Msaada tafadhali: Nitumie njia gani kumsaidia Mtoto wangu ambaye ni mzito kidogo kuelewa Shuleni (Slow learner)?

Msaada tafadhali: Nitumie njia gani kumsaidia Mtoto wangu ambaye ni mzito kidogo kuelewa Shuleni (Slow learner)?

Ni jambo la kawaida pia mchunguze kwa umakini huenda pia ana changamoto ya Learning Disability ( natamani kuelezea hapa ila sio mwandishi mzuri ) hivyo anapofundishwa anahitaji kutiwa moyo ! na kuelekezwa mara nyingi kadri iwezekanavyo na akichoka asilazimishwe mpe muda kumaliza task yake

Kuna malengo hatayafikia vizuri kama unavyotaka mzazi ila usikate tamaa mwangalie vizuri kuna mambo anayoyaweza mpaka unafurahi hivyo muelekeze zaidi kwenye hayo anayoyawaweza maisha sio kusoma tu,

Nina mtoto wa dada yangu ana Learning Disability upande wa Dyslexia walikua wanamchapa sana basi wakati fulani nikamuomba niishi nae nikamnunulia supplements za omega 3 na chakula chake tukawa tunamwekea mafuta ya samaki, kwa kweli ilimsaidia sana na shule nikaongea na walimu nikawaeleza hali halisi ya mtoto !

Kwa hiyo task ambazo watoto wenzie watamaliza baada ya nusu sasa yeye ingemchukua hata masaa matatu ! Muda wenzie wakienda nyumbani anabaki mdogo mdogo na mwalimu mpaka kazi anamaliza ndo anakuja nyumbani !!

Watoto wa hivi wanakua vizuri sana kwenye sphere nyingine , ila upande wa cognitive anakua na changamoto , huyu mwanangu kwa sasa anaendelea vizuri siwezi kumlinganisha na watoto wengine kwa mambo ya darasani ila naona naweza kumuendeleza katika vitu vingine vingi tu.

Zingatia chakula , weka mahusiano mazuri na mtoto , usione aibu kueleza changamoto yake ili iwe rahisi kusaidiwa waeleze walimu , hata watu wako wa karibu ili kuondoa kumfedhehesha bila kujua katika utani na maneno.

Pia usimuendekeze , mpelekeni taratibu kwenye mambo mnayoona kweli anapata ugumu , ila mengine nendeni mchaka mchaka kama watoto wengine hasa upande wa tabia na kujituma na nidhamu!!
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Kwanza muandae kisailojia asijisikie vibaya wala kujiona tofauti. Usimkalishe masaa mengi asome, hataelewa akiwa anajisikia vibaya.
Mpe ratiba ya kujifunza ambayo haitofautiani na wengine, hakikisha anajiona sawa na wengine. Ila kama yeye atataka kutumia muda mrefu kujifunza basi jitahidi kumpa muda huo mrefu.
 
Nanunua watoto wajinga na walio shindikana kama pesa mbovu
 
Mpe vipaji vyake nje ya kusoma. Kisha andaa vitabu vya eneo analopenda. Epuka top 10 za kukariri notes
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Hakikisha asubuhi anapata ndizi mbivu kabla hujaenda shule
Pia mpe vyakula vyenye vitamin B6 kwa wingi

Kwa ushauri kama uko Dar waone kituo cha SALT kilichopo Mbezi Makabe njia ya Madukani watakusaidia
 
Jitahid uwe una mnawisha kichwani na usoni maji ya nazi harafu unamnywesha pia.
Muandalie chakula mayai ya kienyeji, Samaki na dagaa mboga majani!
Chukua majani ya mti wa mbaazi, chumvi ya mawe, majani ya mpera changanya aoge asubuh na jion muda wa kulala.
Nb: ukichagua moja Kati ya hizo hakikisha maji ya nazi unayatumia!
Utakuja kunishukuru
 
Mpe muda ,kuwa mkarimu kwake,jitolee kumwelekeza anapokwama,mtie moyo na umuombee hatabaki kama alivyo Mungu atamuinua.Nina ndugu yangu alikuwa hivyo hivi sasa anakaribia kuhitimu miaka michache ijayo hakuna anaye amini.Sali na mtie moyo usimkatie tamaa
 
Ni jambo la kawaida pia mchunguze kwa umakini huenda pia ana changamoto ya Learning Disability ( natamani kuelezea hapa ila sio mwandishi mzuri ) hivyo anapofundishwa anahitaji kutiwa moyo ! na kuelekezwa mara nyingi kadri iwezekanavyo na akichoka asilazimishwe mpe muda kumaliza task yake

