Mtaji wa biashara zangu umeanza kukua, sasa naombeni mnisaidie jambo hili

Mtaji wa biashara zangu umeanza kukua, sasa naombeni mnisaidie jambo hili

Heshima kwenu wakuu.

Mimi ni mfanyabiashara mdogo wa duka, Ukerewe . Kuanzia mwezi wa 6 kurudi nyuma, nilikuwa mtu wa kuhemea mzigo kwenye maduka ya jumla hapa hapa Nansio kwa pesa taslim laki 4 na kushuka. Yaani uwezo wangu ulikuwa wa kununua mzigo wa bidhaa kwa laki 2, laki 2.5, laki 3-4 basi.

Kuanzia mwezi wa 6+ mambo yakaanza kubadilika tena kwa kasi ya ajabu. Kutoka mwezi huo wa 6 hadi sasa mtaji umekuwa ukikua na sasa nimefikia uwezo wa kuingiza dukani mzigo wa milioni 2+.

SASA NATAKA NIANZE KUWA NANUNUA BIDHAA MWANZA KWENYE MADUKA AU MACHIMBO AMBAYO HAWA WAFANYA BIASHARA WANAOTUUZIA JUMLA JUMLA HUKU UKEREWE WANAPONUNUA LAKINI SASA SIJUI YALIPO HAYO MADUKA AU MACHIMBO.

Je, wanaonunua mizigo yao yote pamoja?? Yaani anaponunua ngano hapo hapo anaenunua sukari, mafuta ya kula, vinywaji baridi, lotion na mafuta mgando au wananunua kila category ya bidhaa kivyake??

Naomba kwa anaejua maduka au machimbo wanaponunua hawa wafanya biashara wa jumla kwa mkoa wa MWANZA anielekeze.

Je, kuna kiwango ambacho lazima ufikie ili mtu aweze kununua huko??

Kwa mkoa wa Mwanza wapi nipate ngano?
Wapi nipate vinywaji baridi?
Wapi nipate sukari?
Wapi nipate mafuta ya kula

Vyote kwa bei ambayo na mimi naweza kuja kuuza kwa jumla ??

Pia NATAFUTA WAUZA NAFAKA KWA BEI YA JUMLA WA JIJINI MWANZA.

Karibuni
Bado mtaji haujakuwa mzee. Wewe kama umeweza kufanya nao zikafika ml2 fanya nao zikue angalau ufike 10 hivyo hivyo. Kumbuka ukishaenda kufuata mwenyewe unapoteza ule uteja wenu unakuwa mshindan. Sasa kwa hiyo hela bado huna nguvu ya kushindana jipange kwanza usiwaonyeshe uwezo mapema
 
Mkuu ubarikiwe sana.

Huyo jamaa yako wa usafiri anaweza akawa anasafirisha kutoka madukani kupeleka Melini??
Yes. Kazi yake n kubeba mizigo kwa bajaji.
Kwaio hayo maduka yooote anayajua maana hua anapaki mitaaa hyo. So kazi yako n kulipia mzigo then ye atakuja aufuate anapeleka hadi hapo kwenye meli unasafiri na mzigo wako
 
Bei ya kiwandani ikoje mkuu na niwe na mtaji kiasi gani
Airtel pic moja ya Tsh 500 ni Tsh 470.....inamaana apo wewe unaweza ukawauzia watu wengine wa jumla kwa 478 au 490....kwa bei ya rejareja unauza 500

....ili uione faid andaa 3Ml adi 4Ml,uweze kuchkua pic zaid ya 10,000 [470×10,000] 4,700,000 apo kwa bei ya rejareja faida 300,000
 
Yes. Kazi yake n kubeba mizigo kwa bajaji.
Kwaio hayo maduka yooote anayajua maana hua anapaki mitaaa hyo. So kazi yako n kulipia mzigo then ye atakuja aufuate anapeleka hadi hapo kwenye meli unasafiri na mzigo wako
Kama hautojali, naomba mawasiliano yake pm for future use
 
Bado mtaji haujakuwa mzee. Wewe kama umeweza kufanya nao zikafika ml2 fanya nao zikue angalau ufike 10 hivyo hivyo. Kumbuka ukishaenda kufuata mwenyewe unapoteza ule uteja wenu unakuwa mshindan. Sasa kwa hiyo hela bado huna nguvu ya kushindana jipange kwanza usiwaonyeshe uwezo mapema
Asante kwa ushauri wako mkuu.
Mimi nataka nichukue mzigo mwanza lakini nitakuja kuuza kwa reja reja, sijafikia kiwango cha kuuza jumla mkuu.

