Mtangazaji mpira Azam Tv anaboa sana

Mtangazaji mpira Azam Tv anaboa sana

Jamaa maneno meeeengi hata hayahusiani na game yenyewe. Akimtaja mchezaji ataanza kumchambua weeee hadi club alizopita, badala ya kutangaza mpira unaochezwa uwanjani yeye ni ujuaji na story tu. Yaani utafikiri yupo kwenye kipindi cha majadiliano.

Too much boring.

Halafu hata tone/sauti yake haiko kiutangazaji wa soka, utafikiri anaimba shairi
Sasa si uombe kazi ili ukatangaze wewe! Haya makasiriko yako yanakusaidia nini ndugu!!
 
Kama ni wewe nakushauri unapotangaza mpira jaribu kukaza sauti, pia focus kwenye mchezo uwanjani na sio kuanza story za na maneno ya MIPASHO. Jifunze kwa manguli kama Chales Hilary. Pia fuatilia watangazaji wa ligi kubwa kama EPL au Laliga uone wenzako wanapojikita na yanayoendelea kwenye pitch.

Eti mtangazaji unatangaza mpira unaanza kusema " huyu Keita anazuia pale na kumuambia wewe siwezi kukuruhusu kirahisi unipite, kwanza hujui mimi ni kisiki cha mpingo waulize wenzako, mimi nimeaga kwetu na taifa linanitegemea kwahiyo hapa ni ngome ya vifaru na mizinga, huyu keita ni mzaliwa wa .... ni baba wa watoto watatu japo hii ni ndoa yake ya pili, pia kijiji Chao kinaitwa.....alikuwa kwa tabu sana huyu".

Imagine umbea wote huo anaoeleza wakati huo game inaendelea na haizungumzii. Halafu anarudi tena kwa mchezaji mwingine anaitwa labda Koulbaly utasikia " Koulbaly anapiga chenga pale anamuambia beki utanijua mimi ni nani, huyu ni mzaliwa wa kijiji kinachoitwa.... alianza mpira kwa kupelekwa academy na mjomba wake ambaye alikuwa na wanawake wanne"
Povu hilo,kama vipi kaombe hiyo kazi utangaze wewe maana una hasira sana
 
Hakuna mtangazaji anayependwa kama Nazareth upete na nurdin . Bongo ukiwa unatangaza kama unasoma risala Hakuna mtu wa kusikiliza watu wanapenda uweke na historia kidogo maneno maneno hio ndio nature ya wabongo vitu wanavyopenda kuvisikia
 
Sasa si uombe kazi ili ukatangaze wewe! Haya makasiriko yako yanakusaidia nini ndugu!!
Mmezoea porojo tu. And this is one of the weakness of Kiswahili language. Ni lugha maneno meeeengi halafu kilichomo hakijai hata kijiko, yaani ni kama furushi la pamba wakati uzito ni robo.
Hata vikao vinavyoendeshwa kwa kiswahili huchukua muda mrefu sana wakati agenda ni mbili tu. Fuatilia hata mijadala ya Bunge letu.

Nadhani hata ahadi za kujenga barabara, maji na Umeme huenda zingeshafaniwa kazi kama tu hizo ahadi zingetolewa kwa Lugha ya Kizungu

Kwa hiyo hata nyie watangazaji mnaotumia muda mwingi kupiga porojo msamehewe tu
 
Labda kama unashida na tune yake... Lakin ukija upande wa historia hata watangazaji wakubwa huko ulaya wanatabia za kutoa historia za wachezaji na binafsi navutiwa sana na inaonesha kuwa mtangazaji kabla ya Mechi kafanya homework yake vizuri
Tatizo wabongo english inatupiga chenga kwahiyo wakati tunaangalia epl au uefa tunakuwa hatuelewi kama kati kati ya utangazaji kuna kuongelea historia za wachezaji ndo maana tunawashangaa kina Nurdin maana wanatumia lugha yetu
 
Yote tisa,kumi ni mtangazaji wa Azam anayetangaza matangazo mubashara ya ligi kuu NBC wanamuita Pascal Kabombe (sijui kapombe) .Aisee jamaa huwa ananiboa sana ,hajui kutangaza na mipasho huwa mingi kuliko mpira anaoutangaza.
 
Halafu wanapenda kiingereza cha kachumbari huku hawakijui. Mara back left sijui back right
 
Mmezoea porojo tu. And this is one of the weakness of Kiswahili language. Ni lugha maneno meeeengi halafu kilichomo hakijai hata kijiko, yaani ni kama furushi la pamba wakati uzito ni robo.
Hata vikao vinavyoendeshwa kwa kiswahili huchukua muda mrefu sana wakati agenda ni mbili tu. Fuatilia hata mijadala ya Bunge letu.

Nadhani hata ahadi za kujenga barabara, maji na Umeme huenda zingeshafaniwa kazi kama tu hizo ahadi zingetolewa kwa Lugha ya Kizungu

Kwa hiyo hata nyie watangazaji mnaotumia muda mwingi kupiga porojo msamehewe tu
Sasa Bosi wangu mimi na utangazaji wapi na wapi! Mimi nimekushauri tu upunguze hasira.
 
Jamaa maneno meeeengi hata hayahusiani na game yenyewe. Akimtaja mchezaji ataanza kumchambua weeee hadi club alizopita, badala ya kutangaza mpira unaochezwa uwanjani yeye ni ujuaji na story tu. Yaani utafikiri yupo kwenye kipindi cha majadiliano.

Too much boring.

Halafu hata tone/sauti yake haiko kiutangazaji wa soka, utafikiri anaimba shairi
Atakuwa mtu wa pwani au visiwani
 
Nurdin Seleman ndio mtangazaji bora kabisa kwa taarifa yako, style yake ya utangazaji inatukosha wengi, jana niliposikia anatangaza yeye nikaangalia gemu ya saa 5 azam sports 3, kumbuka mechi zote za afcon naangaliaga Dstv channel 222.Nikimsikia Nurdin nard azam tv.Acha wivu wa kike.
Nurdin ukizingua tunakusema tu
 
Jamaa maneno meeeengi hata hayahusiani na game yenyewe. Akimtaja mchezaji ataanza kumchambua weeee hadi club alizopita, badala ya kutangaza mpira unaochezwa uwanjani yeye ni ujuaji na story tu. Yaani utafikiri yupo kwenye kipindi cha majadiliano.

Too much boring.

Halafu hata tone/sauti yake haiko kiutangazaji wa soka, utafikiri anaimba shairi

Wale watangazaji wa mpira kwa lugha ya Kiingereza huwa unawasikiliza na kuwaelewa wakitangaza mathalani Premier League, WC, AFCON n.k?

Maana hata wao kuna muda huwa wanapiga soga kuhusu mchezaji au jambo lolote linalohusiana na mchezo/wachezaji husika...
 
Kama ni wewe nakushauri unapotangaza mpira jaribu kukaza sauti, pia focus kwenye mchezo uwanjani na sio kuanza story za na maneno ya MIPASHO. Jifunze kwa manguli kama Chales Hilary. Pia fuatilia watangazaji wa ligi kubwa kama EPL au Laliga uone wenzako wanapojikita na yanayoendelea kwenye pitch.

Eti mtangazaji unatangaza mpira unaanza kusema " huyu Keita anazuia pale na kumuambia wewe siwezi kukuruhusu kirahisi unipite, kwanza hujui mimi ni kisiki cha mpingo waulize wenzako, mimi nimeaga kwetu na taifa linanitegemea kwahiyo hapa ni ngome ya vifaru na mizinga, huyu keita ni mzaliwa wa .... ni baba wa watoto watatu japo hii ni ndoa yake ya pili, pia kijiji Chao kinaitwa.....alikuwa kwa tabu sana huyu".

Imagine umbea wote huo anaoeleza wakati huo game inaendelea na haizungumzii. Halafu anarudi tena kwa mchezaji mwingine anaitwa labda Koulbaly utasikia " Koulbaly anapiga chenga pale anamuambia beki utanijua mimi ni nani, huyu ni mzaliwa wa kijiji kinachoitwa.... alianza mpira kwa kupelekwa academy na mjomba wake ambaye alikuwa na wanawake wanne"
Dah haya unayasema nimetoka kuyasikia jana usiku kwenye mechi ya DRC Congo vs Guinea. Yaani ni style ya kijinga haswa sijui kaipendea nini.
 
Nurdin Seleman anajua vizuri historia ya wachezaji,lakini swala la kutangaza kama anaimba kwangu naona jau.
 
Wanaboa Sana. Sema hawajui Kama wanaboa. Tangaza mpira achana na mambo mengine.
 
Back
Top Bottom