Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability?

Inaonekana anapiga kwenye mshono
 
Hoja inashindwa na Hoja iliyo bora shida yenu wadanganyika mnaamini katika Porojo
 

Watu wenye tabia ya kujipendekeza na kuogopa maisha ndio huona lugha za Lisu ni uropokaji. Ikiwa unajiamini na hutegemei mbeleko huwezi kuogopa kusema ukweli.
 
Maneno ya Lissu tusiyachukue kwa kumuangalia yeye na uchama wake wa CHADEMA bali katika hali halisi. Kimsingi Lissu hupo sawa kwa aslimia kubwa...CHADEMA kwasasa imekua assimilated na CCM jambo ambalo kwetu ni ushindi. Siasa zetu ni ngumu kwa kuzielewa ingawa ni rahisi kwa kuziangalia.
 
Kuna fukuto huko ndani na akitoswa sijui ataenda Kugombea chama gani Sasa..

Lisu asisahau kwamba Chadema iliwahi muuza Slaa na mambo yakaenda.
Lissu nguvu yake ni kubwa kuliko chadema kwa sasa,na aijua chadema nje ndani kwa sasa,cha maana chadema watakachofanya wakiona atawaharibia ni kum Chacha Wangwe tu kisha zigo kurushiwa CCM
 
Yupo very straight na sahihi kabisa.

Nikionacho hapa umeweka pembeni na rehani taaluma yako na kuamua kuvaa sare za Chama chako kuingia front kukipambania, sababu wewe unaona athari za mikutano ya Tundu Lissu kwa Chama chako, hivyo unataka kuvuruga kwa kuibua mijadala chonganishi.

Labda unisaidie, ni kiongozi gani wa CHADEMA uliyemsikia akitoa kauli za kuwa wamekubali kugawiwa majimbo? Maana anachofanya Lissu ni kushambulia kauli za namna hiyo, maana ni kweli kauli hizo zipo lakini hazitoki ndani ya CHADEMA ila waanzilishi wake ni nyie wenyewe ndani ya CCM.

Kuhusu maridhiano, binafsi sijawahi kuwasikia CHADEMA kama Chama wakitoa tamko la kuwa wameshafanya maridhiano, bali kuna mambo wameridhiana lakini hawajafika mwisho kwani vikao vya maridhiano vinaendelea, hata rais alikiri kuwa hata yeye anakumbana na vikwazo kutoka kwa wahafidhina ndani ya Chama lakini akatoa wito wayapokee maridhiano na waendelee kumpa muda wakati vikao vinaendelea.

katika hili, Pascal Mayalla unataka kutubeba ufala.
 
Nyerere alisema, "ujinga sio tusi", bali upumbavu.
 
Samia anajua kujishusha kwa faida ya wengi. Yupo diplomatic na mijadala inasaidia nchi kuliko yeye mwenyewe.
 
Paskali, acha tafsiri ambayo hailingani na alichosema Lisu. Kwenye clip uliyoweka Lisu anatoa mifano ya waliopigwa changa la macho ktk chaguzi zilizopita na anasema itakuwa ni ujinga kuingia mtego ule ule. Hakuna mahali popote kwenye clip anasema maridhiano ni ujinga. Pili hatujaambiwa kwenye maridhiano wamekubaliana nini ili uweze ku-conclude kuwa Lisu anayaita ujinga.
 
Lissu nguvu yake ni kubwa kuliko chadema kwa sasa,na aijua chadema nje ndani kwa sasa,cha maana chadema watakachofanya wakiona atawaharibia ni kum Chacha Wangwe tu kisha zigo kurushiwa CCM

Hakuna chama cha upinzani kinaweza kufanya mauaji kwa mfuasi wake kisiingie hatiani. Chama tawala tu ndio huweza, maana ndio chenye maamuzi dhidi mamlaka za kiuchunguzi.
 
Jemadari Tundu Lissu akiendelea kuliamsha Taifa Mkoani Singida Kijiji cha Mtinko amesema tukienda kwenye Uchafuzi wa 2025 bila Katiba mpya TUMEKWISHA!.

KATIBA MPYA! KATIBA MPYA! KATIBA MPYA!

NO HATE NO FEAR.
 
Matumizi ya lugha inayotumika kwangu sio jambo kubwa sana, japo ni muhimu.

Kwangu ninachopigania ni kiongozi kufuata taratibu walizojiwekea, asiwepo mmoja akataka kujiweka juu ya wenzie chamani, kwamba iwe kama vile yeye ndie pekee mwenye mdomo wa kusema, basi ndio anasema popote, na chochote anachoamua.

Ukiwa kama kiongozi halafu unakwenda nje ya vikao vyenu unaanza kuwasema wenzio, tena mbaya zaidi mpaka kuuliza kama wana akili kweli, huu kwangu ni ujuaji wa kitoto uliovuka mipaka, kukosa hekima kabisa, ni kuropoka tu.
 
Kwangu ninachopigania ni kiongozi kufuata taratibu walizojiwekea, asiwepo mmoja akataka kujiweka juu ya wenzie chamani, kwamba iwe kama vile yeye ndie pekee mwenye mdomo wa kusema, basi anasema popote chochote.
Hili hatjui kama hivyo ndivyo.
Sijawasikia CHADEMA wenyewe wakilisemea hili kama unavyoliweka wewe.

Pamoja na kukubaliana na msingi wa hoja hiyo, kuna mengi ambayo bado tulioko huku nje ya chama hatuyajui.
Kwa mfano. Mbowe kama Mwenyekiti wa chama alitoa msimamo wake (sijui kama ulikuwa msimamo wa kushirikisha na wenzake kwenye chama), alipozungumzia habari za maridhiano kwa mara ya kwanza kabisa, kwenye ule mkutano wake kule na Diaspora; na kuurudia msimamo huo huo mara kadhaa sehemu nyinginezo; kama pale viwanja vya Furahisha Jijini Mwanza.

Msimamo huo pia hatujasikia ukizungumziwa kwa uwazi ndani ya chama.

Kwa hivi karibuni kaamua kunyamaza, kamwachia Lissu naye aseme yake

Kwa hiyo, kwa upande wangu sijui kama unayoyasema wewe kuhusu haya yanayoendelea ndani ya chama ni kweli au siyo kweli. Hili sijui.
Lakini naunga mkono anayosema Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, labda arekebishe lugha tu kidogo ili isitumiwe na watu wasiokitakia chama hicho mema, kama inavyofanyika sasa hivi.
Tazama mada zote zilizowekwa hapa kumhusu Lissu na aliyoongea, zimeanzishwa na watu wa aina gani utajua Lissu kagusa waya hasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…