Mradi wa SGR umeendeshwa vibaya na utalitia Taifa hasara kizazi hadi kizazi

Mradi wa SGR umeendeshwa vibaya na utalitia Taifa hasara kizazi hadi kizazi

Nafikiri kwa uwekezaji, unaofanywa kwenye Reli,ni lazima lengo.liwe n biashara.
Nina mashaka makubwa na hii miradi ya Mwendazake!
Kuna kila dalili tutakujakulia huko mbeleni.
Nafikiri kinachoendelea Kenya kwenye SGR ya Nairobi Mombasa ni mfano.mzuri ,sana!
Haiwezekani nchi ikajiingiza kwenye miradi mikubwa hivi ,bika mjadala wa kutosha!
Usidhani kila wakati unatakiwa kufikiria kibiashara la hasha serikali inachochea sekta binafsi ziweze kufanya biashara kwa faida siyo serikali.Reli inatengenezwa ili ichochee sekta za kibiashara.Acha uvivu wa kufikiri
 
Uchumi wa China ulianza kukua kwa kasi miaka ya 1980 baada ya kufunguliwa na kuruhusu sekta binafsi kushamiri chini ya Deng Xiaoping, hii China yenye uchumi mkubwa unayoina leo ni matokeo ya Sekta binafsi kuruhusiwa kuchukua hatamu japo kwa kuendelea kubanwa na sera za kikomunisti. Kwa sasa viwanda na makampuni mengi China yanamilikiwa na watu binafsi au umma kupitia mfumo wa hisa.

Russia ilishatoka kwa kiasi kikubwa kwenye mfumo wa serikali kufanya biashara,ilifanya ubinafsihaji mkubwa wa makampuni ya umma miaka ya 1990 chini ya Boris Yeltsin na imeenda mbali sana kwenye sekta binafsi.

Fahamu pia kuna nchi nyingi zina utajiri mkubwa kiasi kwamba kuna mambo ya kibiashara zinafanya bila dhana ya biashara, Hizo ni pamoja na Russia, Saudi Arabia, Qatar n.k.Hizi ni nchi ambazo zitajenga na kuendesha miradi ya reli, mwendokasi, mashirika ya ndege bila kujali upatikanaji wa faida yoyote, zina huo uwezo, sisi hatuna.

North Korea ni shit hole country haifai hata kuzungumziwa.
Mkuu Yoda, sijasema kwamba serikali ijiingize katika kufanya kila aina ya biashara inayoweza kufanywa na yeyote, na siyo maana yangu kusema kwamba sekta binafsi izuiwe kufanya biashara.

Kuna baadhi ya mambo ambayo serikali inahitajika kuyafanya kwa ufanisi kwa manufaa ya jamii nzima. Haya ndiyo tunayoyazungumzia hapa

Ni vyema umeanza andiko lako kwa hayo maneno "Ni nadra" ikiwa na maana kwamba inawezekana hata ikiwa ni mara chache.

Umetoa mfano wa serikali ya Marekani na mashirika binafsi, lakini hujatolea mfano na serikali ya China, au Soviet, enzi zile, au Korea Kaskazini leo hii wanapotengeneza 'hypersonic' missiles.

Hata hizo kodi unazosema serikali ikusanye, itazikusanya vipi iwapo inashindwa kuendesha hata shirika moja la kutoa huduma kwa wananchi kwa ufanisi! Unachojisahaulisha hapa ni kwamba serikali haifanyi kazi inavyotakiwa na wananchi ifanye, halafu unachukulia hali hiyo kuwa ndiyo hali ya kawaida inayotakiwa kuwa nayo serikali! Hili sikubaliani nalo.
 
