Mradi wa Bwawa la Nyerere tulijilisha upepo au ndiyo mwendelezo wa siasa chafu za kibepari?

Mradi wa Bwawa la Nyerere tulijilisha upepo au ndiyo mwendelezo wa siasa chafu za kibepari?

Tenesse Valley Authority (TVA) haikuwa mahususi kwa ajili ya kuzalisha umeme bali kuinua uchumi wa maeneo yanayoizunguka kupitia usafiri wa majini, uwekezaji wa viwanda vya mbolea,mipango mji na pia kupambana na mafuriko.Hii ni tofauti sana na bwawa la Stiglerz ambalo uharibifu mkubwa wa mazingira unafanyika kuzalisha umeme ambao ungeweza kuzalishwa na kuzidi kwa gesi na vyanzo vingine vya nishati mbadala.
Wazungu husema hivi "Once is an accident, Twice is a Coincidence, but Thrice is a Pattern".

Hapa namaanisha nini, duniani kote ambako miradi ya namna hii yenye lengo la kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini lazima kuwepo na malalamiko.

Tena nimefuatilia kwa umakini na kufahamu kwamba malalamiko hayo ni lazima yafanane. Mbaya zaidi makundi ya wanaoleta haya malalamiko huwa ni ya watu wa aina ileile, tena huja na sababu zilezile.

Ukifuatilia kwa umakini, utatambua kwamba mfanano wa hawa watu ni mkubwa sana hadi utakubaliana na ule msemo wa kiingereza kwamba "History does not repeat itself, but people do repeat themselves".

Fanya utafiti wako binafsi, utakubaliana na nilichokiandika hapa.

Muda ni mchache, leo hii ntazungumzia nchi tatu ambazo ni Marekani, Ethiopia na Tanzania. Ambako kote katika nyakati tofauti kumekuwa na miradi mikubwa ya kuzalisha umeme wa maji ambao kwa mkono wa serikali, ambayo imelenga kuzalisha umeme wa gharama nafuu kwa wananchi huku miradi hiyo ikiendeshwa na serikali.

Hapa nazungumzia miradi ya The Tennessee valley Hydro-electric Power Projects (TVA), The Grand Ethiopian Rennaisance Dam (GERD) na Julius Nyerere Hydro- Power Project (JHPP).

Nimefuatilia kwa karibu nimeona kwenye hii miradi ya TVA, GERD na JNHPP ni lazima utakutana na majina kama WHITE-ELEPHANTS, DEBT-RIDDEN PROJECTS, UNSUSTAINABLE ENERGY SOURCE, ENVIROMENTAL HAZARDOUS, GOVERNMENT MONOPOLY, UNCOMPETITIVE SOEs na SOCIALIST EMBARKED PROJECT.

Mpaka sasa sijafahamu kwanini tokea kule Marekani, Ethiopia hadi Tanzania mambo yafanane hivi. Imetokea TVA (Once=An Accident), Imetokea GERD (Twice= A Coincidence) na Imetokea Tanzania (Thrice= A Pattern).

Pia sehemu nyinginezo yanaendelea kutoka tu, mpaka najiuliza nini hiki. Labda, huenda ni mawazo yangu hafifu tu, ambapo wazungu husema "A figment of your own imagination"

HEBU TUANGALIE MRADI WA UMEME CHINI YA TENNESSEE VALLEY AUTHORITY

Raisi Franklin Delano Roosevelt alianzisha The Tennessee Valley Authority (TVA) mwaka 1933 ili kuwezesha Marekani izalishe umeme wa bei ndogo ambao utasaidia majimbo kama saba ambayo yanazunguka lile eneo.

Lengo kubwa ni kusaidia kiuchumi ukanda ambao uliachwa nyumba kimandeleo, kutoa ajira kwa vijana na kusukuma uchumi wa viwanda eneo hilo.

Tokea mwaka 1933 mpaka sasa Marekani imefanikiwa kutengeneza mabwawa 50 ambayo yanasaidia kuzalisha umeme wa bei ndogo unaotumika kuendesha viwanda na uchumi wa majimbo karibia saba ya eneo ambalo bonde la Tennessee limepita.

Ila huwezi amini mpaka leo hii mwaka 2022, wanaharakati wa kimazingira wanapinga huu mradi kwa kusema unaleta madhara.

Wakati nasoma shule kuhusu huu mradi, tuliambiwa kwamba ulipigwa vita sana na makampuni binafsi ya umeme, wanasiasa, wanaharakati na wanasheria.

Ambapo walitumia mbinu mbalimbali kufanikisha hujuma dhidi ya huu mradi lakini hawakufanikiwa. Sababu kubwa ni kwamba raia wengi wa Marekani walikuwa ni watu wanaojielewa mno, siyo wajinga wanaopelekeshwa bila kufahamu linaloendelea (Dumbed-Down Citizenry) nchini kwao.

Upinzani haukishia kwenye uanzishwaji wa huu mradi mwaka 1933, mwaka 1936 mmoja wa wamiliki wa hisa kwenye kampuni binafsi la umeme THE ALABAMA POWER COMPANY aitwaye ASHWANDER alipeleka kesi mahakamani kuzuia serikali kuuza umeme kupitia The Tennessee Valley Authority (TVA) akisema kwamba serikali haitakiwi kabisa kuuza umeme hivyo kuna uvunjifu wa katiba ya Marekani.

Unaweza kutafuta kesi ya: Ashwander V Tennessee Valley Authority (1936)

Mahakama ya juu ya Marekani ilikataa na kusema uzalishaji huu wa umeme siyo wa faida tu, bali ulilenga kutoa huduma kwa kukuza uchumi wa eneo ambalo lilikuwa nyuma kimaendeleo na kuimarisha ulinzi wa nchi kwasababu viwanda vya silaha vilikuwepo eneo hilo.

Hivyo mabwanyeye wakapigwa chini na serikali inauza umeme kwa raia mpaka leo hii. Ikumbukwe inayofanya hivi ni serikali ya Kibeberu ya ulimwengu wa kwanza na siyo serikali ya Kijamaa ya ulimwengu wa tatu.

Wamarekani zaidi ya milioni 9 wanapata huduma ya umeme nafuu kutoka kwenye miradi 29 ya umeme wa maji kutoka Tennessee Valley Authority (TVA).

Kubwa zaidi ni kwamba huduma ya umeme kwenye majimbo hayo yanayopitiwa na bonde la Tennessee ni moja kati ya umeme wenye gharama nchini Marekani, kama siyo ndiyo wenye gharama nafuu zaidi kwenye nchi hiyo.

Kitakachoshangaza watu werevu ni kwamba PROPAGANDA CHAFU na UZANDIKI dhidi ya mradi huu hazijaisha tokea mwaka 1936. Raisi Dwight Eisenhower alishawahi kuutukana huu mradi kwa kuuita maneno kama "Ujamaa nyemelevu" (Creeping Socialism), ilhali mamilioni ya Wamarekani ni wanufaika.

Maneno kama haya hayatakiwi kabisa kutoka kwenye kinywa cha mkuu wa nchi mwenye lengo la kuwakwamua kiuchumi raia wa kawaida, kwasababu faida za mradi ni dhahiri kwa watu wote.

Lengo la Raisi Eisenhower lilikuwa siyo kupinga UJAMAA bali ni kubinafsisha (TVA), lakini akakumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa wazalendo wa kimarekani na mwishowe akawa mpole.

Kilichomshangaza zaidi ni kwamba waliompinga ni wenzake kutoka REPUBLICAN PARTY ambao husifika kwa kuchukia UJAMAA hasa pale ambapo serikali yenyewe hufanya biashara. Nini kilipelekea Raisi na jopo la wataalamu wake kupingwa hivi ???

Sasa kubwa na baya zaidi dhidi ya mradi huu ni lile la mwaka 2013, ambapo Raisi Barrack Obama aliandaa muswada ili kubinafsisha The Tennessee Valley Authority (TVA) kwa watu binafsi.

Moja ya sababu kubwa ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ni kwamba mamlaka ya Tennessee Valley (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni mzigo kwa serikali.

Walikuwa na hoja nzito sana maana ukweli ni kwamba mamlaka hiyo (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni takribani dola za kimarekani bilioni 25.

Lakini hili halikuwa sababu ya kusema kwamba serikali ibinafsishe shirika hili la kiserikali na kuwaumiza raia wapatao milioni 9 kwa kupanda kwa gharama za umeme.

Sababu ya pili ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ili kufanikisha ubinafsishwaji wa The Tennessee Valley Authority (TVA) ni ile ambayo hata kwetu huku inatusumbua ya kutunza mazingira.

TVA mbali na miradi 29 ya umeme wa maji, imeongeza pia miradi 12 ya umeme wa makaa ya mawe, miradi 3 ya umeme wa nyuklia, miradi 15 ya umeme wa gesi na mradi 1 wa umeme wa upepo.

Inasemekana TVA inahitaji dola za kimarekani bilioni 25 ili kupunguza uchafuzi wa mazingira unaosababisha na huu mradi hasa kutoka kwenye vinu vya makaa ya mawe. Hivyo ili serikali isiingie kwenye hizi gharama zisizo za msingi, basi ni kheri ibinafsishe tu shirika hili.

Kuna nchi fulani hivi viongozi wake, wasomi na wafanyabiashara wanapenda kuzungumza kauli kama hizi za Raisi Barrack Obama na Dwight Eisenhower, bila shaka ndugu msomaji utakuwa unaifahamu.

Hivyo njia rahisi kwa Serikali ya Raisi Obama, kukwepa deni kubwa la TVA na gharama za marekebisho, wakaona ni bora wauze hii SOE (State Owned Enterprise).

Ila ukweli mchungu ni kwamba wangefanya hivyo ina maana gharama za umeme kwa wananchi wa Marekani zaidi ya milioni 9 ingepanda sana na wangeathiri biashara nyingi na maisha ya raia wa kawaida.

Mbali na madhaifu yake mengi, Marekani ni taifa ambalo raia wake wengi wanajielewa mno.

Wahafidhina wa chama cha REPUBLICAN hasa wawakilishi kutoka majimbo hayo, pamoja na watu binafsi walipinga kwa nguvu mswada ambao ungefanikisha ubinafsishwaji wa kiholela wa hii mamlaka ambayo lengo lake kuu ni kutoa huduma kwa raia na kuimarisha ulinzi wa nchi.

