Mkuu ukabwa wa msanii una sifa zipi? Samahani lakini tunaomboleza ila tukibadilishana mawili matatu kwenye msiba wa MBALAMWEZIKundi kubwa la mziki hawana special security wa kutembea nao?
Na ukishakua msanii mkubwa kutembea tembea ovyo sio sawa , bora ukae nyumbani ulale. ,tembea kwa lengo maalum labda either unaenda kusain deal au kufanya airtime kwenye redio, na zaidi ukiwa unaelekea huko hakikisha una ulinzi na usiende na miguu....kama huna gari, basi ita hata UBER.
Saturday , 15th Dec , 2018
Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.
Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari ya moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin.
Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu.
Meneja wa kundi la The Mafik aliyejitambulisha kwa jina la Kapasta amesema ni kweli kuna hilo tukio, lakini ndio yuko njiani akielekea kituo cha Polisi Oysterbay ambako msanii huyo amewekwa rumande ili ajue kinachoendelea.
East Africa Television ilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, lakini alijibu hawezi kuzungumza kwa wakati huo kwani alikuwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu.
Msanii wa The Mafik akamatwa kwa wizi | East Africa Television
Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.www.eatv.tv
[Duh...! R I P
Kwa pale walipokuwa wanakaa sijaskia issue hiyoKwahiyo ndio ilikua maskani,ukiona vijana wanaishi hivyo twn kuna mawili aidha wanavuta pamoja plus uwizi wa vifaa vya magari na ndio wengi sana wenye kula bata wkend masaki
American chips au makaburi ya Kino ya mwanzoUfipa unaingilia barabara gani
Uliyoyaandika yanakuhusu wew kabisa.Ingekuwa mimi ndio wewe ningekuwa na utamaduni wa kusoma thread kwa makini. angalia hiyo habari ilitolewa lini na huyo kafa lini!!!
halafu mkipata supp mnakilimbilia ku apply kumbe hujasoma swali vizuri unajibu unachojua sio ulichoulizwa!!!
aisee... kumbe inawezekana chanzo ni wizi.Saturday , 15th Dec , 2018
Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.
Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari ya moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin.
Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu.
Meneja wa kundi la The Mafik aliyejitambulisha kwa jina la Kapasta amesema ni kweli kuna hilo tukio, lakini ndio yuko njiani akielekea kituo cha Polisi Oysterbay ambako msanii huyo amewekwa rumande ili ajue kinachoendelea.
East Africa Television ilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, lakini alijibu hawezi kuzungumza kwa wakati huo kwani alikuwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu.
Msanii wa The Mafik akamatwa kwa wizi | East Africa Television
Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.www.eatv.tv
Kama kweli basi wanakipaji sana...maana ile "passenger" ni bonge la ngoma..Aya...aya....ayaa... Hawa panya road siku hizi wanaimba
Moja ya nyimbo chache sana bora kwangu za bongoflava.Daah Dogo alikimbiza sana kwenye nyimbo yao "passenger"
Nasikia mwili wake umeokotwa ukiwa hauna nguo, sijui alikumbwa na nini kaka wa watu maskini.
Ama kweli watu mnakurupuka hiyo habari ni ya 2018.. haina uhusiano na yeye kuuawa.This means polisi ndo wamemuua
JF ni mm na ww na yule ukisema inalala sana inamaana hata ww umelala sana.Sure Jf inaanza kupungua kasi
Alikuwa mgonjwa au ni ajali? Pole kwa ndugu jamaa, marafiki na mashabiki wake. Binafsi ndio nimemjua kupitia habari hizi ingawa kundi lake nimelisikia mara kadhaa.
Gsri ndiyo inagua nguo...za yule aliyegongwa?Hapana Mkuu hiyo taarifa ni ya Mwaka Jana,inaonyesha ni mtu wa Matukio ,Maana kuna utata wa kifo wengine wanasema kapigwa wengine wanasema kagongwa na gari....Ndio nimejaribu kuunganisha dot matukio yake ya nyuma.
Nenda u tube..Hakuna video ya wimbo wake? R. I. P