Serikali inapaswa kujenga reli kisha waiachie sekta binafsi kuendesha treni kama inavyojenga barabara kisha inaachia kampuni za mabasi kusafirisha watu na mizigo.
Usidhani kila wakati unatakiwa kufikiria kibiashara la hasha serikali inachochea sekta binafsi ziweze kufanya biashara kwa faida siyo serikali.Reli inatengenezwa ili ichochee sekta za kibiashara.Acha uvivu wa kufikiri
 
Ccm imetawala hii nchi miaka 60 80% ya watu ni masikini wa kutupwa, hata uwape miaka milioni hakuna kitu watafanya.

kwan wanaofanya wananchi kua maskini ni serikali? socialism mlikataa mkamuona nyerere anaharibu uchumi wakati ilikua ni kwa ajili ya usawa! basi tumeingia capitalism sasa kelele za nn tena ama hujui maaana ya SURVIVAL FOR THE FITTEST? ni wap duniani hakuna maskini?
 
Naona uwezo wako wa kutambua mambo ni wa chini, inatosha.

unachoongea ni upuuzi ndo maaana! biashara ya reli ipo duniani kote mdogo wangu, isitoshe nchi zilizoendelea znategemea reli zaidi lakini malori bado yapo, so unaongea ujinga!
 
Hizi ndizo mojawapo sababu biashara za serikali huwa zinashindwa vibaya sana @Kalamu1

bila serikali hata hilo bundle unalotumia kuongea ujinga usingekua nalo, ni uwekezaji kama huu unaofanya maumivu ya uchumi kupungua kwa wananchi mfano kikwete aliwekeza kujenga mkongo wa taifa unaomilikiwa na serikali hivo kupunguza maumivu ya uchumi, same applies kwenye mambo mengine! kwahio acha kuongea ujinga
 
kwan wanaofanya wananchi kua maskini ni serikali? socialism mlikataa mkamuona nyerere anaharibu uchumi wakati ilikua ni kwa ajili ya usawa! basi tumeingia capitalism sasa kelele za nn tena ama hujui maaana ya SURVIVAL FOR THE FITTEST? ni wap duniani hakuna maskini?
Masikini wapo sehemu zote Duniani lakini serikali ambayo inatengeneza ama inazalisha 80% ya raia masikini ni serikali ya wapi hiyo, ya kishetani.

Kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira watu watoke kwenye umasikini, hiyo survival for the fittest iwe fair, sasa hii serikali ya ccm imeshindwa kwa miaka 60 sasa. Bora apewe Rungwe.
 
Masikini wapo sehemu zote Duniani lakini serikali ambayo inatengeneza ama inazalisha 80% ya raia masikini ni serikali ya wapi hiyo, ya kishetani.

Kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira watu watoke kwenye umasikini, hiyo survival for the fittest iwe fair, sasa hii serikali ya ccm imeshindwa kwa miaka 60 sasa. Bora apewe Rungwe.

naomba kujua elimu yako
 
Uchumi wa China ulianza kukua kwa kasi miaka ya 1980 baada ya kufunguliwa na kuruhusu sekta binafsi kushamiri chini ya Deng Xiaoping, hii China yenye uchumi mkubwa unayoina leo ni matokeo ya Sekta binafsi kuruhusiwa kuchukua hatamu japo kwa kuendelea kubanwa na sera za kikomunisti. Kwa sasa viwanda na makampuni mengi China yanamilikiwa na watu binafsi au umma kupitia mfumo wa hisa.

Russia ilishatoka kwa kiasi kikubwa kwenye mfumo wa serikali kufanya biashara,ilifanya ubinafsihaji mkubwa wa makampuni ya umma miaka ya 1990 chini ya Boris Yeltsin na imeenda mbali sana kwenye sekta binafsi.

Fahamu pia kuna nchi nyingi zina utajiri mkubwa kiasi kwamba kuna mambo ya kibiashara zinafanya bila dhana ya biashara, Hizo ni pamoja na Russia, Saudi Arabia, Qatar n.k.Hizi ni nchi ambazo zitajenga na kuendesha miradi ya reli, mwendokasi, mashirika ya ndege bila kujali upatikanaji wa faida yoyote, zina huo uwezo, sisi hatuna.

