Hapana ilifuatia hii kwanza ya kifo cha kwanza cha Clemence Mtenga⤵️
Clemence Mtenga:Familia ya Mtanzania aliyefariki Gaza yazungumza
CHANZO CHA PICHA,MASHAV ISRAEL
20 Novemba 2023
Na Alfred Lasteck
BBC Dar es Salaam
Familia ya Marehemu Clemence Mtenga inasubiri Serikali ifanye taratibu za usafirishaji wa mwili wa marehemu kutoka nchini Israel ili waweze kufanya maziko.
Clemence alikuwa miongoni mwa wanafunzi wawili kutoka Tanzania ambao Serikali ya Israeli hapo awali ilithibitisha kuwa walitekwa na kundi la Hamas baada ya shambulio la Oktoba 7.
Akizungumza na BBC, Msemaji wa familia ya marehemu, Boniface Mtenga alisema kuwa kwa sasa hakuna wanachoweza kukifanya mpaka pale serikali itakapowaambia lini mwili utakapofika nchini kwa ajili ya maziko.
Mtenga alisema, “Tulipata taarifa ya kifo cha kijana wetu siku ya Ijumaa, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Rombo alifika nyumbani akiwa na ujumbe huo kutoka kwa serikali…
“…Tulipokea taarifa hiyo kwa majonzi kwasababu tumeondokewa na kijana wetu ambaye ndio kwanza alianza kupambania ndoto zake za maisha. Kwa sasa hatuna cha kufanya mpaka pale serikali itakapotuletea mwili kwa ajili ya maziko,” alisema Mtenga na kuongeza kuwa wanatarajia kuwa leo watapata taarifa rasmi ya lini mwili utakapowasili.
Serikali kuthibitisha kifo chake
Ijumaa iliyopita, Serikali ya Tanzania ilitangaza kuwa Clemence, mwanafunzi mwenye miaka 22, ndiye aliyefariki.
Kwenye taarifa yake, serikali ilieleza kuwa inaendelea kuwasiliana na Israel juu ya taarifa za Mtanzania mwingine, Joshua Mollel ambaye bado anashikiliwa mateka.
Kwa mujibu wa Israel, jumla ya watu 230 walichukuliwa mateka baada ya shambulio la Oktoba 07. Mateka hao, ambao walipelekwa katika ukanda wa Gaza na wanatoka katika mataifa 25 tofauti, ikiwemo raia mmoja wa Afrika Kusini ambaye hadi sasa hajatambulika.
Safari ya kwenda Israel
Kwa mujibu wa familia, Clemence aliondoka nchini Tanzania Septemba mwaka huu ambapo alienda nchini Israel kushiriki mafunzo ya kilimo biashara kwa utaratibu ulio chini ya mpango wa ushirikiano kati ya serikali za Tanzania na Israel.
Kijana huyo ni miongoni mwa wanafunzi wa kitanzania 260 waliokuwa nchini humo kwaajili ya masomo ya vitendo katika eneo la kilimo.
Ndio ikaja kufuatia hiyo ya Desemba 14⤵️
Serikali ya Tanzania yathibitisha kifo cha raia wake aliyeuawa baada ya kukamatwa na Hamas
14 Desemba, 2023
Gari la Shirika la Msalaba Mwekundu likiwa limewabeba mateka wa Israel wenye asili ya Russia Novemba 26,2023. Picha na Belal Al SABBAGH / AFPTV / AFP
Ona maoni
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania siku ya Alhamisi imethibitisha kifo cha mmoja wa Watanzania ambaye “aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas” wakati wa mashambulizi ya Oktoba 7, huko Kusini mwa Israel.
Siku ya Alhamisi Waziri wa Mambo ya Nje, Januari Makamba amesema mamlaka “imearifiwa na serikali ya Israel kuwa Joshua Mollel, mwanafunzi wa Kitanzania aliyekuwa akisoma nchini Israel, ambaye alipoteza mawasiliano tangu Oktoba 7, 2023…aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas.”
Waziri Makamba alisema kupitia mtandao wa X kuwa mamlaka ya Tanzania inafanya mipango kwa familia ya Mollel, akiwemo baba yake, kwenda Israel na afisa wa serikali “kukutana na balozi wetu na maafisa wa Israel na kupata taarifa zaidi” kuhusiana na kifo chake.
Serikali ya Israel iliwataja wanafunzi wawili kutoka Tanzania waliokuwa wakisoma nchini Isreal -- Clemence Felix Mtenga mwenye umri wa miaka 22 na Joshua Loitu Mollel mwenye umri wa miaka 21.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania ilitangaza kifo cha Mtenga mwezi uliopita, bila ya kutoa maelezo kuhusu mauaji yake
Wanafunzi hao wawili ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania wapatao 260 ambao walikwenda Israel kwa mafunzo ya kazi kwa vitendo katika kilimo cha kisasa chini ya mpango wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP
Na kweli hizi taarifa zinaleta mkanganyiko mkubwa unaozalisha maswali mengi kama ukifuatilia kwa makini.