Msiba wa Lowassa ni gunia la misumari kwa Kikwete

Msiba wa Lowassa ni gunia la misumari kwa Kikwete

Kivipi?!!! [emoji38][emoji38][emoji38] hivi wewe ulikuwepo wakati mkapa anagombea u Rais unajua alichuana na nani?!!! Na alikua wa ngapi baada ya mkapa?!!
Itakua ulizaliwa juziii..
LOWASSA ZAIDI YA URAFIKI WAO NA KIKWETE HAKUMSAIDIA KUA RAIS, kikwete nyota yake ilishang’aaa hakukua wa kumstopisha..
Lowassa na wengine wote walikua ni wapambe wa kikwete upo!!!
Huna ujualo, Huyo Kikwete hata hiyo miaka 1995 hakuwa na mawazo kugombea Urais. Ni ushawishi wa EL na RA

Sent from my SM-A107M using JamiiForums mobile app
 
Leo nimemuona Kikwete pale kwenye msiba Monduli. Hali yake haikuwa ya kawaida kabisa na mwishowe aliondoka na sijui hata alipoenda.

Sasa sijui alikuwa na tatizo la kiafya au ni kitu gani? Alikuwa hawezi kukaa kwa utulivu kwenye kiti chake. Na sura yake ikionyesha kama vile alikuwa na maumivu flani.

Mwili wake ulikuwa una swing back and forth akiwa amekaa kwenye kiti. Na ni jambo ambalo naona kama alikuwa akishindwa kuji control. Baada ya muda kile kiti chake kilikuwa wazi kabla hata Rais hajaondoka. Kwasababu kiitifaki, hakuna anayeruhusiwa kuondoka kabla ya rais.
Kumbe!
 
sikia rafiki yawezekana wewe hujui,jk kwenye issue ya lowassa alifanya sawasawa na wala hana baya lolote alilofanya,sasa kuhusu haiba yake,wajihi wake,jk anaumwa kansa ya tezi dume hivi unategemea awe na nguvu vipi?,umri pia umekwenda hawezi kuwa mkakamavu,hebu tumwache jk please
Sio kweli! Alimtenda sana Lowasa!
 
sikia rafiki yawezekana wewe hujui,jk kwenye issue ya lowassa alifanya sawasawa na wala hana baya lolote alilofanya,sasa kuhusu haiba yake,wajihi wake,jk anaumwa kansa ya tezi dume hivi unategemea awe na nguvu vipi?,umri pia umekwenda hawezi kuwa mkakamavu,hebu tumwache jk please
Hiyo tezi dume si alitibiwa?
 
Heshima aliyopata ni kwasababu ya Kikwete. Lowassa alikuwa mwizi asiyeshiba ulitaka aachwe? Yeye si wa kwanza kujiuzulu hata Warioba alipigwa chini. Rais ndiye mkuu wa nchi
Maneno ya DrMwakyembe kuwa kuna taarifa zilifichwa na endapo wangeziweka wazi wangeangusha serikali ndio yanafanya Lowassa aonekane alitolewa sadaka ili JK na serikali yake apone
 
Hakuna wakati ambapo Kikwete amesemwa vibaya na kusutwa kama wakati huu wa msiba wa Lowasa. Mzee huyu amesutwa na kuzodolewa ktk namna ambayo siyo rahisi kwa nafsi yake kukosa maumivu.

Ni kwa vile tu moyo wa mtu ni kichaka huwezi kujua unaongea nn. Lkn hata kwa kumuangalia tu anaonekana usoni kwake kapoteza nuru, furaha na bashasha. Badala yake amejaa wasiwasi, wahaka na hofu.

Nimemuangalia leo alipoinuliwa ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Lowasa alitembea kwa uoga na almanusura apepesuke mbele ya jeneza.

Familia ya Lowasa imewashukuru watu wengi sana lkn Kikwete hakutajwa hata kwa bahati mbaya. Yaani urafiki wake na Lowasa wakati wa ujana na uwepo wake msibani vyote vimepuuzwa. Huu ni msumari wa moto uliopigiliwa utosini kwa Kikwete.

Mwito.
Tujifunze kuishi vema na watu ili tuwe na mwisho mwema.
Lakini sababu hasa ya Jakaya Mrisho Kikwete kulaumiwa kwa ajili ya Edward Ngoyai Lowassa ni zipi?

Je, zaweza kuwa ni hizi mbili?

1. Inasemekana tangu mwaka 1995 walifanya alliance ya mmojawao either by hooks or by crooks ni lazima aje kuwa Rais na mwingine PM.


Mwaka 1995 waliingia kwenye mchujo. Hawakupenya kwa sbb mwasisi wa taifa hili Hayati Mwl. Julius K. Nyerere aliwapiga "veto". Nyota ikamzukia Hayati Benjamin William Mkapa

Hawakufa moyo. Waliendelea mbele na mipango yao hadi 2005. Mchuano ulikuwa mkali sana kati yao. Mazungumzo yakafanyika nje ya kapu la mchujo. Mkataba ukaingiwa kati yao kuwa EL amwachie JK na yeye zamu yake ingekuwa 2015 na sharti lingine ktk mapatano hayo likawa, angeshinda (JK), basi mzee EL angekuwa PM wake. Ndivyo ilivyokuwa.

2. Mambo yaliharibika mara baada ya safari yao ya matumaini ilipoanza Novemba, 2005.

Katikati hapo (mwaka 2008) ikazuka kashfa ya kampuni ya ufuaji umeme ya Richmond PLC.

Zigo la kashfa hiyo likamwangukia EL pekee. Rais na rafiki yake JK akashindwa kumlinda wala kumtetea.

Wapambe wakavuruga kila kitu. Na kwa sbb hiyo PM - Edward Lowassa akajiuzuru u - PM mwaka huo 2008.

