Msanii Ruby amlipua Majizzo: Rushwa ya Ngono na mambo faragha

Msanii Ruby amlipua Majizzo: Rushwa ya Ngono na mambo faragha

Sasa kama anajirahisisha alitaka Majizo afanyaje?

Unakuta demu anakuja home na kisketi mapaja yote nje halafu unategemea Majizo amkaushie

Je akitoka hapo akienda kumtangaza kwa kashfa mbaya kuwa Majizo ni shoga kwasababu haku respond chochote?

Ipi ingekuwa kashfa mbaya kati ya ushoga na hii ya kumtaka kimapenzi huyo demu?
 
Hii ni tabia ya wengi sana mjini, kuna thead moja nimewahi kuona humu ya Dada fulani aliyeambukuzwa VVU na Mwalimu wake ili amtafutie kazi taasisi fulani ya serikali na kweli alipata, kwa ajili hiyo tuseme rushwa ya ngono ni kubwa sana nchi hii, na hili la Ruby ni kwa vile hakumpenda tu.

Nikusahihishe kidogo hapo kwenye iyo thread ya uyo dada sio kwamba alijiingiza huko ili apate kazi hapana iyo ilitokea wakiwa wako kwenye mahusiano tayari na uyo lecture wake kama mpenz wake kwakuwa amemaliza chuo kaamua kumfanyia mchakato wakupata kazi kwenye taasisi kubwa tu ya kiserikali kama muhasibu nadhani na iyo ilitokana n an kw am ba alishajua kuwa amemuambukiza Vitu Vya Umamtoni
 
You think, Vanessa mdee was well connected .she didn’t have to say that . Unless he was serious & wanted to marry Vanessa she said no . Which I could agree . Shule na media experience ipo pale . Lulu is a useless wife .

Mkuu hii kitu ungeongea kwa kiswahili na tandale tungeleewa
 
Kuna movie moja nimeisahau jina, inaelezea maisha ya binti alikua muimbaji, mama ake akampeleka kwenye kampuni kubwa baada ya majaribio akapita, kivumbi kikaja wakaanza kumcontrol kuanzia uvaaji, aina ya marafiki, na vitu kibao, akawa anapigishwa picha za uchi ili ziwekwe kwenye makava, ndio kujua kumbe wakina Riri na Bey yale mapicha ya uchi sio kama walikua wanapenda ila ni maelekezo ya wadau, mfano mzuri hata Zuchu alivyoanza alikua anavaa kwa stara siku hizi ni uchi tu, sasa pale ndio utu unapovuliwa na kujiona hana thamani, mawazo yanamjaa na kupata depression,

Good Girl gone Bad.
 
Wewe mama ukishakosolewa huwa unakimbiliaa huku lkn wengine wakikosea lazima uwaulize huko shule walienda kusomea ujinga,ptuu
 
Kampuni ni yake ana haki ya kuiendesha anavyotaka hakuna wa kumpangia. Ile sio ofisi ya serikali kusema anawazuia watanzania kufanya nae kazi.

Kama kaomba gemu (hajatumia nguvu yaani kubaka) then demu ana haki ya kukubali au kuchomoa sio lazima. Ila ulalamishi waache.

Tunawaambia kila siku hapa Dunia au ulimwengu una mambo yake, the only safe space ambayo mwanamke una guarantee ya kupewa attention na care ni kwenye familia ya wazazi wako au kwenye familia yako ya ndoa. Huku nje usitegemee any special treatments as if anybody owes you special treatments.

Waache kulalamika wachague kupigwa mashine then wapate wanachoomba au wapite hivi. Wanaume wanazinguliwa kila siku na walishalalamika nao ila wameamua kukubali.

Mliyasikia pale clouds Media why mshangae kwa majizo. Yaani mtu ajenge empire lake wewe mtoto wa kike uende kirahisi rahisi akubebe utoboe ujenge maisha yako yeye asipate chochote, how is that benefits both sides?
Dadeki!! Umeandika kibabe Sana Mkuu.

Mwanaume ndo anapaswa kuwa hivi Aiseeh!!
 
Na cha ajabu wanawake ndio wako mstari wa mbele kumtetea!!
Seems tumeshaharibikiwa hadi kuna mambo tunaona ni sawa tu[emoji134][emoji134][emoji134]
Wala hatutetei ila tunaelezea uhalisia, music industry huwezi kuitenganisha na ngono, pia mtu ukiombwa rushwa nenda kashtaki mamlaka zipo wazi, sio unakaa nalo unakuja kulitoa miaka imepita tena kwenye mitandao ya kijamii, rushwa ya ngono ni udhalilishaji kwanini mtu afumbie macho udhalilishaji kama ushahidi upo,

Ila kwenye suala la Ruby na Majizzo, maelezo ya Ruby ndio yanayomtoa Majizzo kwenye lawama, kwanini wakati Majizzo anamlipia sessions za studio na kumconnect na watu aliona anapewa sapoti ila yeye kushiriki kwenye mabonanza ya Majizzo na kulipwa laki tano aone ni unyanyasaji na sio sapoti???
 
Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuna kitu nyuma ya pazia,
Kesi ya Ruby inakuwa tofauti sababu inaonekana walikuwa wanaflirt huko nyuma sasa jizo akampotezea ukiongeza na maisha ya mahusiano yake yamekuwa hayasomeki kaona hasira zote aziangushie kwa jizo, na inawezekana kabisa hata huyu binti aliitumia hiyo flirting km kumblackmail jizo ili ampe support,
 
Salamu kina kaka, epuka kuanza mahusiano na mwanamke ambae hata simu ya mkononi hana. Huyo ni kiashiria kwamba ni mwanamke asiye mtafutaji.

Pia kama simu yake ni mbovu ni kiashiria kuwa maisha yake ni magumu na atakuchuna sana.
Wewe Binti inaelekea una mafanikio kiasi fulani katika maisha yako,lakini pia inaelekea unadharau sana watu ambao hawajafanikiwa kimaisha.Inaelekea pia kwamba una-amini mafanikio katika maisha haya ndio kila kitu,sio, kwa kuwa hapa duniani tunapita tu.Kumbuka kwamba maskini naye ni mtu,kwa hiyo anastahili kupendwa na kutiwa moyo katika umaskini wake.Sikiliza Binti,hata ungekuwa na nini, kama huna upendo si kitu wewe.

Naomba nikufahamishe kwamba Mungu anapenda maskini kuliko matajiri kwa sababu matajiri wamepata utajiri wao kwa kuwanyang'anya maskini.Mungu anapenda maskini pia kwa kuwa "mara nyingi" wao wana imani zaidi kuliko matajiri na wanampenda Mungu.Tena Mungu hapendi matajiri kwa kuwa wana tegemea zaidi utajiri wao kuliko kumtegemea Mungu.Niseme bila kumung'unya maneno kwamba inaelekea wewe ni mtu muovu sana.

Mwisho naomba usikatishe tamaa wanaume wanaotaka kuoa wanawake wasio na uwezo,kwa kuwa moja, inawezekana wanataka kuwanyanyua kimaisha,lakini pili,inawezekana hawataki tabia nyingi za hovyo walizo nazo wanawake wenye uwezo kama wewe.
 
Wala hatutetei ila tunaelezea uhalisia, music industry huwezi kuitenganisha na ngono, pia mtu ukiombwa rushwa nenda kashtaki mamlaka zipo wazi, sio unakaa nalo unakuja kulitoa miaka imepita tena kwenye mitandao ya kijamii, rushwa ya ngono ni udhalilishaji kwanini mtu afumbie macho udhalilishaji kama ushahidi upo,

Ila kwenye suala la Ruby na Majizzo, maelezo ya Ruby ndio yanayomtoa Majizzo kwenye lawama, kwanini wakati Majizzo anamlipia sessions za studio na kumconnect na watu aliona anapewa sapoti ila yeye kushiriki kwenye mabonanza ya Majizzo na kulipwa laki tano aone ni unyanyasaji na sio sapoti???
Mi nachojua hili jambo linakera sana na km hujawahi hata kuflirt na mwanaume mnyanyasaji utamchukulia hatu thabiti km kumshitaki kumfanyia figisu apoteze kibarua ama kumpuuza,, lakini kitendo cha kuishi nalo miaka nenda rudi baada ya kufungiwa vioo na kutopokelewa simu yake ndo kaona alinyanyaswa,, huu ni uhuni