HEBU TURUDI NCHINI TANZANIA SASA, TUANGALIE TANESCO NA JNHPP

Bunge la Marekani lilichofanya ni kukataa mamalaka isiuzwe na kuiwekea ukomo wa deni, ambayo mamlaka haitakiwi kuvuka, ambapo ukomo ni dola za kimarekani bilioni 30.

Hivyo madeni hayapo tu kwenye shirika letu la TANESCO lakini hata TVA wana madeni tena yanakera. Sisemi haya kusema TANESCO inafanya vizuri, la hasha kuna mambo mengi ya ajabu yanafanyika.

Lakini naamini wakijipanga vizuri na kupunguza siasa tunaweza kufika sehemu nzuri sana. Mbona TVA wafananya vizuri na bado ni shirika la serikali ???

Jambo jingine ambalo nalisikia sana nchini Tanzania ni hilo la kusema umeme wa maji siyo endelev. Mimi siyo mtaalamu lakini naweza kufahamu wapi nadanganywa, kiukweli hili linanipa ukakasi mkubwa sana.

Mradi wa TVA umeanza mwaka 1933 na upo hadi leo hii, utasemaje kwamba umeme wa maji siyo endelevu jamani ???

Unaweza kumtukana Raisi Magufuli kwamba ni mjinga, lakini kumbuka huu mpango wa JNHPP umekuwepo tokea enzi za Mzee Nyerere, Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa, ina maana hawa wote na wataalamu wao walikuwa ni wajinga kabisa wasitambue kwamba Hydro-Electric Power is not sustainable source of energy ??? Aidha ni kweli sisi watanzania ni watu wajinga sana pamoja na viongozi wetu, AU kuna kitu kinachoendelea nyuma ya pazia sisi raia wa kawaida hatukioni.

Jambo kubwa zaidi la kujiuliza hapa: Ni kwamba kama mradi wa TVA ambao manufaa yake yanaonekana kwa mamilioni ya wananchi wa Marekani unapigwa vita kali hivi, tena hadi na viongozi wa serikali wakiwemo maraisi, sisi huku kwetu Tanzania tusipingwe kweli ???

Mwaka jana miezi ya mwishoni nilikuwa nafuatilia wanaharakati mitandaoni, nikasikia baadhi wakisema mamilioni ya miti yamekatwa na uharibifu mkubwa wa mazingira umefanyika kwenye mradi wa JNHPP ndiyo maana mvua zimegoma Tanzania.

Lakini, wengine wanasema kwamba JNHPP ni tembo mweupe (A White Elephant Project). Majibu ya Waziri Makamba, yamakuwa yakibadilika-badilika. Lakini naamini, ukweli tutaufahamu tu.

Wanaharakati wetu wangepinga huu mradi (JNHPP) peke yake sisi tungeelewa labda na binafsi ningesema hebu tujifanyie tathmini. Lakini hakuna mradi wowote mkubwa ambao umewahi kufanyika nchini Tanzania bila kupata upinzani mkubwa:

Uwe ni mradi wa msaada, uwekezaji au mkopo. Nasema hili kwa UJASIRI WOTE, kama upo naomba nitajiwe ili nijifunze.

Ukifuatilia kinachoendelea kwa wanasiasa wetu kuna sababu nyingi sana zinazoletwa ambazo hazina kichwa wala miguu.

Wengi wetu ni UJINGA, WOGA, BENDERA FUATA UPEPO lakini kubwa ni ULAJI TU wa watu wachache ambao wamevaa ngozi ya kutunza mazingira, kulinda katiba, matumizi ya mbinu za kisasa za kisayansi na kibiashara kuendesha sekta ya nishati nchini. Lakini ni hivi: UKWELI UKO KAMA MIMBA, HUWEZI KUUFICHA MILELE. Tutafamu tu...

NAMALIZIA NA ETHIOPIA, MRADI WA THE GRAND ETHIOPIAN RENNAISANCE DAM

Ingekuwa Tanzania ndiyo nchi pekee ndiyo inayopigwa vita kwa kuanzisha mradi kama huu ningesema, basi tujifanyie tathmini kidogo.

Ila hadi kule kwa ndugu zetu Ethiopia yametokea machafuko makubwa sana kupinga uanzishwaji wa The Grand Ethiopia Rennaisance Dam (GERD) ambalo litakuwa msaada mkubwa sana kwa mamilioni ya wahabeshi nchini humo.

Upinzani umekuwa mkubwa imefika kipindi kwamba Raisi wa Marekani Donald Trump akaweka bayana kabisa kwamba Misri inaweza kulipua bwana hilo" Egypt might blow up the dam".

WIKILEAKS wanasema kwamba, mradi huu ukimalika hautaisaidia Ethiopia peke yake kuzalisha umeme wa bei ndogo, bali utazalishwa umeme mwingi (Megawatts 5,250) ambao utauzwa hadi nchi jirani kama Sudan na serikali ya Sadani inafahamu hili vizuri kabisa.

Sasa ukifuatilia kwa umakini, kuna wanasiasa wakubwa ambao walisema wazi kwamba mradi wa GERD, hauna manufaa na ni tembo mweupe ( A WHITE ELEPHANT). Moja kati ya watu waliowahi kusema hivi ni Raisi Isaias Afwerki wa Eritrea.

Lakini mradi huu ukikamilika, umeme wa gharama nafuu utafika hadi nchini kwake. Watanzania tujiulize kitu hapa: Kama umeme wa maji siyo wa muda mrefu (Not Sustainable), hivi iweje serikali ya Uchina itupe zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1, ambazo ni sawa na trilioni mbili za kitanzania au zaidi kwenye mradi ?

Asasi za kiraia (NGOs) nazo haziko nyuma katika kutuonesha madhara ya mradi huu wa GERD. NGO maarufu iitwayo INTERNATIONAL RIVERS kutoka California, nchini Marekani iliandaa ripoti kubwa kabisa kuonesha madhara ya mradi huo kwenye mazingira. Wakaenda mbali zaidi na kusema kwamba bwana hili linaweza kuchangia mabadiliko ya hali ya nchi.

Ikumbukwe hawa ndugu zetu wamezungumza sana juu ya miradi ya umeme wa maji nchini Tanzania na Ethiopia.

MWISHO KABISA: MAONI YA WANAZUONI KUHUSU SIASA ZA UMEME NA MABWAWA

Kama umefuatilia siasa za Afrika kwa muda mrefu, utatambua kwamba huu mchezo haujaanza na Tanzania wala Ethiopia. Prof Mike Muller ambaye ni mhandisi kutoka chuo cha Witswatersrand Afrika Kusini, amawahi kuandika na kusema siasa za kupinga miradi mikubwa ya umeme wa maji zilianza mapema nchini Misri kipindi cha Gamal Abdi Nasser ambapo alitaka kujenga bwawa la Aswan (ASWAH HIGH DAM) ambalo lingezalisha MegaWatts 2,100.

Prof Asit K. Biswas amtaalamu wa maji na mazingira, ambaye ndiye anaongoza kwa kufanyiwa rejea za kitaalamu linapokuja suala za mazingira na maji, akishirikiana na Prof Cecilia Tortajada waliandika chapisho ambalo limesema kwamba mradi wa BWAWA LA ASWAN una madhara makubwa kwenye mazingira.

Lakini ukweli ni kwamba wataalamu mradi huo ulipokamilika mwaka 1970, ulikidhi nusu ya mahitaji ya umeme nchini Misri.

Ikimbukwe kwamba siasa za ASWAN HIGH DAM ziliwahi kupelekea Misri ivamiwe kijeshi na Uingereza, Ufaransa na Israeli. Nasser alisema alitaifisha Mfereji wa Suez kwasababu maji yake ni muhimu kwa ujenzi wa bwawa la Aswan.

Nasser aliomba msaada kwa serikali ya Raisi Eisenhower ili kujenga bwana la Aswan, lakini Eisenhower aligoma.

Raisi Kennedy alikosoa sana haya maamuzi ya kuvuruga miradi ya Afrika akisema hivi "When we abruptly abandoned the Aswan Dam in Egypt, the Russians went ahead to finance it. While we starve the Development loan Fund, the Sino-Soviet bloc has already passed us in economic assistance to selected key areas" Hili ndilo lilitokea bwawa lilijengwa na Warusi.

Maajabu barani Afrika huwa hayaishi kabisa: Kinachotushangaza wengi wetu leo hii ni kwamba Misri ambao miaka ya nyumba walionewa katika kujengwa bwawa la Aswan (ASWAN HIGH DAM), leo hii wao nao wakishirikiana na mataifa makubwa nje, wanaharakati na asasi kubwa za kiraia, wanafanya hujuma kubwa sana dhidi ya mradi wa GERD nchini Ethiopia.

NB 1: Siasa kama hizi, zilionekana pia kule nchini GHANA kipindi cha marehemu Nkhrumah ambapo alikuwa anataka kujenga bwawa la AKASOMBO (The Akasombo Dam) ili kuzalisha umeme.

Uliundwa mtandao mkubwa sana wa watu ndani na nje ya nchi ili kumzuia. Muda ni mchache sana siwezi kuzungumza kilichotokea.

NB 2: Fanya utafiti wako kuhusu miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme kupitia maji (TVA, GERD, JNHPP) pia hata ASWAN HIGH DAM na AKASOMBO DAM utatambua kwamba siasa zake zinafanana.

Wahusika ni walewale, wakitumia mbinu zilezile, sema tu huja wakiwa wamevaa vingago (Masks) tofauti-tofati. Kiufupi hizi siasa zinachezwa sana kitaalamu na wengi wetu tunafuata upepo bila kufanya tafiti binafsi.

Mimi siyo mtaalamu sana wa haya mambo, hivyo naomba wale wajuvi wanisaidie zaidi kuelewa. Nitafurahi kurekebishwa na kuelekezwa pale ambapo nimepotoka na kutofahamu kinachoendelea.

