Msimamo wa Rais Samia kuhusu demokrasia ya kisiasa, fujo za kisiasa na fujo za kidini: Tutaelewana tu!

Msimamo wa Rais Samia kuhusu demokrasia ya kisiasa, fujo za kisiasa na fujo za kidini: Tutaelewana tu!

Wanazo hoja ni kweli.
Lakini, ni hoja gani ambayo haijajibiwa hadi sasa?
Ilete hapa tuidadavue.
Hoja tumezijibu kijumla jumla sana..

Zuio la mikutano ya kisiasa ni takwa la kisheria au la mtu binafsi?

Katiba mpya isubiri tunajenga uchumi..lini tutaacha kujenga uchumi na kuliangalia sasa jambo la Katiba?

Maandamano ya kumpongeza Mwenyekiti wetu kutimiza siku 100 madarakani ni sawa ila makongamano ya wenzetu si sawa?

Naogopa sana maana naiona hiyo siku ikifika wajukuu zetu wakihoji tulikuwa wapi kama wananchi hadi kukubali kukaa na shida ya maji,matundu ya vyoo,madarasa chini ya mti kwa miaka zaidi ya 50..?
 
Hayo mambo yote yanafanyikaje wakata kwa mazingira ya siasa Tanzania vyama vya upinzani hawapewi nafasi hata kukutana na wanachama wao na hata ikitokea wamekutana tunaona vyombo vya usalama (polisi na Tiss) wanaingilia.
Kwenye suala la kutembeza bakuli wanatembeza vipi wakati vyombo wa usalama vinaingilia
Kimsingi kwa namna uliyoieleza wewe Tanzania haifanyiki tunaona jinsi chama tawala kinavyotumia vyombo vya usalama kuvuruga kwa lengo la kudhoofisha vyama mbadala
Naona kuna jambo unalifahamu lakini nikukumbushe kwa vile umelisahau.

Ukichukua Katiba ya Chama cha siasa kama vile Chadema utaona vikao vya maamuzi. Kuna
  1. Mikutano mikuu kila mwaka, kila wilaya, kila kata, kila kijiji, kila kitongoji
  2. Kamati za utendaji kila baada ya miezi mitatu, katika kila wilaya, kila kata, kila kijiji, kila kitongoji
  3. Sekretarieti zinazokutana kila siku katika kila Kanda, kila mkoa, kila wilaya, kila kata, kila kijiji, kila kitongoji.
Mfano, kuna:
  1. Mkutano mkuu Taifa
  2. Baraza la Mashauriano Kanda
  3. Baraza la Mashauriano Mkoa,
  4. Mkutano Mkuu wilaya
  5. Mkutano mkuu kata
  6. mkutano mkuu kijiji
  7. mkutano mkuu kitongoji
Mikutano kama hii imetamkwa kikatiba kwa ajili ya mabaraza ya chama, yaani
  1. Bavicha
  2. Bawacha
  3. Bazecha
Mikutano hii ndiyo inaweka, kutekeleza na kusimamia utekelezaji wa mipango ya chama,
Mikutano hii, kwa mujibu wa Rais Samia haina kizuiz, isipokuwa kizuizi cha uchumi dhaifu wa kukifanya chama kushindwa kukusanya wajumbe.

Tanzania kuna mikoa 26, wilaya 160+, Kata zaidi ya 6000, vijiji zaidi ya 12,000 na vitongoji kibao. Kwa hiyo, kuna vikao vingi vya kukiruhusu chama cha siasa kusonga mbele.

Bila shaka sasa umeelewa somo la Rais Samia.
 
Hoja tumezijibu kijumla jumla sana..

Zuio la mikutano ya kisiasa ni takwa la kisheria au la mtu binafsi?

Katiba mpya isubiri tunajenga uchumi..lini tutaacha kujenga uchumi na kuliangalia sasa jambo la Katiba?

Maandamano ya kumpongeza Mwenyekiti wetu kutimiza siku 100 madarakani ni sawa ila makongamano ya wenzetu si sawa?