Njiani pale wakapozana kwa namna walivyojua. Lakini wapambe wa katikati wasiotaka EL aje kuwa Rais, wakajaribu kila njia kumchafua na hata kumuua kwa sumu.

Hilo lilimsumbua sana EL kiasi cha kujiuliza nini kimempata rafiki yake (Rais JK) ambaye ana resources zote za kuhakikisha anamlinda lakini akashindwa kufanya hivyo hata kuacha mifumo ndani ya serikali na chama chao CCM kumsakama na ku - tarnish image yake kiasi kile.

Mzee akasubiri hadi 2015. JK alijaribu kutunza ahadi yake kumwachia rafikiye. Vurugu zilizotokea Dodoma mwezi Juni, 2015 wakati wa mkutano mkuu? Halmashauri kuu ya CCM? kuteua mgombea kila mtu anakumbuka na kuelewa vyema. Jakaya Mrisho Kikwete akamtosa rafikiye mchana kweupe!!.

EL kwa hasira akaondoka CCM na kujiunga na CHADEMA. Huko akapata nafasi ya kutimiza ndoto yake. Akagombea Urais kwa udhamini wa CHADEMA kushindana na mgombea wa CCM John P. Magufuli.

Ushindani ktk uchaguzi huo ulikuwa mkali sana. Kura zikapigwa na kuhesabiwa. Eti John P. Magufuli wa CCM akatangazwa mshindi. Lakini wachunguzi wa mambo wanasema wazi kuwa Lowassa ndiye aliyeshinda kwenye ballot box lakini ktk kutangazwa, akatatangazwa John P. Magufuli!!

Hilo likathibitisha pasipo shaka kuwa rafikie alikuwa na dhamira ya kumtosa tangu mwanzo. Angekuwa ni mtu wa kusimama ktk mapatano yao na kama huko CCM mlango ulijifunga pasipo kutarajua, basi JK alikuwa na uwezo wa kumpa rafikie u - Rais wake hata kupitia CHADEMA. Hakufanya hivyo!!

Hiki ndicho kinachomuumiza Jakaya Mrisho Kikwete. Dhamira yake inamsuta. Anaona aibu. Na yule mtu waliyempa u - Rais kupitia CCM (John P. Magufuli) alitumia nafasi na mamlaka yake sawasawa kuwanyoosha akiwemo yeye mwenyewe Kikwete.

Yaani Jini walilolifuga na kulilisha wenyewe (John P. Magufuli), likawageuka na kuanza kunyonya damu zao. Mwisho wa siku wakaona kuwa, ipo siku linaweza kuja kuwaua. Wakaamua kutumia umafia kuliondoa!!
 
sikia rafiki yawezekana wewe hujui,jk kwenye issue ya lowassa alifanya sawasawa na wala hana baya lolote alilofanya,sasa kuhusu haiba yake,wajihi wake,jk anaumwa kansa ya tezi dume hivi unategemea awe na nguvu vipi?,umri pia umekwenda hawezi kuwa mkakamavu,hebu tumwache jk please
Unalazimisha tuwaze unavyotaka wewe?
 
Kikwete ni rafiki wa Hayati Lowassa au familia ya Lowassa? Asiyejua maana haambiwi maana..

Kama Kikwete na Lowassa ndio walikuwa marafiki ,familia hata imtaje au isimtaje haifuti urafiki wao na pia familia ndio inatakiwa itambue ni Kikwete ndio amefanya mzee akazikwa kwa heshima hivyo Kwa sababu ya kuteuliwa Uwaziri mkuu.

Kama utaendelea kushabikia vitu vidogo vidogo na kuacha kujadili mambo makubwa tutakuwa hatuna namna zaidi ya kukupuuza
Wewe umejadili lupi kubwa hapa.
 
Mwacheni JK,Lowassa kamati kuu ilishamkataa kipindi cha mwalimu,yaliyomkuta ni ajali ya kisiasa na ni political vibes tu hizo,kwani Lowassa aliandikiwa lazima awe Rais wa nchi hii?watu wanataka kutengeneza story tu,amemaliza Muda wake ,apumzike kwa amani,tutaendelea kumshukuru JK kwa kutuletea Chuma Magufuli
 
Hata kama ni wewe rafiki yangu uje unisukumie kashfa nipate ajali ya kisiasa nianguke kukulinda wewe, nijikongoje niinuke, uje tena unifyekelee mbali nisiyafikie maono yangu, huo moyo wa kukuvumilia undava wako mimi rafiki yako mkubwa nitautoa wapi?
 
sikia rafiki yawezekana wewe hujui,jk kwenye issue ya lowassa alifanya sawasawa na wala hana baya lolote alilofanya,sasa kuhusu haiba yake,wajihi wake,jk anaumwa kansa ya tezi dume hivi unategemea awe na nguvu vipi?,umri pia umekwenda hawezi kuwa mkakamavu,hebu tumwache jk please
Hata muandike nini, itakuwa na itabaki kuwa kwamba JK alimsaliti rafikiye Lowasa , hakuna wa kubadilisha hilo duniani, mbinguni wala baharini.

Hata uje na majini kama yake ya Yanga ukweli utabaki hivyo. Usaliti!
 
Tushike lipi si wanasema bila Mkapa jpm asingekua Raisi sasa jk analaumiwa kwa lipi
Baada ya kuzidiwa na upepo na nguvu ya Lowassa wakati anampambania BM ndipo akaomba msaada wa mzee wa Lupaso,hapo ndipo mzee akatumia fursa hiyo kuingiza kijana wake.Alikubali ni bora kachero aukose ukuu lakini EL asiingie jumba jeupe
 
Back
Top Bottom