Msaada: Nina 30,000 hapa, nahitaji kuanza biashara yoyote ile sasa hivi. Niko DSM

Niliwapa under 3.5 pamoja na tz
Me nliweka washinde tz siwekag kwenye mkeka wangu siwaamini, ila huu uzi umenifundisha kitu, kama huyu dada kweli ni hause g basi huyu sister ana roho ya kihustler na kama hadanganyi kuna siku atakuja kutusua yan kama kweli ana 30000 na ana confidence ya kuanza kuiinvest hiyo hiyo kweli hapo nimemkubali aisee, akiwa na M3 huyu ni mtu hatari sana mastaaa
 
Njoo ligi ya brazil inaelekea ukingoni cheza corners tu zinatoa balaa chukua timu mbili over 8.5/9.5/10.5 tia laki mbili
 
Tatizo la jf sometimes story za kusadikika ni nyingi mno kuliko uhalisia unaweza taka saidia baadae unakuta ni mtu anajitungia tu ili watu wacomment.
 
Tatizo la jf sometimes story za kusadikika ni nyingi mno kuliko uhalisia unaweza taka saidia baadae unakuta ni mtu anajitungia tu ili watu wacomment.
Waongo wamekuwa wengi, ndio tatizo la watu humu na watu wa masihara wengi ila me nimechagua kumwamini akiwa anadanganya anajidanyanya mwenyewe
 
Elfu 30 hela za madafu ni sawa na US Dollar 12.Biashara inayowezekana hapo ni ,"Nunua beseni halafu uza mbogamboga na matunda".Unaweza kwenda buguruni kununua mbogamboga na matunda,nenda katembeze mitaani.Ukinunua chungwa mfano mia 100 hakikisha unauza mia 200 n.k
 
Nenda mabibo sokoni kanunue ndizi mbivu uza kitaa kwa mama ntilie, stand za mabasi

Waambie kula ndizi uongoze nguvu za kiume.

Zitaisha fasta. Sana
 
Kama umepata mwenyeji baada ya kutoka hapo ulipokuwa tumia vifaa vya mwenyeji wako choma chapati jiko weka nje ya nyumba unayoishi utakuja kinishukuru hiyo hela inatosha sana.
 
Huu mwezi nataka nifunge hesabu na 10 mil, nishafikisha 7.4 mil game za weekend nishaweka Mapema nasubiri matokeo.
Nlifikishaga 11m nikaongezea hela kidogo nkauza gari yangu nikanunua gari ya fuel consumpion ndogo ili nipunguze ukali wa maisha saivi nna kama 1.5m kama kepitol nataka niende nayo mdogo mdogo sitaki tamaa.
 
Duh hii imeenda
 
Nimejaribu kufuatilia kwa wauzaji wake. Hazina faida ndugu. Sio za kukurupukia kaka
Niliwahi kuuza karanga . Nilikuwa napata faida asilimia 100 na zaidi.
Ila nilibahatika nikawa nasupply kilo 50 na zaidi kwa mara moja, karanga zilizokaangwa. Baada ya wiki nalipwa pesa yangu safi kabisa.

Ila kupeleka kidogo kidogo kwenye maduka hutaona faida kivile.
 
Uza Mihogo

Nunua Mihogo ya 10k
mafuta 5k
karai,jalo,chumvi,deli 10k
5k ilobaki nunua magazeti nusu 1500
Vipakti vile vilaini vya 1000
Hilo 2500 ilobaki utajua uifanyie nn..

Kaanga vitumbua jioni

Mahitaji
Ndoo ndogo 2500
unga wa mchele
Kikaangio
deli la kuwekea vitumbua
magazeti/vifuko

Sitaji JIKONkwa sababu JIKO utatumia matofali mafiga matatu hutokosa wewe n mdada kuwa mpole tafuta mkaka akutaftie matofali na Vibao kwa mafundi seremala.

Piga Kazi.

Siku ya 1 mtaji wako utarudi na Faida itacheza 1000-5000

ikizidi 5000 TRUST me huna miezi miwili ya kuteseka. ikiwa chini ya Hapo pia Usikate tamaa utavuka tu ila fahamu. Hamna jambo jepesi eneo hili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…