CC: JokaKuu , Nguruvi3 , UmkhontoweSizwe , TUJITEGEMEE
 
Marekani, Misri na kwingine kokote walipojenga mabwawa makubwa ya umeme uharibifu wa mazingira umekuwepo, huwezi kujenga bwawa kubwa la umeme bila kuharibu mazingira.
Mkuu, mimi siyo mtaalamu. Nachotaka kueleweshwa ni kwamba kwanini sehemu nyingine duniani kama Marekani na Misri madhara kwenye mazingira yasiwepo, lakini yawepo tu nchini Tanzania. Naomba unidadavulie zaidi nipate kufahamu.......
 
Unapofanya miradi mikubwa ya nchi hutakiwi kuangalia gharama nafuu kwa wananchi, kuna mambo mengine mengi mtambuka ya muhumu yanayopaswa kutazamwa kwa kina.
Management ya uchumi inatakiwa ifanyike katika level ya macro sio micro.

Gesi ingesimamiwa vizuri ingezalisha umeme mwingi kuliko wa Stiglers hata kama ungekuwa wa bei juu kidogo, gesi ingezalisha maelfu ya ajira za moja kwa moja na laki za ajira indrect, gesi ingefungua uchumi wa kusini eneo ambalo liko nyuma sana kimaendeleo, gesi ingeleta kodi kwenye uchumi wa nchi. Umeme wa Stiglers zaidi ya porojo za kuwa wa bei nafuu hautukapa hizi faida nyingine za moja kwa moja kwa uhakika.
Umeme ni huduma muhimu sana kwa uchumi na uhai wa taifa lolote katika dunia hii ya sasa. Hivyo mbali na kupata huduma hii, lazima pia tuzingatie gharama nafuu kwa wananchi. Unadhani tukiruhusu makampuni binafsi kuzalisha, kusafirisha na kuuza umeme tunaweza kupata umeme wa gharama nafuu ??? (Kama ndiyo, naomba utusaidie kutuonesha ni kipivi itakuwa hivyo)

Nchini Marekani umeme wa Tennessee Valley Authority (TVA) ambalo ni shirika la kiserikali una gharama nafuu zaidi kuliko ule kutoka kwenye mashirika binafsi. Unadhani hili linawezekana kufanyika nchini Tanzania ???
 
Wazungu husema hivi "Once is an accident, Twice is a Coincidence, but Thrice is a Pattern".

Hapa namaanisha nini, duniani kote ambako miradi ya namna hii yenye lengo la kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini lazima kuwepo na malalamiko.

Tena nimefuatilia kwa umakini na kufahamu kwamba malalamiko hayo ni lazima yafanane. Mbaya zaidi makundi ya wanaoleta haya malalamiko huwa ni ya watu wa aina ileile, tena huja na sababu zilezile.

Ukifuatilia kwa umakini, utatambua kwamba mfanano wa hawa watu ni mkubwa sana hadi utakubaliana na ule msemo wa kiingereza kwamba "History does not repeat itself, but people do repeat themselves".

Fanya utafiti wako binafsi, utakubaliana na nilichokiandika hapa.

Muda ni mchache, leo hii ntazungumzia nchi tatu ambazo ni Marekani, Ethiopia na Tanzania. Ambako kote katika nyakati tofauti kumekuwa na miradi mikubwa ya kuzalisha umeme wa maji ambao kwa mkono wa serikali, ambayo imelenga kuzalisha umeme wa gharama nafuu kwa wananchi huku miradi hiyo ikiendeshwa na serikali.

Hapa nazungumzia miradi ya The Tennessee valley Hydro-electric Power Projects (TVA), The Grand Ethiopian Rennaisance Dam (GERD) na Julius Nyerere Hydro- Power Project (JHPP).

Nimefuatilia kwa karibu nimeona kwenye hii miradi ya TVA, GERD na JNHPP ni lazima utakutana na majina kama WHITE-ELEPHANTS, DEBT-RIDDEN PROJECTS, UNSUSTAINABLE ENERGY SOURCE, ENVIROMENTAL HAZARDOUS, GOVERNMENT MONOPOLY, UNCOMPETITIVE SOEs na SOCIALIST EMBARKED PROJECT.

Mpaka sasa sijafahamu kwanini tokea kule Marekani, Ethiopia hadi Tanzania mambo yafanane hivi. Imetokea TVA (Once=An Accident), Imetokea GERD (Twice= A Coincidence) na Imetokea Tanzania (Thrice= A Pattern).

Pia sehemu nyinginezo yanaendelea kutoka tu, mpaka najiuliza nini hiki. Labda, huenda ni mawazo yangu hafifu tu, ambapo wazungu husema "A figment of your own imagination"

HEBU TUANGALIE MRADI WA UMEME CHINI YA TENNESSEE VALLEY AUTHORITY

Raisi Franklin Delano Roosevelt alianzisha The Tennessee Valley Authority (TVA) mwaka 1933 ili kuwezesha Marekani izalishe umeme wa bei ndogo ambao utasaidia majimbo kama saba ambayo yanazunguka lile eneo.

Lengo kubwa ni kusaidia kiuchumi ukanda ambao uliachwa nyumba kimandeleo, kutoa ajira kwa vijana na kusukuma uchumi wa viwanda eneo hilo.

Tokea mwaka 1933 mpaka sasa Marekani imefanikiwa kutengeneza mabwawa 50 ambayo yanasaidia kuzalisha umeme wa bei ndogo unaotumika kuendesha viwanda na uchumi wa majimbo karibia saba ya eneo ambalo bonde la Tennessee limepita.

Ila huwezi amini mpaka leo hii mwaka 2022, wanaharakati wa kimazingira wanapinga huu mradi kwa kusema unaleta madhara.

Wakati nasoma shule kuhusu huu mradi, tuliambiwa kwamba ulipigwa vita sana na makampuni binafsi ya umeme, wanasiasa, wanaharakati na wanasheria.

Ambapo walitumia mbinu mbalimbali kufanikisha hujuma dhidi ya huu mradi lakini hawakufanikiwa. Sababu kubwa ni kwamba raia wengi wa Marekani walikuwa ni watu wanaojielewa mno, siyo wajinga wanaopelekeshwa bila kufahamu linaloendelea (Dumbed-Down Citizenry) nchini kwao.

Upinzani haukishia kwenye uanzishwaji wa huu mradi mwaka 1933, mwaka 1936 mmoja wa wamiliki wa hisa kwenye kampuni binafsi la umeme THE ALABAMA POWER COMPANY aitwaye ASHWANDER alipeleka kesi mahakamani kuzuia serikali kuuza umeme kupitia The Tennessee Valley Authority (TVA) akisema kwamba serikali haitakiwi kabisa kuuza umeme hivyo kuna uvunjifu wa katiba ya Marekani.

Unaweza kutafuta kesi ya: Ashwander V Tennessee Valley Authority (1936)

Mahakama ya juu ya Marekani ilikataa na kusema uzalishaji huu wa umeme siyo wa faida tu, bali ulilenga kutoa huduma kwa kukuza uchumi wa eneo ambalo lilikuwa nyuma kimaendeleo na kuimarisha ulinzi wa nchi kwasababu viwanda vya silaha vilikuwepo eneo hilo.

Hivyo mabwanyeye wakapigwa chini na serikali inauza umeme kwa raia mpaka leo hii. Ikumbukwe inayofanya hivi ni serikali ya Kibeberu ya ulimwengu wa kwanza na siyo serikali ya Kijamaa ya ulimwengu wa tatu.

Wamarekani zaidi ya milioni 9 wanapata huduma ya umeme nafuu kutoka kwenye miradi 29 ya umeme wa maji kutoka Tennessee Valley Authority (TVA).

Kubwa zaidi ni kwamba huduma ya umeme kwenye majimbo hayo yanayopitiwa na bonde la Tennessee ni moja kati ya umeme wenye gharama nchini Marekani, kama siyo ndiyo wenye gharama nafuu zaidi kwenye nchi hiyo.

Kitakachoshangaza watu werevu ni kwamba PROPAGANDA CHAFU na UZANDIKI dhidi ya mradi huu hazijaisha tokea mwaka 1936. Raisi Dwight Eisenhower alishawahi kuutukana huu mradi kwa kuuita maneno kama "Ujamaa nyemelevu" (Creeping Socialism), ilhali mamilioni ya Wamarekani ni wanufaika.

Maneno kama haya hayatakiwi kabisa kutoka kwenye kinywa cha mkuu wa nchi mwenye lengo la kuwakwamua kiuchumi raia wa kawaida, kwasababu faida za mradi ni dhahiri kwa watu wote.

Lengo la Raisi Eisenhower lilikuwa siyo kupinga UJAMAA bali ni kubinafsisha (TVA), lakini akakumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa wazalendo wa kimarekani na mwishowe akawa mpole.

Kilichomshangaza zaidi ni kwamba waliompinga ni wenzake kutoka REPUBLICAN PARTY ambao husifika kwa kuchukia UJAMAA hasa pale ambapo serikali yenyewe hufanya biashara. Nini kilipelekea Raisi na jopo la wataalamu wake kupingwa hivi ???

Sasa kubwa na baya zaidi dhidi ya mradi huu ni lile la mwaka 2013, ambapo Raisi Barrack Obama aliandaa muswada ili kubinafsisha The Tennessee Valley Authority (TVA) kwa watu binafsi.

Moja ya sababu kubwa ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ni kwamba mamlaka ya Tennessee Valley (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni mzigo kwa serikali.

Walikuwa na hoja nzito sana maana ukweli ni kwamba mamlaka hiyo (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni takribani dola za kimarekani bilioni 25.

Lakini hili halikuwa sababu ya kusema kwamba serikali ibinafsishe shirika hili la kiserikali na kuwaumiza raia wapatao milioni 9 kwa kupanda kwa gharama za umeme.

Sababu ya pili ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ili kufanikisha ubinafsishwaji wa The Tennessee Valley Authority (TVA) ni ile ambayo hata kwetu huku inatusumbua ya kutunza mazingira.

TVA mbali na miradi 29 ya umeme wa maji, imeongeza pia miradi 12 ya umeme wa makaa ya mawe, miradi 3 ya umeme wa nyuklia, miradi 15 ya umeme wa gesi na mradi 1 wa umeme wa upepo.

Inasemekana TVA inahitaji dola za kimarekani bilioni 25 ili kupunguza uchafuzi wa mazingira unaosababisha na huu mradi hasa kutoka kwenye vinu vya makaa ya mawe. Hivyo ili serikali isiingie kwenye hizi gharama zisizo za msingi, basi ni kheri ibinafsishe tu shirika hili.

