Uchaguzi 2020 Msemaji Tume: Kila Mgombea aliyefika kwa wakati Kupokelewa Fomu zake

Uchaguzi 2020 Msemaji Tume: Kila Mgombea aliyefika kwa wakati Kupokelewa Fomu zake

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa elimu Mama Aswile, vyama ambavyo wadhamini wake walihakikiwa na wasimamizi wa majimbo vimehudumiwa kwa haraka, vile vingine kama CHADEMA ambavyo havikufanya hivyo, uhakiki wake unafanywa kwanza ndani ya tume kabla ya kuthibitishwa.

CHANZO: MAHOJIANO TBC1
Kinachotakiwa ni kuidhinishwa tu kama hawavunja sheria yeyote ya uchaguzi .
Hata kama form za Lissu zingekuja wiki moja kabla ya mda sababu msingezikosa za kuchelewesha haki ambayo kwa sasa hamuwezi kuipora tena.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mbowe amewahi kugombea urais, kwanini asingewaongoza wenzie ipasavyo ili kuipa wepesi NEC?!
Tatizo si kuipa tume wepesi, ukiwa mtoto wa kambo utatafutiwa sababu yoyote na utapewa jina baya tu. Hapa kuna kitu kipo jikoni ni suala la muda tu.
 
Keli nyie wasanii. Lakini mwaka huu ntajua mbichi na mbivu.
Soma tena post ya kwanza.

Kama aliwahi kuhakiki majina ya wadhamini na namba zao za kupiga kura majimboni basi zoezi lake linaenda haraka.

Kwa wale manguli ambao hawakuona haja ya kuhakiki wapigakura wao a.k.a. wadhamini huko jimboni basi wawe wapole maana majina yanapitiwa.

Si unajua kuna janja janja katika baadhi ya hao wanapgombea?
 
Tukiwaambia chadema ni mbumbumbu wanakataa!

Haya muiteni amsterdam sasa amusaidie huyo mwansheria wenu asiejua kitu
Wewe ndiyo mbumbumbu kilaza na waliokutuma huo ufala mnaofanya unawasaidia nini? ni kwa nini CCM wanaogopa ushindani? Kama CCM mmenunua ndege mmejenga SGR mmeleta maendeleo iweje kuwaogopa chadema hivyo?
 
Technical knock out, sijui Armstaderm atasemaje, alitakiwa aje amsadia mteja wake
 
Uelewa mdogo wa wanasaccos ndiyo shida. Msaliti Lissu anajifanya anajua sana, sasa alikuwa anahangaika na mikutano tuuu amezidiwa hata na CHAUMA. Halafu huyu anataka aongoze Tanzania??!! Never Ever!!
Chadema wana tabia moja ambayo ni nadra kuielewa kama unatanguliza mahaba kuwashabikia.

Wanafanya makosa na wanajua kabisa wamefanya kosa. Ila wanakimbilia media kutangaza wameonewa na kamwe hawawezi kutaja kilichowafanya wawe katika situation husika.

Mashabiki wao nao waliowengi kwasababu wanatanguliza mahaba...wanaanza kupiga kelele hata hawafuatilii kilichotokea kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Wao wapo sahihi kwa kila wafanyalo...hataka kama wanafanya isivyotakiwa. Si watapata support! Kwanini wasiwe sahihi.
 
Tatizo si kuipa tume wepesi, ukiwa mtoto wa kambo utatafutiwa sababu yoyote na utapewa jina baya tu. Hapa kuna kitu kipo jikoni ni suala la muda tu.
Ni umbumbumbu na kujifanya wanajua pia wanajua hawawezi shinda uchaguzi sasa wanafanya makusudi ili waonewe huruma
 
chadema ilianza kushiriki chaguzi mwaka 1995 unataka kunambia huu mwaka 2020 ndio hawajui taratibu za uchaguzi zilivyo?
Hivi Nani wa kulaumiwa hapo..?
Hata chama Cha juzi ACT kimewazidi Jana membe alienda kuhakiki lkn chama kikuu pinzani hamkwenda sahivi mnaleta malalamiko yasiyo msingi nawakati nec walitoa siku tatu!.. licha ya hivyo kwenye majimbo pia Kuna uhakiki wa wadhamini..