Naogopa sana maana naiona hiyo siku ikifika wajukuu zetu wakihoji tulikuwa wapi kama wananchi hadi kukubali kukaa na shida ya maji,matundu ya vyoo,madarasa chini ya mti kwa miaka zaidi ya 50..?

SWALI: Zuio la mikutano ya kisiasa ni takwa la kisheria au la mtu binafsi?

Jibu: Ni takwa la kisheria. Soma vizuri ibara ya 14 ya emergency powers act. Hii ndiyo inatumika kusimamisha baadhi ya vifungu vya Katiba katika vita dhidi ya UVIKO19

SWALI: Katiba mpya isubiri tunajenga uchumi..lini tutaacha kujenga uchumi na kuliangalia sasa jambo la Katiba?

Jibu: Swali la LINI linapaswa kujibiwa na andiko la kiserikali. Unalifahamu andiko hilo? Kama halipo, maana yake ni kwamba hicho sio kipaumbele cha kitaifa bado. Ushawishi na utetezi wa dhana uendelee kufanyika hadi hapo upande wa pili utakapoona kwamba hapa hatuwezi kuendelea kuziba masikio. Siasa za fujo hapana.

SWALI: Maandamano ya kumpongeza Mwenyekiti wetu kutimiza siku 100 madarakani ni sawa ila makongamano ya wenzetu si sawa?

Jibu: Soma vizuri ibara ya 14 ya emergency powers act. Haki zote zinagawanyika mara nne. Kuna claim rights, liberty rights, power rights, immunity rights. Lakini, Rais wa ncho anayo power right ya kutengua baadhi ya haki za baadhi ya vyama vya siasa na baadhi ya raia. Hilo ni gumu kueleweka.

SWALI: Naogopa sana maana naiona hiyo siku ikifika wajukuu zetu wakihoji tulikuwa wapi kama wananchi hadi kukubali kukaa na shida ya maji,matundu ya vyoo, madarasa chini ya mti kwa miaka zaidi ya 50?

Jibu: Endelea kujenga hoja zenye mashiko. Siasa za fujo hapana.
 
Naona kuna jambo unalifahamu lakini nikukumbushe kwa vile umelisahau.

Ukichukua Katiba ya Chama cha siasa kama vile Chadema utaona vikao vya maamuzi.

Mfano, kuna:
  1. Mkutano mkuu Taifa
  2. Baraza la Mashauriano Kanda
  3. Baraza la Mashauriano Mkoa,
  4. Mkutano Mkuu wilaya
  5. Mkutano mkuu kata
  6. mkutano mkuu kijiji
  7. mkutano mkuu kitongoji
Mikutano kama hii imetamkwa kikatiba kwa ajili ya mabaraza ya chama, yaani
  1. Bavicha
  2. Bawacha
  3. Bazecha
Mikutano hii ndiyo inaweka, kutekeleza na kusimamia utekelezaji wa mipango ya chama,
Mikutano hii, kwa mujibu wa Rais Samia haina kizuiz, isipokuwa kizuizi cha uchumi dhaifu wa kukifanya chama kushindwa kukusanya wajumbe.

Tanzania kuna mikoa 26, wilaya 160+, Kata zaidi ya 6000, vijiji zaidi ya 12,000 na vitongoji kibao. Kwa hiyo, kuna vikao vingi vya kukiruhusu chama cha siasa kusonga mbele.

Bila shaka sasa umeelewa somo la Rais Samia.
Kwenye hiyohiyo mikutano tumeshuhudia baadhi ya wanachama wa CHADEMA wamewekwa rumande wengine wametoka leo
 
Kwenye hiyohiyo mikutano tumeshuhudia baadhi ya wanachama wa CHADEMA wamewekwa rumande wengine wametoka leo
Hizo ama ni isolated cases au transitional cases kwa sababu maalum.
Mfano, ukitangaza kuwa unakusudia kunyoa mav*zi mkuu wa nchi maana yake ni kwamba umejipanga kufanya siasa za fujo.
Na kiusalama, mikutano ya ndani ni hatari kuliko mikutano ya hadhara.
Kwa hiyo, utapekuliwa pekuliwa tu.
Hili nalo gumu kueleweka?
 