Kuna nchi fulani hivi viongozi wake, wasomi na wafanyabiashara wanapenda kuzungumza kauli kama hizi za Raisi Barrack Obama na Dwight Eisenhower, bila shaka ndugu msomaji utakuwa unaifahamu.

Hivyo njia rahisi kwa Serikali ya Raisi Obama, kukwepa deni kubwa la TVA na gharama za marekebisho, wakaona ni bora wauze hii SOE (State Owned Enterprise).

Ila ukweli mchungu ni kwamba wangefanya hivyo ina maana gharama za umeme kwa wananchi wa Marekani zaidi ya milioni 9 ingepanda sana na wangeathiri biashara nyingi na maisha ya raia wa kawaida.

Mbali na madhaifu yake mengi, Marekani ni taifa ambalo raia wake wengi wanajielewa mno.

Wahafidhina wa chama cha REPUBLICAN hasa wawakilishi kutoka majimbo hayo, pamoja na watu binafsi walipinga kwa nguvu mswada ambao ungefanikisha ubinafsishwaji wa kiholela wa hii mamlaka ambayo lengo lake kuu ni kutoa huduma kwa raia na kuimarisha ulinzi wa nchi.

HEBU TURUDI NCHINI TANZANIA SASA, TUANGALIE TANESCO NA JNHPP

Bunge la Marekani lilichofanya ni kukataa mamalaka isiuzwe na kuiwekea ukomo wa deni, ambayo mamlaka haitakiwi kuvuka, ambapo ukomo ni dola za kimarekani bilioni 30.

Hivyo madeni hayapo tu kwenye shirika letu la TANESCO lakini hata TVA wana madeni tena yanakera. Sisemi haya kusema TANESCO inafanya vizuri, la hasha kuna mambo mengi ya ajabu yanafanyika.

Lakini naamini wakijipanga vizuri na kupunguza siasa tunaweza kufika sehemu nzuri sana. Mbona TVA wafananya vizuri na bado ni shirika la serikali ???

Jambo jingine ambalo nalisikia sana nchini Tanzania ni hilo la kusema umeme wa maji siyo endelev. Mimi siyo mtaalamu lakini naweza kufahamu wapi nadanganywa, kiukweli hili linanipa ukakasi mkubwa sana.

Mradi wa TVA umeanza mwaka 1933 na upo hadi leo hii, utasemaje kwamba umeme wa maji siyo endelevu jamani ???

Unaweza kumtukana Raisi Magufuli kwamba ni mjinga, lakini kumbuka huu mpango wa JNHPP umekuwepo tokea enzi za Mzee Nyerere, Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa, ina maana hawa wote na wataalamu wao walikuwa ni wajinga kabisa wasitambue kwamba Hydro-Electric Power is not sustainable source of energy ??? Aidha ni kweli sisi watanzania ni watu wajinga sana pamoja na viongozi wetu, AU kuna kitu kinachoendelea nyuma ya pazia sisi raia wa kawaida hatukioni.

Jambo kubwa zaidi la kujiuliza hapa: Ni kwamba kama mradi wa TVA ambao manufaa yake yanaonekana kwa mamilioni ya wananchi wa Marekani unapigwa vita kali hivi, tena hadi na viongozi wa serikali wakiwemo maraisi, sisi huku kwetu Tanzania tusipingwe kweli ???

Mwaka jana miezi ya mwishoni nilikuwa nafuatilia wanaharakati mitandaoni, nikasikia baadhi wakisema mamilioni ya miti yamekatwa na uharibifu mkubwa wa mazingira umefanyika kwenye mradi wa JNHPP ndiyo maana mvua zimegoma Tanzania.

Lakini, wengine wanasema kwamba JNHPP ni tembo mweupe (A White Elephant Project). Majibu ya Waziri Makamba, yamakuwa yakibadilika-badilika. Lakini naamini, ukweli tutaufahamu tu.

Wanaharakati wetu wangepinga huu mradi (JNHPP) peke yake sisi tungeelewa labda na binafsi ningesema hebu tujifanyie tathmini. Lakini hakuna mradi wowote mkubwa ambao umewahi kufanyika nchini Tanzania bila kupata upinzani mkubwa:

Uwe ni mradi wa msaada, uwekezaji au mkopo. Nasema hili kwa UJASIRI WOTE, kama upo naomba nitajiwe ili nijifunze.

Ukifuatilia kinachoendelea kwa wanasiasa wetu kuna sababu nyingi sana zinazoletwa ambazo hazina kichwa wala miguu.

Wengi wetu ni UJINGA, WOGA, BENDERA FUATA UPEPO lakini kubwa ni ULAJI TU wa watu wachache ambao wamevaa ngozi ya kutunza mazingira, kulinda katiba, matumizi ya mbinu za kisasa za kisayansi na kibiashara kuendesha sekta ya nishati nchini. Lakini ni hivi: UKWELI UKO KAMA MIMBA, HUWEZI KUUFICHA MILELE. Tutafamu tu...

NAMALIZIA NA ETHIOPIA, MRADI WA THE GRAND ETHIOPIAN RENNAISANCE DAM

Ingekuwa Tanzania ndiyo nchi pekee ndiyo inayopigwa vita kwa kuanzisha mradi kama huu ningesema, basi tujifanyie tathmini kidogo.

Ila hadi kule kwa ndugu zetu Ethiopia yametokea machafuko makubwa sana kupinga uanzishwaji wa The Grand Ethiopia Rennaisance Dam (GERD) ambalo litakuwa msaada mkubwa sana kwa mamilioni ya wahabeshi nchini humo.

Upinzani umekuwa mkubwa imefika kipindi kwamba Raisi wa Marekani Donald Trump akaweka bayana kabisa kwamba Misri inaweza kulipua bwana hilo" Egypt might blow up the dam".

WIKILEAKS wanasema kwamba, mradi huu ukimalika hautaisaidia Ethiopia peke yake kuzalisha umeme wa bei ndogo, bali utazalishwa umeme mwingi (Megawatts 5,250) ambao utauzwa hadi nchi jirani kama Sudan na serikali ya Sadani inafahamu hili vizuri kabisa.

Sasa ukifuatilia kwa umakini, kuna wanasiasa wakubwa ambao walisema wazi kwamba mradi wa GERD, hauna manufaa na ni tembo mweupe ( A WHITE ELEPHANT). Moja kati ya watu waliowahi kusema hivi ni Raisi Isaias Afwerki wa Eritrea.

Lakini mradi huu ukikamilika, umeme wa gharama nafuu utafika hadi nchini kwake. Watanzania tujiulize kitu hapa: Kama umeme wa maji siyo wa muda mrefu (Not Sustainable), hivi iweje serikali ya Uchina itupe zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1, ambazo ni sawa na trilioni mbili za kitanzania au zaidi kwenye mradi ?

Asasi za kiraia (NGOs) nazo haziko nyuma katika kutuonesha madhara ya mradi huu wa GERD. NGO maarufu iitwayo INTERNATIONAL RIVERS kutoka California, nchini Marekani iliandaa ripoti kubwa kabisa kuonesha madhara ya mradi huo kwenye mazingira. Wakaenda mbali zaidi na kusema kwamba bwana hili linaweza kuchangia mabadiliko ya hali ya nchi.

Ikumbukwe hawa ndugu zetu wamezungumza sana juu ya miradi ya umeme wa maji nchini Tanzania na Ethiopia.

MWISHO KABISA: MAONI YA WANAZUONI KUHUSU SIASA ZA UMEME NA MABWAWA

Kama umefuatilia siasa za Afrika kwa muda mrefu, utatambua kwamba huu mchezo haujaanza na Tanzania wala Ethiopia. Prof Mike Muller ambaye ni mhandisi kutoka chuo cha Witswatersrand Afrika Kusini, amawahi kuandika na kusema siasa za kupinga miradi mikubwa ya umeme wa maji zilianza mapema nchini Misri kipindi cha Gamal Abdi Nasser ambapo alitaka kujenga bwawa la Aswan (ASWAH HIGH DAM) ambalo lingezalisha MegaWatts 2,100.

Prof Asit K. Biswas amtaalamu wa maji na mazingira, ambaye ndiye anaongoza kwa kufanyiwa rejea za kitaalamu linapokuja suala za mazingira na maji, akishirikiana na Prof Cecilia Tortajada waliandika chapisho ambalo limesema kwamba mradi wa BWAWA LA ASWAN una madhara makubwa kwenye mazingira.

Lakini ukweli ni kwamba wataalamu mradi huo ulipokamilika mwaka 1970, ulikidhi nusu ya mahitaji ya umeme nchini Misri.

Ikimbukwe kwamba siasa za ASWAN HIGH DAM ziliwahi kupelekea Misri ivamiwe kijeshi na Uingereza, Ufaransa na Israeli. Nasser alisema alitaifisha Mfereji wa Suez kwasababu maji yake ni muhimu kwa ujenzi wa bwawa la Aswan.

Nasser aliomba msaada kwa serikali ya Raisi Eisenhower ili kujenga bwana la Aswan, lakini Eisenhower aligoma.

Raisi Kennedy alikosoa sana haya maamuzi ya kuvuruga miradi ya Afrika akisema hivi "When we abruptly abandoned the Aswan Dam in Egypt, the Russians went ahead to finance it. While we starve the Development loan Fund, the Sino-Soviet bloc has already passed us in economic assistance to selected key areas" Hili ndilo lilitokea bwawa lilijengwa na Warusi.

Maajabu barani Afrika huwa hayaishi kabisa: Kinachotushangaza wengi wetu leo hii ni kwamba Misri ambao miaka ya nyumba walionewa katika kujengwa bwawa la Aswan (ASWAN HIGH DAM), leo hii wao nao wakishirikiana na mataifa makubwa nje, wanaharakati na asasi kubwa za kiraia, wanafanya hujuma kubwa sana dhidi ya mradi wa GERD nchini Ethiopia.

NB 1: Siasa kama hizi, zilionekana pia kule nchini GHANA kipindi cha marehemu Nkhrumah ambapo alikuwa anataka kujenga bwawa la AKASOMBO (The Akasombo Dam) ili kuzalisha umeme.

Uliundwa mtandao mkubwa sana wa watu ndani na nje ya nchi ili kumzuia. Muda ni mchache sana siwezi kuzungumza kilichotokea.

