Mshahara wa Dkt. Ndugulile akishaanza kazi WHO ni noma. Rais wa India akasome

Milioni 360 kwa mwaka ni hela ndogo mkuu? Watanzania wangapi unaowajua wanaingiza hiyo hela?
Mnapoongelea value/thamani msiwe na vitabia vya kujilinganisha na umasikini. Nyie ndo mnaenda kuburgain mikataba mnasaini bilioni moja kwa mkataba wa trillion 2 au 3 kisa umeona watanzania hawana hata milioni mia. Tokeni kwenye poverty trauma
 
Mnapoongelea value/thamani msiwe na vitabia vya kujilinganisha na umasikini. Nyie ndo mnaenda kuburgain mikataba mnasaini bilioni moja kwa mkataba wa trillion 2 au 3 kisa umeona watanzania hawana hata milioni mia. Tokeni kwenye poverty trauma
Umeongea point sana. Wabongo tuache kujidharau.
 
Rais wa India anapokea Hela ndogo hivo wakati mama Samia ambaye nchi yake ni masikini ya kunuka anapokea mabilioni ya mabilioni wakati huohuo Kila kitu anapewa Bure kuanzia kuhudumiwa watoto wake ,wajukuu,mfugo,nyumba,gari,shule(international,chakula matibabu,yaani hitaji lolote analotaka anahudumiwa Bure na serikali.
 
Sisi tunataka ainue watanzania waingie huko WHO wa kutosha na siyo mshahara wake
 
Shangaa India ambaye ni Giant kiuchumi mkuu wake wa nchi ameachwa mbali sana mara mbili na ushee ila niamini mimi Hiyo pesa bado ndogo sana kwa mzigo anauchukua mama ushungi.
Mama ushungi unamaanisha Chra kiziwi?
 
Ni makasiriko kwa kweli
 
364m@yr ni hela kidogo tu hiyo boss, ingekuwa ni kwa mwenzi hapo sawa.
 
Milioni 360 kwa mwaka ni hela ndogo mkuu? Watanzania wangapi unaowajua wanaingiza hiyo hela?
Gross salary ya TSH 360 million kwa mwaka ni sawa na TSH 30 million kwa mwezi, baada ya kodi (net pay) ni chini ya hapo. Kiasi hicho hata baadhi ya wacheza mpira wa timu kama za Yanga na Simba wanamzidi. Wakurugenzi wakuu wa baadhi ya mashirika yetu ya umma hususani tanesco walikuwa wanapata hadi 40 million kwa mwezi, JPM akadhamiria kuzishusha, haijulikani kama alifanikiwa.

Wabunge wetu mishahara yao inakaribia na hapo. Mbowe alitaja milioni 19 kwa mwezi. Ukizingatia kuwa wengi wa wabunge wana kazi zao nje ya bunge including za kibiashara, ni dhahiri kuwa jumla ya kipato chao kinazidi hapo. Hata madaktari wenzake walio na hospitali zao binafsi hapa nchini wanapata zaidi ya hizo.

Wewe kwa sababu huna, unaziona ni nyingi sana. Cost of living huko WHO ni ghari sana. Hivyo si ajabu baada ya utumishi wake wa miaka 5 huko WHO hatakuwa na uwezo wa kujenga mansion ya billion 1.5 TSH huku bongo.
 
Hata kwa nje, si hela ndogo hiyo.

Wastani wa kipato cha Wamarekani hakifiki hata $100,000.00 kwa mwaka.

Mshahara wa $11,000.00 kwa mwezi si mdogo, ingawa si mkubwa kivile.
Mkuu aliyeleta taharuki ni mleta mada kwa jinsi alivyochagiza 😂😂

Kwa jinsi kichwa cha habari kilivyokaa nilitarajajia ntakuta mshahara wa maajabu kweli kweli😂
 
Anayeingiziwa nyingi Tanzania ni Rais ambaye akishaingiziwa anaanza kutoa kwenye miradi mbali mbali katika nchi.
 
Ingekuwa tunazungumzia mapato halali, wachache sana katika ya viongozi, wanasiasa, na wafanyakazi Tanzania wangekuwa na jeuri ya kusema hiyo hela ni ndogo.

Wachangiaji wengi hapa wanatukuza mapato ya kifisadi yanayopatikana kwa rushwa, wizi na hujuma za uchumi ndani ya nchi.

Halafu mishahara ya UN haina kodi wala tozo. Hayo ni mambo ya nchi anakotoka mfanyakazi. Kwa US, kwa mfano, raia wake wote popote walipo duniani lazima wawasilishe mapato yao na kutozwa kodi stahiki. Ni sharti la uraia.

Tanzania na nchi nyingi hasa za dunia ya tatu hazitozi kodi diaspora wake.
 
Wastani wa 1M kwa siku ,pesa mdogo sana,sema posho na marupurupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…