Hizo ama ni isolated cases au transitional cases kwa sababu maalum.
Mfano, ukitangaza kuwa unakusudia kunyoa mav*zi mkuu wa nchi maana yake ni kwamba umejipanga kufanya siasa za fujo.
Na kiusalama, mikutano ya ndani ni hatari kuliko mikutano ya hadhara.
Kwa hiyo, utapekuliwa pekuliwa tu.
Hili nalo gumu kueleweka?
Tukiachana na hayo mengine lakini Tanzania bado tunahitaji mazingira sawa ya kufanya siasa kushindwana kwa hoja sio wenye madaraka kutumia vyombo vya dola ili waendelee kubaki kwenye nafasi zao na kiukweli kuwa na upinzani ni afya kwa Demokrasia pia hata maendeleo
 
Tukiachana na hayo mengine lakini Tanzania bado tunahitaji mazingira sawa ya kufanya siasa kushindwana kwa hoja sio wenye madaraka kutumia vyombo vya dola ili waendelee kubaki kwenye nafasi zao na kiukweli kuwa na upinzani ni afya kwa Demokrasia pia hata maendeleo
Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa, halafu nakuuliza swali. Wakati Dr Slaa na Katibu Mkuu wa CDM uliona mapambana kati ya CDM na dola kama sasa? Tafakari juu sababu zake.
 
Hizi ni nadharia za kishuleshule, kwenye uhalisia utakwama sana. Mambo haya ndio yanapelekea wasomi wengi kuishia kuajiriwa, au kuwa matajiri uchwara.
Theory-Action-Review cycle haikwepeki kama unataka kufanya siasa za kitaifa.
Na theory maana yake ni yale yote uliyoyapata shuleni.
No short cut
 
Angeulizwa watu kuanza chokochoko maana yake nini.
Maana ya chokochoko hii hapa...

1628714974770.png


Huu ni uhalifu.
 


Msimamo wa Rais Samia kuhusu demokrasia ya kisiasa, fujo za kisiasa na fujo za kidini ni wa kujadiliwa kwa kina kusudi watu wengi wauelewe na kuukubali.

Tayari kuna maoni kadhaa yametolewa tangu alipofanya mahojiano yake na BBC, na kuuweka bayana.

Kuna maoni ya Askofu Bagonza, Kauli za Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, mawazo ya Godbless Lema na maoni ya watu baki. Nami napenda kutoa maoni yangu leo.

1. Tofauti kati ya "demokrasia ya kisiasa na fujo za kisiasa" haikuanzishwa na Rais Samia.

Ipo siku zote kwa sababu ya mstari unaotenganisha siasa za watu wengi zinazoendeshwa kwa kutumia nguvu ya ushawishi wa hoja (democratic people's power) na siasa za watu wengi zinazoendeshwa kwa kutumia nguvu za ubabe na mitulinga (coercive people's power).

Fujo za kisasa zinazofanywa na vyama vya upinzani huwa ni mkakati wa kuiondoa serikali katika vipaumbele vyake. Hilo jambo halikubaliki popote duniani. Viongozi wa Chadema wanapaswa kuzingatia ukweli huu.

2. Kuna fujo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akipinga kauli za Rais Samia. Mnyika anasema kuwa uhuru wa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara na maandamano hauna mipaka.

Hapana. Hakuna haki isiyo na mipaka. Ni kweli vyama vya siasa vina haki ya kufanya mikutano ya hadhara ili kueneza sera zake.

Lakini pia vinalo jukumu la kujizuia kuikwamisha serikali katika azima yake ya kutekeleza programu ambazo ni vipaumbele vya kitaifa kwa mujibu wa Ilani ya chama tawala.

