Msaada tafadhali: Nitumie njia gani kumsaidia Mtoto wangu ambaye ni mzito kidogo kuelewa Shuleni (Slow learner)?

Msaada tafadhali: Nitumie njia gani kumsaidia Mtoto wangu ambaye ni mzito kidogo kuelewa Shuleni (Slow learner)?

Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Peleka veta mapema utanishukuru.
 
Mkuu
Ikiwezekana Jaribu Kubadilisha Mfano Eneo Labda La Masomo Ya Ziada
Nina Mtoto Nilimpeleka Chekechea Miaka 2
Mwalimu Alikuwa Anawaimbisha Songs Tu


Kuanza Darasa La Kwanza Ikawa Shida
Nikampeleka Kwa Mwalimu Tofauti Sasa Hivi Yupo Sawa Anajua Kusoma Na Kuandika (KK,)
 
Mwache usimpe pressure kubwa,mtoto anetejifunza taratibu ni muelewa zaidi ,jambo la msingi mjengee kujiamini
 
Jaribu pia kumpatia huu mlo , imesaidia kwa upande wa watu wengine kuimarika kiakili na afya ya ubongo kiujumla.
 

Attachments

  • Screenshot_20250216-215656~2.png
    Screenshot_20250216-215656~2.png
    353.2 KB · Views: 2
Kushukuru ni kuomba tena.
Hebu jaribu hivi:
1. Akirudi kutoka shuleni uwe unakagua madaftari yake kuona ni katika masomo gani ndo kuna changamoto kubwa. e.g. Hesabu au Jiografia Haya ni kati ya masomo yanayowachanganya watoto.
2. Mwelekeze kwa kuzingatia alivyoelekezwa na Mwl. wake i.e. unakazia maarifa.
Halafu umtake afanye masahihisho then mpe kazi /homework ya aina hiyo hiyo na akimaliza sahihisha mkiwa pamoja.
3. Akifanya vizuri umpongeze au mpe zawadi yoyote. Akikosea usimgombeze hata kidogo bali mwelekeze tena kwa maneno ya kirafiki e.g. unaanza hv: Mmm; wee fulani mbona hapa umefanya vizuri halafu hichi kiswali kidogo namna hii kinakushinda? Hebu tufanye tena mm na ww.(mnafanya).........Umeona? umeelewa? Hebu sasa nenda tena karudie kwa uangalifu kufanya haya yafuatayo e.g. 5qns. zinatosha.
4. Jitahidi sana sana TV isiwe on; kusiwe na mazungumzo ya aina yoyote wakati akifanya H/W zake e.g. kuongea na simu au kuagiza kwa sauti kubwa jambo fulani lifanyike huko nje, kucheka-cheka hovyo n.k..Hayo yana-disrupt sana attention yake na kuhafifisha concentration ya kile anachofanya
NB: Na mimi nimekuwa na changamoto hiyo hadi sasa,nilijitahidi hata kuweka mwl. wa kumfundisha hapa nyumbani, kumpeleka Tuition lakini wapi - Ngoma ikagoma. Lakini nilishangaa na kufurahi sana hapo juzi kati (Feb 2025) nilipozingatia na.2 na 4; sasa anaweza kufanya hesabu(Maths) kuzidisha na kugawanya kwa njia ndefu, anazijua kwa kichwa orodha(Tables) 2-13; anajua kutumia dira (Cardinal compass rose) kueleza uelekeo wa kitu fulani kilipo (Cardinal na Ordinal compass directions).
Huyu wa kwangu yupo darasa la Nne(4) na ni Ke. Zawadi ninazompaga ni e.g. Namsifia-sifia na kumpongeza; namwahidi kesho tutaongozana kanisani au nampa pipi kijiti au namwacha akacheze na wenzake huko nje uani au namwuliza anapenda zawadi gani n.k. Tena huwa nafuatilia sana huko shuleni marafiki zake ni akina nani? Ninakuwa karibu sana na Waalimu wake esp. mwl. wa darasa.
 
Sasa ndio tumuache Mtoto apate Urithi mbaya bila kujaribu kumsaidia. Historia mbaya inaweza kuishia kwetu Wazazi na Watoto wetu wakawa tofauti nasi. Sitaki kumkatia Tamaa mwanangu
Kweli kabisa, jukumu lakupambania watoto lipo kwa wazazi, Allah atamfanyia wepesi na atakuwa sawa, mimi binafsi yalishanikuta kwa mwanangu wa kwanza, ila kwasasa namshkuru mungu yuko vizuri kwa kweli
 
wazazi wengi wanaharibu sana watoto kwa kuwachagulia njia ambazo sio sahihi..kila mtu duniani hapa amezaliwa akiwa na hatima yake yaani mungu amempa kipawa chake maalum iwe kipawa cha elimu,burudani,ufundi,afya,ujenzi,kilimo,uongozi,biashara,hostoria,usuluhishi na upatanishi,kusaidia jamii,michezo,urembo na mitindo,sayansi na vipawa vingine vingi sana yaani kila mtu ana kipawa chake specific ishu ni kufungua code tu ili ujipate njia ya hatima yako ambayo ndio itakupa mafanikio ikiwemo pesa na mali..kwa huyo mtoto kama ataendelea kuwa mzito kielimu basi jua elimu sio njia ya hatima yake.mzazi unatakiwa mchunguze mtoto ana kipawa gani kisha msaidie kufikia ndoto yake hiyo elimu iwe kama wajibu tu wa kuelimika..ila hiyo kumforce shule atafika hata chuo kikuu ila atakuja kuishia kuwa jobless si unaona tuna wasomi wengi wame graduate lakini wanafanya mishe tofauti na walichosomea tena wanaanza moja kujitafuta upya vyeti vya elimu havina msaada wakati huo..yote sababu elimu sio njia ya kufikia vipawa vya hatima zao..watu wanahangaika na elimu kumbe hagima zao zipo katika biashara au ufundi..kabla ya kumfosi mtoto apite njia utakayo mzazi msome kwanza amelalia upande gani ili uweze kujua kipawa cha hatima yake kisha muongoze afike kwenye hatima yake. sio ww mzazi umefeli kufikia hatima yako au huijui kabisa unaunga unga tu mjini alafu utake kumtoa na mtoto kwenye reli naye afeli kama ww na hii ndio sababu familia nyingi kurithi umaskini vizazi na vizazi kwa kutojua vipawa vya hatima zao ili wavitumie kuleta mafanikio ya kimaisha,mali na pesa..wengi wetu tunaishia kubangaiza mkono uende kinywani basi.
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni

