bizzle for shizzle
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 1,012
- 741
Ha ha ha du! Ila kweli mkuu umenena hawa jamaa hawatoelewa kitu[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]kama kaacha,mbona haitwi "mstaafu" au atumie jina lisilo na asili ya jeshI,atumie majina yake tu?
halafu hii ya kurundika wanajeshi,je ikitokea ccm imeshindwa kwenye uchaguzi,hawa wanajeshi wataelewa? au wanachonganishwa na wananchi?
NI UKIUKWAJI WA KATIBA AU MAJINA YAMEFANANA KATI YA MSEMAJI WA JWTZ NA HUYU MTEULE WA NEC YA CCM?
JPM JITOKEZE KUUELEZEA UMMA KUHUSU UTATA HUU.
Msemaji wa JWTZ ni Kanali Ngemela Lubinga.
Katibu Mteule wa NEC ya CCM Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ni Kanali Ngemela Eslom Lubinga.
Katiba ya Jamhuri 1977 inasema :-
SURA YA TISA
MAJESHI YA ULINZI
Ibara ya 147.
Ibara ndogo ya (3),
Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.
Ibara ndogo ya (4),
Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa.
Unamaana huyo mteule alikuwa na Kadi ya Chama?Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Kwa hiyo uteuzi wake uliegemea kwenye lugha ya mawasiliano sio? Ingekuwa lugha ya mawasiliano ndiyo kigezo cha uteuzi hivi leo ungemteua mtu anayozungumza broken english?Mkuu, unaweza ukawa na hoja lakini unasahau ukweli kwamba ndani ya CCM kuna wanajeshi.
1. Luteni kanali Abdulrahman Kinana
2. Kapteni George Mkuchika
3. Luteni Kanali Jakaya Kikwete
4. Kapteni John Zefania Chiligati
Na wengine wengi tu, sembuse huyu kanali Lubinga?
Kanali Lubinga alitoka jeshini akaenda kuwa DC Mlele Mkoani Katavi na baadae jeshi likamhitaji kuwa mkurugenzi wake wa habari na mahusiano (eneo ambalo ana utaalam nalo).
Hawa ni watu ambao ambao unaweza kusema kwamba wanacheza mpira kama "box to box midfielders" na ndicho kilichomsukuma JPM kumteua kuziba nafasi ya mama Migiro khasa lugha ya mawasiliano jamaa ametulia.
Huu utetezi hauna mashiko kabisaSio lazima awe alikuwa mwanachama.Aweza kuwa kaanza jana hiyo hiyo kila kitu kina tarehe ya kuanza
Lowasa anakukera sana kila kitu mpaka utolee mfano kwake, kweni ni mtu wa muhimu sanaaaaaaaaaa kwako YEHODAYASiku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Safari bado ni ndefu sana kwa maoni kama hayaHiyo ni teuzi kama nyingine....yeye ni kama wewe utoke kwako uteuliwe kuwa mkuu wa majeshi.Piga kazi
Kuna sehemu ya katiba inayomkataza askari kuwa mwanachama wa chama cha siasa ?Swali ni kuhusu uteuzi bro, kwa sababu mtu hawezi kuteuliwa tena kwenye nafasi kama ya msemaji kama sio mwanachama wa muda mrefu
Umesema wakati tukiwa mfumo wa chama kimoja, sasa hivi tuna mfumo wa vyama vingi.Nimegundua si kosa lako, tatizo lako unataka kuonyesha wana JF kuwa unajua lakini hujui chochote. Acha tukukumbushe-wakati tukiwa na chama kimoja asilmia kubwa ya wafanya kazi wote na wafanyabiashara walikuwa wanachama wa ccm, majeshi yote walikuwa wanachama wa ccm na siasa ilifundishwa hadi majeshini, na ndo maana tokea nyakati hizo wanajeshi waliteuliwa katika nyadhifa mbalimbali mfano-Mh. Jakaya Kikwete, Mh.Kinana na wengine wengi-si ajabu hicho kinachofanyika
Jadili mada husika achana na umbeaKwani katiba ya Chadema inasemaje, mwanachama mpya lazima amalize miaka 2, bila kupewa wadhiwa wowote, lakini lowasa aliingia asubuhi jioni mgombea urais mbona hili hamkuhoji
Sio lazima ujibu ujinga,katiba ya CCM inataka uwe mwanachama miaka miwili ili upate wadhifa huoSiku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Hivi watu kama nyie mnaishi dunia ya wapi?Nimegundua si kosa lako, tatizo lako unataka kuonyesha wana JF kuwa unajua lakini hujui chochote. Acha tukukumbushe-wakati tukiwa na chama kimoja asilmia kubwa ya wafanya kazi wote na wafanyabiashara walikuwa wanachama wa ccm, majeshi yote walikuwa wanachama wa ccm na siasa ilifundishwa hadi majeshini, na ndo maana tokea nyakati hizo wanajeshi waliteuliwa katika nyadhifa mbalimbali mfano-Mh. Jakaya Kikwete, Mh.Kinana na wengine wengi-si ajabu hicho kinachofanyika
Hoja yangu si uwepo wa majenerali na maluteni ndani ya chama,hoja ni je,walianza lini kuwa wanachama wa CCM?Mwaka jana Taifa lilipigwa na butwaa baada ya kumshuhudia aliyekuwa jaji Mh.Augustine Ramadhani akichukuwa fomu kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa urais kupitia CCM,orodha ni ndefu,wapo wakina Tibaigana na wengine wengi waliostaafu lakini ndani ya muda mfupi tuliwaona wakijitosa kwenye siasa kupitia CCM,hoja ni je,lini walianza harakati zao za kisiasa hadi kuamua kujiingiza katika kuwania uongozi?Au walikiuka viapo na katiba za vyombo vyao na ile ya nchi inayowakataza wao kuwa wanachama wa Chama cha siasa?