Mrejesho wa taarifa ya ajali iliyotokea Kisutu mnamo majira ya saa 05:45

Mrejesho wa taarifa ya ajali iliyotokea Kisutu mnamo majira ya saa 05:45

Madogo Sana,?

Flame- frame
Itirafu- hitilafu
Sheli ya puma- petrol station ya puma

Wana Hali sio nzuri Sana - Wana Hali mbaya

Yaani makosa kibao ya kisarufi na kilugha bado huoni ?
Chukua chupa isage iwe vipande vidogovidogo karibia sawa na mchanga kisha changanya na pilipili halafu chukua glass ya maji unywe huyo mchanganyiko. Itasaidia kukutibu huo upumbavu wako.
 
Chukua chupa isage iwe vipande vidogovidogo karibia sawa na mchanga kisha changanya na pilipili halafu chukua glass ya maji unywe huyo mchanganyiko. Itasaidia kukutibu huo upumbavu wako.
Ndio upeo wa Akili yako ulipoishia
Kilaza period,Rudi shule matusi na ubaradhuli hayatokusaidia
Tatizo Elimu, Elimu, Elimu
Alijisemea lowasa
 
Natamani wangetokea waandishi wa habari aidha wa radio au magazeti.

Wafatilie taarifa za huyu muenda kwa miguu kujua familia yake ikoje wanaomtegemea nyuma yake.....😔😔😔😔
Wakiamini baba/mume/kaka/shemeji/baba mdogo/mjomba.... atarejea leo jioni na chochote kwa ajili ya rizki ya familia.....

Walau kama ana mke au watoto basi tulioguswa tutoe mchango wa kufariji familia...😔😔😔

Na wakiweza onesha mahala familia yake ilipo kila atayeguswa na huyo mtembea kwa miguu basi kila mmoja atapeleka alichonacho kama huruma iliyotujia kwa lililompata binadamu mwenzetu.

Najua matukio ni mengi, hili sio la kwanza na sio la mwisho, huwezi changia yote ila binadamu huwa kila mmoja kwa namna yake huwa anaguswa mahala kutoa.

Kutoa ni moyo.😔😔😔
Imeniumiza mno mno naitafakari familia yake ...hakika binadamu tunatembea na kifo kwenye viganja vyetu vya mkono hatujui hata sekunde 10 zijazo jina linaweza badilika likawa marehemu.
 
Kila taaluma ina uwasilishaji wake ulitaka aandike kama bar vicha anatoa tamko

USSR
Wewe unaona sarufi alizotumia zipo sahihi officially?

Hivi mzee kifimbo cheza wa "sani" alipotelea wapi?
 
Sijui ni kwanini waTanzania tunapenda sana ujuaji......yaani unaacha kuzingatia mambo ya misingi katika jambo la msingi unazingatia vitu vingine having msingi.......??

Katika hali ya kughafirika mtu unapoteza umakini wa mambo........

NB
Yule bwana mpita inawezekana kapona, tusipende kubishana mambo yaliyo nje upeo wetu kwa kutumia utashi wetu......Mungu naye ana shani zake.......
 
Madogo Sana,?

Flame- frame
Itirafu- hitilafu
Sheli ya puma- petrol station ya puma

Wana Hali sio nzuri Sana - Wana Hali mbaya

Yaani makosa kibao ya kisarufi na kilugha bado huoni ?
Wewe nae acha ujuaji wakati hujui kitu.
Petrol station ya puma-kituo cha mafuta cha puma.
 
Me too jamani nilitamani angekua mbio moja na huyo mwenzie wakanusurika
Mi nimeangalia kwa makini.

Inaonekana hakukandamizwa kwenye huo ukuta bali amepushiwa akabwagwa chini na kasi ya gari ikawa imepozwa na ukuta.

Ninavyoelewa mambo ya ajali, huyo jamaa yaweza kuwa "kudra" imemuokoa na baada ya shock ile akasimama na kujikung'uta mavumbi na kusepa ama amejeruhiwa kidogo tu.
 