North Korea ni shit hole country haifai hata kuzungumziwa.
Mkuu Yoda, nadhani hatuendi popote na mjadala huu endapo kama tutabaki kuzungukia kwenye hizo habari tunazozijuwa kila mara, kama zinavyoelezwa kwa maksudi maalum.
Mimi sijakataa mchango wa sekta binafsi. Ninachokataa ni hiyo dhana potofu ya kunag'ang'ania kwamba "serikali haiwezi".
Maendeleo ya China huwezi kuondoa ushiriki mkubwa wa serikali, eti kwamba yalipatikana tu pale sekta binafsi iliporuhusiwa.

Nimekupa hiyo mifano ya Korea na Soviet kujibu hoja yako ya mashirika binafsi katika utengenezaji na uendelezaji wa silaha, bado unatafuta visababu.
Unaweza kuiita Korea Kaskazini 'shithole', lakini kamwe huwezi kuondoa ukweli kwamba sasa hivi hakuna anayeweza kwenda kuichezea bila kutoka yeye kamasi, na hakuna sekta binafsi iliyowezesha hivyo iwe hivyo.
 
Mwaka 1970-1974 mchina alijenga reli ya Tazara ya kisasa kwa wakati huo na watanzania waliaminishwa makubwa Sana juu ya faida ya mradi husika. Miaka 25 tu baada ya mradi kukamilika reli ikachoka, ikakosa wateja, usimamizi mbovu. Zile hadithi na simulizi tamu za manufaa ya mradi huo walioaminishwa watanzania hakuna Tena na njia kuu ya uchukuzi Tanzania to Zambia kubaki NI barabara ya Rami.

Pia Serikali ililithi reli ya Kati kutoka kwa mkoloni. Na reli ilibaki njia kuu ya uchukuzi Hadi miaka ya 90s katikati. Lakini shirika liliendeshwa kihuni Sana. Shirika liliuza tiketi chache Sana. Zaidi ya 80% ya abilia walilipa Ela keshi zilizoishia mikononi mwa walinzi na wafanyakazi wa shirika lenyewe.

Mpaka leo reli haikujiendesha. Inakula Kodi zetu kila siku kukarabatiwa lkn maingizo hakuna NI hasara tu.
Nisiwachoshe kabisa. Sizungumzii kbs mradi wa Mabasi ya mwendokasi unavyoumiza taifa ikiwa NI chini ya miaka kumi tu uanshwe. Serikali inamwaga fedha kuuokoa Ila watachoka tu. Mabasi kibao yameharibika yakatelekezwa na kuoza.
Ndege zipo kwaajili ya kujisifu lkn hakuna faida ya . Kila mwaka Serikali inakula lose ya mabilioni

Ambao wanachukulia Mambo kirahisi hawataelewa. Wataamini propaganda na hadidhi za bulicheka na ndoto za abunuasi za kuvuka bahati kwa kugeuza meza na kupanda juu yake.

Ukweli NI kuwa mradi utakausha kau fedha mtaani, Utajiendesha kwa hasara, hautaleta faida.

Serikali ingejitoa kabisa kwenye ujenzi na uendeshaji ikakaa kusubili kodi.
Ila Kama Serikali itafanya biashara hii ni hatari kwake na Sekta binafsi za usafirishaji. Haina ubunifu. Wanachojua Serikali NI kuwafungia Sekta binafsi ili wao wauze. Kama ilivyofanya Air Tz dhidi ya fast jet. lkn Serikali haifaidiki chochote na abiria wanaumia.

Tunaitaji reli nzuri lkn bila hakukuwa na ulazma wa Serikali yenyewe kuhusika.


Hayo matilioni yatapotea. Tulikuwa tunapiga hatua Ila Sasa tunatumia ma tilion kuliundia taifa zigo la kuhudumiwa na matilioni kila mwaka.
Screenshot_20211017-192537.jpg
 
Masikini wapo sehemu zote Duniani lakini serikali ambayo inatengeneza ama inazalisha 80% ya raia masikini ni serikali ya wapi hiyo, ya kishetani.

Kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira watu watoke kwenye umasikini, hiyo survival for the fittest iwe fair, sasa hii serikali ya ccm imeshindwa kwa miaka 60 sasa. Bora apewe Rungwe.

yaaani nlikua napita twitter nakutana na hii post nkakukumbuka we bongo lala
 
Yaani mpaka iwe bure kabisa ndo ujue ni huduma kwa jamii?
Mwendokasi ni biashara na si huduma na huduma si lazima iwe bure iwe hata kwa malipo ila yawe kidogo chini ya inayotozwa na sekta binafsi.....Sasa cha kushangaza nauli ya usafiri wa serikali ikawa juu zaidi ya usafiri wa wawekezaji binafsi halafu tuuite kuwa ni huduma!!!!
 
Badala ya kuongelea mchango wa sekta binafsi tunapaswa kufikia mahali kuongolea mchango sekta ya umma( lYani sekta binafsi ndio iwe injini halafu ipewe mchango na sekta ya umma). Tunakosea kusema mchango wa sekta binafsi wakati sekta binafsi ndio inapaswa kuwa 'main'.

Serikali inaweza kufanya biashara yoyote ikiamua, na ina uwezo wa kufanya hivyo kwa sababu ina uwezo wa kupata pesa kupitia kodi na dola ya kulazimisha mambo, ila haiwezi kufanya biashara YOYOTE kwa ufanisi kama sekta binafsi, hii ni kanunu ya uchumi.
Zipo sababu milioni za kiuchumi kwa nini huwa inakuwa hivyo.

Korea Kaskazini kuwa na makombora ya nuclera na kutochezwa sio kwa sababu ya ufanisi wa sekta ya umma katika biashara. Hakuna biashara yoyote inayofanyika Kiduku anapoenda kuchukua wataalamu wavujisha siri za nuclear "nuclear proliferators" kutoka Iran na kwingineko wamjengee nuclear. Mkuu Kalamu1 Korea ya Kaskazini ni shithole country na " odius dictatorship", ni taifa la kijuha sana linaloendeshwa na psychopaths, huwezi kuwa unarusha makombora hewani kila siku huku watu wako wanakufa njaa na kutumia kinyesi cha binadamu kama mbolea.
Kutamani kuwa kama Korea ya Kaskazini ni wendawazimu au kuwa mtu wa akili ndogo sana.
Mkuu Yoda, nadhani hatuendi popote na mjadala huu endapo kama tutabaki kuzungukia kwenye hizo habari tunazozijuwa kila mara, kama zinavyoelezwa kwa maksudi maalum.
Mimi sijakataa mchango wa sekta binafsi. Ninachokataa ni hiyo dhana potofu ya kunag'ang'ania kwamba "serikali haiwezi".
Maendeleo ya China huwezi kuondoa ushiriki mkubwa wa serikali, eti kwamba yalipatikana tu pale sekta binafsi iliporuhusiwa.

Nimekupa hiyo mifano ya Korea na Soviet kujibu hoja yako ya mashirika binafsi katika utengenezaji na uendelezaji wa silaha, bado unatafuta visababu.
Unaweza kuiita Korea Kaskazini 'shithole', lakini kamwe huwezi kuondoa ukweli kwamba sasa hivi hakuna anayeweza kwenda kuichezea bila kutoka yeye kamasi, na hakuna sekta binafsi iliyowezesha hivyo iwe hivyo.
 
yaaani nlikua napita twitter nakutana na hii post nkakukumbuka we bongo lala

Wewe na huyo taahira mwenzako hamuelewi role ya serikali katika kusaidia kuondoa umasikini.

Kama serikali haijatengeneza mazingira mazuri ya kukufanya wewe shughuli unayofanya ifanikiwe na utokane ama uondokane na umasikini hata ufanyeje haiwezekani.

Kwa nini watu walikua wanamlaumu JPM kwamba amefanya mazingira ya biashara kua magumu? Kwani biashara ilikua haifanyiki?