1: Kufanya tathmini ya tatizo unaweza kumhusisha mwalimu au daktari wa watoto mwenye utaalamu mahsusi. Hii itakupa uelewa mzuri na kiasi cha tatizo na uwezo au ukomo wa mwanao katika uhalisia.

2: Kutambua maeneo husika anayopata shida, kutasaidia eneo halisi la kujielekeza. Kuna maeneo tofauti katika kujifunza au kupokea maarifa mapya.

3: Kujielekeza kwenye maeneo husika ili kumsaidia kupata mwelekeo chanya kirahisi bila kutumia harakati nyingi/resources.

4: Kuambatanisha lishe bora na mazoezi zingatifu kwa mhusika kulingana na ushauri wa mhudumu wa afya.

4: Kuhusisha/kuendelea kuwasiliana na wataalamu pale tatizo linapokuwa kubwa kwa uwezo wako kulimudu au mwendelezo usioridhisha.
 
Utakuwa umemuambukiza uzito. Maana nawe unaletaga habari hapa, mtu akiuliza zaidi hujawahi fafanua😂
Miaka 8 bado sana. Wanaokuwaga wazito mwanzoni huwaga na akili sana baadaye. Ni kwamba akili zao haitaki kuelewa juu juu tu. Wanataka kuzama ndiyo maana wanaonekana wanachelewa.

Mtafutie vitabu na zana za kujifunzia za kutosha awe anajifunza nyumbani.
 
Sasa ndio tumuache Mtoto apate Urithi mbaya bila kujaribu kumsaidia. Historia mbaya inaweza kuishia kwetu Wazazi na Watoto wetu wakawa tofauti nasi. Sitaki kumkatia Tamaa mwanangu
Haponi maombi tu,genes kuzibadili ni ngumu sana
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Hata wangu wa miaka 7 yuko very smart ila anachelewa kuelewa.

Kwa mfano dada yake kajuwa kusoma kabla ya kuanza shule . Lakini yeye mpaka dalasa la kwanza bado hajajuwa vizuri.

Ila ukiwa unaongea naye unaweza ukafikiri ni mtu mzima.

Kitu kingine wakati nawafundisha basikeli dada yake ilimchukuwa week moja kujifuza na kuendesha peke yake. Lakini huyu wakiume ilinichukuwa mwaka mzima kumfundisha basekeli.

Sasa hivi huyu wa kiume anajuwa kuendesha basikeli vizuri kuliko dada yake. Kitu ambacho nimejifuza

slow learner wanajifuza tafauti na watu wengine ila wakijuwa kitu wanakijuwa kwa mapana yake.

Kama mzazi unacho takiwa kufanya ni kuwa mvumilivu. Pia unapo ongea na mtoto wa hivyo usiwe mkali uwe mtulivu wa kusikiliza. Pia umuonyeshe upendo zaidi .

Kinacho wafanya kuwa slow sio upungufu wa akili bali ni mtazamo wao kuwa tafauti juu ya vitu vingi.
 
Mzngatie msosi wa kujeng kumbukumbuk
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Ana miaka mingapi
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Kuwa slow learner siyo shida hata kidogo, unaweza kuwa slow learner lakini ukawa unafanya vizuri class tena ukawa unabutua kuliko hao fast learners.

Slow learner ni mtu ambaye anapata kuelewa jambo kwa kuchelewa Yani processing speed yake inakuwa chini.

Kuna sababu kadhaa zinasababisha mtoto kuwa slow learner

1. Curiosity (udadisi)
Kuna mtoto anakuwa slow learner kwasabab ya kuwa mdadisi wa mambo Yani hataki kuweka mambo kwenye long term memory bila kuyathibitisha kuwa ni y kweli na mtu kama huyu huchukuwa mda mrefu kuelewa kwasabab ni lazima afanye uthibitisho kuliko kujikita ana kitu inayoitwa cognitive dissonance (mkanganyiko wa kiuelewa juu ya concept flan).

2. Sceptical learning (kujifunza kunakoambatana na wasiwasi)

Hapa mtoto anakuwa na wasiwasi juu ya anachojifunza kwahyo huhitaji muda mrefu ili kuondoa wasiwasi na kuruhusu kujifunza kitu (akili kukubali anachojifunza)

Solutions juu ya hii issue ya slow learning

Nasuggest huyo mtoto wako umtengee muda na mwalimu maalumu ambaye atatumia njia maalumu ambazo ni active learning methods yani njia ambazo zinamkeep mtoto kuwa activu muda wote

Njia ya pili ni kujifunza Kwa role playing yani learning through imitation and acting. N.k
 
Back
Top Bottom