Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Tatizo la kusoma st kayumba unakuwa huna strong connections unless ziwe zile special schools. Yaani utajikuta unamaliza lakini marafiki zako wengi watakuwa katika positions ambazo hazimsaidii mtu kati yenu kuondoka katika poverty circle

Yaani circle nzima ya marafiki si ajabu ukakuta huna contact ya kukuambia kuna nchi flani ulata ina fursa flani
Kwenye hizi english medium wazazi wengi wanasomesha kwa vipato vya ofisini nje ya hapo ni chaalii
Ambapo wakishastaafu kama hawakuwekeza vizuri basi maisha yanabaki kuwa ya kawaida tu
Kama ni connections peleka international schools na wa huko wote wanajiweza
 
Miezi michache iliyopita nilianzisha Uzi hapa jf wenye title" Tunaowatoa watoto wetu shule za English Medium na kuwarejesha kayumba njooni tufarijiane hapa"

Soma: Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane

Lengo la Uzi lilikuwa kupata watu watakao nipa "faida" nitakazozipata kwa kuwarejesha watoto wangu Kayumba plus maneno ya kunifariji ambayo yatasaidia kujustify uamuzi wangu.

Sababu ya kuwarejesha kayumba wanangu ni kuyumba kiuchumi. Nilipata maoni mengi mazuri. Miongoni mwa maoni niliyopata hapa JF ni pamoja na:

1. Itanisaidia kuokoa pesa ambayo ninaweza ku invest katika maeneo mengine muhimu kama vile kuwanunulia viwanja na kuwajengea nyumba watoto wangu so that wanapofika level ya chuo at least kila mtu awe na nyumba yake moja.

2. Sitokuwa na stress za ada plus mbaya kuliko zote ile stress maalumu ambayo mzazi unaipata wakati mtoto wako amerudishwa nyumbani ada, wakati wenzake plus jirani zako wanaosoma kayumba wanaenda shule.

Nje ya JF nilipata ushauri kutoka kwa

1. Binti yangu; yeye yupo form three shule ya kayumba pia. Nilimsomesha English Medium kuanzia la kwanza. Anasema daddy kuna watoto wamesoma shule za kiswahili lakini wapo vizuri sana darasani kuliko waliosoma shule za kiingereza.

2. Brother wangu wa mtaani ambaye na yeye kawarudisha watoto wake kayumba. (huyu kasomesha hadi chuo but still bado ana watoto wa primary). Alikuwaga kichaa wa shule za English medium.

Anasema mdogo wangu mtoto wako umsomeshe kayumba au English Medium mwisho wa siku wote watakufa watazikwa…(anataja jina la makaburi ya mtaani kwetu)

Akaongeza: Tofauti ya kayumba na English Medium ni lugha tu lakini mwisho wa siku wote wanaandaliwa kuajiriwa..

Kingine siku hizi watoto wanaharibika sana so hakuna guarantee mtoto wako atakuja kuwa nani hapo baadae.

Akaongeza "shule nyingi za English Medium zinawafanya wanafunzi hasa watoto wa kiume kuwa watoto walaini laini (ana experience na watoto wake mwenyewe na rafiki zake). Halafu haziwafundishi watoto kuhusu uhalisia wa maisha zaidi ya kuwakaririsha masomo so bora umpeleke kayumba akapambane na kukomaa huko.


MIEZI MIWILI BAADA YA KUFANYA UAMUZI.

1. Nimenunua kiwanja nje ya mji ( ilala rural/ mvuti) kwa Tsh. laki tisa na mwezi ujao Insha'allah nitapiga msingi( fundi wangu yupo Kinondoni ambae alinijengea nyumba yangu ya kwanza utaratibu wake wa kazi huwaga ni wewe ukiwa na hela yoyote hata laki tano niite kwa lako tano hiyo hiyo nitafanya kitu. Next time ukipata laki tatu niite. Hadi nyumba yako itakamilika. Huyu ndo alinifanya nikajenga nyumba yangu ya kwanza. Tukiwa Kinondoni shamba au Hananasif tunaangalia ndondo anapokea simu za watu anaowajengea nyumba anasema “huyu anauza mchicha, huyu mama lishe etc”. Nikawa inspired.

2. Kuhusu somo la kiingereza nimenunua vitabu na CDs ambayo madogo watakuwa wanajifunza wakiwa home plus tuition ya nguvu ya kiingereza.

Mungu akinipa uhai nitafanya vitu vikubwa sana kwenye familia yangu.

Kama uwezo wako mdogo, unaishi nyumba ya kupanga uswahilini, uchumi wako umeyumba, sikushauri uhangaike na English medium.

Mpeleke mwanao kayumba wewe upambane kutafuta hela.
Safi yote heri
 
Mi mtoto wangu atasoma shule bora zisizo karirisha kufaulu.

