Msumbiji: Inasemekana Magaidi wamevamia Msafara wa Wanajeshi wa Tanzania na Lesotho

Msumbiji: Inasemekana Magaidi wamevamia Msafara wa Wanajeshi wa Tanzania na Lesotho

Haya njoo uone mode ya ulinzi wa benki ili ujue utayari wetu una dosari, pale bank kuna vibanda wamejengewa askari wanajificha huko, akija mteja au hata mtu wa kujitoa muhanga akiwa na bomu la kurusha kwa mkono anaingia nalo ndani anafanya tukio kirahisi sana , kwani mlangoni penyewe hakuna hata iron detector maskini ya mungu, na wale askari wanatakiwa wasinigiche ndani wakae mita chache kwa nje waone kila kitu kinachoendelea
 
Ambush haina mjanja hata marekani inapigwa ambush za mara kwa mara kwenye convoys zao za kijeshi
Hapa maybe ushauri jeshi lipate drone za kuescort misafara kama hii ukizingatia geografia ya msumbiji ni misitu
 
Angalieni udhaifu mwingine wa ulinzi wa ndani, hivi eneo kama kariakoo ni wakua na kituo kimoja cha polisi? Pale msimbazi tu! Ilitakiwa vituo kama vitano pale kariakoo na standby force ya majanga hasa ya moto iwepo pale karibu maana ile ni sura ya nchi, haya 24/7 road patrol watu walindwe tu yaani askari sio awe mchukua rushwa hapana yeye alinde usalama mambo ya risiti, na blahblah nyingine wasihusike nazo kabisa zaidi wakiona usumbufu au wakashtakiwa na mtu haraka sana wachukue hatua, tatizo jamaa wamejaa rushwa haijawahi kutokea, wanaweza kua wasumbufu kwa wafanyabiashara wa ndani na nje, halafu huwezi kukuta askari wa nchi zinazojitambua akifukuzia rushwa au kupanga matukio ya kihalifu hapana hayo utayakuta kwenye nchi za kishenzi kishenzi kama ile nchi ya upande wa kushoto,
 
Aisee sijui ndio intelijensia yenyewe yaani mjeshi in AK47 inakuuliza kitambulisho tu
Juzi tulienda kutoa mahari karibu na chikongo tukakutana na mageti kama 4 hivi,tukaanza kuhojiwa tangu saa 4 mpaka saa 7 hatukuwa na barua ya mtendaji yenye picha bali tulikuwa na vitambulisho vingine tu wakaanza kutuhoji maswali yasiyo na kichwa wala miguu,,,, mara kama vipi tugawane hiyo mahari na blah blah kibao mwishoni wakaomba buku 5 wakatuachia tukapita mageti yote,ndipo nikawaza kwahali hii kazi ipo
 
Angalieni udhaifu mwingine ulinzi wa ndani, Day patrol ni kama hakuna, tuna night patrol nayo pia haipo active huu ndio ukweli pamoja na kua na aksari wachache tukaongeza na mgambo na hao shirikishi japo hao ni watu wa hovyohovyo tu, nguvu nyingi kuliko akili Day patrol muhimu maana mchana watu wanapiga tukio na kuondoka kama kawaida
 
Angalieni udhaifu mwingine wa ulinzi wa ndani, eneo kama muhimbili pale ukitoa main entrance tena na wao wako na virungu tu ni eneo gani lenye ulinzi tena pale? Wakati inatakiwa wawe triangular au four angles centered ambao wako na utayari muda wowote ikitokea dharura hali hiyo utaikuta Benjamin mkapa Dom, KCMC moshi na Bugando mwanza kote hali ni hiyohiyo yaani inasikitisha
 
Vitengo vya uokoaji na dharura kwa Tanzania wao kwanza hawana vifaa maana hata drone za kuzima moto hatuna nahisi, ndio maana matukio mengi sana hua yanatuacha na aibu za karne anzia meli ya bukoba, ndege, vivuko yaani kila tukio hatujawahi kulidhibiti inavotakiwa tunakuja kuambulia aibu tu baadae, lazima majeshi yetu yabadilike
 
Hata kama naishi kwa dada yangu bado ukweli utabaki vilevile kuwa kazi ya jeshi ni ya kijinga.
Unaishi kwa amri mpaka unastaafu.
Hata CDF anaishi kwa amri, je hawa ma junior!!
Kazi gani ambayo waweza fanya halafu usiishi kwa Amri labda uwe unajiuza mwili wako

Hiyo ndio kazi pekee uwezayo kujiamulia

Kwani wewe unafanya kazi gani ni changuoa wa kike au kiume unayejiuza?
 
