Msiba wa Lowassa ni gunia la misumari kwa Kikwete

Msiba wa Lowassa ni gunia la misumari kwa Kikwete

Wewe lazima una tatizo kubwa la uelewa. Ni kwa asili yako una akili kidogo cha kushindwa kuelewa au unajifanya huna akili?

Hakuna anayemsema Kikwete ni msaliti kwa vile hakumpa Urais. Usaliti na unafiki wa Kikwete ni pale ambapo Kikwete aliweza kumhadaa Lowasa kuwa ni rafiki yake kumbe ni adui yake mkubwa.

Lowasa alichohitaji toka kwa Kikwete, hata bila ya urafiki wao, ni kutendewa haki. Kikwete alimnyima Lowasa haki yake ya kuomba kupitishwa kuwa mgombea wa CCM. Kikwete alihakikisha jina la Lowasa halimo miongoni mwa majina ya kupigiwa kura na wajumbe wa CCM.

Lowasa, bila hiyana, akaondoka CCM, akagombea Urais kupitoa CHADEMA. Lowasa akachaguliwa na mamilioni ya Watanzania, na kwa hakika ya 100% alishinda. Kutangazwa kuwa ni mshindi ilikuwa ni haki yake, hata asingekuwa rafiki wa Kikwete, lakini Kikwete kwa ushetani wake, akaamua kuzuia kutangazwa kwake, na kisha kuwakamata na kuwaseka magerezani watu wote waliokuwa wanajumlisha kura za Lowasa.

Ushetani huo wa Kikwete haukuishia kwa Lowasa, alifanya hivyo hivyo kwa Hayati Maalim Seif. Kimwete inaonekana kudhulumu haki za watu ni asili yake. Na mtu mwenye moyo wa dhuluma lazima ni zao la shetani.

Mwenye mamlaka ya kukata majina ya watu kamati kuu ni JK (mwenyekiti ) peke yake?

Una ushahidi gani usio na shaka unaoonyesha EL alishinda uchaguzi na sio JPM? Tume ya uchaguzi Tanzania ilimtangaza JPM na sio EL.

Kukamatwa wajumlisha matokeo ya uchaguzi ni suala la dola na mamlaka zake, una uhakika gani kama hao watu hawakuwa wajumlisha uchaguzi bali walikuwa wanamanipulate kura.

Tujiepushe sana na "hearsay" za mitaani, maana Kila mtu anaweza kuongea la kwake ilimradi linamfavor na kumfurahisha yeye.

Toka 1995 mpaka uchaguzi wa mwisho 2020 wapinzani hulalamika wameibiwa kura na matokeo ni kwamba wameshinda, kuanzia Lyatonga Mrema mpaka TL, lakini ukijaribu kuutafuta ukweli unakutana na "hearsay" na story za vijiweni tu.

2025 tunakwenda kwenye uchaguzi mwingine huku tukilalama tume sio huru na blah blah nyingi halafu tukishindwa tunasema tumeibiwa kura, kwanini tusihakikishe tume inakuwa huru na Kila kitu tunajiridhisha nacho ndio twende kwenye uchaguzi ili tuepuke maneno ya tumeibiwa kura.
 
Kikwete ni mtu mnafiki Sana.Ila sishangai Sana watu wengi wa pwani Wana Tania hizo,ni watu wa kuogopa sana.

Unafiki ni tabia ya Watanzania wote tusitake kusingizia watu wa Pwani.

Watu wengi wa Pwani ni waislamu, kwenye uislamu moja ya kipengele kinachokemewa sana ni unafiki sasa sijui tunawezaje kuwahusisha watu wa Pwani na unafiki.

Watu wa Pwani wangekuwa wanafiki sidhani kama wangeweza kumkaribisha JKN aka Nyerere na kuishi naye Dar es salaam na kuwa naye kwenye harakati za uhuru mpaka kutoa hela zao mifukoni.