Sijui ni kwanini waTanzania tunapenda sana ujuaji......yaani unaacha kuzingatia mambo ya misingi katika jambo la msingi unazingatia vitu vingine having msingi.......??

Katika hali ya kughafirika mtu unapoteza umakini wa mambo........

NB
Yule bwana mpita inawezekana kapona, tusipende kubishana mambo yaliyo nje upeo wetu kwa kutumia utashi wetu......Mungu naye ana shani zake.......
Alivyonyenyuliwa na kubwagwa bila kukanyangwa ile ilikuwa ndiyo manusura yake, mi ajali nazijua vizuri.

Kama ni majeruhi, basi inaweza kuwa ni michubuko midogo tu.
 
Sijui ni kwanini waTanzania tunapenda sana ujuaji......yaani unaacha kuzingatia mambo ya misingi katika jambo la msingi unazingatia vitu vingine having msingi.......??

Katika hali ya kughafirika mtu unapoteza umakini wa mambo........

NB
Yule bwana mpita inawezekana kapona, tusipende kubishana mambo yaliyo nje upeo wetu kwa kutumia utashi wetu......Mungu naye ana shani zake.......
Alivyonyenyuliwa na kubwagwa bila kukanyangwa ile ilikuwa ndiyo manusura yake, mi ajali nazijua vizuri.

Kama ni majeruhi, basi inaweza kuwa ni michubuko midogo tu.
 
Kuna picha inamuonyesha katupwa hapo mbele ya gari kajeruhiwa vibaya sana
Mi nimeangalia kwa makini.

Inaonekana hakukandamizwa kwenye huo ukuta bali amepushiwa akabwagwa chini na kasi ya gari ikawa imepozwa na ukuta.

Ninavyoelewa mambo ya ajali, huyo jamaa yaweza kuwa "kudra" imemuokoa na baada ya shock ile akasimama na kujikung'uta mavumbi na kusepa ama amejeruhiwa kidogo tu.
 
Naiweka hapa muone wenyewe...

MREJESHO WA TAARIFA YA AJALI ILIYOTOKEA KISUTU MNAMO MAJIRA YA SAA 05:45

Mnamo majira ya saa 06:58 niliweza kufika Eneo la tukio nilikuta ajali imetokea gari ya mwendokasi yenye usajili wa
Plate No: T 122 DGW
JINA: SHABANI NGAUGIA
Ilipata ajali Eneo la Kisutu mbele kidogo ya mataa ilikuwa inatoka Kivukoni kwenda Kimara.

Chanzo cha ajali dereva wa mwendokasi alikuwa anatoka Kivukoni kwenda Kimara alifika mataa wakati anavuka kuna gari ndogo aina ya RVA4 yenye namba ya usajili T 978 DHZ ilikuwa ikitokea posta mpya ikielekea Kivukoni ilikuwa inapita pasipo kuangalia dereva wa mwendokasi alimuona akawa anamkwepa ndipo alipoenda kugonga flame za maduka na kuleta itirafu nje ya maduka.

Ndani ya gari ya mwendokasi kulikuwa na abiria wanafunzi na wananchi wamepata majaraha madogo madogo walipelekwa Muhimbili kwa check up ila dereva wa mwendokasi ameumia sana sehem ya mguuni yupo Muhimbili akiendelea na matibabu.

Wakati ajali imetokea gari aina ya RVA4 iliyosababisha ajali ilikuwa inakimbia kuelekea Kisutu kufika mbele ikapata ajali ikagonga ukuta wa shelli ya puma Kisutu na kuaribika. Waliokuwa ndani ya gari hiyo ndogo waliumia na kupelekwa hospital dereva wa gari ndogo alivyofika hospital alikimbia akabaki Majeruhi mmoja ambae ni mwanamke.

Katika ajali hii iliyotokea akuna vifo vilivyotokea isipokuwa kuna Majeruhi na wote wako Muhimbili kwa matibabu ila dereva wa mwendokasi na watu wanne wanahali sio nzuri sana.

Reported by
Overall Incharge
Shani Mussa.
&
Zonal Incharge
Amina Juma.
Uandishi mbaya sana huu. Haueleweki.
 
Back
Top Bottom