Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Mim napenda kuungana na walioshauri hapo juu kama una muda na hutegemei kuajiri mtu kwenye hiyo biashara basi unaweza kufanya 1. mobile money ( mpesa, tigo pesa .....)
2. Fuga hawa kuku wa kisasa kwa kuanzia anza na 1000 kwanza
3. Tafuta sehemu ambayo inakuwa weka hardware simple anza hata kuuza cement kwanza
Angalizo biashara zote isipokuwa zile ambazo ni mpya kabisa kwenye jamii zinahitaji ''mentorship'' mtu wa kukuongoza kila hatua wakati wa kuanza.

Kila la kheri.
 
Mkuu habari yako njoo Uganda huku ufanye biashara ya viatu vya mtumba na nguo za mtu unachukuwa Uganda unareta Tanzania..naauta tumia hiyo milion 8 yako yote unaweza kuanzia milion 3 adi 4..maana huku kuna viatu vizuri sana.

Sent from my SM-N950F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu unaweza kunifafanulia hii??
 
Mfano zp hizo wabongo weng wanazikimbia??
 
Habari za wakati huu;

Leo nimekuwa na mazungumzo na rafiki yangu mmoja aliyeko nje ya nchi na katika mazungumzo yetu aliniambia kwamba anapata shida sana kupata taarifa za kuvutia kuhusu Tanzania,hasa kuhusu utalii,mitindo ya maisha,utalii.Anasema katika ulimwengu wao wanategemea sana mtandao wa internet kupata taarifa.Akanishauri ni kwa nini tusianzishe mradi wa kuitangaza Tanzania kidigitali kwa kuweka taarifa sahih i na njema kuhusu Tanzania,wiliaya zake,mikoa yake na hata kata zake.

Baadhi ya taarifa wanazohitaji ni gharama za maisha,hali za maisha,huduma za kijamii,vivutio vya utalii,historia,n.k.

Nimeona hilo wazo ni Jema ni baada ya kulifanya hesabu kamili nimeona ni wazo ambalo linaweza kutekelezeka kwa mtaji kiasi cha shilingi milioni 10+ kwa kuanzia.Wazo lote litahitaji zaidi ya shilingi milioni 135 na lintakuwa na uwezo wa kutengeneza mapato ya wastani wa shilingi milion 3 had 7 kwa mwezi kwa kutegemea hali ya soko na kiwango cha uwekezaji.

Niko mbioni kulitekeleza wazo hili hata hivyo nimeona nililete hapa Jukwaani ili kama kuna watu ambao wangependa kwa sehemu ya wazo hili ambalo lina tija kibiashara na kimaendeleo kwa taifa basi tuwasiliane.

Sifa za watu wanaohitajika ni kama ifuatavyo:
  1. Wenye Mtaji Pesa kuanzia kiasi cha shilingi laki tatu pamoja kumiliki pc walioko popote Tanzania
  2. Wenye mtajii Maarifa na pesa kuanzia kiasi cha shiling laki 2 pamoja na kumiliki pc waliopo popote Tanzania
  3. Wenye Mtaji maarifa na muda kuanzia masaa 12 kwa wiki pamoja kumiliki PC walioko popote Tanzania
  4. Wenye Mtaji Pesa na uwezo wa Usimamizi watakao kuwa Tayari kuwa SPONSORS wa PROJECT nzima
  5. Kama unafikiri unaweza kuwa sehemuya utekelezaji kama mtu binafsi yaani usimamie kuliuza na kuliporomote eneo moja,mfano mkoa wako,wilaya yako au kata yako unaweza pia kuwasiliana namiili tufanikishe lengo.Uwe unaufahamu mzuri wa eneo ulilopo na uwezo wa kulielezea na kulipromote
Sifa za ujumla,uwe na uwezo wa kuandika kwa kiingereza /kifaransa/kijerumani/kihispania/kichina/kijapani au lugha yoyte ya kigeni yenye wazungumzaji wengi duniani.
Kama unapenda kuwa sehemu ya hii project tafadhali tuwasiliane masokotz@yahoo.com.
Wale wataonesha kuwa na seriousness tu ndo watapewa taarifa zaidi.

Karibuni na kila la heri

NB:Hii sio fursa ya ajira,wala mwito wa kuwekeza katika hisa au biashara.Ni fursa ya kuanzisha aina ya biashara ambayo utaisimamia mwenyewe.SISI kama Masoko Consult tutaratibu tu wazo zima na kukuonesha FURSA ilivyo ambapo tutakupatia huduma zifuatazo:
  1. Kupa mwongozo wa nini cha kukufanya
  2. Kukushauri katika utekelezaji
  3. Kukushauri katika usimamizi
 
Hili wazo nzuri kweli, nimeona hadi America wana websites za kila states zinaonyesha hivyo vyote na hizo websites zinamilikiwa na manispaa ya jiji. Na mm natamani Tanzania tuwe na kitu kama hicho.
 
Hili wazo nzuri kweli, nimeona hadi America wana websites za kila states zinaonyesha hivyo vyote na hizo websites zinamilikiwa na manispaa ya jiji. Na mm natamani Tanzania tuwe na kitu kama hicho.
Asante kwa kuanza kuelewa,Hata hivyo hii nataka kuifanya kama Private initiative ingawa tutaangalia namna ya kushirikisha wadau wengi iwezekanavyo kwa kadiri ya uwepo wa rasilimali muda na rasilimali pesa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…