Msishangae Diamond siku baba yake akifa akaandaa mazishi ya kifahari

Msishangae Diamond siku baba yake akifa akaandaa mazishi ya kifahari

Sijawahi kusikia "mazishi ya kifahari" kwa Waislam.

Halafu nakushauri kuwa wachana na mambo ya kufatilia ya watu, huyajuwi. Wewe fata yako na familia yako. Ya Diamond na familia yake yatakusaidia nini?

Unajuwaje nani atatangulia?
Kajambe kule wewe bibi shika adabu yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
baba baba tuu mkikua mtajua thamani yake!!
long time dingi alkua nandunda had nkamchukia nkimuomba ela ya daftari ananambia sina na nnajua anazo.... mambo n mengi ila asaiv siezi mwacha adhalilike kwan naanza kudhalilika mie then family

na wamama punguzeni kuwalisha sumu watoto.. baba yenu ivi baba yenu vile....
m hata simshangai diamond namlaumu mama ake
Point yanii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wamama tunakuwaga na fitina sana
Point. Jamii imezoeleka kumwona baba ndo kavunja mahusiano kwenye ndoa. Ila ukweli ni kwamba kuna wanawake wengine huku duniani hawakuletwa kuolewa, najua wengi mtalipinga hili ila simlazimishi yeyote akubaliane nami. Sio kila mwanamke afaa kuwa MAMA! Ila kwa wanaume walio kwenye ndoa muda mrefu kwa asilimia kubwa wanatunza ile heshima ya ubaba kwa watoto wao, hawapendi kuwaona watoto wao wakimkosa mama yao ndo maana wanaendelea ku share chumba. Sikatai kuwa wapo pia wanaume wasiojitambua ila si jukumu au sahihi la mtoto kumrithi adui wa mamaake au babake. Hayo si yake bali ya wazazi wenyewe. Kids need to be neutral kwenye magomvi ya wazazi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa Diamond ndo anavaa, wee anza kupitia picha zake mitandaoni kisha uje utuambie kama Diamond ni Muslam
Kuvaa msalaba hakukutoi kwenye Uislam. Si kigezo cha kutoka kwenye Uislam.
 
Mkuu kuna tofauti kati ya baba na spermdonor ...kuna wanaume akisha kutia mimba kala kona (spermdonor)kuna mwingine akisha kutia mimba anakua responsible na we we mpka mwisho na mtt analea (baba) sio kila mwanaume anauweza ubaba mkuu ...

am better here
Hiyo tofauti naielewa sana mkuu. Katika jamii yetu haya mambo ya kutia mimba na kula Kona hayakuwepo huko nyuma, nazungumzia kizazi cha miaka ya 80s kwenda juu. Kina baba walikuwa hawakimbii majukumu kwa sababu ilikuwa ni Aibu kwa jamii. Hata ikitokea kwa kesi chache za kina baba waliokimbia majukumu yao kimalezi ya familia basi ndugu wa upande wa Baba mara nyingi walichukua jukumu la kujitwisha majukumu hayo. Mifano iko mingi katika familia na jamii iliyotuzunguka.

Hata huyo uliyemuita "Sperm donor" bado ni baba tu. Maana bila kuchangia hizo "Sperm" zake za Mama peke yake sizingejitosheleza kuleta kiumbe duniani.
Wanaume kwa asilimia kubwa sana huwa tunaweka/tunahifadhi mambo mazito sana katika vifua vyetu na ndio maana huwa tunakufa mapema sana ukilinganisha na Wanawake.

Kuna kesi moja ilitokea Zambia au Malawi kama sijakosea, jamaa alikuwa na Mke wake na walibahatika kupata watoto wanne (4). Yule bwana aliwajali kwa kuwapa matunzo bora na kuwasomesha wale watoto katika Shule bora kabisa za pesa nyingi. Mwisho wa siku kulitokea mfarakano katika ndoa, mwanamke alifumaniwa. Jamaa akachukua uamuzi wa kufanya DNA ya watoto wake. Kilichotokea ni AIBU.
Jamaa alichukua Begi lake la nguo tu na kuondoka. Wanaume tunapitia mengi sana sana ila ndio hivyo hatuna mtetezi wala msemaji. Tunakufa na Tai shingoni.
 