Watanzania tungekuwa sio wanafiki basi sidhani kama CCM Leo hii ingekuwa madarakani, Watanzania tungekuwa sio wanafiki sidhani kama Taifa hili lingekuwa masikini na watanzania wenzetu kutoka baadhi ya community wasingekuwa masikini.
Taifa lingekuwa sio la wanafiki basi ukabila na udini usingekuwepo maofisini na mitaani.
 
Mwenye mamlaka ya kukata majina ya watu kamati kuu ni JK (mwenyekiti ) peke yake?

Una ushahidi gani usio na shaka unaoonyesha EL alishinda uchaguzi na sio JPM? Tume ya uchaguzi Tanzania ilimtangaza JPM na sio EL.

Kukamatwa wajumlisha matokeo ya uchaguzi ni suala la dola na mamlaka zake, una uhakika gani kama hao watu hawakuwa wajumlisha uchaguzi bali walikuwa wanamanipulate kura.

Tujiepushe sana na "hearsay" za mitaani, maana Kila mtu anaweza kuongea la kwake ilimradi linamfavor na kumfurahisha yeye.

Toka 1995 mpaka uchaguzi wa mwisho 2020 wapinzani hulalamika wameibiwa kura na matokeo ni kwamba wameshinda, kuanzia Lyatonga Mrema mpaka TL, lakini ukijaribu kuutafuta ukweli unakutana na "hearsay" na story za vijiweni tu.

2025 tunakwenda kwenye uchaguzi mwingine huku tukilalama tume sio huru na blah blah nyingi halafu tukishindwa tunasema tumeibiwa kura, kwanini tusihakikishe tume inakuwa huru na Kila kitu tunajiridhisha nacho ndio twende kwenye uchaguzi ili tuepuke maneno ya tumeibiwa kura.

Wewe inaonekana ni mtu wa blabla sana. Watu wanaongea kwa evidence, wewe unaleta hadithi.

Timu ya ujumlishaji matojeo ya Lowasa ilikuwa inapokea nakala za nakala za fomu za matojeo zenye sahihi za wahusika wote. Kikwete baada ya kupata habari hizo, akaamuru kituo hicho cha ujumlishaji kura za Lowasa kivamiwe na kumbukumbu zote zipotezwe.

Katika hali ya kawaida, kama Kikwete asingekuwa na ushetani ndani mwake, si angewaachana hizo kumbukumbu zao, na kama kumbukumbu zilichezewa, sizingeletwa fomu original ambazo kila chama na wasimamizi wa uchaguzi walikuwa wanapewa?

Hivi unajua kwa kuogopa kuonekana wazi uhuni uliofanyika, walitangaza tu tarakimu za jumla bila hata ya kusema kila mgombea alipata kura ngapi toka kila mkoa, kama sheria inavyotaka?
 
Wewe inaonekana ni mtu wa blabla sana. Watu wanaongea kwa evidence, wewe unaleta hadithi.

Timu ya ujumlishaji matojeo ya Lowasa ilikuwa inapokea nakala za nakala za fomu za matojeo zenye sahihi za wahusika wote. Kikwete baada ya kupata habari hizo, akaamuru kituo hicho cha ujumlishaji kura za Lowasa kivamiwe na kumbukumbu zote zipotezwe.

Katika hali ya kawaida, kama Kikwete asingekuwa na ushetani ndani mwake, si angewaachana hizo kumbukumbu zao, na kama kumbukumbu zilichezewa, sizingeletwa fomu original ambazo kila chama na wasimamizi wa uchaguzi walikuwa wanapewa?

Hivi unajua kwa kuogopa kuonekana wazi uhuni uliofanyika, walitangaza tu tarakimu za jumla bila hata ya kusema kila mgombea alipata kura ngapi toka kila mkoa, kama sheria inavyotaka?

Sasa Mimi nawewe nani ni blah blah, weka ushahidi unaoonyesha EL aliibiwa kura na alikuwa ameshinda uchaguzi.

Hao vijana hawakukamatwa na JK walikamatwa na dola kwa kutiliwa shaka kufanya vitendo vya kutiliwa shaka, wapi walikuwa registered na mamlaka na kutambulika kufanya hiyo kazi? Tume ya uchaguzi iliwapa kibali na kuwa aware na hao watu?