Kwa mujibu wa
tangazo la Mbowe pale Mwanza, Chadema hawatambui jukumu hilii. Wanapaswa kulazimishwa kulitambua jukumu hili.

3. Kuna viongozi wa Chadema wanafanya fujo za kisiasa kupitia mgongo wa dini makanisani.

Wanazunguka makanisani na kuwaomba viongozi wa makanisa kuingiza katika ratiba zao za kikanisa kumwombea Mbowe ili aachiwe huru.

Kwa kitendo hiki, viongozi wa kidini wanashiriki kutekeleza programu za chama cha siasa. Aidha, kwa njia hii viongozi na wanachama wa Chadema wanatumia dini kufanya siasa.

Naona kwamba hapa inakuja hatari kama ile ya "mitano kwanza" ya Askofu Bagonza dhidi ya "mitano tena" ya Shehe nanihii.

Na bado hadi sasa Askofu Bagonza anaendeleza chokochoko kwa sababu ya
ugonjwa wa theomania unaomsumbua.

Theomania ni ugonjwa wa kichaa cha kidini kinachomfanya mhusika kuamini kwamba yeye ama ni Mungu au mpaka mafuta wa Mungu, na kwamba kwa sababu hiyo, yeye ni mtu mwenye uwezo wa kujua kila kitu, kufanya kila kitu, kusikilizwa na kila mtu, na kupewa utii na kila mtu.

Naye Askofu Mwamakula ametunga novena ya kumwombea Mbowe yenye kibwagizo "Mwanakondoo Ameshinda," na hivyo, kuigeuza CHADEMA kuwa Chama cha Demokrasia na Mwanakondoo Ameshinda"

Hatua za haraka zichukuliwe kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi kusimamia kanuni inayokataa jaribio lolote kuanzisha na kuendesha chama cha siasa chenye kutafuta ufuasi kwa kutumia mafundisho ya kidini.

Nawasilisha.


Mkuu naweza kukubaliana na wewe.

Lakini what about CCM ?

iT IS THE WORST OF ALL
 
Mkuu naweza kukubaliana na wewe.

Lakini what about CCM ?

iT IS THE WORST OF ALL
Usihitimishe haraka hivyo.
Weka vigezo huru mezani kuhusu utayari wa vyama vya siasa kuendesha nchi, tufanye objective scoring.
Utashangaa kwamba bado CCM inaibuka kidedea.
 
SWALI: Zuio la mikutano ya kisiasa ni takwa la kisheria au la mtu binafsi?

Jibu: Ni takwa la kisheria. Soma vizuri ibara ya 14 ya emergency powers act. Hii ndiyo inatumika kusimamisha baadhi ya vifungu vya Katiba katika vita dhidi ya UVIKO19

SWALI: Katiba mpya isubiri tunajenga uchumi..lini tutaacha kujenga uchumi na kuliangalia sasa jambo la Katiba?

Jibu: Swali la LINI linapaswa kujibiwa na andiko la kiserikali. Unalifahamu andiko hilo? Kama halipo, maana yake ni kwamba hicho sio kipaumbele cha kitaifa bado. Ushawishi na utetezi wa dhana uendelee kufanyika hadi hapo upande wa pili utakapoona kwamba hapa hatuwezi kuendelea kuziba masikio. Siasa za fujo hapana.

SWALI: Maandamano ya kumpongeza Mwenyekiti wetu kutimiza siku 100 madarakani ni sawa ila makongamano ya wenzetu si sawa?

Jibu: Soma vizuri ibara ya 14 ya emergency powers act. Haki zote zinagawanyika mara nne. Kuna claim rights, liberty rights, power rights, immunity rights. Lakini, Rais wa ncho anayo power right ya kutengua baadhi ya haki za baadhi ya vyama vya siasa na baadhi ya raia. Hilo ni gumu kueleweka.

SWALI: Naogopa sana maana naiona hiyo siku ikifika wajukuu zetu wakihoji tulikuwa wapi kama wananchi hadi kukubali kukaa na shida ya maji,matundu ya vyoo, madarasa chini ya mti kwa miaka zaidi ya 50?

