Mrithi wa Samia ana kazi nzito kurudisha uchumi wa Tanzania kwenye Mstari

Mrithi wa Samia ana kazi nzito kurudisha uchumi wa Tanzania kwenye Mstari

Uwe na adabu wewe kwa Rais wetu ,hata Kama umekosa malezi ya wazazi wako jaribu kuwa na heshima kwa mh Rais.usiandike hapa Kama mlevi wa gongo.
Heshima ya kiongozi hutokana na kuingia madarakani kwa njia za heshima. Uchaguzi wa 2020 haubebi jazba yako.
 
Haya ni maoni yako na unaruhusiwa kuwa nayo. Ukiuliza wafanyabiashara halisi watakwambia namna SSH anavyoufufua uchumi uliokufa kipindi cha awamu ya tano.

Nenda kaongee na wenye frames zao kula Masaki , Kinondoni na katikati ya jiji watakwambia ahueni wanayoipata kipindi hiki cha Samia kulinganisha na cha JPM.

Sijui ulikuwa na umri gani wakati wa Magufuli kiasi cha kupitwa na ule unyama aliokuwa anawafanyia wafanyabiashara wa kanda ya kaskazini mpaka wakafunga mashamba ya maua wakati soko likiwa bado lipo kule Uholanzi.

JPM pengine alikuwa na nia njema lakini kuonyesha ule utayari wa kuumiza baadhi ya watu na wakati huo huo akawa na utayari tena wa wazi wazi kabisa wa kuwabeba baadhi, ule ulikuwa ni ufa mkubwa sana wa uongozi wake.

Ukosefu wa hekima ya kuishi na watu haswa jamii ya wafanyabiashara. Hakuwa na kule kujali vilio vya wadau wake muhimu wa maendeleo pia akawa na ukosefu wa busara za kuongoza taifa la Tanzania.

Samia anao uwezo wa kusikiliza na hafanyi maamuzi bila ya kufanya utafiti wa kina juu ya faida na madhara ya maamuzi atakayofanya.

Hii account imekuwa hacked!🙆
 
Back
Top Bottom