Msemaji wa Serikali: Helikopta zetu ni za usafirishaji siyo kuvutia Ndege au Meli

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Msemaji Mkuu wa Serikali amesema hayo na kuongeza kuwa watu wanaolalamika na kuhoji juu ya kutotumika Helikopta katika uokoaji kwenye ajali ya Ndege ya Pecision Air wapuuzwe.

Amesema Serikali haiwezi kuwa na dhamira ya kuacha wananchi waangamie pale majanga yanapojitokeza na ndiyo maana walitumia kila njia kuhakikisha wanapunguza madhara ya ajali.

Your browser is not able to display this video.
 
 
Serekali wakiweza wakae kimya kabisa. Wasianze kabisa kubishana na watu kuhusu hili, ni busara ukiumbuka kukaa kimya yapite.

Yaani majanga yanatokea mita 100 kutoka airport mnashindwa kuokoa? Sasa mnakuwaga na fire na vikosi vya uokoaji vya nini. Ingekuwa watanzania wamekufa kwa kishindo au moto uliojitokeza ingekuwa sawa lakini maji! tena maji yanayoingioa pole pole ndani ya ndege?

Serekali kaeni kimya msituzidishie machungu

Alafu eti anasema ndio maana serekali ilifanya kila njia kuhakikisha wanapunguza madhara. Dah!
 
Kwani wale wavuvi ni waokoaji? Angetafuta namna tofauti kujibu hasira ya wananchi.
Ndege imeanguka majira ya saa moja asubuhi hatusikii au kuona taarifa au juhudi yoyote ya serikali hadi saa saba mchana. Yaani hadi wanunue helkopta au mtumbwi wa kuokoa ndio tuone wanaokoa watu toka ajali?

Tukisema wahuni wamerudi serikalini msikatae. Maana kuna mtu anajua hapo ataagiza helkopta au mtumbwi wa kuokoa aweke cha juu.

Heko kijana majaliwa na wavuvi wote wa tanzania. Mungu anawaona.
 
Kuna wakati unatamani umnase mtu vibao,Comment yangu haihusiani na maada
 
Huyu mtu aelewe watu walimaanisha helicopter kama tunazo za kufanyia mambo ya ajabu ajabu kwanni tukose hela yakuwa na vifaa vya uokoaji kwenyekila mkoa ? Kweli ajali imetokea bukoba mnaomba machine kutoka Geita tena kwa mwekezaji GGM umbali wa Zaidi ya KM 310 ?? Aibu Aibu tele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…