Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni


Ukiwa na Kampuni na mfano hii biashara ya Lodge ikawa ni sehemu ya hiyo Kampuni itahesabika kama ni sehemu ya Mtaji wako.

Kwahiyo unavyokuwa unalipa Kodi kule TRA Kwa Mwaka, utajikuta unafunga mahesabu na Deni maana bado hela uliyo wekeza bado haijarudi...

Kwahiyo kama ni Kodi, utaanza kulipa mwaka 4 Kwa mujibu wa hesabu zangu hapo juu za PBP baada ya kwamba mwaka wa 4 utaanza kufunga hesabu na +ve Net Present Value (NPV).

Lakini Kwa sasa utajikuta bado una loss hence Investment Capital yangu bado haijawa recovered
 
nina ujuzi juu ya masuala ya umeme na IT.... kwenye hii kero yako ya vijana kuharibu kamera,. muelekeze mtaalamu wako anaekufungia kamera, naamini atakusaidia kwa urahisi tu....kwasasa tuna mini-cameras unazoweza connect na Smart phone yako lakini itakutaka uwe na internet connection muda wote...hivyo unaweza ongeza huduma ya wi-fi kwa wateja wako, hata wa VIP tu kwa kuanza lakini huku ikiendelea kukusaidia na wewe kwenye ulinzi wa mapato yako... kipindi najitafuta nimechimba sana madini huko, kwanzia mawelu,mapapai,soweto,sangambi, isoko mpaka igundu huko...hivyo huko ni nyumbani naamini naweza kuja kukutembelea ndugu... KAZI NJEMA kwako
Biashara ya Uchimbaji ina changamoto nyingi sana hasa Kwa small scale Mining.

Nilijaribu wakati fulani, lakini Kila nikifanya tathmini mwisho wa mwaka naona napata hasara tu za vibarua na materials

Hivyo nili- quit

Shukrani Kwa mchango wako Chanya, nitafanyia kazi hili.

Barikiwa 🙏🙏🙏
 
Haya ndiyo mambo tunahitahi humu kwakuwa ni mafunzo kwa sisi wajasiliamali, hongera sana
Shukrani Mkuu, tunaendelea kupata uzoefu na kujifunza wote hapa.

Kuna vitu nilikuwa sivijui but kuna watu wamevieleza hadi nimepata mwanga.

Tusiache kujaribu na kufanya Tena hata kama utaanguka mara kadhaa
 
Safi mkuu! Hongera, toa location tuje kukuunga mkono, swali la kizushi huna unoko wa kutaka vyeti vya ndoa hapo kwako mkuu?.
Masharti yangu ni ya kawaida tu, isipokuwa nimeandika Watu wa Jinsia Moja hawapaswi Kulala Chumba Kimoja.

Hii ni kutokana na maadili

Cheti cha Ndoa sijaweka katazo, maana Kuna Uchumba mwingine watu wanakaa hata miaka 10 ndiyo wanakuja kuoana 🤗
 
Umenihamasisha Nina viapartment vyangu vya chumba sebule choo na jiko zaidi ya kumi nimevipanga sehemu Kwa saša vina wapangaji .
Ni wastaarabu nacharge laki 2 Kwa unit Kwa mwezi.
Kwa sasa eneo limechangamka nafikiria kubadili niondoe wapangaji wa mwezi nifanye biashara ya lodge.
ITS good idea lodge zinalipa ukiwa na usimamizi mzuri na eneo lililochangamka na nyumba haichakai
 
Umenihamasisha Nina viapartment vyangu vya chumba sebule choo na jiko zaidi ya kumi nimevipanga sehemu Kwa saša vina wapangaji .
Ni wastaarabu nacharge laki 2 Kwa unit Kwa mwezi.
Kwa sasa eneo limechangamka nafikiria kubadili niondoe wapangaji wa mwezi nifanye biashara ya lodge.
ITS good idea lodge zinalipa ukiwa na usimamizi mzuri na eneo lililochangamka na nyumba haichakai
Vifanyie ukarabati Mkubwa then vifanye Lodge.

Kama utaweza kuweka sofa, Meza, Tv sebuleni na kule chumbani ukaweka kitanda/godoro na kifriji kidogo then ukafunga Wi-Fi utakuwa na uhakika wa kutoza 50k na zaidi.

Niliwahi Kulala Lodge ya hivyo nililipa shilingi 70,000 Kwa usiku Mmoja japo Kuna Vyumba vingine vya 120,000

Kama umesema Kuna Mzunguko wa watu, lazima Mradi ukulipe 💪
 
Vifanyie ukarabati Mkubwa then vifanye Lodge.

Kama utaweza kuweka sofa, Meza, Tv sebuleni na kule chumbani ukaweka kitanda/godoro na kifriji kidogo then ukafunga Wi-Fi utakuwa na uhakika wa kutoza 50k na zaidi.

Niliwahi Kulala Lodge ya hivyo nililipa shilingi 70,000 Kwa usiku Mmoja japo Kuna Vyumba vingine vya 120,000

Kama umesema Kuna Mzunguko wa watu, lazima Mradi ukulipe 💪

Nimekupata mkuu mawazo yako mazuri sana .
Kuna mada nimeziona kuhusu Airbnb nazo nazisoma Kwa kina kujifunza .
Kuna jamaa nimeona kabadili nyumba zake za kupanga kuwa lodge na anapata wateja . Nyumba zangu nzuri kulipo Kwa huyo mshkaji wangu
 
Kuna mada nimeziona kuhusu Airbnb nazo nazisoma Kwa kina kujifunza .
Kuna jamaa nimeona kabadili nyumba zake za kupanga kuwa lodge na anapata wateja . Nyumba zangu nzuri kulipo Kwa huyo mshkaji wangu
AiBnB ni nzuri kwa mikoa mikubwa hasa ukiwalenga wataliii. Unaweza kupangisha kuanzia dollar 20 kwa chumba hadi dollar 500 kwa siku kutokana na nyumba yako iko wapi na viwango vyake.

Pia unaweza kupangisha kwa muda flani hivi tu. Mfano unaweza ukahama kwa siku mbili tatu, weekend, wiki moja, mbili ukapangisha halafu ukarudi ukakaa mwenyewe kukaa au ukaishi na mteja as host family.

Ukishapata review nyingi za kutosha inakuwa rahisi. Kupata pesa nzuri, na wateja wengi. Nyumba inabidi iwe na viwango.

Hosteli nayo ni biashara nzuri, Unaweza ukapangisha hadi vijana hadi 100 au zaidi. Ila inahitaji usimamizi wa karibu.
 
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.

ivi watanzania type yako kumbe bado wapo!!

mi naona humu yamejamaa mambumbu
 
Back
Top Bottom