Msiba kwa wanaofanya biashara ya kuagiza vitu China

Msiba kwa wanaofanya biashara ya kuagiza vitu China

Hakuna watu wana madeni kama hao wanaochukua hela za watu advances n.k na kuahidi kuletea watu bidhaa toka nje ya nchi hususa China.

Yani wamekuwa full matapeli. [emoji57][emoji57]
 
Wengi hawako knowledgeable na maswala ya biashara.

Wanatamaa ya maisha ya kujirusha na show off chungu nzima [emoji108][emoji108] kwa kutumia hela za watu .

Hawajui hata jinsi ya kufanya risks profiling
 
Wengi hawako knowledgeable na maswala ya biashara.

Wanatamaa ya maisha ya kujirusha na show off chungu nzima [emoji108][emoji108] kwa kutumia hela za watu .

Hawajui hata jinsi ya kufanya risks profiling
Mtu ambae anajua maana ya biashara atahakikisha mzigo wa mtu unafika ndio afanye matumizi wengi wanaingia kichwa kichwa kutokana na kukosa ajira tu ila kusems ukweli hawajui chochote
 
Unafanikiwa vipi sajili n we chart payment ukifika china mkuu ukafungua akaunti or manake wanasheria sana Hawa viumbe
Hapana hujanifahamu mimi kuna agent wana ofisi yao ipo hapa na china. Wao ndio huwapa hela na wao ndio huwalipa hao wachina kwa kutumia WeChat mimi sina hio wechat. Nategemea umenifahamu vyema
 
Mifumo ipo clear kwa makampuni yote:
1.Unaongea na shipping agent mfano Mapembelo, GNM cargo, silent ocean, Unique, shamwaa, Faith Royal cargo nk utachagua wewe moyo wako unapoangukia then watakupa ADDRESS YAO YA CHINA, hyo address utaicopy kama ilivyo.

2. Utaenda Alibaba, madeinchina, 1688 hao wote ni wauzaji wa jumla, utachagua bidhaa unayotaka utarequest alaf muuzaji atakujibu na utamuuliza maswali yote unayoona kwako ni sahihi kama sizes, color, quality, pia unaweza kumuomba akutumie real picture/video.

3.Utakubalina na supplier bei kama ukiridhia bei aliokutajia na mmenegotiate mpaka mkaafikiana atakuomba ADDRESS YA CHINA ili iwe rahisi na kuokoa gharama ya shipping then hile address ulioCOPY kwa shipping agent ndio utampa alaf yeye atakupa gharama ya shipping kutoka kiwandani/warehouse yao mpaka kwa shipping agent wako, hyo bei itajumuishwa kwenye gharama ya bidhaa yako.

4. Kama ni bei ndogo mfano chini ya $500 unaweza kutumia VISACARD ya voda kama huna card ya Bank inayoruhusu transaction online then utalipia kazi itabak yeye kuship kwenda kwa agent wako, ila kam ni mzigo mkubwa sana huwa wanataka 50-60% ya malipo alaf wao wanaanza kuprocess mfano kama ni order ya kiwandani ukilipa hyo wataanza kukutengenezea kutokana na makubaliano yenu wakimaliza utamalizia alaf wanakusafirishia kama taratibu za bidhaa zingne ndogo ndogo.

Jitahidi sana kuongea na supplier ili ujue muda atakaotumia mpaka mzigo wako unafika kwa shipping agent ili nawewe uendane na timetable za meli.

5. Baada ya taratibu hzo kukamilika na mzigo kufika kwa shipping agent wako kazi itakuwa imebaki kwa agent wako kukusafirishia kuja Tanzania kama ni kwa meli huwa inachukua siku 30-45 mpaka kupokea mzigo wako japo wapo wengne wanachelewesha sana mizigo.
Agent wako atakupa gharama ya mzigo wako ili ujiandae mapema pale mzigo unapofika uweze kulipia na kwenda kwenye ofisi zao kuchukua.
Meli wanapina kwa CBM (Cubic meter) ila ndege mizigo yote inapimwa kwa KG.

Pia inakuwa vizur kuomba Supplier wako wa kichina kukupa makadirio ya CBM u Uzito wa bidhaa yako ili upige hesabi zako kama utapata faida au Maana unaweza ukajikuta umeingia hasara so lazma uwe makini hapo.

Mambo mengine namna ya kumchagua supplier wadau wengne wataongezea maana mambo ni mengi hatuwez kumaliza kwa article moja labda ningekuwa kwenye computer ningeiandaa vizur zaid.

Karibuni kwenye ulimwengu wa digitali ambao unaagiza mzigo china na unapambana bei na wauzaji wa jumla kariakoo.



Umeiweka vizuri sana. Kuna kodi zozote mzigo ukifika??
 
Umeiweka vizuri sana. Kuna kodi zozote mzigo ukifika??
Hao shipping Agent wa bongo almost wote wanakamilisha kila kitu mfano wakikwambia CBM moja ni $400 na mzigo wako ni 0.06CBM basi utalipia $24 tu yaan hapo kila kitu.
Na kama ni kwa ndege na umeambiwa kg ni $13.5 na mzigo wako ni kg 2 basi utalipia $27 hyo kila kitu, wewe utaenda tu kuchukua mzigo wako ofisini.

Ila kama unaagiza Marekani na unatumia forwading agents ujue kuna gharama utakuwa respobsible kuzilipa mzigo ukifika.
 
Ndo wanaoharibu biashara za watu hao leo online wote uonekana ni DECO. Sijui kwann wabongo hawapo serious na life, uona ni bora apige sh 200 ya leo aache elf 10 ya kesho.

