Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Nimejitahidi kusoma uzii huu mpka hapa ninaogopa, yani siku ya leo kwangu haitokua nzuri.
Naomba kuuliza hivi unaondoaje hofu ya nyoka maana inanitesa kupitiliza. Nikiona picha yake usiku lazima nimuote, mara amepanda ukutani mara anatamba yan mradi niteseke usiku.
Naoondoaje hii hofu maana ni zaidi ya 10 yrs nahishi na fear ya nyoka, sikuwahi kugongwa na nyoka ila nikiwa nasoma shule enzi hizo, nilifua begi la shule kumbe lilidondoka sasa nyoka aliingia ndani ya begi, jioni baada ya prepo kufungua begi nieke madaftari nyoka akatoka ndani ya begi, kwanza sikuwahi kujua kua nna uwezo wa kuruka kiasi kile maana niliruka dekani nikarukia kitanda cha tatu bila kujua nliruka vipi
 
Nimejitahidi kusoma uzii huu mpka hapa ninaogopa, yani siku ya leo kwangu haitokua nzuri.
Naomba kuuliza hivi unaondoaje hofu ya nyoka maana inanitesa kupitiliza. Nikiona picha yake usiku lazima nimuote, mara amepanda ukutani mara anatamba yan mradi niteseke usiku.
Naoondoaje hii hofu maana ni zaidi ya 10 yrs nahishi na fear ya nyoka, sikuwahi kugongwa na nyoka ila nikiwa nasoma shule enzi hizo, nilifua begi la shule kumbe lilidondoka sasa nyoka akingia ndani ya begi, jioni baada ya prep kufungua nieke madaftari nyoka akatoka ndani ya begi, kwanza sikuwa kujua nna uwezo wa kuruka kiasi kile maana nlikua dekani nikatukia kitanda cha tatu bila
Kujua nliruka vipi
Yule nyoka mwenye jicho moja mbona humuogopi? 😂 😂 😂
 
Nyoka kamuuma paka anakukufa. [emoji849]

Then kamuuma mwanafunzi na hajakufa.[emoji56]

Ebu nyorosha maelezo mkuu, otherwise mnaweza mwagia mafuta ya taa ama diesel kuzunguka maeneo ambayo mnahisi huyo mgeni anaonekana.

Ama, nashauri mchome moto eneo linalo zunguka hiyo nyumba na hata ikiwezekana hayo maua mengi myateketeze kwa moto.
Hofu ni kitu mbaya sana
Amesema mwanafunzi kwenye kiatu wewe bwiga
 
Mmoja huyo alipitiliza kwenye homeground na pana kuku, sivyo aliishia kwenda ahera. 😂 😂 😂
Hiyo ndiyo size ya kuku, nyoka wengine size kubwa, kuku hatoboi! 🤣
IMG_20210527_123930.jpg
 
Msaada, kuna jirani yangu Kaingiliwa na nyoka mazingira ya nyumbani kwake, huyu nyoka ana week tangu aonekane mara ya kwanza, ila upo uwezekano ni zaidi ya week maana kabla ya hapo ilikua inatokea tu kuku kapotea, kelele za kuku bandani, usumbufu dirishani akiwa amelala n.k n.k.

Baada ya muda ndio akaonekana live. Kumtafuta imekua changamoto kwanza ni kwa mashaka maana yaweza kua naye anakutafuta au mshtukiziane akuwahi.

Na inaonesha ni mkali na ana sumu mbaya, Juzi paka wake alikua naye ndani, ile anatoka tuu nje paka akapiga kelele kutoka anamkuta paka ndio anakaukia, chini ya dk akawa tayari kafa.

Japo inaonekana alimjeruhi, maana mdomoni alikua na damu na ngozi.

Imebidi ahamishe watoto huku, hawakai tena pale. Mwenyewe anaenda kwa machale.

Nyumbani kwake kuna maua mengi sanaa yale yanayotanda mpaka ukutani, bustani ya mboga, kama mita 50 hivi kuna kijimto na nyasi nyingi, tumepatana leo tupulize ile dawa ya kuua mimea.

Kuna uwezekano anakuja na kuondoka, na si mara ya kwanza kuonekana maeneo ya nje, wanafunzi washamuona sana Kwa maelezo yao ashawahi mgonga mmoja wao kwenye kiatu.

Huyu ndugu tunamsaidiaje?
Jana kakutana na michirizi nje, akaishia nje.
Juzi katika kumsaka tukaambulia gamba tukasepa.
Mara anoe maua yanacheza au kuanguka.