Mwisho watu wetu kupenda kwao pombe, ngono zembe, na masihara vitakuja kutugharimu sana iko siku itakua na emergence call on duty watu wote washalewa sijui itakuaje
 
Kazi gani ambayo waweza fanya halafu usiishi kwa Amri labda uwe unajiuza mwili wako

Hiyo ndio kazi pekee uwezayo kujiamulia

Kwani wewe unafanya kazi gani ni changuoa wa kike au kiume unayejiuza?
Hata kuuza mwil mteja anakuamrisha u change style..
 
Lakinj tahadhari pia mkae mkijua, hawa wanamgambo, au magaidi ujifanikiwa kuwatimua kibiti kamwe usifanye sherehe kwani wenzenu wanaenda kujipanga upya, nanmatukio kama yale yatufundishe sasa kubadili hata ukaaji wa vituoni sio crew nzima iko ndani kama mna kikao, yaani vituo vyote vya polisi toka yale matukio nilitarajia kuona ukaaji mpya wa utayari lakini sijaona kitu ambacho sio kizuri kabisa,
 
Hilo ni jambo jema sana, kuweka GPS kwenye silaha na kuzitelekeza huku mkizimonitor is good methods ya kufahamu machimbo yao na kuwamaliza.
Hiyo kazi wameifanya sana Israel. Kuna missions nyingi wametumia eavesdropping na geolocation kwa msaada wa vitu wanavyotumia magaidi. Wanatengeneza mtandao feki wa fedha na resources kama redio, camera, simu na silaha kisha wanasikiliza mission imepangwa wapi, viongozi wakuu ni nani, silaha nyingine ziko wapi, wafadhili wenu kina nani. Waarabu nao sio wazembe
 
Utachekwa.
AK-47 hata sights za kuweka infrared scope uitumie usiku haina. Ikifika usiku unapigana kama mpuuzi tu wa Boko Haram wakati wewe ni mwanajeshi wa taifa. Huwezi funga sight ya kupima umbali na kulenga shabaha, inategemea uwezo binafsi wa kulenga na uzoefu wa mwanajeshi. Kama unadhani Tanzania ina wanajeshi exceptional kiuwezo basi hujui kulinganisha majeshi au unapumbazwa na uzalendo feki ule unaoamini kujikweza ndio kuipenda nchi.

Hamza pale Salender unajua walimrushia risasi ngapi kabla ya kumuua, wakati ni bonge nyanya refu, kijana mzembe wa familia ya kitajiri hata rifle ukute alikuwa anaziona kwenye movie na aliuwawa barabarani. Sasa angekuwa ni trained terrorist kwa zile AK-47 na SMG unamuua saa ngapi.

Hawa ni Botswana wanazo kama FN FAL na SAR 21View attachment 2423673

Hawa ni Kenya nao wana hizi na AK-47 bado zipo nyingiView attachment 2423674

Hawa ni Russia standard rifle yao kijeshi kwa sasa ni AK-12 ambayo ni derivative ya AK-47 ila ya kisasa ingawa characteristics ni zilezile. Na hii ndio iko very simplified na basic. Waasisi wake wanaziacha kama sio outdated kwa niniView attachment 2423676

Hawa ni China na QBZ-191 ambayo ndio standard rifle. JW niliwaona na kitu kama QBZ-95 mwaka jana/juzi walipopigwa ambush na hawa magaidi ikakamatwa APC ya Kichina. Wachina walikuwa na SMG zao na copycat ya AK-47 wanaita Type 56 wakaziacha. Kama sio outdated kulikuwa na haja ganiView attachment 2423677

Bunduki design ya 1947 haiwezi tumiwa na taifa serious kujilinda. Hiyo ni very cheap ila hata effective range yake ndogo kiasi, accuracy ndio kwa standard za sasa ni ndogo na sights hamna. Hizo bunduki nilizotaja wala sio expensive, sio lazima ziwe hizi. Wajerumani ndio wana bunduki nyingi hatuwezi afford
Akili kubwa sana,,, vita ni technology sikuhizi,,,
 
Niliwahi sikia eti jeshi la ardhin linaongoza ni kweli?
Kwa uhakika zaidi halipo hata top 5 bara la Afrika. Sijamaanisha tuko namba 6 ila nina uhakika 100% hatupo 5 of the best armies in Africa. Egypt, South Africa, Morocco, Algeria na nchi fulani.

Niliandika sana ila nikafuta. Bado kuna nchi naziona kabisa hizi hapana ila sikatishi tamaa watu
 
Back
Top Bottom