Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuja mda pesa haitaki mazoea dah...Tumia pesa ikuzoee
Ukiitumia itakuzoeaKuja mda pesa haitaki mazoea dah...
😪😂😂😂
Labda wewe sio mtu wa starehe/kula bata.But kumbuka hiyo pesa ilikuwa nje ya mipango mkuu....
400K plus ,Kwa masaa 4 ,
Maisha ndio hayahaya.."SIKU MOJA MOJA SIYO MBAYA"
Leo nimekumbuka mwaka 2020 kipindi cha Pasaka,Jijini Arusha,hapo dili la ku-design michoro ya Majengo kadhaa ya Taasisi ya Kanisa limetiki na nka kabidhiwa pesa ya Advance Millioni +.
Sikukuu ya Pasaka ilipofika mwenyeji wangu akasema twende kusherekea kwenye Bar flani,yeye atasimamia show (ipo pembezoni mwa Barabara ya Moshono-Impala).
Tulivyofika eneo la tukio, tukaanza shushia maji ya dhahabu mimi, mwenzangu na wadogo zake wawili.
Ghafla tukasikia tumeitwa ,kugeuka ni mshikaji wa mtaa mmoja (mtaa wa Baraa).
Sasa hapo mjamaa wangu gambe zipo kichwani,akainuka na kwenda kucheza,alivyorudi ,kaambatana na wadada wa4 (nao ni wa mtaani ) wakajumuika.
Mjamaa akantonya hela imekata,nimuokoe mana kuna mdada mmoja wapo anamuelewa.
Kwakuwa nami nipo Gambe nkasema "mwana usihofu ".
Hapo jumla tupo 9,wote wakaagiza supu nzito,wengine kiepe kuku.
Kila mtu akapata chupa zake tano za gambe ,round zikarudiwa na kurudiwa, wengine wanataka Whisky...
Kuja kufika saa 9 usiku mda wa kusepa
nkalipia Bili.Lipia usafiri wa kila mtu,Nkapitia mjamaa na hela ya kuhonga,Nyingine sijui nilitupa.
Asubuhi ilivyofika, kuja kucheki nimetumia zaidi ya 400K
Hapo nikajifariji kwa kusema "SIKU MOJA MOJA SIYO MBAYA"
😂😂😂Maisha ndio hayahaya..
Huko jikoni nitengenezeeni kuku sekela mzima na chips mtumio alfu na pilipili km ya siku zote..
Tukio gani hilo lilikufanya ujifariji hivyo..."Ukipata tumia, ukikosa jutia"
Maisha mafupi, afu tunaishi mara 1 tyuu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nile PESA kaburini,.
Hela yenyewe huwezi kununua Ferrari,
kujenga huwezi,hata chochote hauwezi.
Sasa ushindwe hata kunywa bia tena au kiroba,hata gongo unatwanga tu.
Mi hadi vilabuni ukinikuta utashangaa.
Napiga pombe za kienyeji ka sina akili nzuri.
Kesho bar za kueleweka
nshabadilika pedeshee tayari.
Kesho utanikuta Masaki Karambezi ndo utachoka
Ilikua 2022 nilipata mchongo wa 800k afu nlikua nna jambo langu LA maana nifanye,Tukio gani hilo lilikufanya ujifariji hivyo...
Tupe story madam
Hapo kwa coca sasa"Ukipata tumia, ukikosa jutia"
Maisha mafupi, afu tunaishi mara 1 tyuu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Yaani hapo ndo nakupendea kujibana bana ili iweje."Ukipata tumia, ukikosa jutia"
Maisha mafupi, afu tunaishi mara 1 tyuu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ikawa full kuvurugwa, alafu kanakuja kale ka msemo ka faraja, kama nilipata hizi ntapata zingineIlikua 2022 nilipata mchongo wa 800k afu nlikua nna jambo langu LA maana nifanye,
Shost akanipelekaa Mikocheni kuna duka LA viwalo, aseeh nlinunua nguo ambazo hata sikuwaza, kuja kutazama imebaki 260k
Hatariii tupuu.