Mradi wa LNG: Tukicheza Vizuri wakati huu ni hakika Umasikini tutausahau Tanzania na Samia anaweza kuwa Rais Bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania

Yaani tuuze gesi nchi za ulaya wakati hapo mttwara kwenyewe hawatumii gesi
 
Tanzania kwa East tu tumepitwa na congo na Rwanda kwa gesi nyingi
 
Naunga mkono hoja, Mama Samia aendelee na kasi hii hii bado kitambo tutafika.
 
Kitu gani kinakufanya uamini Tanzania tuna akili sana tofauti na Waafrika wengine Manelezu ?!
Nchi zote ulizozitaja sio Tanzania. Hata Algeria ni Africa ila wanatumia vizuri resources zao

Watanzania tuna akili nyingi sana. Tulip uone matokeo ndo useme
 
uzi wako ni mzuri sana na wenye kutia matumaini hasa kwa sisi watanzania tuliokwisha poteza matumaini

Ila tambua ya kuwa hii sio fursa ya kipekee kwa nchi yetu

tumekuwa na fursa nyingi sana tangu enzi za mwalimu lakini chakuskitisha tumeshindwa kutumia hata moja

lord; nina imani wewe ni mtanzania kama nilivyo mimi na watanzania wengine, nina iman unaijua hii nchi vizur utajiri tulionao

swali la kujiuliza tumenufaika vipi na raslimari tulizo nazo?

madini, bahari, bandari, mawziwa, mito mikubwa, mbuga za wanyama, kilimo, mifugo nk! raslimar zote hizo kwa ujumla zinafanana na iyo gas ukizijumlisha?

lakin cha ajabu mpaka leo hii bado tunalia umaskini
 
Gas yenyewe akina 'sultani mang'ung'o' walishaiuza kwa vipande vya fedha kwa wale pua ndefu.
 
Ninukuu katika aya yako ya mwisho, ati, '.....Umasikini itakuwa Historia Tanzania',
Ninasubiri takwimu za kutokomeza umasikini kwa kutumia LNG Plant hapo Lindi.
LNG inamilikiwa na Makampuni makubwa ambayo yaliisha ingia Mikataba na Serikali.
Mgao wa Serikali ni ASILIMIA ngapi ili tuweze kuzungumzia kutokomeza Umasikini?
 
Tanzania kwa East tu tumepitwa na congo na Rwanda kwa gesi nyingi
takwimu zako sio sahihi ndugu, kwenye swala la gas tanzania tuna lita nyingi sana za ujazo, yaan kitakwimu tunaweza tukawa juu sana kidunia
 
Nani kakwambia Lindi Kuna LNG plant?
 
takwimu zako sio sahihi ndugu, kwenye swala la gas tanzania tuna lita nyingi sana za ujazo, yaan kitakwimu tunaweza tukawa juu sana kidunia
Huyu msafisha kabuli wa chato pale achana nae tu
 
Tutacheza vipi vizuri wakati mikataba ishasainiwa?
 
Usiongelee yaliyopita tuongelee sasa kwenda mbele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…