Msaada: Naomba kupewa gharama za hatua hizi za ujenzi

Boss haina mjadala hio, Spanish Tiles.
Ulisema kuna mchina grade A na ni nzuri je utazitambuaje kama ni grade A.... Maana spanish bei yake mkuu naona parefu maana nyumba yangu tiles inakula 148.67 m² na nimeulizia pale mikocheni naona box 49,000 spain tiles, naona nitafute mchina mzuri na za ukutani nitafute za india. Karibu kwa ushauri.
 
Chinese grade A nyingi ni 50*50 na 60*60 hata thickness yake ni kubwa kuliko nyingine. Nenda dukani linganisha utaona tofauti,maelezo hayawezi kutosheleza.
 
Sitting room na corridors weka Spanish, vyumbani na bafuni weka mchina.
 
Tiles inategemea unataka Spanish au Mchina.
Mchina grade 1 sitting room 50*50 ndio zinapendeza box moja 30,000-35,000/- box moja sqm 1.5. Sitting room yako 20sqm utahitaji 14boxes ambayo ni 490,000/-.
Fundi anachaji sqm moja 5,000 -
Sikuiona hii ya gharama za fundi wa tiles thanks prond
 
Tiles inategemea unataka Spanish au Mchina.
Mchina grade 1 sitting room 50*50 ndio zinapendeza box moja 30,000-35,000/- box moja sqm 1.5. Sitting room yako 20sqm utahitaji 14boxes ambayo ni 490,000/-.
Fundi anachaji sqm moja 5,000/-
Mkuu kujua mchina makini yani grade 1 unazitambuaje mkuu nisije ingia choo cha kike, hapa ndipo shida ilipo
 
Inategemea unataka finish ya aina gani ila standard rate mkuu uwe na 25 milion imenyooka pale nyumba finish mkuu hapo ndo utajua umejenga au umebomoa ila 25 milion inaondoka kweupe
 
Tembelea maduka wewe mwenyewe. Tronic nzuri. Kwa nyumba zetu watu wa chini huwezi kuwaepuka wachina ila unaangalia mchina kiwango kizuri kidogo. Tembelea maduka ya Kariakoo mwenyewe utajua bei.
Wire 6mm,4mm,1.5mm,2.5mm switch zote,circuit break tronick, 1 gain 1 way, 3gain 2 way vyote hivi tayari nimeshanunua sasa swali ni hivi wakati wa kusuka wire kwenye roof nifanye ya surfaces au nitumie conduct pipe.... Maana ya surface nimeona panya wasije kula hizo wire mbeleni au sio rahisi maana kutumia tena pipe ni gharama inanitoa kwenye railway
 
Huko kwenye waya sijui zimesukwaje sijawahi kupanda kuangalia. Hakikisha unazuia panya....sio kwa kula waya tu ila hata kiafya,usafi.
 
Hapo namba 7 naongeza na kufunga switch za umeme pia kazi ya mwisho baada ya rangi yaani akifanya wiring aache nyaya zimechomoza kisha akimaliza rangi aweke shitch sasa na hata aluminium

Kama rasilimali fedha inaruhusu, mtiririko wako ni mzuri ila kwa wazee wa rasilimali ni chache ila mahitaji ni mengi mtiririko utakuwa hivi
1.Pulambingi
2.Blandaringi
3.Plasta ili kuzifukia zile konduti paipu za kupitishia nyaya
4.Kuweka gipusamu bodi
5.Aluminiamu ila kama fedha ni utata ana haraka ya kuhamia aluminiam inaweza ikawa namba 4 alafu jipusamu inakuwa namba 5
6.Vigae kwa kuwa wakati wa kuweka jipusamu bodi fundi atakaefunga jipusamu bodi inatakiwa ampe na kazi ya kufanya skimingi ya jiusamu na ukuta hivyo kazi ya uchafu itakuwa imeisha katika hatua namba 4 hivyo itabaki kupiga rangi tu anayoitaka muda wowote akipata fedha (hata yakimshinda anakoishi anaweza akaamua kuingia lakini kazi za karaha zinakuwa zimeisha
7. Wiring alafu inafuata rangi na kufunga switch socket etc
 
Mm yangu nliiwekea mil9 nihamie kumbe nlikuwa nawaza kitoto. Saiz ina mil30 haijaisha na nlihamia ikiwa na 15mil, ikiwa haina lipu, sakafu,blandaring, wala umeme nliweka solar but akat naingia hata solar sikuwa nayo
Kupanga ni kuchagu mkuu hahahaha expected budget and actual budget havijawahi kuwa halisi[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Sitting room na corridors weka Spanish, vyumbani na bafuni weka mchina.
You have a good point ila vipi kwenye mng'aro hazitatofautiana sana[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
watakupotosha humu wana makadirio ya juu sana za juu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…