Kuna mtu katupiga zaidi ya bilioni moja jumla ya watz 200 Dodoma, Dar na Arusha Mimi amenipiga milioni 6 wengine hadi milioni 30 hizi hizi kampuni za kuuza viwanja vya kulipa kwa awamu tena imesajiliwa kabisa inaitwa VKP investment mmiliki jina Yona hana hata 10 ya kutulipa, kesi ipo mahakamani mwaka wa nne huu. Yaani mtu unafika uwezo wa kuzungusha hadi bilioni moja kwenye uuzaji wa viwanja then unashindwa kuendesha kampuni pesa zinaishia kwenye chupi na chupa.

Wapo waliopata viwanja vyao wengine tumepigwa kwa kuonyeshwa viwanja wasivyomiliki yaani wanakuuzia kiwanja au Shamba kumbe mwenye Shamba awajamalizana nae unalipa pesa kampuni badala ya kumlipa mwenye eneo wao wanazipeleka kwenye starehe, chochote afanyacho mswahili kuwa makini Sana unaweza geuzwa wewe ndo fursa.
Duuuh, nlitaka kununua kiwanja kupitia hayo makampuni nimeshtuka.
 
Duuuh, nlitaka kununua kiwanja kupitia hayo makampuni nimeshtuka.
Vipo nilivyonunua kwenye kampuni na vipo poa havina migogoro kabisa,sio kampuni zote ni wahuni bali wapumbavu wachache.
Nilichojifunza usikubali kuuziwa kiwanja kwenye makaratasi then wanakupeleka kukuonyesha pori eti ohoo mkishalipia ndio tutaanza kusafisha na kuweka mawe na kugawa mitaa.Usikubali kuonyeshwa pori na ukanunua.Nunua viwanja ambavyo tayari eneo walishafisha wakaweka na biconi kabisa ambayo unaiona na ndio isomayo kwenye ramani,pili ukiweza nenda wizaarani kabisa kama eneo limesajiriwa kwa kampuni husika utaona then ndo unaingia mkataba.Tatu ulizia serikali husika ya mtaa au kijiji wao huwa na taarifa kuhusu kinachoendelea ikiwemo umiliki wa muhusika.
 
Ndo wanaoharibu biashara za watu hao leo online wote uonekana ni DECO. Sijui kwann wabongo hawapo serious na life, uona ni bora apige sh 200 ya leo aache elf 10 ya kesho.

Kuna mtu katupiga zaidi ya bilioni moja jumla ya watz 200 Dodoma, Dar na Arusha Mimi amenipiga milioni 6 wengine hadi milioni 30 hizi hizi kampuni za kuuza viwanja vya kulipa kwa awamu tena imesajiliwa kabisa inaitwa VKP investment mmiliki jina Yona hana hata 10 ya kutulipa, kesi ipo mahakamani mwaka wa nne huu. Yaani mtu unafika uwezo wa kuzungusha hadi bilioni moja kwenye uuzaji wa viwanja then unashindwa kuendesha kampuni pesa zinaishia kwenye chupi na chupa.

Wapo waliopata viwanja vyao wengine tumepigwa kwa kuonyeshwa viwanja wasivyomiliki yaani wanakuuzia kiwanja au Shamba kumbe mwenye Shamba awajamalizana nae unalipa pesa kampuni badala ya kumlipa mwenye eneo wao wanazipeleka kwenye starehe, chochote afanyacho mswahili kuwa makini Sana unaweza geuzwa wewe ndo fursa.
Huyu tapeli hana tofauti na jatu
 
Lizweni tu[emoji16][emoji16] unawezaje nunua vitu kwa watu kati kiasi hiko si bora kununua kariakoo.
Mimi sijawahi amini mtu
Naagiza mwenyewe.
Nilianza AliExpress siku nikawa mzoefu siku hizi sitaki hata kuiona.

Nikahamia Alibaba, nimeshaichoka, nikazama kule taobao, nikasituka hawana bei Rafiki, nikaingia soko la fish market lipo china wanauza used walizotumia kama unavyoona kupatana[emoji1787][emoji1787] huko sikukaa sana nikawajaribu 1688, sasa napiga huko, JD na Tmall.

Mambo safi.
Duh we ni noma
 
Jiunge na Alibaba.com na ukishapata unachokitafuta safirisha kwa Silent Ocean (GSM) Namba zao za simu ni 0746 813 813 watakuelekeza! Kwa njia hii huwezi ibiwa hata kama ni kununua njiti ya kiberiti.
Nimefanikiwa kudownload app lakin maelekezo ya jinsi ya kununua bidhaa na nin kinafanyika mpaka isafirishwe na silent ocean nmeshindwa msaada tafadhali
 
Wale tunaoagiza mzigo kwa the late Shinzo Abe tuna comment wp?
Mkuu wewe unaagizaga mizigo Japan? Mimi kuna mazaga kibao yapo Japan ila napata changamoto kwenye shipping i.e kulepeka sehemu watakayonipakilia kwa LCL...unatumia njia gani?
 
Nimefanikiwa kudownload app lakin maelekezo ya jinsi ya kununua bidhaa na nin kinafanyika mpaka isafirishwe na silent ocean nmeshindwa msaada tafadhali
Inaonesha hujajiunga (registration) tumia email yako. Na kuhusu silent ocean wasiliana na mwakilishi wao aliye China anaitwa Janeth kwa WhatsApp +86 130 6092 2422. Mpaka hapo utafanikiwa! Ukikwama nijulishe au nieleze unatafuta nini nikupee link
 
Inaonesha hujajiunga (registration) tumia email yako. Na kuhusu silent ocean wasiliana na mwakilishi wao aliye China anaitwa Janeth kwa WhatsApp +86 130 6092 2422. Mpaka hapo utafanikiwa! Ukikwama nijulishe au nieleze unatafuta nini nikupee link
Ahsante
 
Back
Top Bottom