Hakuna njia yoyote zaidi ya kumuua, ila njia gani sasa?

Naomba imani za kishirikina uwe ushauri wa mwisho.
Andika getini "Nyumba hii inalindwa na nyoka mkali"

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Fuga kuku. Kuku wangu juzi nilimuona anakula nyoka aliyejileta kiwanjani kwangu. Nafikiri watakusaidia sana.
 
Jana usiku Kama saa 6 nimeishiwa bando nilikuwa nafuatilia live fainali ya Europa Sasa kufika hatua za penati bqndo likaisha ikabidi nitoke nikaulizie matokeo Sasa ile narudi nikaona paka wawili Kama wanapigana na kimtindo palikuwa Giza.


Ile nakaribia nikagundua hawapigani Kama wanacheza na kitu ikanibidi nipakaribie kuangalia vzr wanacheza na kitu gani

Ase kumbe nyoka walikuwa wanacheza nae huku wakimpiga makofi na kuruka sasa wkt nimewasha tochi ya simu kumulika niangalie vzr wale paka wakakimbia na ndio walikuwa kizuizi wa yule nyoka

Ikanibidi nichukue jukumu la kuokota mawe na kumpiga yule nyoka ,Sasa kwenye ile nyumba kwa dirishani nasikia vijana mabishoo wa chuo bila Shaka wale wanabishana kuhusu mpira ,nikawa nawaita waje kusaidia maana yule nyoka alikuwa anataka kuingia kwenye tobo pale kwao walivyo wajinga wakawa wananiona chizi sijui wakakaa kimya na kuacha kubishana nikaendelea kuwaita wakajikausha


Nikajisemea kwanza sio kwangu najihangaisha bure wacha aingie ndani kwao watajijua wenyewe na ubisho wao,nikazima tochi nikasepa zangu, na nyoka alikuwa mrefu kweli


Paka wanasaidia ase nimegundua Jana night
[emoji23][emoji23][emoji23]mkuu hebu tufatie mrejesho kwenye hiyo nyumba!
 
Siyo nyegere tu mnyama yeyote ambaye atadevelope kinga ya nyoka hatokufa.

Nyegere amedevelope kinga kwa nyoka waliomzunguka maeneo yake ikatokea ameenda eneo jipya akakutana na aina mpya akigongwa anaweza akafa au akazima kidogo mpaka mwili wake utakapodevelope kinga mpya dhidi ya huyo nyoka.

Kuna binadamu hafi akigongwa na koboko na wote tunakubaliana kwamba koboko ana sumu kali.
Tufahamishe hii vzr ndugu.
 
Wazee kuna Nyoka wengine ninwakubwa mno..awali dikujua wapo nyoka ninwakubwa kiasi ukimuona kama uko pekeyako unaweza kimbia nyumba. Home miaka ya 2012 alitokea nyoka mmoja alikuwa anakula bata, bata walikuwa 200 waliliwa mpaka wakabaki 30, mwanzo tulihisi ninwatu wanawaiba ila kuna siku sasa akaonekana live yule mjuba. Kwanza alikuwa anaishi katika choo, yaani kile choo kiliterekezwa kilikuwa hakitumiki sana sababu kilijengwa kwa ajili ya mgahawa ( mgahawa ukafunhwa hivyo kile choo kikawa hakitumiwi ) sasa yule kiumbe ndimo alifanya makazi yake humo..

