Ni sahihi kumfanyia binadamu mwenzio kama hivi?..
26/6 majira ya saa 1500Hrs, nilipata kipigo kikali ambacho sijawahi kupata maishani mwangu.
Miguu haikuweza kusimama tena, mgongo ulikuwa na maumivu makali sana kwa vipigo vya UBAPA WA MAPANGA, na mafimbo.
Mabega yalikuwa kwenye maumivu makali mno kiasi cha kuhisi huenda nimevunjwa mabega maana sikuwa napata hisia za mabega na mwili.
Kwanzia CHINI ya kiuno kwenda kwenye unyayo huko ndio ilikuwa balaa. Sio magoti, sio enka, sio unyayo, vilipigwa na MAGOGO na fimbo nyingi kwa muda wa dakika 50 mpaka saa moja.
Mateso haya yalikuwa ya watu wanne, hawa walikuwa wanapiga kama wanaua NYOKA. Kila mtu kashika kifaa chake anachoona kinafaa kuniumiza.
Kisha nikaambiwa "tunakurudisha Dar, uende ukatulie". Hapo nikapata nafuu huenda nitaishi tena, nilikuwa nimevimba sana miguu, nikajua hata nikirudishwa Dar hawatanirudisha nyumbani kwangu watanitupa njiani.
Nikawa nawazia ile hali yangu vipi nitaweza kutembea? Ila hayo hayakuwa ya muhimu nikashukuru tuu kuambiwa narudishwa nyumbani.
Safari ilikuwa ndefu sana, ndani ya gari walikuwa Wanavuta sana Bangi Na kunywa Pombe, huku kukiwa kumewashwa AC ya gari. Ile hali ya AC ilikuwa inapelekea kupata maumivu makali sanaaaa.
Nilikuwa naona kama ile AC inaingia ndani kwenye MIFUPA mule nilimo vimba sana, hivyo nilikuwa nalia tuu, wananitishia kukaa kimya kuwa nawapigia makelele. Wananipiga na Chupa za Bia kuwa nitulie, niweke miguu chini.
Ilikuwa safari ndefu sana, nililia sana. Gari ikasimama, na kisha wakashuka wote nikabaki na mmoja kulia kwangu, nikamuuliza swali moja "kwani leo lini?" Akanijibu leo "Alhamisi".
Basi nikajua siku ishapinduka, kumbe ile safari toka walivyonitoa pale Arusha tulitembea usiku kucha. Basi nikiwa ndani ya ile gari, akaja mmoja ya wale walioshuka, akasema "twende ukakojoe" kumbuka hapo sikuomba kuenda kukojoa.
Basi ikabidi nijivute kwenye kiti kujaribu kushuka, nilipokanyaga unyayo wangu chini kwa mara ya kwanza nilisikia maumivu makali sana. Nikadondoka kama mzigo. Wale jamaa wakasema nawachelewesha nisimame.
Wakaanza upya kunipa kipigo, ilikuwa kipigo kizito cha mabapa ya upanga na MAKOFI, huku wakiniburuza kuelekea ndani ndani huko. Sikuweza kujua wala kuona wapi napelekwa maana nilikuwa nimevalishwa MASK wakati wote huo.
Mikononi nikiwa na PINGU, basi baada ya vuta ni kuvute ya muda, wakanifikisha mahali walipotaka, kisha nikiwa nimesimama kwa kupepesuka, ndipo nikasikia sauti kutoka MBALI ikisema "piga chumaaaaaa".
Basi nikasikia tuu kichwani mwangu Mlio wa "tiiiiiiiiiiiiiinnnnngggggg" kisha nikajikuta nimeanguka chini, damu zinatoka mdomoni, puani, masikioni. Kisha nikaona mtu ananivua Pingu kwa haraka, mwingine ananivua Mask kisha wakaondoka kwa kukimbia.
Hapo nikaanza kupambana kupata PUMZI , mana kila kitu kilisimama wakati ule, nikafosi nikapata pumzi, ndio kuanza kuona sass nipo wapi.
Ilikuwa ni msitu, na mwinuko kidogo, na Mto mbele. Nikasema hapa mimi nimepona, acha nianze kujikongoja kutoka hili eneo. Ndio nikaanza kubilingika mule porini, najivuta , ndani ya lile pori, mpaka niliposikia sauti ya gari ndipo nikajua kuna barabara upande huu.
Hapo ndio nikaelekea ule upande wa barabara, na kuenda kuketi pale kusubiri msaada wa Watu.
Jana nimepigiwa simu na Alieniokoa, alikuwa ni dereva wa zile Gari za abiria aina y "Eicher" tumezungumza mengi sana, moja ya mazungumzo yetu nikamuomba picha ya ule mto uliopo pale mbugani.
Na huo ndio Mto ambao mm nilipigwa risasi pembezoni mwake. Ni mto wenye MAMBA NA VIBOKO kama mnavyoona, ila walikaa kimya hawakuweza kunidhuru.
Msitu una wanyama wengi wakali kama SIMBA , FISI, MBWA MWITU, nikiwa navuja damu nikitafuta msaada porini ila hakuweza kunidhuru.
Huo ndio ukuu wa Mungu, haya yote nimefanyiwa na jeshi la polisi Tanzania @tanpol chini ya maagizo ya ZCO FAUSTINE JACKSON MAFWELE.
SATIVA17🫡