Mpira ni nini? Kama ni pesa, mbona Marekani wanazo na hawajawahi kutwaa kombe la dunia? Kama ni vipaji, mbona vimejaa Afrika na hatufanyi maajabu?

Sio liliwashinda bali hawalipendi,
Mkuu, kama kitu haukipendi si unaachana nacho. Sasa mbona wao hawalipendi soccer lakini bado ni wanachama wa FIFA? Mbona hawajitoi kama Burundi walivyojitoa ICC?...
 
Mkuu, soccer liliwashindwa wanaume wa Marekani ndio maana wakaamua kuanzisha michezo yao wenyewe?...
Wamarekani wamekufanya nini wewe?

Walikunyima visa?

Maana si bure.

Nishakueleza Wamarekqni hawapendi mifumo ya Waingereza.

Hawapendi chai, wanapenda kahawa.

Hawaendeshi gari kushoto, wanaendesha kulia.

Hata tai za Wamarekani stripes zake zinaenda tofauti na za Waingereza.

Hawapendi soccer, wanapenda American Football na Basketball.

Sasa unataka kuwalazimisha wapende kitu wasichopenda?

Idea nzima ya watu kuhama huko ikd world, Ulaya, Asia na Africa, na kuja Marekani, ilikuwa kuachana na mambo ya hiyo dunia ya zamani ya kuanzisha mambo mapya ya dunia mpya.

Ndiyo maana Marekani imeleta umeme, imeleta internet etc, na hata kwenye michezo imeanzisha michezo mioya kama basketball.

Sasa kama hujui historia, ni vigumu kuelewa hayo.
 
Kama hawapendi soccer mbona bado wanachama wa FIFA mkuu? Burundi hawakuipenda ICC wakajitoa. Wao USA bado wanafanya nini FIFA?...

Kwani lazima soka iwe ni mchezo wako pendwa ili uwe FIFA?

Cricket ni mchezo number 1 India ila bado ipo FIFA. Nao unataka watoke?

Inadhuru nini kuwa FIFA hata kama wanaume wenu hawapendi soka let alone nchi nzima kama India.

Basi tuseme USA ipo FIFA sababu ya USWNT if that makes you happy.
 
Kama hamna nyavu je?[emoji1]
 
Mpira si kipaumbele kwao, kama ambavyo HAKI si kipaumbele cha CCM.
 
Mkuu, kama kitu haukipendi si unaachana nacho. Sasa mbona wao hawalipendi soccer lakini bado ni wanachama wa FIFA? Mbona hawajitoi kama Burundi walivyojitoa ICC?...
Yaani unafananisha uanachama wa FIFA na ICC?!
Tambua kwamba nchi kuwa mwanachama wa mchezo fulani ngazi ya dunia haimaanishi kwamba hiyo nchi inaupenda mno huo mchezo. Nchi Kama Argentina, England, Brazil, nk raia wake wanapenda sana soccer kuliko mchezo wowote ule, na wachezaji wa timu ya taifa wanatokana na raia haohao, so vijana hujiingiza katika huo mchezo wao pendwa na hivyo kufanikisha kuwa na timu ya taifa bora. Kwa US wananchi hawapendi sana soccer Kama wanavyopenda basket, swimming, Boxing, Music, Movies,nk hivyo vijana wengi wa kimarekani huchagua michezo yao pendwa ya basket, nk.
 
Timu za MLS zinajitahidi sana kuchukua malegend wa soka ili kushawishi wamarekani kufatilia mpira lakini bado impact ni ndogo, Zlatan kidogo alipokuwa huko alileta amshaamsha kama unavyoona dongo alilowapiga hapo alipomaliza muda wake[emoji23][emoji23]
 
Kwa watasha huwa wana vipaumbele vyao kitu kama kwao hakitakuwa na faida pamoja na upekee basi huwa wanakitupa mbali na kuhusu afrika tatizo ni vipaumbele na kutokuwa na uwezo wa kutosha wa kushughulikia jambo husika na sababu za kushindwa huko zinajulikana dhahiri
 
Kuna siku nilimuuliza mmoja kwanini wanasema football is boring, anasema kwenye football timu zinaweza kucheza dakika 90 na kusipatikane goli, lakini kwenye basketball ni amshaamsha mwanzo mwisho atleast kwenye kila dakika 1 lazima washangilie goli, anasema kwenye 'soccer' hizo raha hazipo[emoji1][emoji1]
 
Daaah jibu la huyo mwamba kweli ni kiboko mkuu wakati mimi hapa sijui hata sheria moja ya basketball
 
Kwa watasha huwa wana vipaumbele vyao kitu kama kwao hakitakuwa na faida pamoja na upekee basi huwa wanakitupa mbali
Siku watakayojitoa uanachama wa FIFA ndio nitajua kuwa ni kweli hao USA hawana interest na soccer...
 
Hii maelezo imekaa sawa jombaa hongera, tukomae na bao letu na rede
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…