NDINDA
Platinum Member
- Apr 4, 2011
- 10,572
- 48,607
- Thread starter
- #161
Ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo haraka - Kimara Mwisho
Ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo haraka - Kimara Mwisho - wavuti.com
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Safi sana NDINDA. Vipi lakini mradi utakamilika kwa wakati wake kwa kasi wanauokwenda nayo?
mkuu kutokana na maoni ya watu walio karibu na wanavyoona vifaa na watu wanavyopiga kazi, kuna matumaini kazi inaenda kama ilivyopangwa ila sijui hao tanesco na wengine ambao wanatkaiza kusogeza vitu kama nguzo na mabomba ya maji, mengine sina uhakika mkuu mi huwa naweka tu updates nikiziona:smiling:
Haya ni Majibu ya Rais waliyemuita DHAIFU. Ukweli ni kuwa, JK Amefanya makubwa kuliko Awamu zote kwani ametumia fursa ambazo waliotangulia hawakuzipata. Kila kiongozi ana nyota na enzi yake. Nataja baadhi ya mambo ambayo yanaitwa ndoto. Daraja la Maragalasi 80bil, limekamilika kwa zaidi ya 70%, Daraja la Kigamboni 200bil, limeanza kujengwa, Bomba la gesi Mtwara dar for 2700MGW pamoja na kuingiza gesi majumbani mradi umeanza, Mradi wa liganga na mchuchuma ukikamilika 11trillion, umeanza, bara bara za lami 11,000 km nchi nzima awamu tofauti ujenzi unaendelea, Usafiri wa treni dar, october 1, ujenzi reli mpya Tanga, Musoma mkataba umesainiwa, Udom na maendeleo ya vyuo vikuu, Sekondari za kata zimeanza kufaulisha, na kuna listi kubwa ambayo inahusu kilimo, biashara nk. MNYONGE MYONGENI HAKI YAKE MPANI
Usisahau kuwa JK amekuta Tanzania tayari na reserves za kutosha. pamoja na mapungufu yake Mkapa alifanya mambo mengi makubwa hasa kwenye kuubadilisha uchumi wa Tanzania. JK alikuta Tanzania ikiwa na zaidi ya dollar billion tatu kwenye forex. Mkapa hakukuta kitu. Mwinyi ndiyo kabisa alikuwa hata dollar laki tano za kununulia mafuta hazikuwepo.
Ni kweli, lakini usisahau hali aliyoikuta Jk, Pamoja na huo uchumi kukuwa awamu ya awali. Umeme ulikuwa zero, viwanda vyote viliuzwa na vilikuwa haviingizi kitu, misamaha ya kodi, bara bara za lami km 6000 tu, wanafunzi vyuo vikuu wachache na graduands walikuwa chini ya 1%, Watendaji wengi walikuwa wasomi lakini wezi, mfano tanesco. Hakukuwa na uhuru wa kuongea nk. Wakati mwingine watu wanaotegemewa kabisa hutuangusha. Mengi katika uchumi mkubwa kafanya JK kilichobaki ni "Multiplier effect"
Kuuzwa viwanda ni haki kabisa. Viwanda hivyo vilianzishwa na serikali ya awamu ya kwanza na baadaye viligeuka kuwa ni vichaka vya wezi. Labda nikuulize ni viwanda vipi ambavyo Mkapa aliviuza na unaona kuwa visingeuzwa.
Ni rahisi sana kusahau hali aliyoikuta Tanzania wakati anachukua nchi. Nchi zote wahisani pamoja na Benki Kuu ya Dunia na IMF walisimimisha kabisa kuisaidia Tanzania. Walikuwa wanataka Tanzania ianze kulipa madeni kwanza ndiyo waanze kufikiria namna ya kurudi kuisaidia tena. Mkapa vile vile aliamua kuweka uchumi wa nchi sawa. Shilingi ilipotea na ikawa ina thamani tena mikononi mwa watu. Uchumi ulikuwa na ndipo kukawa na pesa ile ambayo JK aliikuta pale Benki Kuu.
Kuhusu kujenga mabarabara ukumbuke kuwa Mkapa alikuwa ndiye Rais wa kwanza Tanzania kuamua kuwa tunaweza kujenga mabarabara na miundo mbinu mingine kwa kutumia pesa zetu wenyewe bila kuomba misaada au kukopa kila wakati. Ilikuwa haijatokea. Ndipo mradi wa barabara ya kutoka Mwanza hadi Mtwara ulipobuniwa. Vilevile aliweza kutoa maji ziwa Victoria na kuyapeleka mpaka Shinyanga.
Mkapa asingeweza kufanya yote hasa ukizingatia hali aliyoikuta. Alipochukua nchi kulikuwa hata hakuna cha maana cha kuiba. Ufukara na umaskini ulikithiri.
Changamoto za Rais anayekuja ni nyingi. Kubwa kupita zote ni kuhakikisha kuwa anawafagia wezi wote waliopo kila kona ya serikali ya leo na kuhakikisha kuwa uchumi unakua zaidi.
Upo sahihi kwa upande mmoja. Kwa upande mwingine JK Kafanya mambo mengi makubwa kuliko wengine wote kwa maana ya uchumi. Nitakupatia orodha na thamani ya miradi. Mmoja wa mfano ni Mradi wa Chuma na MAKAA YA MAWE LUDEWA. Zaidi ya 5Trillioni mwanzo wa mradi na hisa kwa mara ya kwanza tanzania itamiliki 49%. Hakuna Rais Tanzania Amewahi kupata hisa katika mgodi mkubwa ukitoa Mwadui kwa JK Nyerere nadhani alikuwa na hisa kituchul
Tanzania ilikuwa ina hisa za 51% kwenye mgodi wa Mwadui na DeBeers wakachukua 49%. Tanzania iling'ang'ania kuendesha mgodi ule kutokana na wingi wa hisa. Meneja wa mwisho mzungu (Mr. Hunt ) aliondoka Mwadui mwanzoni mwa miaka ya 70 na akachkua Mr. Samwel Rwakatare, na badaye wengne walifuata. Kilicotokea ni kuwa mgodi ulizidi kudorora kiasi cha kwamba walikuwa wantupa mchanga na almasi kwani hawakuweza kununua mashine za kisasa. Mwishoni mgodi ulishndwa kabisa kujiendesha.
Mkapa aliomba De Beers warudi kuuendesha tenma ule mgodi. De Beers waliukuta mgodi ukiwa hoi kwelikweli na wakaiambia serikali na wao watoe pesa kuufufua. Serikali wakawa hawana pesa. De Beers walitoa pesa na hisa za serikali zikapungua thamani kufikia nadhani 25%.
Kuhusu Liganga na Mchuchuma nadhani hali ni karibu hiyo hiyo. Serikali itamiliki 49% ikiwa tu itatoa pesa kununua hisa zake. La sivyo kama serikali itashindwa kutoa hiyo pesa, na watashindwa, basi hisa zake zitapungua kwenda kwenye asilimia ya chini zaidi. Nadhani unaweza kupata taarifa zaidi kutoka NDC.
Mradi wa cuma na makaa ya mawe ni wa miaka mingi sana. Labda sasa kuna kitu kitatokea ijapokuwa bado nina wasiwasi kiasi fulani.