Kuna malengo hatayafikia vizuri kama unavyotaka mzazi ila usikate tamaa mwangalie vizuri kuna mambo anayoyaweza mpaka unafurahi hivyo muelekeze zaidi kwenye hayo anayoyawaweza maisha sio kusoma tu,

Nina mtoto wa dada yangu ana Learning Disability upande wa Dyslexia walikua wanamchapa sana basi wakati fulani nikamuomba niishi nae nikamnunulia supplements za omega 3 na chakula chake tukawa tunamwekea mafuta ya samaki, kwa kweli ilimsaidia sana na shule nikaongea na walimu nikawaeleza hali halisi ya mtoto !

Kwa hiyo task ambazo watoto wenzie watamaliza baada ya nusu sasa yeye ingemchukua hata masaa matatu ! Muda wenzie wakienda nyumbani anabaki mdogo mdogo na mwalimu mpaka kazi anamaliza ndo anakuja nyumbani !!

Watoto wa hivi wanakua vizuri sana kwenye sphere nyingine , ila upande wa cognitive anakua na changamoto , huyu mwanangu kwa sasa anaendelea vizuri siwezi kumlinganisha na watoto wengine kwa mambo ya darasani ila naona naweza kumuendeleza katika vitu vingine vingi tu.

Zingatia chakula , weka mahusiano mazuri na mtoto , usione aibu kueleza changamoto yake ili iwe rahisi kusaidiwa waeleze walimu , hata watu wako wa karibu ili kuondoa kumfedhehesha bila kujua katika utani na maneno.

Pia usimuendekeze , mpelekeni taratibu kwenye mambo mnayoona kweli anapata ugumu , ila mengine nendeni mchaka mchaka kama watoto wengine hasa upande wa tabia na kujituma na nidhamu!!
Swala la.chakula linakaaje.
 
Relax, nenda nae taratibu tu atabadilika. Kuna mambo mawili hapo
1. Kama akishindwa kabisa kubadilika basi huyo mtoto Yuko talented Sana kwenye kitu kingine mtakijua hapo badae na hiyo ndo itakuwa winning spot Yake maishani
2. Anaweza kubadilika badae akaja kuwa na akili Sana mpaka ukashangaa
Mimi mdogo wangu alienifuata alikuwa kilaza Sana sana primary school mpaka Mzee alimkatia tamaa maana hata std 4 alirudia rudia. Std 7 akabahatisha tu akafaulu na akapangwa shule ya kata tu na Mzee kwakua alikuwa ameshamkatia Tamaa wala hakushughulika nae. Aisee gari ikawaka bwana alipofika secondary, Dogo akawa kipanga hatari sote tukawa tunashangaa mabadiliko Yake, mpaka Leo hii alishamaliza chuo na alipata kazi chapchap maana ni kipanga kwelikweli anafanya kazi sehemu ambayo hatukuwahi kutarajia mtu kutoka familia kama ya kwetu anaweza kuwepo. Haya yeye huwa anasema hajui kilichotokea ila NI hivyo alibadilika tu ghafla
So usiwe na Shaka Sana, trust the process
 
Mtoto wangu sio Mjinga ila ana changamoto tu ya kuwa 'Slow' kwenye kuelewa Masomo yake jambo ambalo kidogo linaleta changamoto kwenye Ufaulu wake na kwasasa inamfanya ajisikie vibaya pia kwani anajiona kuwa tofauti na wenzake

Msaada nifanyeje hapa jamani ili kumsaidia mwanangu (yupo Shule ya Msingi)

Asanteni
Kubwa zaidi usimjengee kujisikia vibaya kutokana na kutofanya vizuri. Acha kabisa kumuonesha kwamba hilo ni tatizo kubwa. Acha maneno yoyote kama vile wewe mzito, wewe mjinga, huna akili. Msimjengee hofu kwani ndio mambo yatakuwa mabaya.

Slow learners sio kwamba hawana akili. Yawezekana ni genious mkubwa kuna wakati atafunguka na mtajua akili yake ipo kwenye nini. Albert Einstein alikuwa slow sana kujifunza hadi mwalimu wake aliwashauri wazazi wampe tu kazi za nyumbani lakini kumbe akili yake ilikuwa deep kuliko kawaida na alikuja kuwa mwanasayansi dunia haijapata kuona.
 
Back
Top Bottom