Mrisho Gambo amvaa Lema, amtaka alipe madeni yake kwanza

Mrisho Gambo amvaa Lema, amtaka alipe madeni yake kwanza

Gambo wewe hukumuelewa Dr. Samia, amekataza matusi ya aina zote! Hayo unayo hubiri kuwa Lema ana madeni, awapigie magoti wazungu etc, ni matusi!
Hizo ndizo siasa za kutukanana. Madeni ya Lema ni personal kama sura yake ilivyo personal! Ukisha sema Lema ana kichwa kama cha mbuzi, Lema anakojoa kitandani, Lema ana madeni etc yote hayo ni kumtusi Bwana Lema.
Maana hayo yote angekuwa nayo hayamzuii kutupigania sisi watanzania kupata haki zetu.
Na tusi jingine ulilosema ni kuwa Lema ni mjomba wako! Hiyo inalisaidia nini taifa letu? Awe mjomba asiwe mjomba wewe fanya kazi uliyotumwa kufanya. Na hili liwe onyo kwa viongozi wote, mkae chini mtafakari matusi aliyokataza Dr. Samia ni yapi/nini - nasema hivi maana mpaka sasa hamuelewi siasa Safi ni nini. Kurushiana vijembe, kejeli, ni matusi pia. Na asinge ishia hapo Dr. Samia - angeendelea na kusema atakaye msema vibaya Dr Magufuli (marehemu) ashughulikiwe. Ruto wa Kenya alitamka wazi kwamba siasa za Kumchamba Kenyatta zisitishwe mara moja na ikawa hivyo. Tanzania tunataka siasa za kutuletea maendeleo siyo za vijembe.
Ukweli huwa unauma, dawa ya deni ni kulipa na siyo kujibanza Canada.
 
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mh Mrisho Gambo a.k.a kiboko ya mafisadi, anampongeza Rais Samia kuruhusu mikutano ya hadhara kwani sasa wanaume watapimwa jukwaani na si kwa mbeleko tena.

Bwana Gambo amemtumia salamu Godbless Lema kwamba kabla ya kuliota jimbo la Arusha mjini ahakikishe amelipa madeni yote na pia aongeze juhudi za kuwapigia magoti wazungu ili waendelee kumlea yeye na mke wake pamoja na kumlipia ada za watoto wake.


Gambo Arusha hawamkubali wala nini, na analifahamu.
 
Ana hofu Gambo

Huyu alibebwa kwa mbeleko ya mwendazake

Wabunge wote wa kubebwa wamechanganyikiwa

Yule wa kuwapeleka Birngham City kule kawe..... Bado
Lema hawezi kumshinda Gambo kwa namna yeyote Arusha. Upepo wa CHADEMA wa miaka hiyo haupo tena.
 
Back
Top Bottom