Asante
 
Kaka wazo zuri sana na hapo ndio faida utaiona... Mim nina kibanda tu nachukua mzigo takribani wa mil 1 kwa wiki yan, vocha, sigara, pombe kali, maji na visoda vya jambo ila unajikamua wiki nzima. Unaambulia faida laki tu
Laki kwa wiki au kwa mwezi?
 
Bado mtaji haujakuwa mzee. Wewe kama umeweza kufanya nao zikafika ml2 fanya nao zikue angalau ufike 10 hivyo hivyo. Kumbuka ukishaenda kufuata mwenyewe unapoteza ule uteja wenu unakuwa mshindan. Sasa kwa hiyo hela bado huna nguvu ya kushindana jipange kwanza usiwaonyeshe uwezo mapema
Mi namshauri afanye vyote aendelee kununua kwa hao jamaa halafu kimya kimya awe ananunua mzigo mwingine mwanza
 
Mi namshauri afanye vyote aendelee kununua kwa hao jamaa halafu kimya kimya awe ananunua mzigo mwingine mwanza
Hujui principal za biashara Chief. Wakishagundua na watagundua tu kuwa kuna toleo jipya jiandae hata pale ulipokuwa unachukua mali kauli inakata. So kama umeweza kupandisha mtaji kwa muda mfupi piga kimya kimya ikifika Wakat wa kubadilika unakuta hata wakikubadilikia unakuwa uko salama kimtaji.
 
Heshima kwenu wakuu.

Mimi ni mfanyabiashara mdogo wa duka, Ukerewe . Kuanzia mwezi wa 6 kurudi nyuma, nilikuwa mtu wa kuhemea mzigo kwenye maduka ya jumla hapa hapa Nansio kwa pesa taslim laki 4 na kushuka. Yaani uwezo wangu ulikuwa wa kununua mzigo wa bidhaa kwa laki 2, laki 2.5, laki 3-4 basi.

Kuanzia mwezi wa 6+ mambo yakaanza kubadilika tena kwa kasi ya ajabu. Kutoka mwezi huo wa 6 hadi sasa mtaji umekuwa ukikua na sasa nimefikia uwezo wa kuingiza dukani mzigo wa milioni 2+.

SASA NATAKA NIANZE KUWA NANUNUA BIDHAA MWANZA KWENYE MADUKA AU MACHIMBO AMBAYO HAWA WAFANYA BIASHARA WANAOTUUZIA JUMLA JUMLA HUKU UKEREWE WANAPONUNUA LAKINI SASA SIJUI YALIPO HAYO MADUKA AU MACHIMBO.

Je, wanaonunua mizigo yao yote pamoja?? Yaani anaponunua ngano hapo hapo anaenunua sukari, mafuta ya kula, vinywaji baridi, lotion na mafuta mgando au wananunua kila category ya bidhaa kivyake??

Naomba kwa anaejua maduka au machimbo wanaponunua hawa wafanya biashara wa jumla kwa mkoa wa MWANZA anielekeze.

Je, kuna kiwango ambacho lazima ufikie ili mtu aweze kununua huko??

Kwa mkoa wa Mwanza wapi nipate ngano?
Wapi nipate vinywaji baridi?
Wapi nipate sukari?
Wapi nipate mafuta ya kula

Vyote kwa bei ambayo na mimi naweza kuja kuuza kwa jumla ??

Pia NATAFUTA WAUZA NAFAKA KWA BEI YA JUMLA WA JIJINI MWANZA.