Jibu: Endelea kujenga hoja zenye mashiko. Siasa za fujo hapana.
Nashukuru kwa maelezo haya..kwa mwendo huu bado huoni dai la Katiba ni hoja ya msingi sana?

Ikiwa Mkuu wa Nchi amepewa mamlaka makubwa hivi na huyo Mkuu pia ni Mwanasiasa na Mwenyekiti wa Chama huoni hatatenda usawa kwa Wanasiasa wengine wataokuwa mlengo tofauti na yeye(wao)?

Hapa ndipo wenzetu wanapojenga hoja kwa mifano ya wazi na sisi tukashindwa kuijibu badala yake tukaminya mrija wa hewa ili wapinzani wakose hewa wademke demke..
 
Nashukuru kwa maelezo haya..kwa mwendo huu bado huoni dai la Katiba ni hoja ya msingi sana?

Ikiwa Mkuu wa Nchi amepewa mamlaka makubwa hivi na huyo Mkuu pia ni Mwanasiasa na Mwenyekiti wa Chama huoni hatatenda usawa kwa Wanasiasa wengine wataokuwa mlengo tofauti na yeye(wao)?

Hapa ndipo wenzetu wanapojenga hoja kwa mifano ya wazi na sisi tukashindwa kuijibu badala yake tukaminya mrija wa hewa ili wapinzani wakose hewa wademke demke..
Sawa. Kuna mawili hapo:
1. Umuhimu wa Katiba Mpya
2. Uharaka wa Katiba Mpya

Ushahidi gani unahitajika kwa kila kipengele?

1. Kazi za Wariona na Kisanga ni ushahidi wa kipengele cha kwanza
2. Kipengele cha pili hakina ushahidi hadi sasa, japo Chadema wanakiuma uma midomo tu na kulazimisha kipaumbele cha Chadema kiwe ndio kipamumbele cha Serikali ya CCM.

Mambo hayaendi hivyo.

Tuweke nguvu ya hoja katika kipengele cha pili, cha kwanza kinaeleweka na kukubalika.
 
Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa, halafu nakuuliza swali. Wakati Dr Slaa na Katibu Mkuu wa CDM uliona mapambana kati ya CDM na dola kama sasa? Tafakari juu sababu zake.
Ukweli ulio wazi siasa za kipindi kile mtu kama Dkt.Slaa angekuwa anazifanya sasa sijui kama angekuwa bado anahema..

Wapinzani ni wale wale wanasubiria tuteleze wapate pa kujengea hoja lakini sisi tumekumbwa na ugonjwa wa kukosa uvumilivu hili ndiyo ninaloliona likitusumbua sasa hivi..

Tusilazimishe wanaotupinga waje soft soft,watakuja wakali na sisi tunapaswa kuwavumilia..

WANASIASA WANAPENDA MADARAKA LAKINI HAWAPENDI SIASA..
 
Unawasilisha nini? Huu UPUUZI WAKO? Upuuzi wako beba peleka lumumba.


Msimamo wa Rais Samia kuhusu demokrasia ya kisiasa, fujo za kisiasa na fujo za kidini ni wa kujadiliwa kwa kina kusudi watu wengi wauelewe na kuukubali.

Tayari kuna maoni kadhaa yametolewa tangu alipofanya mahojiano yake na BBC, na kuuweka bayana.

Kuna maoni ya Askofu Bagonza, Kauli za Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, mawazo ya Godbless Lema na maoni ya watu baki. Nami napenda kutoa maoni yangu leo.

1. Tofauti kati ya "demokrasia ya kisiasa na fujo za kisiasa" haikuanzishwa na Rais Samia.

Ipo siku zote kwa sababu ya mstari unaotenganisha siasa za watu wengi zinazoendeshwa kwa kutumia nguvu ya ushawishi wa hoja (democratic people's power) na siasa za watu wengi zinazoendeshwa kwa kutumia nguvu za ubabe na mitulinga (coercive people's power).

