Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Faida ya kusajili kama kampuni ni ipi hapo mkuu tupe shule
Atakuja kusema ila nachofahamu ningekuwa nimeisajiri kama Kampuni ningenufaika na fedha ya Uchakavu (Depreciation) kutoka TRA hivyo ningekuwa na punguzo kidogo la Kodi

Maana Kwa biashara yangu ningepata Fedha ya Uchakavu ya almost 37% kama punguzo la Kodi
 
Asante Mkuu

Watanzania wengi sio waaminifu

Baada ya kuichezea Camera saivi analeta hela anayojisikia maana anasema Leo wamelala wateja 7 kumbe wamelala 9

Nimetengeneza mara 3 lakini baada ya muda inaharibika Tena.

Nina hakika ningekuwa nakaa mwenyewe huenda Payback period ingeshuka hadi miaka 2

Maana nahisi napoteza Mapato mengi Kwa Wizi wao Hawa Vijana

Sio waaminifu kuanzia receptions hadi walinzi hata wamasai siku hizi labda professional companies kama Suma Jkt. Wasipokuibia mapato watawaibia wateja sana.

Kuna trick wanafanya mfano madirisha huwa hayawi locked. Usiku umeme ukikatika walinzi wakishirikiana na vibaka kwa kutumia kama fimbo hivi ndefu ya chuma wanachukua nguo na begi hasa kama vipo karibu na dirisha.

Nyingine ni kuwaambia wateja wakitoka nje waache funguo reception, halafu wanapitia vitu vyao.

Dawa ni kuwa na umeme 24/7 na mfumo thabiti wa CCTV kuizunguka nyumba pande zote, reception na corridors. Unaweza kuwa na mifumo miwili mmoja hata wafanyakazi wote hawaujua ni wewe tu unaojua unakuwa kama taa za kawaida lakini ni camera na mwingine wanaoujua.
 
Sio waaminifu kuanzia receptions hadi walinzi hata wamasai siku hizi labda professional companies kama Suma Jkt. Wasipokuibia mapato watawaibia wateja sana.

Kuna trick wanafanya mfano madirisha huwa hayawi locked. Usiku umeme ukikatika walinzi wakishirikiana na vibaka kwa kutumia kama fimbo hivi ndefu ya chuma wanachukua nguo na begi hasa kama vipo karibu na dirisha.

Nyingine ni kuwaambia wateja wakitoka nje waache funguo reception, halafu wanapitia vitu vyao.

Dawa ni kuwa na umeme 24/7 na mfumo thabiti wa CCTV kuizunguka nyumba pande zote, reception na corridors. Unaweza kuwa na mifumo miwili mmoja hata wafanyakazi wote hawaujua ni wewe tu unaojua unakuwa kama taa za kawaida lakini ni camera na mwingine wanaoujua.
Nitachukua huo Ushauri wa kufunga camera nyingine ya Siri kama ulivyoshauri.

Uaminifu umekuwa changamoto sana miongoni mwa WaTanzania, watu hawakuonei huruma vile ume- hustle kuweza kujiwekeza
 
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.
Mkuu Hongera sana ila Mbinguni huendi.

Umejenga kiota cha watu Kunyanduana?
 
Faida ya kusajili kama kampuni ni ipi hapo mkuu tupe shule
Kwa kujazia alichosema Grahams

Mfano mteja kaja kwenye lodge akapigwa shoti bafuni akafa au akapata tatizo lolote ambalo mmiliki atatakiwa kufidia, ukiwa huna kampuni mahakama itatumia mpaka nyumba yako ya kulala ili kufidia! Ila ukiwa na kampuni mali zitazokua kwenye risk ni mali za kampuni tu!

2. Kingine ni kwenye kodi, ukiwa na kampuni unaweza usilipe hata shilingi moja provided unatunza gharama mapato na matumizi yako. Tena mda huu anapofanya matengenezo let say ya kumbi ndio mzuri zaidi, gharama zote za ujenzi wa kumbi anaweza wasilisha kama gharama za kampuni na akiwasilisha gharama za mwaka akapatiwa nafuu ya kodi.. angalia hii mifano

A. Assume ana mapato ya 20mil kwa mwaka, bila kampuni tra wataangalia hii 20m kama pato na kukisia jamaa alipe kiasi gani! Hapa anakua hana nguvu ya kucontrol kiasi cha kodi.

B. Chukulia amesajili kampuni na ana mapato ya 20mil kwa mwaka, alafu ndani ya mwaka huo huo akaanza ujenzi wa kumbi na akatumia let say 15mil! Kama alisajili hii kumbi ni mali kampuni basi hii 15mil itaingia kama expense za kampuni... so tra wakija jamaa kupitia mhasibu wake watasema tumepata 20mil lakini tulikua na matumizi ya 15mil ya ujenzi wa kumbi ambayo ni mali ya kampuni hii.. hapo watatoa 20mil - 15mil = 5mil!

Kwa hiyo hii 5mil ambayo ndio faida ndio itatumika katika ku estimate kodi na sio 20mil nzima! Na hapo ni rahisi maana inajulikana kodi ya kampuni ni 30% ya faida!