NB 2: Fanya utafiti wako kuhusu miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme kupitia maji (TVA, GERD, JNHPP) pia hata ASWAN HIGH DAM na AKASOMBO DAM utatambua kwamba siasa zake zinafanana.

Wahusika ni walewale, wakitumia mbinu zilezile, sema tu huja wakiwa wamevaa vingago (Masks) tofauti-tofati. Kiufupi hizi siasa zinachezwa sana kitaalamu na wengi wetu tunafuata upepo bila kufanya tafiti binafsi.

Mimi siyo mtaalamu sana wa haya mambo, hivyo naomba wale wajuvi wanisaidie zaidi kuelewa. Nitafurahi kurekebishwa na kuelekezwa pale ambapo nimepotoka na kutofahamu kinachoendelea.

CC: JokaKuu , Nguruvi3 , UmkhontoweSizwe , TUJITEGEMEE
Umetangulia kujihami kuwa hauna maarifa ya kutosha eneo la mazingira kijiografia,sasa ni hivi...

☆Miradi ya H.E.P sio rafiki kwa mazingira ktk dunia ya sasa hususani nchi za tropic na semi-arid state.

☆Pili,fahamu kuwa hali ya hewa ya USA na hizi nchi zetu za Africa zilizo karibu na equator ni tofauti sana hasa ktk masuala ya water tap and conservation as per global warming effects.

☆FYI...miradi ya HEP kwa nchi zetu kimazingira na sustainability hasara ni kubwa kuliko faida,ivyo basi SIO SAHIHI KUCHUKUA MIFANO YA USA NA KUIAPPLY AFRIKA MAANA NYAKATI NA MAZINGIRA NI TOFAUTI SANA. Naungana na wataalamu wanaopinga miradi hii kwa Africa.

Ata ivyo wanaopinga hawakuacha kutoa solution mbadala,yaani umeme wa upepo ambao ni cheaper na more efficient.
 
Umetangulia kujihami kuwa hauna maarifa ya kutosha eneo la mazingira kijiografia,sasa ni hivi...

☆Miradi ya H.E.P sio rafiki kwa mazingira ktk dunia ya sasa hususani nchi za tropic na semi-arid state.

☆Pili,fahamu kuwa hali ya hewa ya USA na hizi nchi zetu za Africa zilizo karibu na equator ni tofauti sana hasa ktk masuala ya water tap and conservation as per global warming effects.

☆FYI...miradi ya HEP kwa nchi zetu kimazingira na sustainability hasara ni kubwa kuliko faida,ivyo basi SIO SAHIHI KUCHUKUA MIFANO YA USA NA KUIAPPLY AFRIKA MAANA NYAKATI NA MAZINGIRA NI TOFAUTI SANA. Naungana na wataalamu wanaopinga miradi hii kwa Africa.

Ata ivyo wanaopinga hawakuacha kutoa solution mbadala,yaani umeme wa upepo ambao ni cheaper na more efficient.

Nashukuru sana mtaalam, lakini ningeomba unifahamishe zaidi. Kwanini sehemu za Afrika kama Misri walisema kuna madhara lakini faida zimekuwa ni kubwa zaidi kuliko hizo hasara ??? Lakini pia niulize, hivi kila mradi wa umeme uliopo hapa barani Afrika umechangia kwa kiasi gani kuharibu mazingira AS PER GLOBAL WARMING EFFECTS ???
 
Kama kuna jambo la kumshukuru E.Lowassa ni jinsi alivyosimamia na kuiwekea ngumu Egypt iliyotumika mkataba wa 1929 na kutaka tuchimbe visima ili wao wapate maji ya kumwagilia
Nguruvi3, asante kwa comment nzuri sana na ambazo zinakubaliana na maoni ya baadhi yetu kuwa shida ya maamuzi muhimu katika Taifa letu ni siasa kutangulia utaalam.
Halafu ningependa kukufahamisha kuwa nchi zote za Africa ambazo Nile imepitia au zina maziwa ambayo ni Nile-feeders, zinachezewa mchezo mbaya sana na Egypt. Mwanasiasa yeyote atakayetaka kutumia maji ya Nile kwa wingi, kama kumwagilia na/au kufua umeme, Egypt iko tayari kuhakikisha anafanyiwa zengewe la kummaliza kisiasa au hata kuuwawa. La kwanza ndilo lililomkuta Lowasa. Lakini lilifanyika kisiri sana kupitia siasa na watu waliokuwa wamelipwa. Sasa hivi wameweza kupenyeza vizuri mno ndani ya siasa zetu, dhubutu atoke mwanasiasa ajaribu ku-support miradi kama iliyokuwa inapendekezwa na Lowassa, hata kwa kutamka nia tu, hatamaliza mwaka. Ili kuua miradi kama hiyo huku kwetu huwa wanajifanya wanatoa ufadhili na fedha za miradi ya kuchimba visima vya maji. Iko kama tunaambiwa, "nyie kiuchumi hamtakiwi kupiga hatua kutuzidi sisi, tulieni kwanza sisi tusonge mbele halafu tutawambia wapi muelekee" Na sisi kupitia siasa zetu tumekubali.
 
Tenesse Valley Authority (TVA) haikuwa mahususi kwa ajili ya kuzalisha umeme bali kuinua uchumi wa maeneo yanayoizunguka kupitia usafiri wa majini, uwekezaji wa viwanda vya mbolea,mipango mji na pia kupambana na mafuriko.Hii ni tofauti sana na bwawa la Stiglerz ambalo uharibifu mkubwa wa mazingira unafanyika kuzalisha umeme ambao ungeweza kuzalishwa na kuzidi kwa gesi na vyanzo vingine vya nishati mbadala.
Umeisoma sheria iliyoanzisha hii mamlaka ???
 
Unapofanya miradi mikubwa ya nchi hutakiwi kuangalia gharama nafuu kwa wananchi, kuna mambo mengine mengi mtambuka ya muhumu yanayopaswa kutazamwa kwa kina.
Management ya uchumi inatakiwa ifanyike katika level ya macro sio micro.

Gesi ingesimamiwa vizuri ingezalisha umeme mwingi kuliko wa Stiglers hata kama ungekuwa wa bei juu kidogo, gesi ingezalisha maelfu ya ajira za moja kwa moja na laki za ajira indrect, gesi ingefungua uchumi wa kusini eneo ambalo liko nyuma sana kimaendeleo, gesi ingeleta kodi kwenye uchumi wa nchi. Umeme wa Stiglers zaidi ya porojo za kuwa wa bei nafuu hautukapa hizi faida nyingine za moja kwa moja kwa uhakika.
Unafahamu dhumuni la kuwa na SOEs ndani ya nchi ???
 
Umetangulia kujihami kuwa hauna maarifa ya kutosha eneo la mazingira kijiografia,sasa ni hivi...

☆Miradi ya H.E.P sio rafiki kwa mazingira ktk dunia ya sasa hususani nchi za tropic na semi-arid state.

☆Pili,fahamu kuwa hali ya hewa ya USA na hizi nchi zetu za Africa zilizo karibu na equator ni tofauti sana hasa ktk masuala ya water tap and conservation as per global warming effects.

☆FYI...miradi ya HEP kwa nchi zetu kimazingira na sustainability hasara ni kubwa kuliko faida,ivyo basi SIO SAHIHI KUCHUKUA MIFANO YA USA NA KUIAPPLY AFRIKA MAANA NYAKATI NA MAZINGIRA NI TOFAUTI SANA. Naungana na wataalamu wanaopinga miradi hii kwa Africa.

Ata ivyo wanaopinga hawakuacha kutoa solution mbadala,yaani umeme wa upepo ambao ni cheaper na more efficient.
Ungefafanua huo uharibifu wa mazingira ni upi ambao gas hauufanyi ila maji ya umeme ndiyo inafanya....Hapa umezungusha tu maneno hujaweka facts
 
Nguruvi3, asante kwa comment nzuri sana na ambazo zinakubaliana na maoni ya baadhi yetu kuwa shida ya maamuzi muhimu katika Taifa letu ni siasa kutangulia utaalam.
Halafu ningependa kukufahamisha kuwa nchi zote za Africa ambazo Nile imepitia au zina maziwa ambayo ni Nile-feeders, zinachezewa mchezo mbaya sana na Egypt. Mwanasiasa yeyote atakayetaka kutumia maji ya Nile kwa wingi, kama kumwagilia na/au kufua umeme, Egypt iko tayari kuhakikisha anafanyiwa zengewe la kummaliza kisiasa au hata kuuwawa. La kwanza ndilo lililomkuta Lowasa. Lakini lilifanyika kisiri sana kupitia siasa na watu waliokuwa wamelipwa. Sasa hivi wameweza kupenyeza vizuri mno ndani ya siasa zetu, dhubutu atoke mwanasiasa ajaribu ku-support miradi kama iliyokuwa inapendekezwa na Lowassa, hata kwa kutamka nia tu, hatamaliza mwaka. Ili kuua miradi kama hiyo huku kwetu huwa wanajifanya wanatoa ufadhili na fedha za miradi ya kuchimba visima vya maji. Iko kama tunaambiwa, "nyie kiuchumi hamtakiwi kupiga hatua kutuzidi sisi, tulieni kwanza sisi tusonge mbele halafu tutawambia wapi muelekee" Na sisi kupitia siasa zetu tumekubali.
Ila wakumbuke siyo miungu wao, ipo weak point yao huwa equation zao huwa zinakataa...God has never left this world to rule by itself...Historia ni mwl mzuri; Egypt iliyotikisa enzi za Yesu leo ipo wapi? Roma iliyotikisa enzi za mafarisayo leo iko wapi...Africa ndiyo ilianza kuebselea kabla ya hizo sehemu zingine na mzunguko unakaribia kutufikia
 
Mkuu MALCOM LUMUMBA nimelisoma bandiko lako kwa umakini.

1. Nimsahihishe Stuxnet bandiko#53. Stigler's Gorge haikuanza na Mwalimu, ilikuwepo' 1936'' n

2.Siasa za Marekani ni '' complex and complicated''. Prof P. Navarro wa UCLA ame publish sana climate change. Alipochaguliwa mshauri wa Trump, Navarro akawa mpinzani wa climate change.