Tume pekee kisheria ndio yenye mamlaka yakujumlisha na kutangaza matokeo na si vinginevyo.

Brother unaniita Mimi blah blah wakati chote ulichoandika na kujibu ni hearsay na hakuna clear evidence yeyote toka hiyo 2015.
 
Unafiki ni tabia ya Watanzania wote tusitake kusingizia watu wa Pwani.

Watu wengi wa Pwani ni waislamu, kwenye uislamu moja ya kipengele kinachokemewa sana ni unafiki sasa sijui tunawezaje kuwahusisha watu wa Pwani na unafiki.

Watu wa Pwani wangekuwa wanafiki sidhani kama wangeweza kumkaribisha JKN aka Nyerere na kuishi naye Dar es salaam na kuwa naye kwenye harakati za uhuru mpaka kutoa hela zao mifukoni.

Watanzania tungekuwa sio wanafiki basi sidhani kama CCM Leo hii ingekuwa madarakani, Watanzania tungekuwa sio wanafiki sidhani kama Taifa hili lingekuwa masikini na watanzania wenzetu kutoka baadhi ya community wasingekuwa masikini.
Taifa lingekuwa sio la wanafiki basi ukabila na udini usingekuwepo maofisini na mitaani.
Unafiki wa some measure kila mtu anao,Ila watu wa pwani wamezidi.
 
JK ni mnafiki sana.Nani unafikiri kasahau alipo

Unafiki wa some measure kila mtu anao,Ila watu wa pwani wamezidi.
Narudia tena, WATANZANI WOTE NI WANAFIKI TU.

CDM: EL fisadi na wakamuweka kwenye list of shame, hao hao wanampa nafasi ya kugombea Urais na kutuliza ushahidi uko wapi El fisadi?
Musukuma Mbunge: alikuwa rafiki mkubwa wa EL na kutumia sana hela ya EL lakini alimkana na hata kumdhaliliisha kisa JPM.
CCM: Ilimuita EL fisadi, mwizi na mgonjwa, hao CCM wakampokea Kwa kishindo eti nimerudi nyumbani.
Watanzania JK akiwa Rais walisema wanataka Rais mkali na dictator, akaja Rais mkali na kaelement kaudikteta wakasema wanataka Rais kama JK mwenye ubinadamu.

Watanzania hawa hawa wanalalamikia wanaibiwa kwenye madini na makelele mengi, anakuja mtu anafumua mikataba ya madini wanarudi kusema tutashitakiwa.

Watanzania hawa hawa wakristo Kwa waislamu Leo hii wanapeleka watoto shule za kidini na kuacha shule za umma, watanzania hawa hawa kuna taasisi zimejaa ukabila na kama wewe si mchaga au mkristo hupati kazi, watanzania hawa hawa kuna taasisi wamejaa wahaya na wakristo kama huna uhusiano nao hupati kazi, zipo taasisi watanzania hawa hawa zimejaa waislamu (japo ni chache) kama wewe sisi muislamu hupati kazi.
 
Hakuna wakati ambapo Kikwete amesemwa vibaya na kusutwa kama wakati huu wa msiba wa Lowasa. Mzee huyu amesutwa na kuzodolewa ktk namna ambayo siyo rahisi kwa nafsi yake kukosa maumivu.

Ni kwa vile tu moyo wa mtu ni kichaka huwezi kujua unaongea nn. Lkn hata kwa kumuangalia tu anaonekana usoni kwake kapoteza nuru, furaha na bashasha. Badala yake amejaa wasiwasi, wahaka na hofu.

Nimemuangalia leo alipoinuliwa ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Lowasa alitembea kwa uoga na almanusura apepesuke mbele ya jeneza.

Familia ya Lowasa imewashukuru watu wengi sana lkn Kikwete hakutajwa hata kwa bahati mbaya. Yaani urafiki wake na Lowasa wakati wa ujana na uwepo wake msibani vyote vimepuuzwa. Huu ni msumari wa moto uliopigiliwa utosini kwa Kikwete.