Na wanawake tuko vizuri kwenye manipulation ndo hiki anachofanya Ruby
 
Wala hatutetei ila tunaelezea uhalisia, music industry huwezi kuitenganisha na ngono, pia mtu ukiombwa rushwa nenda kashtaki mamlaka zipo wazi, sio unakaa nalo unakuja kulitoa miaka imepita tena kwenye mitandao ya kijamii, rushwa ya ngono ni udhalilishaji kwanini mtu afumbie macho udhalilishaji kama ushahidi upo,

Ila kwenye suala la Ruby na Majizzo, maelezo ya Ruby ndio yanayomtoa Majizzo kwenye lawama, kwanini wakati Majizzo anamlipia sessions za studio na kumconnect na watu aliona anapewa sapoti ila yeye kushiriki kwenye mabonanza ya Majizzo na kulipwa laki tano aone ni unyanyasaji na sio sapoti???
Nimemkumbuka na yule msanii wa Nandy jina limenitoka alikuwa anavaa vizuri tu lol ghafla kaanza kuveshwa vidude tu hahaa dunia haina huruma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Previous Vanessa Alisema rushwa ya ngono ni issue kubwa sana kwa industry. Na kuna report Majizzo was after her na aliamua kuacha muziki Kabisa.

Currently ruby Anasema Tena. The same things. Same person yupo accused. Sasa, till when tutachukua hatua hata kumuhoji? Why? What measures anachukua on his company? Why just him? Watu wanamuangalia tu?
Hakuna msaada usio na malengo,
 
Huyu jamaa nina shaka na aina ya utongozaji wake. Ruge hakuna msanii wa kike Ambae ajapita nae Hadi watangazaji wa kike 89% Ruge kawala na hakuna hata mmoja alie wahi kumshutumu na ukitaka ugomvi na hao madem umzungumzie Ruge Kwa ubaya... Huyu majizo itakuwa haijui saikolojia ya wanawake yeye anajua akisha mwaga pesa TU anavuliwa nguo.

Majizo ndugu yangu mwanamke ukimjulia haki vile hupati tabu kumvua ngua, atajileta mwenyewe utamla na Heshima itaendelea kuwepo. Usitumie nguvu tumia akili.​
 
Currently ruby Anasema Tena. The same things. Same person yupo accused. Sasa, till when tutachukua hatua hata kumuhoji?

Wahusika kama kweli walikuwa victimized au kutaka kudhalilishwa, wangechukua hatua za kisheria...

Mfano hicho alichokifanya huyo dogo Ruby, kinaweza kikamtia matatani kwa kushtakiwa na Majizzo kama hana ushahidi...
 
Msanii tumia kipaji kushawishi siyo kujirahisisha kwa kutoa penzi ili uvume na kupata umaarufu...

Rubi kwa sasa anatakiwa atoe tu ushauri kwa wasanii wachanga na si kulalamika, kwa sababu njia iliyompa umaarufu haikuwa sahihi.
 
Rushwa ni adui wa haki, Ruby kanyimwa haki yake ipi?
Labda niwe sielewi maana ya Rushwa.
Kwa mujibu wa Wikipedia.

Rushwa:
ni aina ya mwenendo usio wa uaminifu au usiofaa kwa mtu aliyepewa mamlaka, kumbe anatumia nafasi hiyo ili kupata faida binafsi.

Alimlazimisha? Hii ni kesi ya sexual harassment si rushwa.
Jibu unakuta ni Hapana, waliombana kama watu wazima Ruby akaachiwa haki yake ya kukataa akaitumia vyema. Nini shida hapo.....

Amejuaje hawachezi Ngoma zake kisa Aliwanyima mzigo?
Vipi clouds Mbona hawachezi ngoma zake? Aliwanyima pia?
Wasafi vipi? IPP vipi? Aliwanyima wote hao?
Media zote Bongo? Seems ana mali nzuri kweli Media zote zinaitaka amezinyima ndio maana hazimpi airtime.
Inaonekana aliwanyima pia youtube ndio maana wanamhujumu.
Bodaboda, bajaji na waingiza Nyimbo kwenye simu aliwanyima pia, maana hawachezi Ngoma zake.
Ni rahisi kulaumu wengine ukifeli, huwa inaleta faraja sana.
Jinsia sio ulemavu, kila jambo nyie mnaleta Jinsia.
Tunawaona mnavyoact Mashuleni, vyuoni, makazini na hata mitaani.
Mnapenda kukumbusha watu Nyie ni wanawake na hii dunia haipo Upande wenu kabisa.
 
Back
Top Bottom