TVA ina vitu vingi ndani, hoja ya wanaharakati ni uharibifu wa mazingira, si unafuu wa umeme

Siasa za Marekani zinategemea masilahi. Obama alizuia Iran NUKE deal kwa mkataba.
Trump akafuta mkataba. Obama alikuwa against war. Trump alikuwa pro BB Nyahu.
Katika hali zote objective ni moja kumlinda Israel na ''maadui' au majirani kama Iran na Egypt

3. Egypt na US zina masiahi yanayolenga amani ya Israel. US wanaunga mkono Egypt ''kubomoa GERD ya Ethiopia''. Mradi wa GERD utaathiri blue Nile na mwathirika ni Egypt katika kila nyanja. Vita ya GERD inalenga hapo tu

Vita kama ya GERD mbona ilitupata Tanzania?
Kuvuta maji kutoka ziwa Victoria ilikuwa vurugu kutoka Egypt.

Kama kuna jambo la kumshukuru E.Lowassa ni jinsi alivyosimamia na kuiwekea ngumu Egypt iliyotumika mkataba wa 1929 na kutaka tuchimbe visima ili wao wapate maji ya kumwagilia.

Katika sakata la maji ya Victoria , US ilijifanya msuluhishi lakini ilikuwa upande wa Egypt
Ndicho chanzo cha kuanzishwa kwa NBI (Nile Basin Initiative)

4. China kutoa Billions hailalishi mradi. Pesa ni mkopo, mbinu ya China kupata malighafi na masoko ya Afrika. Hoja kwamba China ingalikataa kama JNHPP ni mradi mbaya haina mashiko.

5. Njia za kisayansi: Hatuna sera za kitaifa za nishati. Mpango wa gesi nishati na matumizi ya ndani umeishaje, ghafla JNHPP. Tungetumia njia za kisayansi tungefanya yote kwa mpangilio.

6. Wanharakati: Wanalaumiwa ingawa tunajua ukweli. Mtera na Kidatu yanajaa mchanga kwasababu ya shughuli za binadamu ikiwemo kuharibu vyanzo vya maji. Upatikanaji wa mvua unaathiriwa na deforestation. Tunatumia njia gani kuondoa hali hiyo isije kujirudia JNHPP?

7. Hoja ya wanaharakati ni athari katika eco-system. Nimesoma hoja za tafiti sijaona hoja mbadala zinazopinga. Ninachokiona ni hoja kutoka mtaa wa Lumumba katika lahaja za mashari na tungo.

Naamini ''Hydro power'' ni sehemu ya suluhisho la matatizo yetu na tulijadili miaka mingi hapa JF.
Ninapinga approach ya kukomoana. Tulibadilikaje usiku mmoja kutoka gesi na kwenda JNHPP?
Je, kulikuwa na mjadala wa kutosha na maandalizi ?
kilichotokea ni kama kile cha Bandari ya Bagamoyo '' knee jerk reaction'

Tuna matatizo yetu, bahati mbaya tupo katika denial. Miaka 60 tunasingizia influence za nje

Nashukuru kwa mchango wako mzito mkuu Nguruvi. Umezungumzia mambo mengi sana na kuna baadhi ya sehemu nadhani hatujaelewana vizuri. Lakini haya tuyaache tujikite kwenye hoja ya msingi kabisa: UMEME WA MAJI. Tukiacha siasa za matumbo, kufuata upepo na propaganda, umeme wa maji unatoa suluhisho la muda mrefu na salama kwa mazingira.

Jambo jingine muhimu, makosa aliyofanya Raisi Magufuli kuhusu huu mradi hayageuzi huu mradi kuwa haramu:Masuala kama fedha za huu mradi, kutelekeza miradi mingine muhimu ya umeme kama ule wa gesi na siasa za kukomoana. Hoja hii tumeizungumza hadi kwenye mradi wa Bandari ya Bagamoyo, ambapo tulisema makosa ya ndugu Jakaya hayageuzi huu mradi kuwa haramu. Siasa za kusema kwamba umeme wa maji hautumiki dunia ya leo wengi tunazishangaa kidogo. Tungeelewa labda pale watu wanasema kwamba ujenzi wa JNHPP ni hatari kwasababu umefanywa ndani ya hifadhi. Lakini siyo kutuambia kwamba umeme wa maji ni hatari kwa dunia ya sasa. Hapa tuwaeleweje labda ???

Lakini pili, nilitoa mfano wa TVA kuonesha kwamba kuna mabwawa ya umeme zaidi ya 20 lakini hayaleti madhara kwenye mazingira kama tunavyoambiwa. Wanaharakati wanachopinga pale ni uzalishaji wa umeme kupitia makaa ya mawe. Upande mwingine ile ni SOE hivyo ina madeni ambayo serikali imeona kuwa ni mzigo, hivyo wanataka kubinafsisha. Mwisho kabisa, ukifuatilia vizuri utafahamu kwamba huu mradi ulianza kupingwa na makampuni binafsi kwasababu yalisema TVA itakuwa ni GOVERNMENT MONOPOLY. Mbona hili liko wazi ???

Lakini tatu, nimesoma chapisho ambalo lilisema kwamba ASWAN HIGH DAM ni janga la kimazingira. Nikaenda zaidi kuweka hadi waandishi, ila mwishoni inaonekana kwamba matokeo yake ule mradi ni mazuri kiuchumi hadi kimazingira. Aliyeyasema haya naye ni mtaalamu ambaye alifanya utafiti wake na nimemuweka hapa. Mambo kama haya yamekuwepo sana hapa Afrika, binafsi siyazungumzii kwasababu nataka kunyoosha kidole kwa wazungu la hasha. Wewe umekuwepo hapa Tanzania kwa muda mrefu, unafahamu dhahiri maneno ya wataalamu naupinzani kutoka nje yamekuwepo tokea tunaanza kufanya miradi kama TAZARA. Sasa hapa utasemaje nawalaumu watu wa nje ilhali huo ndiyo ukweli ???
 
Wazungu husema hivi "Once is an accident, Twice is a Coincidence, but Thrice is a Pattern".

Hapa namaanisha nini, duniani kote ambako miradi ya namna hii yenye lengo la kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini lazima kuwepo na malalamiko.

Tena nimefuatilia kwa umakini na kufahamu kwamba malalamiko hayo ni lazima yafanane. Mbaya zaidi makundi ya wanaoleta haya malalamiko huwa ni ya watu wa aina ileile, tena huja na sababu zilezile.

Ukifuatilia kwa umakini, utatambua kwamba mfanano wa hawa watu ni mkubwa sana hadi utakubaliana na ule msemo wa kiingereza kwamba "History does not repeat itself, but people do repeat themselves".

Fanya utafiti wako binafsi, utakubaliana na nilichokiandika hapa.

Muda ni mchache, leo hii ntazungumzia nchi tatu ambazo ni Marekani, Ethiopia na Tanzania. Ambako kote katika nyakati tofauti kumekuwa na miradi mikubwa ya kuzalisha umeme wa maji ambao kwa mkono wa serikali, ambayo imelenga kuzalisha umeme wa gharama nafuu kwa wananchi huku miradi hiyo ikiendeshwa na serikali.

Hapa nazungumzia miradi ya The Tennessee valley Hydro-electric Power Projects (TVA), The Grand Ethiopian Rennaisance Dam (GERD) na Julius Nyerere Hydro- Power Project (JHPP).

Nimefuatilia kwa karibu nimeona kwenye hii miradi ya TVA, GERD na JNHPP ni lazima utakutana na majina kama WHITE-ELEPHANTS, DEBT-RIDDEN PROJECTS, UNSUSTAINABLE ENERGY SOURCE, ENVIROMENTAL HAZARDOUS, GOVERNMENT MONOPOLY, UNCOMPETITIVE SOEs na SOCIALIST EMBARKED PROJECT.

Mpaka sasa sijafahamu kwanini tokea kule Marekani, Ethiopia hadi Tanzania mambo yafanane hivi. Imetokea TVA (Once=An Accident), Imetokea GERD (Twice= A Coincidence) na Imetokea Tanzania (Thrice= A Pattern).

Pia sehemu nyinginezo yanaendelea kutoka tu, mpaka najiuliza nini hiki. Labda, huenda ni mawazo yangu hafifu tu, ambapo wazungu husema "A figment of your own imagination"

HEBU TUANGALIE MRADI WA UMEME CHINI YA TENNESSEE VALLEY AUTHORITY

Raisi Franklin Delano Roosevelt alianzisha The Tennessee Valley Authority (TVA) mwaka 1933 ili kuwezesha Marekani izalishe umeme wa bei ndogo ambao utasaidia majimbo kama saba ambayo yanazunguka lile eneo.

Lengo kubwa ni kusaidia kiuchumi ukanda ambao uliachwa nyumba kimandeleo, kutoa ajira kwa vijana na kusukuma uchumi wa viwanda eneo hilo.

Tokea mwaka 1933 mpaka sasa Marekani imefanikiwa kutengeneza mabwawa 50 ambayo yanasaidia kuzalisha umeme wa bei ndogo unaotumika kuendesha viwanda na uchumi wa majimbo karibia saba ya eneo ambalo bonde la Tennessee limepita.

Ila huwezi amini mpaka leo hii mwaka 2022, wanaharakati wa kimazingira wanapinga huu mradi kwa kusema unaleta madhara.

Wakati nasoma shule kuhusu huu mradi, tuliambiwa kwamba ulipigwa vita sana na makampuni binafsi ya umeme, wanasiasa, wanaharakati na wanasheria.

Ambapo walitumia mbinu mbalimbali kufanikisha hujuma dhidi ya huu mradi lakini hawakufanikiwa. Sababu kubwa ni kwamba raia wengi wa Marekani walikuwa ni watu wanaojielewa mno, siyo wajinga wanaopelekeshwa bila kufahamu linaloendelea (Dumbed-Down Citizenry) nchini kwao.

Upinzani haukishia kwenye uanzishwaji wa huu mradi mwaka 1933, mwaka 1936 mmoja wa wamiliki wa hisa kwenye kampuni binafsi la umeme THE ALABAMA POWER COMPANY aitwaye ASHWANDER alipeleka kesi mahakamani kuzuia serikali kuuza umeme kupitia The Tennessee Valley Authority (TVA) akisema kwamba serikali haitakiwi kabisa kuuza umeme hivyo kuna uvunjifu wa katiba ya Marekani.

