Nadhani CHADEMA ndo wana matatizo katika uongozi wao hasa wa ngazi za chini. Kwa mfano, Meya wa Ubungo alivuliwa uanachama na katibu wa wilaya katika hali ya sintofahamu kama hii na suala lake mpaka leo halijawahi kushughulikiwa kisheria ili kubatilisha maamuzi yale. siyo ajabu akaja kuwekewa pingamizi huko mbeleni wakati wa uteuzi. Juzi anayejiita mgombea ubunge wa kilombero naye kavuliwa uanachama na katibu wa chama, baadae mwenyekiti wa kanda akaja kubatilisha yale maamuzi, mpaka sasa haijulikani aliyemvua uanachama na aliyebatilisha maamuzi yupi aliyetoa maamuzi ya halali. Sasa kwann hali hii ijitokeze kila mara? ina maana kuna ombwe la uongozi CHADEMA. Kwanni mamlaka zao zinachezewa hivi?
Ukiziangalia Barua za Chadema ukiacha zile za Makao Makuu hazina headed, mihuri inatofautiana kutoka tawi moja kwenda jingine kiasi cha kuweza kufojiwa na mtu yoyote. Kimsingi hatuwezi kumlaumu Mkurugenzi kwa hili, hata ningekua mimi nisingeweza kutoa fomu mbili za uteuzi kwa chama kimoja. Siyo sheria wala taratibu zinaruhusu jambo hilo. Wanaotakiwa kulinda mamlaka zao ni Chadema wenyewe kwa kuweka utaratibu unaoleweka ambao hauwezi kuruhusu mwanya kwa watu wenye nia ovu kufanya uhuni. Wakati mwingine unakuta ndani ya Chadema wamevurugana kwenye uteuzi, mtu anaamua kujiandikia barua anakwenda kuchukua fomu. Mkurugenzi hawezi kujua barua hii imetoka kwa mamlaka halali ama la, kwasababu hakuna kitu chochote kinachoweza kumthibitishaia hilo zaidi ya muhuri na saini.