NB: mimi sio mtaalam wa kodi au mhasibu nimetumia uzoefu na ujuzi wangu mdogo kuhusu makampuni!

Kwa ziada angalia hii video kutoka BRELA:
View: https://youtu.be/DAlo0hOniE4?si=1gD3vPkiHpqUSPxq
 
Kwa kujazia alichosema Grahams

Mfano leo kaja kwenye lodge akapigwa shoti bafuni akafa au akapata tatizo lolote ambalo mmiliki atatakiwa kufidia, ukiwa huna kampuni mahakama itatumia mpaka nyumba yako ya kulala ili kufidia! Ila ukiwa na kampuni mali zitazokua kwenye risk ni mali za kampuni tu!

2. Kingine ni kwenye kodi, ukiwa na kampuni unaweza usilipe hata shilingi moja provided unatunza gharama mapato na matumizi yako. Tena mda huu anapofanya matengenezo let say ya kumbi ndio mzuri zaidi, gharama zote za ujenzi wa kumbi anaweza wasilisha kama gharama za kampuni na akiwasilisha gharama za mwaka akapatiwa nafuu ya kodi.. angalia hii mifano

A. Assume ana mapato ya 20mil kwa mwaka, bila kampuni tra wataangalia hii 20m kama pato na kukisia jamaa alipe kiasi gani! Hapa anakua hana nguvu ya kucontrol kiasi cha kodi.

B. Chukulia amesajili kampuni na ana mapato ya 20mil kwa mwaka, alafu ndani ya mwaka huo huo akaanza ujenzi wa kumbi na akatumia let say 15mil! Kama alisajili hii kumbi ni mali kampuni basi hii 15mil itaingia kama expense za kampuni... so tra wakija jamaa kupitia mhasibu wake watasema tumepata 20mil lakini tulikua na matumizi ya 15mil ya ujenzi wa kumbi ambayo ni mali ya kampuni hii.. hapo watatoa 20mil - 15mil = 5mil!

Kwa hiyo hii 5mil ambayo ndio faida ndio itatumika katika ku estimate kodi na sio 20mil nzima! Na hapo ni rahisi maana inajulikana kodi ya kampuni ni 30% ya faida!

NB: mimi sio mtaalam wa kodi au mhasibu nimetumia uzoefu na ujuzi wangu mdogo kuhusu makampuni!

Kwa ziada angalia hii video kutoka BRELA:
View: https://youtu.be/DAlo0hOniE4?si=1gD3vPkiHpqUSPxq

Umeongea sahihi Mkuu, nimeambiwa Kampuni inasaidia sana kwenye punguzo la Kodi...

Shida ya Nchi hii ni Utitiri wa Kodi

Imagine kabla sijapata hata shilingi 30,000 ya biashara tayari nilikuwa nadaiwa TRA/Halmashauri/Zimamoto n.k
 
Mkuu Hongera sana ila Mbinguni huendi.

Umejenga kiota cha watu Kunyanduana?
Unakumbuka Wazazi wake Yesu walipokwenda ugenini kule kwaajili ya kuhesabiwa na kukosa nyumba za Kulala Wageni hadi kupelekea Walale kwenye Zizi la ng'ombe na Yesu kuzaliwa humo?

Imagine kama hii yangu ingekuwepo nyakati hizo, si wangelala kwangu 🤗

Hilo nimechomekea tu Mkuu.... shukrani sana
 
Asante Mkuu

Watanzania wengi sio waaminifu

Baada ya kuichezea Camera saivi analeta hela anayojisikia maana anasema Leo wamelala wateja 7 kumbe wamelala 9

Nimetengeneza mara 3 lakini baada ya muda inaharibika Tena.

Nina hakika ningekuwa nakaa mwenyewe huenda Payback period ingeshuka hadi miaka 2

Maana nahisi napoteza Mapato mengi Kwa Wizi wao Hawa Vijana
Achana na kamera...weka vitasa vya card ...na software...uhakika zaidi...chumba kikiwa booked unapata notifications online...tumia technology Mzee ...
 
Uzi nzuri Sana ..naomba kuongezea...

Kuhusu wizi tumia technology..nenda jukwaa la IT wakueleze kuhusu vitasa vya card. Na software zake iwe chumba kikipata Tu mgeni unapata notifications hapo hapo...hata kama wa short time.....

Kwingine since wewe ni mpya kwenye biashara nashauri Fanya research ya lodge zilizo kufa au kukosa soko ikiwezekana uzi Kodi upige hela ..

Wengi wanashindwa maintenance Tu...sasa badala ya wewe kutumia hela nyingi kujenga zingine ...jaribu kukodi Kwa mkataba mrefu ..itakusaidia vitu viwili....kwanza utapunguza competition since competition umeinunua...pili utantumia hela ndogo for expansion...

Unaweza amini kkoo kuna hotel inakodishwa Kwa milioni 4 Tu Kwa mwezi wakati ni jengo la ghorofa 8..?

kisa muasisi kafa na watoto wanakula hela yote hawafanyi maintenance..

All in all nakutakia all the best miaka miachache kutoka sasa uwe na lodge hata tano...
 
Back
Top Bottom