Unaweza kutafuta kesi ya: Ashwander V Tennessee Valley Authority (1936)

Mahakama ya juu ya Marekani ilikataa na kusema uzalishaji huu wa umeme siyo wa faida tu, bali ulilenga kutoa huduma kwa kukuza uchumi wa eneo ambalo lilikuwa nyuma kimaendeleo na kuimarisha ulinzi wa nchi kwasababu viwanda vya silaha vilikuwepo eneo hilo.

Hivyo mabwanyeye wakapigwa chini na serikali inauza umeme kwa raia mpaka leo hii. Ikumbukwe inayofanya hivi ni serikali ya Kibeberu ya ulimwengu wa kwanza na siyo serikali ya Kijamaa ya ulimwengu wa tatu.

Wamarekani zaidi ya milioni 9 wanapata huduma ya umeme nafuu kutoka kwenye miradi 29 ya umeme wa maji kutoka Tennessee Valley Authority (TVA).

Kubwa zaidi ni kwamba huduma ya umeme kwenye majimbo hayo yanayopitiwa na bonde la Tennessee ni moja kati ya umeme wenye gharama nchini Marekani, kama siyo ndiyo wenye gharama nafuu zaidi kwenye nchi hiyo.

Kitakachoshangaza watu werevu ni kwamba PROPAGANDA CHAFU na UZANDIKI dhidi ya mradi huu hazijaisha tokea mwaka 1936. Raisi Dwight Eisenhower alishawahi kuutukana huu mradi kwa kuuita maneno kama "Ujamaa nyemelevu" (Creeping Socialism), ilhali mamilioni ya Wamarekani ni wanufaika.

Maneno kama haya hayatakiwi kabisa kutoka kwenye kinywa cha mkuu wa nchi mwenye lengo la kuwakwamua kiuchumi raia wa kawaida, kwasababu faida za mradi ni dhahiri kwa watu wote.

Lengo la Raisi Eisenhower lilikuwa siyo kupinga UJAMAA bali ni kubinafsisha (TVA), lakini akakumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa wazalendo wa kimarekani na mwishowe akawa mpole.

Kilichomshangaza zaidi ni kwamba waliompinga ni wenzake kutoka REPUBLICAN PARTY ambao husifika kwa kuchukia UJAMAA hasa pale ambapo serikali yenyewe hufanya biashara. Nini kilipelekea Raisi na jopo la wataalamu wake kupingwa hivi ???

Sasa kubwa na baya zaidi dhidi ya mradi huu ni lile la mwaka 2013, ambapo Raisi Barrack Obama aliandaa muswada ili kubinafsisha The Tennessee Valley Authority (TVA) kwa watu binafsi.

Moja ya sababu kubwa ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ni kwamba mamlaka ya Tennessee Valley (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni mzigo kwa serikali.

Walikuwa na hoja nzito sana maana ukweli ni kwamba mamlaka hiyo (TVA) ina madeni makubwa ambayo ni takribani dola za kimarekani bilioni 25.

Lakini hili halikuwa sababu ya kusema kwamba serikali ibinafsishe shirika hili la kiserikali na kuwaumiza raia wapatao milioni 9 kwa kupanda kwa gharama za umeme.

Sababu ya pili ambayo Raisi Obama na washauri wake waliitoa ili kufanikisha ubinafsishwaji wa The Tennessee Valley Authority (TVA) ni ile ambayo hata kwetu huku inatusumbua ya kutunza mazingira.

TVA mbali na miradi 29 ya umeme wa maji, imeongeza pia miradi 12 ya umeme wa makaa ya mawe, miradi 3 ya umeme wa nyuklia, miradi 15 ya umeme wa gesi na mradi 1 wa umeme wa upepo.

Inasemekana TVA inahitaji dola za kimarekani bilioni 25 ili kupunguza uchafuzi wa mazingira unaosababisha na huu mradi hasa kutoka kwenye vinu vya makaa ya mawe. Hivyo ili serikali isiingie kwenye hizi gharama zisizo za msingi, basi ni kheri ibinafsishe tu shirika hili.

Kuna nchi fulani hivi viongozi wake, wasomi na wafanyabiashara wanapenda kuzungumza kauli kama hizi za Raisi Barrack Obama na Dwight Eisenhower, bila shaka ndugu msomaji utakuwa unaifahamu.

Hivyo njia rahisi kwa Serikali ya Raisi Obama, kukwepa deni kubwa la TVA na gharama za marekebisho, wakaona ni bora wauze hii SOE (State Owned Enterprise).

Ila ukweli mchungu ni kwamba wangefanya hivyo ina maana gharama za umeme kwa wananchi wa Marekani zaidi ya milioni 9 ingepanda sana na wangeathiri biashara nyingi na maisha ya raia wa kawaida.

Mbali na madhaifu yake mengi, Marekani ni taifa ambalo raia wake wengi wanajielewa mno.

Wahafidhina wa chama cha REPUBLICAN hasa wawakilishi kutoka majimbo hayo, pamoja na watu binafsi walipinga kwa nguvu mswada ambao ungefanikisha ubinafsishwaji wa kiholela wa hii mamlaka ambayo lengo lake kuu ni kutoa huduma kwa raia na kuimarisha ulinzi wa nchi.

HEBU TURUDI NCHINI TANZANIA SASA, TUANGALIE TANESCO NA JNHPP

Bunge la Marekani lilichofanya ni kukataa mamalaka isiuzwe na kuiwekea ukomo wa deni, ambayo mamlaka haitakiwi kuvuka, ambapo ukomo ni dola za kimarekani bilioni 30.

Hivyo madeni hayapo tu kwenye shirika letu la TANESCO lakini hata TVA wana madeni tena yanakera. Sisemi haya kusema TANESCO inafanya vizuri, la hasha kuna mambo mengi ya ajabu yanafanyika.

Lakini naamini wakijipanga vizuri na kupunguza siasa tunaweza kufika sehemu nzuri sana. Mbona TVA wafananya vizuri na bado ni shirika la serikali ???

Jambo jingine ambalo nalisikia sana nchini Tanzania ni hilo la kusema umeme wa maji siyo endelev. Mimi siyo mtaalamu lakini naweza kufahamu wapi nadanganywa, kiukweli hili linanipa ukakasi mkubwa sana.

Mradi wa TVA umeanza mwaka 1933 na upo hadi leo hii, utasemaje kwamba umeme wa maji siyo endelevu jamani ???

Unaweza kumtukana Raisi Magufuli kwamba ni mjinga, lakini kumbuka huu mpango wa JNHPP umekuwepo tokea enzi za Mzee Nyerere, Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa, ina maana hawa wote na wataalamu wao walikuwa ni wajinga kabisa wasitambue kwamba Hydro-Electric Power is not sustainable source of energy ??? Aidha ni kweli sisi watanzania ni watu wajinga sana pamoja na viongozi wetu, AU kuna kitu kinachoendelea nyuma ya pazia sisi raia wa kawaida hatukioni.

Jambo kubwa zaidi la kujiuliza hapa: Ni kwamba kama mradi wa TVA ambao manufaa yake yanaonekana kwa mamilioni ya wananchi wa Marekani unapigwa vita kali hivi, tena hadi na viongozi wa serikali wakiwemo maraisi, sisi huku kwetu Tanzania tusipingwe kweli ???

Mwaka jana miezi ya mwishoni nilikuwa nafuatilia wanaharakati mitandaoni, nikasikia baadhi wakisema mamilioni ya miti yamekatwa na uharibifu mkubwa wa mazingira umefanyika kwenye mradi wa JNHPP ndiyo maana mvua zimegoma Tanzania.

Lakini, wengine wanasema kwamba JNHPP ni tembo mweupe (A White Elephant Project). Majibu ya Waziri Makamba, yamakuwa yakibadilika-badilika. Lakini naamini, ukweli tutaufahamu tu.

Wanaharakati wetu wangepinga huu mradi (JNHPP) peke yake sisi tungeelewa labda na binafsi ningesema hebu tujifanyie tathmini. Lakini hakuna mradi wowote mkubwa ambao umewahi kufanyika nchini Tanzania bila kupata upinzani mkubwa:

Uwe ni mradi wa msaada, uwekezaji au mkopo. Nasema hili kwa UJASIRI WOTE, kama upo naomba nitajiwe ili nijifunze.

Ukifuatilia kinachoendelea kwa wanasiasa wetu kuna sababu nyingi sana zinazoletwa ambazo hazina kichwa wala miguu.

Wengi wetu ni UJINGA, WOGA, BENDERA FUATA UPEPO lakini kubwa ni ULAJI TU wa watu wachache ambao wamevaa ngozi ya kutunza mazingira, kulinda katiba, matumizi ya mbinu za kisasa za kisayansi na kibiashara kuendesha sekta ya nishati nchini. Lakini ni hivi: UKWELI UKO KAMA MIMBA, HUWEZI KUUFICHA MILELE. Tutafamu tu...

NAMALIZIA NA ETHIOPIA, MRADI WA THE GRAND ETHIOPIAN RENNAISANCE DAM

Ingekuwa Tanzania ndiyo nchi pekee ndiyo inayopigwa vita kwa kuanzisha mradi kama huu ningesema, basi tujifanyie tathmini kidogo.

Ila hadi kule kwa ndugu zetu Ethiopia yametokea machafuko makubwa sana kupinga uanzishwaji wa The Grand Ethiopia Rennaisance Dam (GERD) ambalo litakuwa msaada mkubwa sana kwa mamilioni ya wahabeshi nchini humo.

Upinzani umekuwa mkubwa imefika kipindi kwamba Raisi wa Marekani Donald Trump akaweka bayana kabisa kwamba Misri inaweza kulipua bwana hilo" Egypt might blow up the dam".

WIKILEAKS wanasema kwamba, mradi huu ukimalika hautaisaidia Ethiopia peke yake kuzalisha umeme wa bei ndogo, bali utazalishwa umeme mwingi (Megawatts 5,250) ambao utauzwa hadi nchi jirani kama Sudan na serikali ya Sadani inafahamu hili vizuri kabisa.