Mwito.
Tujifunze kuishi vema na watu ili tuwe na mwisho mwema.
Kikwete ni mnafiki kinoma mkuu.Hebu fuata link ifuatayo uone yaliyomtokea Chuo cha Kijeshi Monduli kwa sababu ya unafiki wake.

 
Walalahoi wanajadili ujinga ambao haumdhuru Kikwete yupo na maisha yake hana habari na maisha ya mtu. Kaeni kwa kutulia
Atakufa na wahaka, wewe subiri tu. Si umeona leo kaondoka mapema msibani huku akipepesuka!!?
 
Lakini sababu hasa ya Jakaya Mrisho Kikwete kulaumiwa kwa ajili ya Edward Ngoyai Lowassa ni zipi?

Je, zaweza kuwa ni hizi mbili?

1. Inasemekana tangu mwaka 1995 walifanya alliance ya mmojawao either by hooks or by crooks ni lazima aje kuwa Rais na mwingine PM.


Mwaka 1995 waliingia kwenye mchujo. Hawakupenya kwa sbb mwasisi wa taifa hili Hayati Mwl. Julius K. Nyerere aliwapiga "veto". Nyota ikamzukia Hayati Benjamin William Mkapa

Hawakufa moyo. Waliendelea mbele na mipango yao hadi 2005. Mchuano ulikuwa mkali sana kati yao. Mazungumzo yakafanyika nje ya kapu la mchujo. Mkataba ukaingiwa kati yao kuwa EL amwachie JK na yeye zamu yake ingekuwa 2015 na sharti lingine ktk mapatano hayo likawa, angeshinda (JK), basi mzee EL angekuwa PM wake. Ndivyo ilivyokuwa.

2. Mambo yaliharibika mara baada ya safari yao ya matumaini ilipoanza Novemba, 2005.

Katikati hapo (mwaka 2008) ikazuka kashfa ya kampuni ya ufuaji umeme ya Richmond PLC.

Zigo la kashfa hiyo likamwangukia EL pekee. Rais na rafiki yake JK akashindwa kumlinda wala kumtetea.

Wapambe wakavuruga kila kitu. Na kwa sbb hiyo PM - Edward Lowassa akajiuzuru u - PM mwaka huo 2008.

Njiani pale wakapozana kwa namna walivyojua. Lakini wapambe wa katikati wasiotaka EL aje kuwa Rais, wakajaribu kila njia kumchafua na hata kumuua kwa sumu.

Hilo lilimsumbua sana EL kiasi cha kujiuliza nini kimempata rafiki yake (Rais JK) ambaye ana resources zote za kuhakikisha anamlinda lakini akashindwa kufanya hivyo hata kuacha mifumo ndani ya serikali na chama chao CCM kumsakama na ku - tarnish image yake kiasi kile.

Mzee akasubiri hadi 2015. JK alijaribu kutunza ahadi yake kumwachia rafikiye. Vurugu zilizotokea Dodoma mwezi Juni, 2015 wakati wa mkutano mkuu? Halmashauri kuu ya CCM? kuteua mgombea kila mtu anakumbuka na kuelewa vyema. Jakaya Mrisho Kikwete akamtosa rafikiye mchana kweupe!!.

EL kwa hasira akaondoka CCM na kujiunga na CHADEMA. Huko akapata nafasi ya kutimiza ndoto yake. Akagombea Urais kwa udhamini wa CHADEMA kushindana na mgombea wa CCM John P. Magufuli.

Ushindani ktk uchaguzi huo ulikuwa mkali sana. Kura zikapigwa na kuhesabiwa. Eti John P. Magufuli wa CCM akatangazwa mshindi. Lakini wachunguzi wa mambo wanasema wazi kuwa Lowassa ndiye aliyeshinda kwenye ballot box lakini ktk kutangazwa, akatatangazwa John P. Magufuli!!

Hilo likathibitisha pasipo shaka kuwa rafikie alikuwa na dhamira ya kumtosa tangu mwanzo. Angekuwa ni mtu wa kusimama ktk mapatano yao na kama huko CCM mlango ulijifunga pasipo kutarajua, basi JK alikuwa na uwezo wa kumpa rafikie u - Rais wake hata kupitia CHADEMA. Hakufanya hivyo!!