Fujo za kisasa zinazofanywa na vyama vya upinzani huwa ni mkakati wa kuiondoa serikali katika vipaumbele vyake. Hilo jambo halikubaliki popote duniani. Viongozi wa Chadema wanapaswa kuzingatia ukweli huu.

2. Kuna fujo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akipinga kauli za Rais Samia. Mnyika anasema kuwa uhuru wa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara na maandamano hauna mipaka.

Hapana. Hakuna haki isiyo na mipaka. Ni kweli vyama vya siasa vina haki ya kufanya mikutano ya hadhara ili kueneza sera zake.

Lakini pia vinalo jukumu la kujizuia kuikwamisha serikali katika azima yake ya kutekeleza programu ambazo ni vipaumbele vya kitaifa kwa mujibu wa Ilani ya chama tawala.

Kwa mujibu wa
tangazo la Mbowe pale Mwanza, Chadema hawatambui jukumu hilii. Wanapaswa kulazimishwa kulitambua jukumu hili.

3. Kuna viongozi wa Chadema wanafanya fujo za kisiasa kupitia mgongo wa dini makanisani.

Wanazunguka makanisani na kuwaomba viongozi wa makanisa kuingiza katika ratiba zao za kikanisa kumwombea Mbowe ili aachiwe huru.

Kwa kitendo hiki, viongozi wa kidini wanashiriki kutekeleza programu za chama cha siasa. Aidha, kwa njia hii viongozi na wanachama wa Chadema wanatumia dini kufanya siasa.

Naona kwamba hapa inakuja hatari kama ile ya "mitano kwanza" ya Askofu Bagonza dhidi ya "mitano tena" ya Shehe nanihii.

Na bado hadi sasa Askofu Bagonza anaendeleza chokochoko kwa sababu ya
ugonjwa wa theomania unaomsumbua.

Theomania ni ugonjwa wa kichaa cha kidini kinachomfanya mhusika kuamini kwamba yeye ama ni Mungu au mpaka mafuta wa Mungu, na kwamba kwa sababu hiyo, yeye ni mtu mwenye uwezo wa kujua kila kitu, kufanya kila kitu, kusikilizwa na kila mtu, na kupewa utii na kila mtu.

Naye Askofu Mwamakula ametunga novena ya kumwombea Mbowe yenye kibwagizo "Mwanakondoo Ameshinda," na hivyo, kuigeuza CHADEMA kuwa Chama cha Demokrasia na Mwanakondoo Ameshinda"

Hatua za haraka zichukuliwe kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi kusimamia kanuni inayokataa jaribio lolote kuanzisha na kuendesha chama cha siasa chenye kutafuta ufuasi kwa kutumia mafundisho ya kidini.

Nawasilisha.
 
Mpuuzi kweli wewe!!! Mfumo wa vyama vingi nchini upo kwa miaka 30 sasa ndiyo miongo mitatu sasa ya chaguzi ambazo hazikuwa huru na za haki lakini bado huoni uharaka wa kuwa na Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi. Kwa ufinyu wako wa akili labda tusubiri miaka mingine 30 huku genge la wahuni wa maccm wakiendeleza udhalimu na dhuluma zao kwenye kila chaguzi ikiwemo wizi na mauaji ili kuendelea kung’ang’ania madarakani.


Sawa. Kuna mawili hapo:
1. Umuhimu wa Katiba Mpya
2. Uharaka wa Katiba Mpya

Ushahidi gani unahitajika kwa kila kipengele?

1. Kazi za Wariona na Kisanga ni ushahidi wa kipengele cha kwanza
2. Kipengele cha pili hakina ushahidi hadi sasa, japo Chadema wanakiuma uma midomo tu na kulazimisha kipaumbele cha Chadema kiwe ndio kipamumbele cha Serikali ya CCM.

Mambo hayaendi hivyo.

Tuweke nguvu ya hoja katika kipengele cha pili, cha kwanza kinaeleweka na kukubalika.
 
Back
Top Bottom