka pale.

#Mkisoma sana mnakuwa Missionaries #RIP JKNyerere.
 

Attachments

  • Tanzania.jpg
    20.7 KB · Views: 1
Kwanini umewaza kwa kiwango cha chini kiasi hiki Kaka. Umekurupuka bila sababu. Ungetulia uje vizuri
 
Tuongee ukweli tu bila kupepesa macho hizi kelele zote hizi drama zote toka awali, sababu DP World ni Waarabu.

Hakuna uchungu wa rasilimali za nchi wala nini issue ni Uarabu wa DP World. Period!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…