Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Huwa huyu jamaa simuamini amini, lakini kwa kuwa nina akili timamu alichoongea kwa mtu yeyote anaefanya reasoning kwa umakini, jamaa kaongea point, ila kwa kuwa kaongea yeye basi hakuna atakaejisumbua kulifanyia kazi.

Naunga mkono Kikwete alicheza faulo ambayo haiihitaji var kujua ni penati, kwa kutosaini ule mkataba wa Bagamoyo na kuacha mradi ushaanza kufikia a point of no return, maana kama ingekuwa ipo Kanda ya Ziwa na sio Bagamoyo, mradi ungeendelea bila wasi wasi.

Haya sasa tushakula hasara ya bilioni 56 kulipa zile fidia wakazi wa bagamoyo na mradi kushnei
 
Mipasho ndo mbayo weza hakuna kitu kingine. Ndo uwezo unapo kita kwenye mipasho.

Msha lemazwa akili myu ana leta hoja ntia mnaanza tukana.

Pangua hoja kwa hoja kama unaweza. Ingawa najua huwezi kitu

Wasome wakenya wenye akili wanavyouona huo ni mradi wa kipumbavu kuwahi kutokea Kenya, mimi Siwezi kushabikia huyu zumbukuku anaetaka tuuze nchi yetu kisa kushindana na Kenya, huyu hafai kabisa kuwa kiongozi sababu atafanya maamuzi kimihemko badala ya kutumia weledi
 
ZZK anatueleza mkakati wa Bandari ya Bagamoyo kuwa ni gateway ya imports.
Kwa mchumi yoyote ningetegemea angekuwa na in-depth analysis ya how do we strengthen production ya mazao ghafi na processing ili kuwa na certain ya exports.

JK toka 2013 mpaka 2015 anatoka madarakani alisita kusaini a go ahead. Unadhani kwanini year 1 imepita hakusaini,
Year 2 imepita hakusaini
Year 3 anatoka madarakani early November bila kusaini. Nini alikiona kama sio favourable clauses ya mkataba mpaka 3 years zikakatika hakutia mkono.

Dr. Mpango waziri wa Fedha alikuwa mkuu wa Tume ya Mipango wakati wa JK; bila shaka alikuwa sehemu ya walimshauro JK asiwe "fasta" kusaini.

ZZK uliponda sana initiative za JPM na Prof. Kabudi kukaa na Barick na kushikilia makanikia in the name of tutashitakiwa. Leo hii uongo wako umeonekana wazi mchana peupe.

By the way; show by numerical projections namna gani Bagamoyo port could make a difference kwenye kuongeza revenues ambapo Mtwara, Tanga na Dar zime-fail ili ku-justify hoja yako

Kikwete hakusita kusaini bali alikuwa akisubiria upembuzi yakinifu ukamilike vizuri na ukaja kukamilika akiwa katoka ikulu na sasa aliyepo ikulu yeye kawapa Dili Bandari ya Lamu hataki meli kubwa kuja Tanzania
 
Nilichoelewa ni Kwamba Odinga amechangia kukwamisha mradi wa bandari ya Bagamoyo.

Kwamba zile tripu Za Odinga Dar na Chato alikuwa anatumwa na nchi yake kumlisha sumu Rais wetu kuhusu mradi wa Bagamoyo.

Kama kweli Odinga alipewa na tuzo kwa kazi hiyo, kama nchi inabidi tujitathimini.

Kifupi Odinga alikuwa jasusi wa kiuchumi kwa nchi yake kwa mjibu wa Zitto.
 
Story ndeefu wkt lengo la thread yako ni hapa tu ulipoandika.

'Tanzania ikabadili mpango wake wa Kujenga Reli kutoka Dar es Salaam kupitia Uvinza mpaka Musongati nchini Burundi'

Reli kutopitishwa Kigoma imekua Nongwa.
 
Kwanza hiyo bandari ni white elephant, waliijenga ili kuhudumia shehena ya Ethiopia na Sudan ndio maana mradi unaitwa lapsset lakini cha kushangaza Ethiopia imejenga railway to Djibouti

Wangefaidi kama kipindi kile Ethiopia ilivyokua haina mahusiano mazuri na Djibouti lakini baada ya kusameeana na kuungana mpaka Rais wa Ethiopia kapewa nobel maana yake hiyo Lamu haitapata hata container moja la Ethiopia

Bandari Ya Mombasa ni kubwa na haijatumika yote kiasi cha kuhitaji bandari nyingine ya ziada
Wacha bwana! Kwa hiyo sasa Ethiopia itategemea bandari kubwa kutoka Dola la Djibout! Una undugu na Magufuli? Isije kuwa siyo kosa lako!
 