Ninachokiona ni wewe kua na uelewa mdogo wa haya mambo. Rudi shule uongeze maarifa kisha uje tujadiliane.
 
naomba kujua elimu yako
Elimu yangu hakuna mtu kwenye ukoo wenu anayo ama atakuja kua nayo.

Kama akili huna ya kujua wajibu wa serikali kwenye kupumguza ama kuondoa umasikini, unakopi tweets za waume zako huko Twitter ambao hawana akili kama weww unawezaje kuhoji elimu yangu mimi mtaalam?

Achana na mataahira wenzakowa tweeter, soma hapa kutoka kwa wataalamu wa uchumi kutoka IMF wanasemaje kuhusu serikali kupunguza umasikini


 
Mwaka 1970-1974 mchina alijenga reli ya Tazara ya kisasa kwa wakati huo na watanzania waliaminishwa makubwa Sana juu ya faida ya mradi husika. Miaka 25 tu baada ya mradi kukamilika reli ikachoka, ikakosa wateja, usimamizi mbovu. Zile hadithi na simulizi tamu za manufaa ya mradi huo walioaminishwa watanzania hakuna Tena na njia kuu ya uchukuzi Tanzania to Zambia kubaki NI barabara ya Rami.

Pia Serikali ililithi reli ya Kati kutoka kwa mkoloni. Na reli ilibaki njia kuu ya uchukuzi Hadi miaka ya 90s katikati. Lakini shirika liliendeshwa kihuni Sana. Shirika liliuza tiketi chache Sana. Zaidi ya 80% ya abilia walilipa Ela keshi zilizoishia mikononi mwa walinzi na wafanyakazi wa shirika lenyewe.

Mpaka leo reli haikujiendesha. Inakula Kodi zetu kila siku kukarabatiwa lkn maingizo hakuna NI hasara tu.
Nisiwachoshe kabisa. Sizungumzii kbs mradi wa Mabasi ya mwendokasi unavyoumiza taifa ikiwa NI chini ya miaka kumi tu uanshwe. Serikali inamwaga fedha kuuokoa Ila watachoka tu. Mabasi kibao yameharibika yakatelekezwa na kuoza.
Ndege zipo kwaajili ya kujisifu lkn hakuna faida ya . Kila mwaka Serikali inakula lose ya mabilioni

Ambao wanachukulia Mambo kirahisi hawataelewa. Wataamini propaganda na hadidhi za bulicheka na ndoto za abunuasi za kuvuka bahati kwa kugeuza meza na kupanda juu yake.

Ukweli NI kuwa mradi utakausha kau fedha mtaani, Utajiendesha kwa hasara, hautaleta faida.

Serikali ingejitoa kabisa kwenye ujenzi na uendeshaji ikakaa kusubili kodi.
Ila Kama Serikali itafanya biashara hii ni hatari kwake na Sekta binafsi za usafirishaji. Haina ubunifu. Wanachojua Serikali NI kuwafungia Sekta binafsi ili wao wauze. Kama ilivyofanya Air Tz dhidi ya fast jet. lkn Serikali haifaidiki chochote na abiria wanaumia.

Tunaitaji reli nzuri lkn bila hakukuwa na ulazma wa Serikali yenyewe kuhusika.


Hayo matilioni yatapotea. Tulikuwa tunapiga hatua Ila Sasa tunatumia ma tilion kuliundia taifa zigo la kuhudumiwa na matilioni kila mwaka.

Tanzania bila kuwasulubisha wezi wa mali ya umma, miradi yote haitakaa kuja kujiendesha. Watu wasipojua kujituma ili biashara ijiendeshe kwa faida, hilo kosa la nani? Tungejitendea wema, kama tungeweza kujifunza kwanini Tazara, with all its potential, inasuasua hadi hii leo. Shida ni nini? Ili tusirudie makosa kwenye SGR
 
Mbona sioni faida ya TAZARA ambayo ilianza kabla sijazaliwa? Au hata hiyo TAZARA wajukuu wangu ndio wataona faida?
kujua sababu uwezo wa kuchambua mambo ni finyu.Acha mradi umalizie wajukuu zako wataona faida.Miaka 100 ijayo wataona faida yake siyo wewe
 
Badala ya kuongelea mchango wa sekta binafsi tunapaswa kufikia mahali kuongolea mchango sekta ya umma( lYani sekta binafsi ndio iwe injini halafu ipewe mchango na sekta ya umma). Tunakosea kusema mchango wa sekta binafsi wakati sekta binafsi ndio inapaswa kuwa 'main'.