Sasa ukifuatilia kwa umakini, kuna wanasiasa wakubwa ambao walisema wazi kwamba mradi wa GERD, hauna manufaa na ni tembo mweupe ( A WHITE ELEPHANT). Moja kati ya watu waliowahi kusema hivi ni Raisi Isaias Afwerki wa Eritrea.

Lakini mradi huu ukikamilika, umeme wa gharama nafuu utafika hadi nchini kwake. Watanzania tujiulize kitu hapa: Kama umeme wa maji siyo wa muda mrefu (Not Sustainable), hivi iweje serikali ya Uchina itupe zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1, ambazo ni sawa na trilioni mbili za kitanzania au zaidi kwenye mradi ?

Asasi za kiraia (NGOs) nazo haziko nyuma katika kutuonesha madhara ya mradi huu wa GERD. NGO maarufu iitwayo INTERNATIONAL RIVERS kutoka California, nchini Marekani iliandaa ripoti kubwa kabisa kuonesha madhara ya mradi huo kwenye mazingira. Wakaenda mbali zaidi na kusema kwamba bwana hili linaweza kuchangia mabadiliko ya hali ya nchi.

Ikumbukwe hawa ndugu zetu wamezungumza sana juu ya miradi ya umeme wa maji nchini Tanzania na Ethiopia.

MWISHO KABISA: MAONI YA WANAZUONI KUHUSU SIASA ZA UMEME NA MABWAWA

Kama umefuatilia siasa za Afrika kwa muda mrefu, utatambua kwamba huu mchezo haujaanza na Tanzania wala Ethiopia. Prof Mike Muller ambaye ni mhandisi kutoka chuo cha Witswatersrand Afrika Kusini, amawahi kuandika na kusema siasa za kupinga miradi mikubwa ya umeme wa maji zilianza mapema nchini Misri kipindi cha Gamal Abdi Nasser ambapo alitaka kujenga bwawa la Aswan (ASWAH HIGH DAM) ambalo lingezalisha MegaWatts 2,100.

Prof Asit K. Biswas amtaalamu wa maji na mazingira, ambaye ndiye anaongoza kwa kufanyiwa rejea za kitaalamu linapokuja suala za mazingira na maji, akishirikiana na Prof Cecilia Tortajada waliandika chapisho ambalo limesema kwamba mradi wa BWAWA LA ASWAN una madhara makubwa kwenye mazingira.

Lakini ukweli ni kwamba wataalamu mradi huo ulipokamilika mwaka 1970, ulikidhi nusu ya mahitaji ya umeme nchini Misri.

Ikimbukwe kwamba siasa za ASWAN HIGH DAM ziliwahi kupelekea Misri ivamiwe kijeshi na Uingereza, Ufaransa na Israeli. Nasser alisema alitaifisha Mfereji wa Suez kwasababu maji yake ni muhimu kwa ujenzi wa bwawa la Aswan.

Nasser aliomba msaada kwa serikali ya Raisi Eisenhower ili kujenga bwana la Aswan, lakini Eisenhower aligoma.

Raisi Kennedy alikosoa sana haya maamuzi ya kuvuruga miradi ya Afrika akisema hivi "When we abruptly abandoned the Aswan Dam in Egypt, the Russians went ahead to finance it. While we starve the Development loan Fund, the Sino-Soviet bloc has already passed us in economic assistance to selected key areas" Hili ndilo lilitokea bwawa lilijengwa na Warusi.

Maajabu barani Afrika huwa hayaishi kabisa: Kinachotushangaza wengi wetu leo hii ni kwamba Misri ambao miaka ya nyumba walionewa katika kujengwa bwawa la Aswan (ASWAN HIGH DAM), leo hii wao nao wakishirikiana na mataifa makubwa nje, wanaharakati na asasi kubwa za kiraia, wanafanya hujuma kubwa sana dhidi ya mradi wa GERD nchini Ethiopia.

NB 1: Siasa kama hizi, zilionekana pia kule nchini GHANA kipindi cha marehemu Nkhrumah ambapo alikuwa anataka kujenga bwawa la AKASOMBO (The Akasombo Dam) ili kuzalisha umeme.

Uliundwa mtandao mkubwa sana wa watu ndani na nje ya nchi ili kumzuia. Muda ni mchache sana siwezi kuzungumza kilichotokea.

NB 2: Fanya utafiti wako kuhusu miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme kupitia maji (TVA, GERD, JNHPP) pia hata ASWAN HIGH DAM na AKASOMBO DAM utatambua kwamba siasa zake zinafanana.

Wahusika ni walewale, wakitumia mbinu zilezile, sema tu huja wakiwa wamevaa vingago (Masks) tofauti-tofati. Kiufupi hizi siasa zinachezwa sana kitaalamu na wengi wetu tunafuata upepo bila kufanya tafiti binafsi.

Mimi siyo mtaalamu sana wa haya mambo, hivyo naomba wale wajuvi wanisaidie zaidi kuelewa. Nitafurahi kurekebishwa na kuelekezwa pale ambapo nimepotoka na kutofahamu kinachoendelea.

CC: JokaKuu , Nguruvi3 , UmkhontoweSizwe , TUJITEGEMEE


Mkuu hongera Sana Kwa uchambuzi wa kina ulioufanya. Nimejifunza mambo mengi mno.

Ubinafsi ndio tatizo letu kuu
 
Umetangulia kujihami kuwa hauna maarifa ya kutosha eneo la mazingira kijiografia,sasa ni hivi...

☆Miradi ya H.E.P sio rafiki kwa mazingira ktk dunia ya sasa hususani nchi za tropic na semi-arid state.

☆Pili,fahamu kuwa hali ya hewa ya USA na hizi nchi zetu za Africa zilizo karibu na equator ni tofauti sana hasa ktk masuala ya water tap and conservation as per global warming effects.

☆FYI...miradi ya HEP kwa nchi zetu kimazingira na sustainability hasara ni kubwa kuliko faida,ivyo basi SIO SAHIHI KUCHUKUA MIFANO YA USA NA KUIAPPLY AFRIKA MAANA NYAKATI NA MAZINGIRA NI TOFAUTI SANA. Naungana na wataalamu wanaopinga miradi hii kwa Africa.

Ata ivyo wanaopinga hawakuacha kutoa solution mbadala,yaani umeme wa upepo ambao ni cheaper na more efficient.
Hao wanaopinga huo mradi ni wapumbavu na wanatoa hoja za kipumbavu na nyepesi sana!

Huo mradi umechukua kaeneo kadogo sana ukilinganisha na maelfu kwa malaki ya eka zinazoendelea kupandwa miti kila siku hapa nchini.

Nenda kule iringa na mikoa mingine uone watu wanavyootesha miti kama hawana akili nzuri. Sasa hako kaeneo kadogo kujenga bwawa litakalo tuletea manufaa makubwa kama taifa utasemaje kana haribu mazingira?

Hao wana harakati uchwara wamejifungia ofisini kwenye viyoyozi hawajui chochote zaidi ya porojo tu
 
Unapofanya miradi mikubwa ya nchi hutakiwi kuangalia gharama nafuu kwa wananchi, kuna mambo mengine mengi mtambuka ya muhumu yanayopaswa kutazamwa kwa kina.
Management ya uchumi inatakiwa ifanyike katika level ya macro sio micro.

Gesi ingesimamiwa vizuri ingezalisha umeme mwingi kuliko wa Stiglers hata kama ungekuwa wa bei juu kidogo, gesi ingezalisha maelfu ya ajira za moja kwa moja na laki za ajira indrect, gesi ingefungua uchumi wa kusini eneo ambalo liko nyuma sana kimaendeleo, gesi ingeleta kodi kwenye uchumi wa nchi. Umeme wa Stiglers zaidi ya porojo za kuwa wa bei nafuu hautukapa hizi faida nyingine za moja kwa moja kwa uhakika.
Gesi imeshauzwa
 
Mqkamba kawekwa hapo Kama mtego huonmradi ukifeli ndio utampoteza makmba kwemy siasa

Mam mjanja kamuweka ili amalize kisiasa huyu makamba
 
Umetangulia kujihami kuwa hauna maarifa ya kutosha eneo la mazingira kijiografia,sasa ni hivi...

☆Miradi ya H.E.P sio rafiki kwa mazingira ktk dunia ya sasa hususani nchi za tropic na semi-arid state.

☆Pili,fahamu kuwa hali ya hewa ya USA na hizi nchi zetu za Africa zilizo karibu na equator ni tofauti sana hasa ktk masuala ya water tap and conservation as per global warming effects.

☆FYI...miradi ya HEP kwa nchi zetu kimazingira na sustainability hasara ni kubwa kuliko faida,ivyo basi SIO SAHIHI KUCHUKUA MIFANO YA USA NA KUIAPPLY AFRIKA MAANA NYAKATI NA MAZINGIRA NI TOFAUTI SANA. Naungana na wataalamu wanaopinga miradi hii kwa Africa.

Ata ivyo wanaopinga hawakuacha kutoa solution mbadala,yaani umeme wa upepo ambao ni cheaper na more efficient.

Mkulu, Nina hamu sana kujua madhara ya miradi ya HEP kwa mazingira.

Lingine ni kuwa, kama kule jangwani Misri wanatumia Aswan dam with very little effect of evaporation. What about the place where there is a double maxima rainfall!!?
 
Mkuu huku tunakorudi hatutapiga hatua, ni sawa na kukanyaga mafuta mengi wakati gari iko kwenye free gear!
Hiyo power master plan yenyewe mwendazake aliibadilisha akaweka huo mradi..
Mjadala nadhani ungekua kwamba;
※ Kwanini aliamua kufinance hiyo project kwa mikopo ya kibiashara tena ya muda mfupi na riba kubwa. Juzi tumeambiwa marejesho yameshaanza na project haijakamilika ikabidi tutumie mkopo mwingine kulipa huo mkopo kitu ambacho nakiona kama ukichaa!
Umesikia wapi kua ni mikopo ya muda mfupi?can you provide proof ya haya uyasemayo? au ni maneneo tu ya kuskia aka Umbea?
Mradi hauna ht miaka miaka ht miaka mi3 (construction ilianza 2019)....kwamba walikopa mkopo wa miaka miwili au?imekua personal loan hio au ndo umbumbu wenu?
Acheni kuleta mambo ya vijeweni or story za kuskia zisizokua na evidence humu ndani, msituchukulie wote ma poyoyo.
 
Back
Top Bottom