Mimi nilishawai kusema humu kwamba idara ya usalama wa taifa ya Kenya imeingilia mchakato wa ujenzi wa bandari Bagamoyo na bomba la mafuta kutoka Tanga kwenda Uganda

Bila Magufuli kuchukua hatua na kuacha ukisikiliza watu wanaohongwa kuja kumshauri ujinga hasa maafisa wa TISS hii miradi haitafanikiwa na tutaendelea kuiangalia Kenya ikipaa kiuchumi bandari ya Bagamoyo ikikamilika ina uwezo wa kuhudumia nchi zaidi ya 10 kusini mwa jangwa la Sahara.
 
huwa huyu jamaa simuamini amini,lakini kwa kuwa nina akili timamu alichoongea kwa mtu yeyote anaefanya reasoning kwa umakini,jamaa kaongea point,ila kwa kuwa kaongea yeye basi hakuna atakaejisumbua kulifanyia kazi,NAUNGA MKONO KIKWETE ALICHEZA FAULO AMBAYO HAIIHITAJI VAR KUJUA NI PENATI,KWA KUTOSAINI ULE MKATABA WA BAGAMOYO NA KUACHA MRADI USHAANZA KUFIKIA A POINT OF NO RETURN,MAANA KAMA INGEKUWA IPO KANDA YA ZIWA NA SIO BAGAMOYO, MRADI UNGEENDELEA BILA WASI WASI,HAYA SASA TUSHAKULA HASARA YA BILIONI 56 KULIPA ZILE FIDIA WAKAZI WA BAGAMOYO NA MRADI KUSHNEI

Pesa zilizopotea kulipa fidia wakati wa Bagamoyo zote pengine kenya watamlipa magufuli kimya kimya kwani kama angekuwa na Uchungu angejenga hata Bandari ya mizigo ya ndani ya Nchi pekee, mfano South Africa wana Bandari kubwa zaidi ya Tano, Capetown, east London, port Elizabeth, Darban kila Bandari ina kazi yake maalum, zipo za mizigo ya nje mizigo ya kimataifa nchi jirani nk, kwa Tanzania Bandari ya Dsm ingebakia kupokea meli za mafuta tu, Bagamoyo iwe Bandari ya meli za kimataifa na Bandari za Tanga, mtwara kwa ajili ya mizigo ya ndani tu.
 

Wasome wakenya wenye akili wanavyouona huo ni mradi wa kipumbavu kuwahi kutokea Kenya, mimi Siwezi kushabikia huyu zumbukuku anaetaka tuuze nchi yetu kisa kushindana na Kenya, huyu hafai kabisa kuwa kiongozi sababu atafanya maamuzi kimihemko badala ya kutumia weledi

Wakenya wa wapi? Acha uzushi wako kuuza Nchi kivipi? Zumbukuku ni wewe uliyekula pesa za kenya kuja kutengeneza propaganda za kishamba toka kolomije.
 
Baba yangu aliniambia kuwa katika kila hadithi unayosimuliwa ina pande mbili, asante bwana Zitto kwa hili kwa hiyo natafuta pande ya pili na kuunganisha story nyingine.

Kwa kifupi nitaanza kufanya research katika hili. Maana katika kumbukumbu zangu kipindi kile bado uko CHADEMA mlisema mpango wa Bandari ya Bagamoyo ni malipo ambayo JK alikubaliana baada ya Riz1 kushikwa huko (tusiende huko sana sina nilijualo kwa hearsays) ila kwa hili nitalifanyia kazi na ikibidi kusema waziwazi jamii ijue.

Nikuulize pia vipi ule mpango wa kukuza uchumi, sikumbuki vizuri jina lake lakini ulikua una extend toka chini hadi juu (mikoa inayopakana na ziwa Tanganyika) mpango ambao ungeifanya Kigoma kuwa km Bagamoyo kwa DSM?
 
Bado magati zaidi yanaendelea kujengwa, yatajengwa magati zaidi ya 15 na mpaka sasa yamejengwa manne kwa hiyo yakikamilika hutoona meli zikiwa pending japo hata saivi sio kama zamani

Kina cha maji ya Bandari ya Dsm ni kifupi meli kubwa haziwezi kuja hata zinazokuja hulalamika injini kuvuta tope uchafu chini.
 
Mheshimiwa, wewe ulikuwa mmoja wa wale walionanga serikali kuhusu makemikia na ukatoa sababu mbalimbali za kisheria na uchumi kuhusu hilo. Mwisho wa siku mmebaki midomo wazi.
Wewe endelea na ACT na ubunge wako ila hadhi yako kitaifa inautata kiasi wengine tunaanza kuamini pengine wewe siyo mwenzetu.
Hivi hata aibu huoni?!! Mruma si alisema tumeibiwa madini yenye thamani ya Shilingi Trilioni 425, na hadi sasa hatujalipwa hata senti 5 zaidi ya kuahidiwa kulipwa 700 Billion kwa mikupuo 7!!

Sasa kabisa unatamba kupewa ahadi ya 700 Billions out trillions 425?!! Hivi unafahamu hiyo 700Billions inaingia mara ngapi kwenye trilioni 425?!!
 
Yupo sahihi PK haeleweki sio mtu wa kuaminiwa
Story ndeefu wkt lengo la thread yako ni hapa tu ulipoandika.

'Tanzania ikabadili mpango wake wa Kujenga Reli kutoka Dar es Salaam kupitia Uvinza mpaka Musongati nchini Burundi'

Reli kutopitishwa Kigoma imekua Nongwa.
 
Wakenya wa wapi? Acha uzushi wako kuuza Nchi kivipi? Zumbukuku ni wewe uliyekula pesa za kenya kuja kutengeneza propaganda za kishamba toka kolomije.
Ethiopia imejenga railway to Djibouti mpaka bandarini, hiyo Lamu haina barabara ya kupeleka mzigo Ethiopia, itaanzaje biashara na Ethiopia?

Ethiopia saivi inatumia Djibouti na Eritrea kupitisha mzigo wake wote, Ethiopia haijawahi kupitisha mzigo wake Kenya hata siku moja
 
Back
Top Bottom