Yule nyoka hakuwa chatu, sababu chatu nawafahamu vizuri sana, na kwa ukubwa pengine hao chatu waunganishwe watatu kwa pamoja kwa upana na urefu. Nasema hivi sababu hiyo siku halikuja usiku mnene lilikuja mapema tu saa mbili usiku likaingia jikoni, kule jikoni kulikuwa na mamayangu mdogo anapika bahat nzuri ule muda anaenda kuangalia chakula ndio akawa anasikia mchakacho sasa, dah limejaa jiko zima! Lina macho makali kinyama, sasa ikabidi tuanze kuita watu maana nyumba ipo pembezoni mwa barabara na kuna stendi muda huo watu walikuwa wengi bado, wakaja na fimbo wengine nondo, wengine mawe, hahahaaa cha ajabu mawe yalikuwa yanadunda lijamaa likacharuka sasa linavimba mle ndani pa kutokea hamna , nje watu kama kijiji, yule m$&!ge unajua alibomoa lile jiko aliamsha timbwili mle ndani si la kitoto, watu wanapiga makelele ndo wanazidi mvuruga.. wenye mishale wakarusha, wa mikuki wakarusha, wa upinde wakafanya hivyo na mwisho kuna mdau akaja na Gobole lakini bado shughuri ilikuwa pevu. Sasa ikawa si jiko tena kuanguka na ukuta ukaangushwa upande mzima yule nyoka hafi anataka kue scape arudi kule chooni, sasa home pakageuka kama vita, ila hakuna anayejaribu kulisogelea, saa mbili mpaka inatimu saa nne usiku yule mwamba bado hajafa, wakaja watu wa mali asili toka Moro town nao wakashiriki sasa limeingia kwenye shimo nusu mwili umebaki nje, choo kikashuka kwa kupigwa mawe, boonge la msala kwa mwenye nyumba.. huku na huku mpaka saa tano ndio lile timbwili linaisha baada ya nusu ya nyumba ya marehemi babu kubomolewa kisa lijoka. Likavutwa mle shimoni mali asili wakalipakia kwenye canter wakaondoka nalo wakalichunguze mbelembele huko...hakika sijawahi ona nyoka kama yule iwe katika documentary ama mtaani. Wengi walihusisha na mambo ya tamaduni. ( Mambo meusi ) na mimi pia niliamini hivyo na tangu iyo diku mpaka leo hii siwezi lala nyumba ile aisee...yawezekana hakuwa nyoka wa kawaida.
 
Nenda maliasili ulizia kuna vijana wanakamata nyoka aina yeyote ile, watu wa maliasili wanawajua.
Mwanzo walikua wanakamata kwa ajili ya wafanyabiashara waliokua wanasafirisha nje, tangu biashara ilipopigwa marufuku hawa vijana wapo tu mitaani sema ujuzi hauzeeki. Unakumbuka yule chatu aliyetoroka kwenye box lake pale mpingo house keko? Vijana wa namna hii ndio waliitwa kumtafuta. Haikuchukua muda wakamleta mzima kabisa
 
Kwa kweli hata mimi mwenyewe sina majibu hapo ila ninachohisi aliingia ndani kupitia mlangoni kabla ya kufungwa na tukaishi nae bila kujua kabla ya kupata upenyo hadi chooni ama alichiba tokea kwenye karo nje akatokezea ndani na kuweka makazi pembeni mwa sinki yanamotokea maji.
Siku namuona choo kilikuwa hakijatumika kwa takribani masaa 24 maana hatukuwepo sasa nilipofika tu nilienda chooni kukojoa, ile mkojo unashuka nikamuona amekuja mbio ametoa ulimi (bila shaka alikuwa anataka maji yaani mkojo-nasema hivi kwa sababu nilishaona tena porini nyoka akirukia mkojo wa anaotoa mtu wakati wa jua kali)
Huyo nyoka atakuwa alikuwa na kiu ya maji. Mimi mmoja nilikuwa napishana naye chooni usiku kwa takribani siku mbili bila kujua nikidhani ni mjusi kwa sababu akili yangu haikutegemea kuwa kuna weza kuwa na nyoka ndani. Sema Mungu saidia alikuwa ni mdogo halafu ni hawa jamii ya weusi wanafuata panya ndani. Mara zote nilikuwa nashtukia tu mkia unapoteelea chini ya vitu nikawa najua mjusi lakini akili inakuja inakataa mjusi gani mweusi hivi sasa ukichanganya wenge la usingizi nikawa najipa moyo kuwa atakuwa mjusi tu. Na mara zote nilikuwa napishana naye wakati naingia chooni kujisaidia usiku kabla sijawasha taa yeye anakuwa ameshasikia mapema kuna mtu anakuja kwa hiyo tulikuwa tunapishana kabla sijawasha taa. Siku ya siku nimetoka zangu kwenye mishe mishe usiku nikiwa na chupa ya maji nimenunua mtaani sikuimaliza nikawa nimeiweka pembeni ya kitandani kwangu chini. Sasa kabla sijasinzia vizuri nikawa nasikia sauti isiyo ya kawaida pale chini nilipoweka chupa ya maji kumbe nilikuwa sijaifunga vizuri matone ya maji kidogo yalikuwa yamedondoka pembeni kidogo. Nikiwa na wenge la usingizi nikachungulia kupitia kwenye chandarua nilichokiona ni nyoka anakunywa yale matone ya maji sikushtuka sana kwa sababu nilishaua nje ya nyumba nyoka wakubwa zaidi yake. Nilichofanya nikuchukua ndala ninazotumia ndani wakati wa baridi maana ndio silaha iliyokuwa karibu nikambamiza kweli kweli akafa pale pale.
 
Back
Top Bottom