Mrejesho wa taarifa ya ajali iliyotokea Kisutu mnamo majira ya saa 05:45

Mrejesho wa taarifa ya ajali iliyotokea Kisutu mnamo majira ya saa 05:45

Dereva wa mwendokasi kwanini akwepe Rav4 yenye watu wawili ilhali anajua Gari lake lina watu wengi zaidi tena wengine wakiwa taifa la kesho?! Busara ilikuwa ku-hit head-on Rav4 ili kuokoa majority
Binadamu instincts zinamwambia akwepeshe
 
Lazima itakua edited,bioashaka alikua yupo kwenye panic mode.
Nadhani hii ya kujiweka wazi,kila mmoja anakua na nafasi ya kukosoa,ndiyo inafanya polisi wawe na watu wanaojiona wangekua wao,wangefanya zaidi.
Majeshi mengine hayapati criticism hovyohovyo hivyo,mfano Magereza et al.
Polisi awe kwenye panic mode
 
Naiweka hapa muone wenyewe...

MREJESHO WA TAARIFA YA AJALI ILIYOTOKEA KISUTU MNAMO MAJIRA YA SAA 05:45

Mnamo majira ya saa 06:58 niliweza kufika Eneo la tukio nilikuta ajali imetokea gari ya mwendokasi yenye usajili wa
Plate No: T 122 DGW
JINA: SHABANI NGAUGIA
Ilipata ajali Eneo la Kisutu mbele kidogo ya mataa ilikuwa inatoka Kivukoni kwenda Kimara.

Chanzo cha ajali dereva wa mwendokasi alikuwa anatoka Kivukoni kwenda Kimara alifika mataa wakati anavuka kuna gari ndogo aina ya RVA4 yenye namba ya usajili T 978 DHZ ilikuwa ikitokea posta mpya ikielekea Kivukoni ilikuwa inapita pasipo kuangalia dereva wa mwendokasi alimuona akawa anamkwepa ndipo alipoenda kugonga flame za maduka na kuleta itirafu nje ya maduka.

Ndani ya gari ya mwendokasi kulikuwa na abiria wanafunzi na wananchi wamepata majaraha madogo madogo walipelekwa Muhimbili kwa check up ila dereva wa mwendokasi ameumia sana sehem ya mguuni yupo Muhimbili akiendelea na matibabu.

Wakati ajali imetokea gari aina ya RVA4 iliyosababisha ajali ilikuwa inakimbia kuelekea Kisutu kufika mbele ikapata ajali ikagonga ukuta wa shelli ya puma Kisutu na kuaribika. Waliokuwa ndani ya gari hiyo ndogo waliumia na kupelekwa hospital dereva wa gari ndogo alivyofika hospital alikimbia akabaki Majeruhi mmoja ambae ni mwanamke.

Katika ajali hii iliyotokea akuna vifo vilivyotokea isipokuwa kuna Majeruhi na wote wako Muhimbili kwa matibabu ila dereva wa mwendokasi na watu wanne wanahali sio nzuri sana.

Reported by
Overall Incharge
Shani Mussa.
&
Zonal Incharge
Amina Juma.
Ungetuambia ww wapi alipokosea siye wengine la nne B
 
Kama unatetea uandishi wa Shanni inasikitisha sana. Mkuu ni kweli kila taaluma ina uwasilishaji wake lakini taaluma ya upolisi kama moja ya matawi ya taaluma ya sheria haina uwasilishaji wa hovyo hivi.

Mfano, alipoelezea chanzo cha ajali kazunguuka bila sababu kabisa angeweza kusema hivi;

CHANZO CHA AJALI
''Ni uzembe wa dereva wa gari aina ya RAV4 namba T___ iliyokuwa ikitokea _ kuelekea _ ''

Sio kuleta stori zisizo na maana, ndio maana Mahakamani tunawapiga sana Jamhuri sababu ya ubovu wa uandikwaji wa maelezo polisi.

Hakuna gari inaitwa gari ya mwendokasi, mwendokasi ni kitu gani hicho? angesema tu;

''gari inayomilikiwa na UDART namba _ mwendokasi inayofanya safari zake na ___''

Yasije yakawa ndio maelezo yatakayotumika Mahakamani, atalia mtu
Sasa nimeelewa nadhani ww ni mwanasheria mkuu
 
Mkuu Mungu ndio mweza wa yote. Sisi tulishawahi pata ajali pale karibu na mto Wami Busi ilivingirika kama mara tano hivi na ikawa nyang,anyang,a lakini tulipona wote isipokuwa wanawake wawili walitenguka kiuno na mkono tu lakini ukiiona Busi iliisha kabisa. Mungu ndio mpangaji wa yote.
Mlipona wote isipokua ,

Dah nchi ngumu hii hata uandishi shida
 
Back
Top Bottom