Karibuni
Pia uchunge matapeli wameshasoma mahitaji yako hapa hivyo watakutokea
 
Hujui principal za biashara Chief. Wakishagundua na watagundua tu kuwa kuna toleo jipya jiandae hata pale ulipokuwa unachukua mali kauli inakata. So kama umeweza kupandisha mtaji kwa muda mfupi piga kimya kimya ikifika Wakat wa kubadilika unakuta hata wakikubadilikia unakuwa uko salama kimtaji.
Ni kweli, biashara huwa na mafuriko na kiangazi pia. Hivyo lazima uwe mtu wa research mara kwa mara uweze kupata njia ya ku escape wanapoku suprise.
 
Hujui principal za biashara Chief. Wakishagundua na watagundua tu kuwa kuna toleo jipya jiandae hata pale ulipokuwa unachukua mali kauli inakata. So kama umeweza kupandisha mtaji kwa muda mfupi piga kimya kimya ikifika Wakat wa kubadilika unakuta hata wakikubadilikia unakuwa uko salama kimtaji.
Acha uoga. Kama anaweza kuchukua mzigo mwanza na akaongeza faida afanye hivyo. Kwenye biashara kinachoangaliwa ni kuongeza faida na kupunguza gharama. Hayo mambo ya kuogopa watu ni enzi za Nuhu huko. Na hata kama ukiwa mwema vipi lazima kuna watu wakuone nuksi tu. Huyu jamaa cha muhimu asivunje sheria za jamhuri na za Mungu.
 
Acha uoga. Kama anaweza kuchukua mzigo mwanza na akaongeza faida afanye hivyo. Kwenye biashara kinachoangaliwa ni kuongeza faida na kupunguza gharama. Hayo mambo ya kuogopa watu ni enzi za Nuhu huko. Na hata kama ukiwa mwema vipi lazima kuna watu wakuone nuksi tu. Huyu jamaa cha muhimu asivunje sheria za jamhuri na za Mungu.
Sina uoga mkuu mi nimetoa mawazo na tahadhari. Mi niko kwenye biashara miaka 30 hiv sasa. Nachosema hiyo kasi ya upandaji wa mtaji alitakiwa apande nayo kimya kimya maana bado hakuna kikwazo. Kuwajulisha watu ushalingana nao huku ukijua hujajipanga na matokeo yake ni kujiharibia. Ila haya mawazo sio sheria mi naongea kwa uzoefu wangu sio wake. Biashara sio kuuza na kununua tu ni pamoja na mazingira endelevu ya kuaminika. So kabla hujachukua hatua za juu zaid jipange usiwe na haraka. maana biashara kubwa zaid ni kuaminika kuwa mwaminifu.
 
Sina uoga mkuu mi nimetoa mawazo na tahadhari. Mi niko kwenye biashara miaka 30 hiv sasa. Nachosema hiyo kasi ya upandaji wa mtaji alitakiwa apande nayo kimya kimya maana bado hakuna kikwazo. Kuwajulisha watu ushalingana nao huku ukijua hujajipanga na matokeo yake ni kujiharibia. Ila haya mawazo sio sheria mi naongea kwa uzoefu wangu sio wake. Biashara sio kuuza na kununua tu ni pamoja na mazingira endelevu ya kuaminika. So kabla hujachukua hatua za juu zaid jipange usiwe na haraka. maana biashara kubwa zaid ni kuaminika kuwa mwaminifu.
Mkuu comment yako imejaa busara za hali ya juu ila mimi ninaona kama hana madeni kwa hao suppliers wake wa sasa hakuna madhara yoyote akiagiza Mwanza. Ila kama kuna ambao humpatia mzigo kwa mali kauli anaweza kuanza kutulia kwanza kwa muda kama ulivyosema. Milioni 2 bado ni hela ndogo.
 
Bado mtaji haujakuwa mzee. Wewe kama umeweza kufanya nao zikafika ml2 fanya nao zikue angalau ufike 10 hivyo hivyo. Kumbuka ukishaenda kufuata mwenyewe unapoteza ule uteja wenu unakuwa mshindan. Sasa kwa hiyo hela bado huna nguvu ya kushindana jipange kwanza usiwaonyeshe uwezo mapema
Point hiyo au anza kubadilika kidogo kidogo unakuwa unachukua baadhi ya vitu mwanza vingne unachukua kwao
 
Back
Top Bottom