Hiki ndicho kinachomuumiza Jakaya Mrisho Kikwete. Dhamira yake inamsuta. Anaona aibu. Na yule mtu waliyempa u - Rais kupitia CCM (John P. Magufuli) alitumia nafasi na mamlaka yake sawasawa kuwanyoosha akiwemo yeye mwenyewe Kikwete.

Yaani Jini walilolifuga na kulilisha wenyewe (John P. Magufuli), likawageuka na kuanza kunyonya damu zao. Mwisho wa siku wakaona kuwa, ipo siku linaweza kuja kuwaua. Wakaamua kutumia umafia kuliondoa!!
Ume ongea Historia nzito mkuu, endelea kutujuza je zile Kash Kash kipindi Cha magu.
👉Ali fanya kweli, au ndo mbinu za kina jk??
 
Hakuna wakati ambapo Kikwete amesemwa vibaya na kusutwa kama wakati huu wa msiba wa Lowasa. Mzee huyu amesutwa na kuzodolewa ktk namna ambayo siyo rahisi kwa nafsi yake kukosa maumivu.

Ni kwa vile tu moyo wa mtu ni kichaka huwezi kujua unaongea nn. Lkn hata kwa kumuangalia tu anaonekana usoni kwake kapoteza nuru, furaha na bashasha. Badala yake amejaa wasiwasi, wahaka na hofu.

Nimemuangalia leo alipoinuliwa ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Lowasa alitembea kwa uoga na almanusura apepesuke mbele ya jeneza.

Familia ya Lowasa imewashukuru watu wengi sana lkn Kikwete hakutajwa hata kwa bahati mbaya. Yaani urafiki wake na Lowasa wakati wa ujana na uwepo wake msibani vyote vimepuuzwa. Huu ni msumari wa moto uliopigiliwa utosini kwa Kikwete.

Mwito.
Tujifunze kuishi vema na watu ili tuwe na mwisho mwema.
Kama kawaida JK Huwa hajibu anaendelea na michakato yake
 
Hakuna wakati ambapo Kikwete amesemwa vibaya na kusutwa kama wakati huu wa msiba wa Lowasa. Mzee huyu amesutwa na kuzodolewa ktk namna ambayo siyo rahisi kwa nafsi yake kukosa maumivu.

Ni kwa vile tu moyo wa mtu ni kichaka huwezi kujua unaongea nn. Lkn hata kwa kumuangalia tu anaonekana usoni kwake kapoteza nuru, furaha na bashasha. Badala yake amejaa wasiwasi, wahaka na hofu.

Nimemuangalia leo alipoinuliwa ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Lowasa alitembea kwa uoga na almanusura apepesuke mbele ya jeneza.

Familia ya Lowasa imewashukuru watu wengi sana lkn Kikwete hakutajwa hata kwa bahati mbaya. Yaani urafiki wake na Lowasa wakati wa ujana na uwepo wake msibani vyote vimepuuzwa. Huu ni msumari wa moto uliopigiliwa utosini kwa Kikwete.

Mwito.
Tujifunze kuishi vema na watu ili tuwe na mwisho mwema.
Urais haugawiwi kienyeji hivyo nyie mbumbumbu msiojua Siri.
 
Nyie wajinga kwenye mlitaka fisadi apewe urais , au mnazani urais ni kupeana tu, ndomana kikwete anabaki kuwa best president, kwa kumkataa huyo mzee
 
Jamani nafasi ya uraisi nchini ni moja tu na kuna watanzania wengi wanaiwinda kuwa siku moja inaweza kuwa bahati yao kama ilivyo tokea kwa Marehemu Magufuli.
Sasa marehemu Lowasa ndio Mwenyezi Mungu hakuwa na mipango ya yeye kuwa raisi. Kwa hiyo tukubali na tushukuru kwa neema nyingi alizobarikiwa na Mungu.
 
Back
Top Bottom