Mnatafutaga sababu ili muonekane mnaonewa Tena ajabu anaegombea ni mwanasheria ila hazifuati oneni haya.. hata nanyi Mungu anawaona..
 
Sasa lisu anacomplain nini, wakati chama chake kinakubali kuwa kuna taratibu hazikufuatwa.
Screenshot_20200825-154757_Twitter.jpg
Screenshot_20200825-154513_Twitter.jpg
 
Meko kamaliza dk15 tu pale ofisi za NEC alipowasilisha fomu yake,je tume imetumia muda gan kuhakiki wadhamini wake kama ni wapiga kura kweli?,,
Kuwa muelewa umeambiwa aliye leta fom siku mbili au moja nyuma zilishakaguliwa nadhani cdm wameenda nazo leo
 
Je walimuweka Magufuli waiting room kuhakiki wadhamini wake au hii ni kwa kina Lisu tu? Naiona The Hague kwa watu fulani hapa hivi hawamuulizi Kenyata joto la Hague likoje?
Hebu angalia kwenye TV hata lile bango la tume ya uchaguzi limefunikwa na picha ya Magufuli alafu ulitegemea akae waiting room.
 
Nyumbu ni CCM kwani hata mbugani nyumbu ni wengi kama CCM walivyokuwa wengi lakini wanawaogopa chadema mpaka kuwahujumu kwa kuitumia NECCCM
Ila jamaa mtachoka mapema, maana ni mbishi huyo balaaa.
Hivi Lissu akishinda urais Mbowe atakuwa nani.
 
Meko kamaliza dk15 tu pale ofisi za NEC alipowasilisha fomu yake,je tume imetumia muda gan kuhakiki wadhamini wake kama ni wapiga kura kweli?,,
Kwa mujibu wa mleta taarifa ni kuwa wapo waliowasilisha orodha mapema yawezeka huyo meko akawa miongoni mwao
 
Afisa wa Tume anayehusika na habari na Mawasiliano, punde ametoa ufafanuzi kumtu Kupitia TBC1 kuhusu wagombea waliowaiting room kuwa, kuchelewa kwa baadhi ya wagombea kuingia chumba maalum cha uteuzi/kupokelewa fomu zao kunatokana na zoezi la uhakiki wa fomu zenyewe na uhakiki wa wadhamini. Tume ni lazima ijiridhishe kama waliomdhamini mgombea ni kweli kuwa ni wapiga kura. Na mambo mengine

Kwa wale waliopeleka kabla majina hayo kukaguliwa ktk ngazi ya Jimbo au kupelekea tume kabla, zoezi hili kwao ni la haraka zaidi, ila kama hukuwa umepeleka majina hayo kabla, basi itabidi uwe mpole kidogo kujiridhisha.

Pia ameeleza kuwa, wagombea wote ambao wamefika kituoni hapo kabla ya saa 10 watasikilizwa hadi waishe, isipokuwa kama mtu atafika baada ya saa 10. Kwa hiyo wale walio na wasiwasi kuhusu wagombea wa vyama vyao hasa CHADEMA, bila shaka wote watapata hiyo fursa ya kusikilizwa na Kkwasilosha fomu zao za uteuzi na baadae kuteuliwa kama wamekidhi vigezo vyote kwa kadri ya taratibu walizopewa. Wandugu tuwe na subira.

Tuzidi iombea tume Mungu awajaalie wafanye kazi kwa weledi, kwa kuzingatia maadili, sheria na taratibu, Uwazi na kutenda haki

#maendeleo hayana chama
maana yake ni kwamba wapigiga kura walio mdhamini ni Magumashi... iweje tume iwe na doubt na wapiga kura walio kwenye daftari lao la kudumu? si ni kuangalia tu na kusema kwamba huyu yumo au hayumo... ni haraka sana - kama maji kwa glasi
 
Back
Top Bottom