Serikali inaweza kufanya biashara yoyote ikiamua, na ina uwezo wa kufanya hivyo kwa sababu ina uwezo wa kupata pesa kupitia kodi na dola ya kulazimisha mambo, ila haiwezi kufanya biashara YOYOTE kwa ufanisi kama sekta binafsi, hii ni kanunu ya uchumi.
Zipo sababu milioni za kiuchumi kwa nini huwa inakuwa hivyo.
Hiyo 'para' ya pili ni 'dogma'tu mkuu Yoda iliyozoeleka na inayopendwa kusemwa kama msahafu fulani.

Kwenye 'para' ya kwanza, umenikumbusha jambo ambalo huwa ninalifikiria mara kwa mara: Kwani "Sekta Binafsi" ni kitu gani? Mkulima wa njegere kule Manyara hatuwezi tukamweka kwenye sekta binafsi? Kwa nini? Kama ni uwezo wake, je tukiwaunganisha na wakawa kundi kubwa na uwezo wao ukawa mkubwa, kundi hili hatuwezi tukalitambua kama sekta binafsi?

Nimetumia tu huo mfano wa mkulima, lakini tunaweza kutumia mifano mingi mingine ya aina hiyo.

Bado hatukubaliani kabisa kuhusu uwezo wa serikali kufanya shughuli za kibiashara katika baadhi ya mashirika ikiweka nia ya kuufanikisha.

Kuhusu Korea Kaskazini, naona uamini wako ni ule ule wa kuchotwa akili na propaganda za upotoshaji wa vyombo vya habari na kuufanya wimbo unaoimbwa sehemu zote hadi na watu wenye akili timamu. China pia ilikuwa hivyo hivyo, hadi hapo walipoamua kuunganisha mtindo wao na ule waliokuwa wakiupigia chapuao hao wanaoeneza propaganda duniani.

Korea Kaskazini, usisahau wapo chini ya vikwazo vya kiuchumi, na kila siku wakubwa wanasubiri kusikia nchi hiyo imeangamia! Lakini haijatokea. Waondoe vikwazo basi, ili tuone watakavyodhoofika haraka? Unamwekeaje vikwazo mtu unayejuwa mtindo wake wa siasa ndio utakaommaliza mwenyewe? Ninapoandika haya siyo kwamba nataka Tanzania iwe hivyo, la hasha, ni kuonyesha tu upotoshaji unaofanyika na kuchota akili za watu wengi bila ya kusita na kudadisi kwa kina.
 
Tungejitendea wema, kama tungeweza kujifunza kwanini Tazara, with all its potential, inasuasua hadi hii leo. Shida ni nini? Ili tusirudie makosa kwenye SGR
Mstari mmoja wenye maana nzito kabisa. Badala yake watu wanatafuta majibu kwingine kabisa.
 
Tusipoteze muda na kamati za kutafuta kwa nini mambo ya kijamaa yalishindwa na yanaendelea kushindwa duniani kote. SGR ikikamilika huo mwaka itakaokamilia sekta binafsi ipewe fursa ya kuendesha biashara ya treni.
Tanzania bila kuwasulubisha wezi wa mali ya umma, miradi yote haitakaa kuja kujiendesha. Watu wasipojua kujituma ili biashara ijiendeshe kwa faida, hilo kosa la nani? Tungejitendea wema, kama tungeweza kujifunza kwanini Tazara, with all its potential, inasuasua hadi hii leo. Shida ni nini? Ili tusirudie makosa kwenye SGR
 
Back
Top Bottom