Huwezi kuta hizi shule za International zikitoa ranking baina ya wanafunzi
Ranking kwa wanafunzi haina maana kabisa
Hivi wanategemea darasa zima wote watakuwa wa kwanza 😄
 
Mkuu watu hawaelewi, hao wanaowaona laini ndio wana connections na akili za kuishi soft life zaidi. Imagine mtu kasoma na watoto wa mawaziri, diplomats, businessmen yaani circle nzima ipo loaded. Ndio ulinganishe na mtu kasoma na watoto wa wakulima na wafugaji

Halafu humu watu wanajitoa akili, yaani unawatumia kina Nyerere, Mkapa au Pinda leo hii kama successful stories na wakati dunia yao na yetu ni mbingu na ardhi..

Kiukweli hata kama primary ntawasomesha shule za kawaida ila kuanzia o level acha wakapambane na kutengeneza future connections na exposure
Connections inatakiwa iwe mutual broh
Ukijikakamua kupeleka huko iwe kwa ajili ya elimu bora sio connections za kujipendekeza sabb huko no body gives a f#@&^
 
Hizi ni stori tu kama una Hela uchumi wa uhakika peleka mtoto English medium kama huna peleka kayumba lakini hizi habar kwamba mtoto akisoma kayumba anakuwa strong sijui anakuwa na uwezo zaidi na kwamba anaesoma Medium anakuwa nyolonyolo sjui hajui hesabu hizo ni stori za vijiweni sawa na kusema tajiri akifa hazikwi angani atazikwa ardhini na maskini
 
Hizi ni stori tu kama una Hela uchumi wa uhakika peleka mtoto English medium kama huna peleka kayumba lakini hizi habar kwamba mtoto akisoma kayumba anakuwa strong sijui anakuwa na uwezo zaidi na kwamba anaesoma Medium anakuwa nyolonyolo sjui hajui hesabu hizo ni stori za vijiweni sawa na kusema tajiri akifa hazikwi angani atazikwa ardhini na maskini
Story za vijiweni kweli.
JamiiForums1220832395.jpg
 
Connections inatakiwa iwe mutual broh
Ukijikakamua kupeleka huko iwe kwa ajili ya elimu bora sio connections za kujipendekeza sabb huko no body gives a f#@&^
Mkuu usidharau ishu ya connections! Tuna mifano hai kitaa. Ebu fuatilia stori ya Makonda ndio utajua maana ya connections Bro!
 
It’s a shame kwamba wanaochangia mada humu ni wanaume!!! Tangu lini mwanaume akawa na uchungu na watoto? Mostly wanawake ndo wanatamani watoto wao wasome shule nzuri wapate exposure ya kujipambania. Shule anaenda kusoma hayo mengine unamfundisha wewe nyumbani. Sadly hao wanawake wenye uchungu na watoto ndo wameruhusu ‘jamii’ iwa label as servants of the house wanatulia nyumbani wanasubiri mwanaume akatafute alete watoto watasoma shule anayotaka baba.

From my experience the last time, Baba mtu alimtoa mtoto wake english medium akampeleka kayumba. Mwanamke anakuja kustuka mwaka unaofuata mume anasomesha
mtoto wa dada ake st Mary’s, wa mchepuko yuko english medium na ameanza kumjengea huyo mwanamke nyumba. Sasa najiuliza, mtoto wake kamkosea nini hadi amfanyie hivyo? Wanaume wengine mmepewa mamlaka ya kuongoza familia but you are dumb!
 
Mimi mwenyewe nimesoma hizo english mediums kwahio naongea kitu nakijua
Kwanza wazazi wachache unakuta wana bizz kubwa kama kina bakhresa etc
Inawezekana umeishia wapi! Kuna T.O mmoja wa hivi karibuni kutoka Kanda ya Ziwa. Anatoka familia ya kimaskini sana hadi alikuwa anaahirisha masomo akapige vibarua. Baada ya kuwa T.O. form four, akapewa ofa ya kusoma Feza Boys. Sasa hivi kamaliza form six na sio tena yule wa kupiga vibarua! Connections zipo hadi Ulaya Bro!
 
Hapo tupo pamoja ila hilo toto chafu la kishua bila shaka kwa sasa lina maisha safi 😁😁. Maana ukitokea familia nzuri halafu kichwani akili ikiwepo, kutoboa ni must
Yuko mbali sana kimaisha sababu Advance alikuja kutulia na kuachana na ujinga akapiga PCM one ya 4. Chuo alisomea nje. Mara ya mwisho nilikutana nae ana kampuni yake na kuna kazi alikuwa anafanya na Tigo. Mimi nimetoka poor family ila kusoma na watoto wa kishua imenisaidia sana... imenitoa tongotongo nyingi tofauti na ningesomea kijijini kwetu. Mimi pia sasa hivi ni wa kishua self-made
 
Back
Top Bottom