Hapo hapo Diamond endelea kukaza hivyo hivyo, haiwezekani usababishe Mimba halafu utelekeze au ukatae kulea.Mfano mimi nilipata kusimuliwa kuwa baba ako alichomoa mimba eti kisa ana mke wake (nimekuwa mali ya babu na bibi mzaa Mama).Nashangaa eti mtu anajitokeza alivyosikia niko nachukua Shahada yangu,,,,,,,yaaani upo above 20yrs ndiyo unamsikia baba.Hapo bora niendelee kuwa sina baba wala mashangazi,,,,,mbona Mungu amesaidia miaka yote hiyo bila yeye.
 
Kwangu siwez mlaumu kwa lolote sasa hivi maana huwez jua huyo mzee alivowaumiza alipokuwa na nguvu.
Kuna wazaz wengine wakiwa katika position nzur hujisahau sana. Kuna mzaz unaweza ombea mpaka afe. Somo tu kwa kina baba tusijisahau kwa michepuko pia mtoto kufundishwa sio lazima uogopeke nyumban, ukiogopeka hapo ndo wake zetu huchukua nafasi za kutengeneza na watoto.
Mtu unakuwa na mtoto wa kiume lakin hata stori mbili hakuna. Mtoto wa miaka mitatu akisikia baba karudi anajifungia kabatini.
Raha ya mtoto ni pale unaporudi maanza mishemishe za kucheza, kama ni mkubwa unamfanya rafiki kiasi kwamba hata mambo yake ya ndan anakusimulia.
Kuna jamaa yangu mmoja ni dume anawatoto watatu. Anavoishi nao mpka raha. Mama inafikia hatua anasena watoto mimi nimeshusha ila hawana habar na mie yaan hata nikisafiri hawaniulizii ila baba sasa hayapiti masaaa. Ukweli ni kuwa wadogo anatawaza, anatoka nao out mara kwa mara. Ukimkuta nyumban anakimbizana nao kama nae ni mtoto. Anawaogesha. Akienda kunywa bia lazina arudi na nyama ya watoto na hazidishi saa tatu. Na sio kuwa ni maskinj la hasha mke mwalimu baba ana vibiashara vyake vya milion
ubalikiwe umetusema sana
 
Kuna mambo kamwe hauwezi kuyaelewa mpaka utakapokuwa Baba na kuyapitia. Sikatai ya kwamba Mama zetu huwa wanapitia changamoto nyingi katika ndoa,mahusiano na malezi ya watoto, ila kuna mengine husababiswa na wakinamama. Haswa unapoona baba anaamua kuondoka na kuendelea na maisha yake huwa kuna mengi sana nyuma ya pazia. Kwa kuwa jamii yetu imejikita kuwatetea na kuwabeba kinamama ndio maana kina Baba huwa wanaonekana kavu sana.
Mwisho wa siku kwa haswa kwa sisi watoto wa Kiume huwa tunakuja kuwaelewa mababa zetu kwa kina zaidi pale tunapokuwa kwenye Taasisi ya Ndoa na Ubaba wa familia. Mifano iko mingi tu.

Ndio Maana katika Amri kumi za Mungu namba 4 huwa inasema "Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako." Haikumtaja mama peke yake wala kusema baba aliyekulea na kukupa matunzo, bali imemtaja BABA na Mama.
Tunaangamia kwa kukosa maarifa.
Hii sms ni bora tena naipa nafasi ya kwanza hasa kwa kuelezea ujumbe mkubwa mno.

Hongera sana Kaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom